Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,798
- 12,240
Tundu Lissu amewarai wananchi kuichagua CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu 2025 ili tuweze kupata katiba mpya itakayolinda rasilimali zetu na kumuwajibisha Rais asiyezingatia kiapo chake cha kulinda katiba na sheria za nchi. Hayo ameyasema alipowahutubia wananchi wa Chato jana tarehe 2 Agosti katika mwendelezo wa operation +255 kupinga kuuzwa kwa bandari zetu kwa DP World.
Hivyo wamekubali kushiriki uchaguzi Mkuu tofauti na vitisho vya awali ambapo walisema wasingeweza kushiriki uchaguzi wo wote bila kuwepo kwa katiba mpya. Kwa hiyo pamoja na operation wanayofanya pia wanapiga kampeni ya kutaka kuchaguliwa kuongoza dola.
Hivyo wamekubali kushiriki uchaguzi Mkuu tofauti na vitisho vya awali ambapo walisema wasingeweza kushiriki uchaguzi wo wote bila kuwepo kwa katiba mpya. Kwa hiyo pamoja na operation wanayofanya pia wanapiga kampeni ya kutaka kuchaguliwa kuongoza dola.