Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 81,416
- 94,338
NI wachache sn umma ukiamuaPolisi je?
NI wachache sn umma ukiamuaPolisi je?
Hao mliokuwa mnaona ni mtaji wenu huko vijijini walimalizika baada ya TV na internet kuingia. Kizazi hiki sio kile cha zamani kilichokuwa kinaona mbolea na zahanati nyingi hisani ya serikali. Kwa taarifa yako hata ikiingia serikali ya kijeshi, itajenga zahanati, shule, kupeleka mbolea nk maana huo ni wajibu wa serikali inayokusanya kodi.Jibu ktk maelezo yako yapo ktk nukuu yako hii "Ukitaka kuwa masikini nchi hii, danganywa kwenda kulima. Utalima kwa gharama zako lakini wakati wa kuuza utapangiwa bei na anayeishi mjini"
Nami nakazia tu kuwa ukitaka kudanganywa kushinda kiti cha Urais kuwa na wanachama wengi mijini tu, halafu ukose kujulikana na ukose wanachama vijijini. Hata kwa kupata katiba mpya haitasaidia.
Ruzuku za mbolea vijijini utaziita HONGGO NA RUSHWA, ujenzi wa zahanati na madarasa vijijini utaita matope n.k
Tanzania katiba yetu ni Rais, Magufuli alishaonyesha katiba sio lolote zaidi ya makaratasi tuNi shukrani au ni kwa mujibu wa katiba na sheria!
Hahahaaaaa! Si nyie ndio mlikuwa mnapiga picha watoto wa shule msingi wakisomea chini ya miti huku mvua ikinyesha. Hivi kodi zilikuwa hazikusanywi? Mtaji huu kama hoja ya kuwaingiza IKULU hautajitokeza tena. Poleni!Hao mliokuwa mnaona ni mtaji wenu huko vijijini walimalizika baada ya TV na internet kuingia. Kizazi hiki sio kile cha zamani kilichokuwa kinaona mbolea na zahanati nyingi hisani ya serikali. Kwa taarifa yako hata ikiingia serikali ya kijeshi, itajenga zahanati, shule, kupeleka mbolea nk maana huo ni wajibu wa serikali inayokusanya kodi.
Mngekuwa mnategemea kura za huko vijijini tusingeona chaguzi za kihayawani vile. Danganyeni wajinga sio werevu.
Mkuu '1000Digits', nimekusoma kwa uangalifu mkubwa sana hadi mwisho wa andiko lako, na ni nadra sana kwangu kutaka kurudia nilichosoma mara ya kwanza (huwa nasoma kwa spidi kubwa sana), ili niliyoyasoma kwa mara ya kwanza yaniingie vizuri akilini.Chadema wanafeli kwenye Suala la Matumizi ya fedha na namna ya kuhamasisha upatikanaji Wa fedha Kwa ajili ya watu Wa Chini yaani wale viongozi Wa matawi ya Chini au mitaa.
Bila fedha hakuna ushindi popote Kwa Karne hii. Hata Vita bila fedha hakuna ushindi. Mbele ya fedha Hata nchi imepigwa Bei.
Pesa ni Kila Kitu. Hata Uzalendo Kwa Sasa unahitaji fedha.
CCM walionufaika sana na kifo cha Ndesamburo mana alikua ndiye nguzo kubwa ya Chadema ukanda Wa Kaskazini. Alikua anauwezo Wa kugharamikia shughuli Zote za chama na kuzuia wasaliti kununuliwa na CCM.
Sasa cha KUFANYA ni Chadema kuwakubali Wazalendo wote popote walipo.
Pili kufanya uhakiki Wa Wanachama wao NDANI na nje ya nchi. Kuwajua Kwa majina na Kwa idadi Yao. Kuwapanga Wanachama Kwa makundi na Kwa Uwezo wao .
Baada ya kuwajua Wanachama Wa Chadema waliopo tayari Kupinga ukiukwaji Wa Sheria za uchaguzi Sasa waanze kuhamasisha michango KUANZIA wenye uwezo Wa kuchangia elfu moja mpaka million Kumi .
Kama Chadema itaweka watu waaminifu kukusanya michango bila tamaa kama zile za CCM basi Kwa Miezi Kumi na moja kufikia uchaguzi wa Serikali za mitaa watakua wamekusanya zaidí ya bil.20.
Pesa hizo zisikae makao makuu mana ni za Wananchi . Zitumike kuwagharamikia wagombea wote Wa Serikali za mitaa nchi Nzima. Hawa wagombea Wa Chini wakipatikana Kwa Wingi basi ni rahisi kuwapanga Wanachama kuelekea uchaguzi mkuu Wa wabunge na madiwani ambao kimsingi wanahitajika kupata hamasa ya kukabiliana na wagombea Katili na wenye fedha wa CCM.
Na KUANZIA Sasa Chadema inapaswa kuwasaidia wale wote wanaopingwa na CCM Kama akina Dr. Slaa, Mwabukusi, Shivj, Mbatia, pia wale waliopo kuwaunga mkono au kuwakaribisha wale wanCCM wachache sana ambao Kwa dhahiri Wanapinga nchi kukabidhiwa Kwa wakoloni Kwa mgongo Wa Nyuma.
Chadema ikiendelea kuangalia uchaguzi Wa wabunge na madiwani tuu watapoteza uchaguzi mkuu Hata kama watashinda. Hakuna watu Wa kuhamasisha maandamano nchi Nzima kuanzia vijijini.
Pia ni vyema wakaanzisha será ya kuwalipa pesa za vikao wenyeviti Wa mitaa Ili kuwapa Nguvu na moyo Wa kujitoa .
Nisikilize boss, haya wanayofanya CCM ni wajibu sio hisani, na yoyote atakayeingia madarakani anapaswa kutekeleza, tena kwa speed kubwa katika kuliko hiyo ya CCM. Kizazi limebadilika na CCM sio chama cha kizazi hiki. Hao wajinga wa kuamini kuwa wajibu wa serikali unaweza kutekelezwa na CCM tu walishazeeka. Kizazi hiki kinataka ladha mpya na sio utawala wa shuruti na mazoea.Hahahaaaaa! Si nyie ndio mlikuwa mnapiga picha watoto wa shule msingi wakisomea chini ya miti huku mvua ikinyesha. Hivi kodi zilikuwa hazikusanywi? Mtaji huu kama hoja ya kuwaingiza IKULU hautajitokeza tena. Poleni!
Bwawa la umeme la Nyerere si ni mpango uliokuwepo toka enzi za Nyerere- Hivi wakati wote kodi zilikuwa hazipo. Fly over hizo nazo, Daraja la Busisi, SGR, N.K. Hivi huko nyuma kodi hazikuwepo? Jamani anayestahili, mpeni maua yake! Msiwe na choyo.
TV na internet vijijini bado sana. Simu huko vijijini hutumika sana katika sms, m-pesa, tigo/halo-pesa. Bando la Internet kama mjini mnalalamika unafikiri vijijini wanalo la kusikiliza hotuba ya kuboa ya LISSU, Dr Slaa n.k? Mnajidanganya mchana kweupeeeee!