Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

Chama Kipya (CCJ) na Hatima ya CCM - lisemwalo...

kama ccj haiwasumbui si mgebana kimya tuu?

kwa kutoa tamko rasmi ina maana ccj imeleta maneno kweli kweli
ndani ya ccm.
 
kama ccj haiwasumbui si mgebana kimya tuu?

kwa kutoa tamko rasmi ina maana ccj imeleta maneno kweli kweli
ndani ya ccm.


Nimesoma kwa karibu maelezo ya Chiligati lakini kuna jambo moja naomba kupingana naye. Kuruhusu vyama vingi haukuwa uamuzi wa CCM kama chama ulikuwa uamuzi wa mzee wa busara, Baba wa Taifa hili Marehemu Mwl. J.K Nyerere. It is a pity leo Chiligati kusema ulikuwa uamuzi wa CCM. Nakumbuka Nyerere alitoa mwito wa kukubaliwa vyama vingi akiwahutubia umoja wa vijana kule Mwanza. Ingekuwa ni Chiligati angesema Watanzania hawataki vyama vingi hivyo CCM iendelee kutawala bila upinzani kwa maoni ya Watanzania walio wengi ambao hawakujua hata wanaongelea kitu gani wakati wa kutoa maoni.

Chiligati, kama CCJ hasiwasumbui kaa kimya matamko ya nini?

Tiba
 
Tangu vyama mbalimbali vianze kuanzishwa hakuna wakati wowote ambapo CCM wamehangaika kutoa matamko juu ya chama kisicho na mpango, kisicho na tofauti na ambacho hata usajili wa muda hakijapata!!
 
just want to know who is the party founder so i can fiter the mortives
 
Ni dhahiri ya kwamba vigogo wa ccm wanajua maovu wayafanyayo kila iitwapo leo, wengine hofu yao si tu kuanzishwa kwa ccj bali hofu ya kupoteza chansi za ulaji na ndio maana roho zinawadunda. kwani wao kama wanaongoza vizuri na wanalinda maadili kwanini wahofu??

Hapo hofu yangu mimi isijekuwa ni wale mafisadi kuona wanashindwa kutimiza azma zao kwa ndani ya ccm kuna walio safi na wasioendekeza upuuzi kama huo na ndio iwe wao wanaanzisha hicho chama cha ccj, mwisho wa siku tutapata kuzijua mbivu na mbichi maadamu wachafu wote tunawajua. Tusishawishike kwa fedha tukauza hadi haki zetu kwa mafisadi, na kama vipi hii iwe kampeni ya kitaifa ya kuwabaini wasiotutakia mema sisi walala hoi wa nchi hii tena tusiokuwa na mahali pa kupeleka vilio vyetu, kweli JF the home of great thinkers.
 
Sasa hivi tumepata chama kipya,CCJ.Kimeungana na TLP,CUF,UDP,Chadema,NCCR
kutaka kuleta demokrasia ya kweli nchini!!Time will tell.
Tupeni CV ya hawa viongozi wao:
Mwenyekiti: Richard Kiyabo
Katibu :Renatus Muhabhi
 
  • ATOA USAJILI WA MUDA,
  • ATANGAZA KUKICHUNGUZA KUANZA SIASA KABLA YA USAJILI
Ramadhan Semtawa

SIKU moja kabla ya kutoa hati ya usajili wa muda hapo jana kwa Chama Cha Jamii (CCJ), Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, tayari aliiweka hatma ya kisiasa ya chama hicho njia panda baada ya juzi kutangaza kuanza uchunguzi kuona kama kilianza shughuli za kisiasa miaka miwili iliyopita kabla ya usajili.

Jana Tendwa alihitimisha safari ya miezi miwili ya CCJ kusaka usajili wa muda, lakini tayari akiwa amekiweka pabaya chama hicho, baada ya juzi kunukuliwa na kituo cha ITV akisema ofisi yake inafanya uchunguzi wa kina ili kuthibitisha kama chama hicho kilianza siasa kabla ya kusajiliwa miaka miwili iliyopita na ikithibitika atakifuta.


Kauli hiyo ya kitisho ya Tendwa akiitoa siku moja kabla ya kukabidhi hati hiyo huku akisisitiza kwamba, chama hicho kitapaswa kufuata taratibu za kisheria katika utendajikazi wake.


CCJ chama ambacho kimesababisha mtikisiko ndani ya CCM kimekuwa kikifuatilia usajili wa muda katika Ofisi ya Msajili kwa karibu miezi miwili sasa tangu kuwasilisha maombi yao Januari 20, mwaka huu.


Hofu ya CCJ kuanza kazi za kisiasa miaka miwili nyuma, inaangaliwa na wadadisi wa mambo ya kisiasa kama inayotokana na nguvu zake ikiwemo mtandao mpana nchi nzima huku viongozi wake wakitangaza jana kwamba, wanatarajia kukamilisha kazi ya kuzunguka nchi na kupata idadi ya wanachama 200 katika kipindi cha mwezi mmoja na nusu baada ya kupata hati hiyo badala ya miezi sita.


Habari zaidi zinadai kwamba kwamba baadhi ya vigogo serikalini na katika CCM walikwishafuatwa wakiwemo wakuu wa mikoa ambao baadhi walikubali kuunga mkono na wengine kukataa.


Lakini wakati Tendwa akitoa hati hiyo na onyo la kukifuta chama hicho, Mwenyekiti wa CCJ Richard Kiyabo, alitumia fursa hiyo kutoa ufafanuzi wa tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hicho na kusema hakina uhusiano wowote na Idara ya Usalama wa Taifa kwani mpango huo una lengo la kukivuruga ili kionekane ni chama pandikizi.


Kiyabo alifafanua kwamba, CCJ ni chama tofauti na vingine vya upinzani kwani kimejipanga vema kuhakikisha kinakidhi mahitaji ya msingi ya kidemokrasi kwa Watanzania.


"CCJ siyo chama cha Idara ya Usalama wa Taifa, ni chama cha usalama wa maisha ya Mtanzania, ni chama makini tofauti na vingine vya upinzani kwa hiyo kuna tofauti kubwa," alisisitiza.


Mwenyekiti huyo ambaye alikuwa akibebwa juu pamoja na katibu wake Renatus Muabhi na baadhi ya wanachama waanzilishi, alisema lengo, nia na madhumuni ya CCJ ni kushiriki uchaguzi wa Oktoba.


Aliweka bayana mkakati huo kwamba, katika kufanikisha azma hiyo CCJ imejipanga kukusanya wanachama wanaotakiwa kisheria ndani ya kipindi cha mwezi mmoja na nusu.


"Tumejipanga kushiriki uchaguzi, nia tunayo na hadi sasa maandalizi ni mazuri tu kwani tutaweza kukusanya wanachama wetu ndani ya kipindi cha mwezi mmoja na nusu," aliongeza.


Kuhusu usajili wa wanachama, alisema tayari walizundua mchakato huo rasmi siku hiyo ya jana baada ya kupata usajili huo na kuongeza: "Hata ninyi waandishi wa habari mnakaribishwa."


Akizungumzia kuhusu kuwepo vigogo ndani ya CCM, Kiyabo alirudia kwamba wao wanalenga wanachama 20 milioni na hadi sasa hawana vigogo wowote ndani ya chama hicho tawala.


"Sisi hatuzungumzii sijui vigogo, hatuna vigogo ndani ya CCM tunachozungumzia ni namna ya kuwapata wanachama 20 milioni nchini kote, inawezekana sasa wanachama ukichanganya na CCM waliopo ni 10 milioni," aliongeza.


CCJ ujio wake unaangaliwa na wadadisi wa mambo ya kisiasa kama tishio kwa CCM na Rais Jakaya Kikwete, kutokana na kutajwa kuhusisha vigogo wa chama hicho tawala ambao wanataka kujitenga na kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.


Tayari Spika wa Bunge Samuel Sitta, aliwahi kusema kwamba, haoni tatizo la kusajiliwa CCJ huku pia akisema hawezi kuzuia watu kumhusisha na chama hicho kama mgombea hapo Oktoba.


CCJ imekuwa ikitikisa nchi tangu taarifa zake kuchapishwa kwenye vyombo vya habari, kwani kuna majina makubwa yanatajwa kuwemo akiwemo Spika Sitta, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba, John Malecela, lakini wote wamekanusha.


Hata hivyo, mwasisi wa CCM Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kuonya kwamba bila CCM madhbuti nchi itayumba na upinzani wa kweli ungetoka ndani ya CCM onyo ambalo wadadisi wa mambo ya siasa anaona kama linakaribia.


Source: Mwananchi

Mie huwa najiuliza what is so fuzz about CCJ? Is it just media fan wapate kutuuzia magazeti? Au CCM propaganda kuondoa attention ya wananchi kuhusu ufisadi? au ni chama cha wanyonge!!!!
 
JANA Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, alitoa cheti cha usajili wa muda kwa Chama Cha Jamii (CCJ), baada ya kupokea maombi ya chama hicho na kuyafanyia kazi kwa zaidi ya miezi miwili.

Makumi ya mashabiki na wafuasi wa chama hicho walikuwepo kwenye ofisi za msajili kushuhudia tukio hilo muhimu kwa chama chao chenye maskani yake Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Kwa mbwembwe na tambo, wafuasi wa CCJ walibeba mabango huku wakifurahia hatua hiyo. Nawapongeza kufikia hapo.

Hii ilinikumbusha miaka kadhaa nyuma wakati wa kusajiliwa kwa Chama cha Democratic (DP) chini ya uenyekiti wa Mchungaji Christopher Mtikila, ambacho sasa kimebaki kwenye historia na orodha ya vyama vyenye usajili wa kudumu nchini.

Mamia ya wafuasi wa DP, wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake wakisindikizwa na ngoma ya mdundiko walikuwepo nje ya ofisi za msajili hali iliyomlazimu kukabidhi cheti cha usajili nje ya ofisi kutokana na wingi wa watu japo kwa jana, hali haikuwa hivyo.

Baada ya kukabidhi cheti cha usajili wa muda, kwa mara nyingine Tendwa alirudia kauli yake kwamba CCJ haiwezi kushiriki kwenye uchaguzi mkuu Oktoba, mwaka huu.

Msajili huyo alieleza sababu za chama hicho kutoshiriki kwenye uchaguzi huo kuwa ni muda wa kukamilisha taratibu za kuwasilisha majina ya wanachama 200 kila mkoa kwa mikoa 10 kutoka Tanzania Bara na Visiwani ambao ni miezi sita kwa ajili kupata usajili wa kudumu kabla ofisi ya msajili nayo kutumia muda wake kuhakiki majina hayo.

Miezi sita kutoka siku waliyopokea cheti cha usajili wa muda ni Septemba 2 mwaka huu kipindi ambacho kampeni za wagombea mbalimbali waliosimamishwa na vyama vyao zitakaposhika kasi.

Si hivyo tu, kwa mujibu wa Tendwa mchakato wa kuwapata wagombea watakaowakilisha vyama vyao kwenye uchaguzi kwa nafasi ya urais, ubunge na udiwani zinaanza Mei mwaka huu.

Katika akili ya kawaida, naona wazi kwamba hata CCJ wakipeleka majina ya wanachama wao mwezi mmoja baadaye, sina hakika kama ofisi ya msajili itaacha kila kitu na kushughulikia chama hicho.

Inaingia akilini mwangu kwamba sheria inamtaka msajili kupata majina ya wanachama 200 kila mkoa kwa mikoa 10 nchini kisha kuyahakiki na kujiridhisha kabla ya kuwapa usajili wa kudumu utakaowaruhusu kushiriki kwenye uchaguzi ujao. Sasa muda wa kukamilisha haya utatosha kabla ya Septemba?

Japo si kazi ndogo kuwapata wanachama hao, ila muda waliopewa kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992 ikifuatwa ipasavyo, ni wazi kwamba chama hicho hakitashiriki kwenye uchaguzi.

Katibu wa CCJ, anajitapa kuwa chama chake kipo tayari kumaliza kazi ya kuzunguka mikoa 10 katika kipindi cha mwezi mmoja kutoka sasa. Hili linawezekana ingawa litaacha maswali mengi ikiwemo ya wao kuvunja sheria za usajili wa vyama vya siasa inayowazuia kufanya shughuli zozote za chama kabla ya kupata usajili wa muda.

Msingi wa mtazamo wangu ni mkanganyiko na mlolongo wa matukio uliokuwepo kabla na baada ya CCJ kupata usajili wa muda hali inayoniacha na swali pengine ujio wa chama hiki ni mkakati wa CCM ama usalama wa taifa kutaka kuchafua hali ya hewa kwenye kambi ya upinzani.

Chama hiki kilianza kusikika mwishoni mwa mwaka jana ingawa hakikupewa nafasi masikioni mwa wafuatiliaji wa siasa za Tanzania. Januari mwaka huu kikaja kwa kasi na kubeba uzito wa juu kwenye vyombo mbalimbali vya habari.

Kilipoanza, baadhi ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walihusishwa nacho ingawa wapo waliokanusha na wengine kuendelea kuwa kimya hali inayonipa majibu ya kwamba ni kweli wanahusika.

Vigogo wanaohusishwa na CCJ ni Spika wa Bunge Samuel Sitta, makundi ya wanachama watiifu wa CCM walio mstari wa mbele kupambana na ufisadi, ambao wote leo hii wamekula matapishi yao kwa kukubali kufungwa midomo kwa vitisho na hofu ya kutopitishwa kwenye kura za maoni wakielekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba.

Wakongwe wengine wanaotajwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba, John Malecela na wengine.

Ujio wa chama hiki kwa kiasi kikubwa ninaamini una mkono wa vijana kutoka usalama wa taifa na kwenye kambi ya siri ya watawala wetu wakubwa ambao wapo tayari kutumia gharama zozote kujisafisha machoni pa wapiga kura ili waendelee kututawala.

Japo wananchi waliaminishwa kupitia taarifa mbalimbali kutoka kwenye vyombo vya habari kwamba kuna hofu ya kumeguka na kuyumba kwa CCM ambacho ni chama kikongwe nchini baada ya CCJ kujitokeza, baada ya kutafiti dhamira yangu inakataa kulikubali hili.

Zipo pia taarifa za kuaminika kwamba vijana wanaoongoza CCJ kwa muda wapo kwenye kile tunachokiita ‘system'. Kwa akili yangu, ninaamini kabisa kuwa wapo kwa ajili ya kazi maalum ya kuusambaratisha upinzani na kuwavuruga Watanzania walio mashabiki wa siasa.

Hawa wameamua kuchezea kivuli cha CCM ili kupima nguvu ya wapinzani wanaoonyesha kukubalika zaidi Tanzania Bara, huku viongozi wa chama tawala wakitumia nguvu kidogo kuipaka matope CCJ kana kwamba hawajui kinachoendelea. Binafsi siipendi siasa kutokana na wengi wa waliomo ndani yake kuwa ‘wasanii', ingawa napenda kuwaona wanasiasa wanavyoshindwa kueleza ukweli umma wanaouongoza, badala yake wanauma maneno hasa kipindi cha uchaguzi.
 
Atoa usajili wa muda, atangaza kukichunguza kuanza siasa kabla ya usajili
 
Hofu ya CCJ kuanza kazi za kisiasa miaka miwili nyuma, inaangaliwa na wadadisi wa mambo ya kisiasa kama inayotokana na nguvu zake ikiwemo mtandao mpana nchi nzima huku viongozi wake wakitangaza jana kwamba, wanatarajia kukamilisha kazi ya kuzunguka nchi na kupata idadi ya wanachama 200 katika kipindi cha mwezi mmoja na nusu baada ya kupata hati hiyo badala ya miezi sita.

Sasa hili linatatizo gani, labda wamejipanga vyema ili kulikamilisha.

CCJ ujio wake unaangaliwa na wadadisi wa mambo ya kisiasa kama tishio kwa CCM na Rais Jakaya Kikwete, kutokana na kutajwa kuhusisha vigogo wa chama hicho tawala ambao wanataka kujitenga na kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Tatizo viongozi wengi walio ndani ya SISIMU wana uroho na uchu wa madaraka ndio maana wanapata hofu.

Tayari Spika wa Bunge Samuel Sitta, aliwahi kusema kwamba, haoni tatizo la kusajiliwa CCJ huku pia akisema hawezi kuzuia watu kumhusisha na chama hicho kama mgombea hapo Oktoba.
May be yeye ana uhakika kurudi tena bungeni msimu ujao.
 
...
Baada ya kukabidhi cheti cha usajili wa muda, kwa mara nyingine Tendwa alirudia kauli yake kwamba CCJ haiwezi kushiriki kwenye uchaguzi mkuu Oktoba, mwaka huu.

Msajili huyo alieleza sababu za chama hicho kutoshiriki kwenye uchaguzi huo kuwa ni muda wa kukamilisha taratibu za kuwasilisha majina ya wanachama 200 kila mkoa kwa mikoa 10 kutoka Tanzania Bara na Visiwani ambao ni miezi sita kwa ajili kupata usajili wa kudumu kabla ofisi ya msajili nayo kutumia muda wake kuhakiki majina hayo...
Huyu Msajili yeye afanye kazi yake iliyopo sasa, CCJ watakapoishia ndo itajulikana hawawezi kushiriki uchaguzi au la. Kwani ni nani amemwambia kwamba uchaguzi ujao LAZIMA ufanyike Oktoba 2010? Hivi anafikiri CCJ ni wajinga hadi waendelee kukomalia usajili? CCJ wameshaona dalili kwamba uchaguzi ujao unaweza ukawa mbele zaidi, maybe hadi katikati ya 2011. Sababu kubwa ni mambo makuu mawili; Hoja ya mgombea binafsi na serikali ya mseto Zanzibar. CCJ endeleeni na usajili, uchaguzi ujao haupo hivi karibuni!
 
mkuu.. you might be very right.. wakati mwingine ili kujua maji ya moto kiasi gani inabidi utumbukize mkono. CCJ ilivyo na itikadi yake haijatoa sababu ya kwanini inataka kuwa chama kipya! Karibu malengo, nia, madhumuni, muundo na mfano ni carbon copy ya CCM tofauti ni herufi tu "J" na "M".. wao wameelezea yale yale yaliyoelezewa na CCM kwa maneno mengine! Labda ningependa kujua zaidi ni ajenda yao hasa ni nini?

Sometimes siyo mbaya kurudi nyuma kidogo
 
View attachment 233991View attachment 233998View attachment 233999View attachment 234000


Leo nimewakumbuka wale jamaa zangu wa CCJ

Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo kuna MAKADA wa CCM wakiongozwa na SAMWEL SITTA,ambao ni Nape Moses Nnauye Benard Membe na Haryson Mwakyembe na PAUL MAKONDA walijaribu kufanya uharamia ndani ya TAIFA na CCM kwa kujaribu kuunda chama cha SIASA ndani ya Chama cha siasa ambacho ni CCM....


Lakini cha kushangaza hivi leo makada hao hao ambao ni wasaliti wameanza kuwasema wenzao kuwa ni wasaliti na ni watu wasioitakia mema CCM.....


Najiuliza huyu NAPE,MEMBE na SITTA wameanza lini kuwa wazalendo wa CCM? je kadi zao za CCJ wamerudisha? je wanakumbuka walivyoitwa IKULU na JK kuwa wavunje CCJ yao?


Sasa nawaambia kuwa hawa WAHAINI wa CCM waache kuwachafua wenzao ambao ni WATIIFU wa CCM tokea mwaka 1977 na hawajawahi kufikiria kusaliti chama wala kuhama,,,,,,,,,,,
 
Wanavyotuibia haikuumi?
Kwa kuwa wanatuibia kwa utii wa chama wewe waona sawa tu!!!!!!!

Ccm ni tatizo kubwa kuliko tunavyofikiria na kufahamu.
 
Back
Top Bottom