CHADEMA vs CCM: Nani Mbabaishaji?

Kama alishindwa kupigania demokrasia ndani ya Chadema, angeweza akiwa CCM? if it is true that alitaka kuhamia CCM, anajionyesha jinsi ambavyo alivyo
 
Na ingekuwa ni vyema Makamba akajibu a kuhusu hili la Wangwe kutaka kuhamia CCM.Hii ni habari nene..

Nimeambiwa habari hii iko katika Gazeti la Raia mwema la leo,nimemwambia jamaa aliscan na anitumie..

Na Kizitto Noya

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, kumhoji Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe.


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alisema jana kuwa, chama chake kina wasiwasi na jinsi CCM ilivyopata waraka wa marehemu kuhusu mgogoro wake na Chadema na kuanza kuusambaza siku moja kabla ya kifo chake.


Alisema, Makamba anapaswa kuhojiwa ili aeleze uhusiano wake na marehemu ambaye alikuwa Mbunge Chadema, hata akapata nyaraka hizo za siri katika kipindi kifupi kabla ya kifo chake na kuzisambaza.


''Hatutaki kuhitimisha kwa sababu sisi ni wanademokrasia, ila tunataka IGP sambamba na maombi yangu ya awali ya kumhoji Mkurugenzi wa TBC1, amhoji Makamba ili tujue uhusiano wake na marehemu na jinsi alivyopata waraka huo na kuusambaza siku moja kabla ya kifo chake,'' alisema Kabwe na kuongeza:


''Waraka huo ulipotolewa kwa mara ya kwanza na TBC1, mimi (Kabwe) nilikuwa na mashaka na Jumamosi iliyopita, niliwasiliana na IGP na Mkuu wa Usalama wa Taifa kuwataka wamhoji Mkurugenzi wa taasisi hiyo ya umma. Lakini leo (jana) tumefumbuliwa macho kwamba waraka huo ulianzia CCM na ikabidi niwasiliane naye (IGP), tena ili zoezi hilo limguse pia Makamba,'' alisema.


Alisema Makamba anapaswa kueleza alikopata waraka huo na sababu za kutumwa kwake muda mfupi kabla ya kifo cha marehemu ikiwa ni pamoja na msukumo uliomfanya ausambaze kwa viongozi wa CCM.


Kwa mujibu wa Kabwe, sheria ya usalama wa taifa ya mwaka 1996 inatambua ndugu wa marehemu kuwa wamiliki wa mali na taarifa muhimu zinazomhusu marehemu, hivyo ni ajabu CCM kumiliki waraka huo wakati haina uhusiano wa kindugu wala kiitikadi na marehemu Wangwe.


''Hivi CCM ina uhusiano gani na mbunge wa Chadema au ndugu wa marehemu hata ikahalalisha kumiliki waraka huo na kuusambaza bila woga?'' alihoji Kabwe na kusisitiza kuwa Chadema haijauona waraka huo na wala kuambiwa na ndugu wa marehemu.


Akizungumzia suala hilo, Makamba alikanusha kuhusika na waraka huo na kueleza kuwa, CCM haina haja wala sababu ya kuwa nao na kuusambaza.


Alisema CCM haihusiki na waraka huo na kubainisha kuwa wanaofanya hivyo ni watu wanaomwunga mkono marehemu Wangwe katika migogoro yake na chama chake.


''Mimi sijauona waraka wenyewe na sina taarifa nao, lakini kwa nini CCM iusambaze, ina shida gani na Chadema?'' alihoji na kuongeza:


"Chadema sisi hatuiogopi, tuliishinda Jimbo la Kiteto na tutaishinda mwaka 2010, hatuna haja nayo wala haitusumbui."


Kauli za Makamba na Zitto zimefuatia taarifa kwamba, CCM imekuwa ikisambaza waraka wa marehemu Wangwe wenye kurasa sita unaoelezea jaribio la Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kutaka kumvua wadhifa wake na uanachama.


Waraka huo unadaiwa kusambazwa kwa viongozi wa CCM kwa lengo la kuwafahamisha mgogoro wa Chadema ambao umekuwa ukihusishwa na chanzo cha kifo cha mbunge huyo.


Ukurasa wa nne wa nakala ya waraka huo unaonyesha kwamba, kwa mara ya kwanza ulitumwa kutoka Dodoma Julai 27 mwaka huu majira ya saa 9:42 alasiri toka namba (026) 2322965 ambayo imeonyesha kusajili kwa jina la ‘KATIBU MKUU CCM DOM’ tarehe ambayo ni siku moja kabla ya kifo cha Wangwe.


Uchunguzi umebaini kuwa waraka huo ulianza kusambazwa kutoka Dar es Salaam kwa namba za faksi 2667457 iliyotanguliwa na kodi namba ya mkoa (022) ikimaanisha kutumwa kutoka Dar es Salaam Julai 31, mwaka huu saa 5:50 asubuhi na mmiliki wa namba hiyo akitambuliwa kama SIGMA ICT.


Waraka huo, umetumwa kwa baadhi ya viongozi wa CCM mikoani, wakiwemo Makatibu wa Mikoa na Wilaya na wengine ukiwa ni mahususi kwa ajili ya kuwaonyesha kwa kina mgogoro wa Chadema ulivyo.


''Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa 2005, Mbowe alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama dola za Kimarekani 181,949.00, sawa na Sh 218,338,546 na mpaka sasa chama kimemlipa Sh175 milioni.


''Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha wilayani na makao makuu, niliamua kumshauri Mbowe asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku, kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa pesa za ruzuku kwa vyama vya siasa kutoka serikali.


''Mbowe alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo, basi atuthibitishie pesa hizo anazodai alikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya Chadema kupitia hundi ipi na lini?'' ilieleza sehemu ya waraka huo.
 
Hata Samuel alilia machozi . Yalikuwa ya majonzi kweli au mipango ilifeli? Can someone tell us more about the other side of Wangwe Chacha ? He had dreads . (Rasta) What happened because he never had one before ?
 
Kama alishindwa kupigania demokrasia ndani ya Chadema, angeweza akiwa CCM? if it is true that alitaka kuhamia CCM, anajionyesha jinsi ambavyo alivyo


Kwani marehemu alikuwaje?

Mod naomba uirudishe ile thread ya kumsimamisha Wangwe
 
Tumeanza "kusingizia" hata waliofariki? Ngoja tulisubiri RAIA MWEMA, mimi naliamini gazeti hili. Kaka wa marehemu Chacha Wangwe, Prof. Samwel Wangwe ni MNEC wa CCM na alikuwa na ushawishi mkubwa kwa mdogo wake.
 
Hivi mbona wanasiasa walioshiriki kikamilifu katika kutumia takrima kupata viti vya ubunge sasa ndio wako mstari wa mbele kukemea ufisadi na mafisadi? Ina maana wameongoka/wameokoka na kuzaliwa upya kisiasa hivyo wamekuwa wanasiasa safi/waadilifu? Au wanaona ufisadi walioufanya kwa takrima ni cha mtoto kwa huu utatu mkuu wa ufisadi, yaani EPA, KIWIRA na RICHMOND? Pengine wamegundua kuwa kweli katika siasa hakuna rafiki na adui wa kudumu hivyo wameamua tu kutoa kibanzi kwenye macho ya wenzao na kuacha boriti kwenye macho yao? Hivi kweli kuna Usalva wa kubadilika kisihasa?
 
Wewe Mwananchi Wa Tanzania Mbona Kila Siku Tunaongelea Upande Mmoja Tu Wa Kuhukumu Hawa Wapendwa Wetu Hata Siku Moja Hatutoi Suluhisho Ya Matatizo Ya Nchi Yetu ? Mimi Naona Hii Haifai Sasa Tuanze Tulalamike Halafu Chini Tuandike Suluhisho La Matatizo Haya Nafikiri Itakuwa Ni Nzuri Sana Kwa Jukwaa Tuanze Na Wewe Uliyanzisha Mada Hii
 
Tumeanza "kusingizia" hata waliofariki? Ngoja tulisubiri RAIA MWEMA, mimi naliamini gazeti hili. Kaka wa marehemu Chacha Wangwe, Prof. Samwel Wangwe ni MNEC wa CCM na alikuwa na ushawishi mkubwa kwa mdogo wake.

Kuhusu kuwa Prof.alikuwa na ushawishi kwa mdogo wake sio kweli kwani walikuwa na ugomvi wao na walikuwa hata hawasalimiani.

Kumbuka kilichotokea wakati wa uchaguzi wa Bunge la E.A pale marehemu alipokataa kumpa kura ndugu yake na hata ikamfanya wakati wa kumpigia kura Prof. Alitoka nje ya Bunge na zoezi lilipomalizika alirudi ndani.

Kuhusu kuhamia CCM , Tuendelee kulifuatilia ,ila najua kuwa alikuwa tayari amewekea mikataba ya kuishambulia na kuisambaratisha CHADEMA na CCM ndio maana kuna haya mapya yanajitokeza sasa kutokea huko CCM/.
 
Kila kukicha CCM inazidi kujidhihirisha ni chama kinachoongozwa na viongozi wa aina gani.Mimi nafikiri matatizo makubwa yako kwenye safu ya juu ya uongozi maana wao wana nafasi ya kurekebisha mambo na kuwadhibiti wa chini yao,lakini sio hivyo kwa hao walioko ambao kila siku ni kuzua mambo ambayo hayafanani na Chama kikongwe kama CCM. Ukiona chama kilichoko madarakani kina taka kutumia kifo cha mtu kujitafutia kukubalika na kujengea chuki na mfarakano katika chama kingine ujue wamefilisika kisiasa na kiuongozi.
Jambo la muhimu ni kuwatoa haraka madarakani kabla hawajasababisha maafa makubwa katika jamii iliyostarabika. Hata Mwakyembe alishasema NCHI HII SIO YA MABWEGE ! tumeshaelewa kinachoendelea.
 
Wewe Mwananchi Wa Tanzania Mbona Kila Siku Tunaongelea Upande Mmoja Tu Wa Kuhukumu Hawa Wapendwa Wetu Hata Siku Moja Hatutoi Suluhisho Ya Matatizo Ya Nchi Yetu ? Mimi Naona Hii Haifai Sasa Tuanze Tulalamike Halafu Chini Tuandike Suluhisho La Matatizo Haya Nafikiri Itakuwa Ni Nzuri Sana Kwa Jukwaa Tuanze Na Wewe Uliyanzisha Mada Hii

'Anza wewe'
 
Kama Katibu mkuu wa CCM ni Makamba nini kisichowezekana?

Kama mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya CCM ni Chenge ,nini kisichowezekana?

Kama wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM ni KIKWETE,MAKAMBA,ROSTAM,LOWASSA,CHENGE,nini kisichowezekana?
 
Msisahau taarifa zilizosema marehemu lionekana akiingia katika chumba cha Rostam Aziz kwa mazungumzo yasiyofahamika mpaka sasa.
 
Gembe huyoooooooo!!!!!
Nazidi kuamini kuwa CCM kweli WAKALI. WanatumbukiaMO ndani ya MSIBA na kuleta KALUFUNDI kao ku MAITI lwa watu.
Huyu Wangwe naanza kupata wasiwasi juu ya mwenendo wa Wangwe in GENERAL. Huyu bwaba alikuwa NDUMILA KUWILI. Heri angelikuwa PANYA akauma na kupuliza ila yeye akaamua KIVYAKE. Watu kama yeye, hasa anapodili na MAFIA huwa kuna dawa yao moja. Russian Mafia (KGB), Sisilian Mafia, Irish Mafia, ...... Mafia, CCM Mafia hizi zote ukiwa NDUMILA KUWILI dawa yako huwa moja. Sidhani hata CCM walikuwa wanamtaka Wangwe baada ya kujua kuwa kwa PESA ananunulika ki-RAHISI. Heri angelijileta mwenyewe, ila kaja kwa PESA? Akija Mbowe na kumwambia nipe siri za CCM, si atauza?
Kwangu mie, kama MADHARA, basi kwa Chadema alishafanya siku nyingi. Ila nashindwa kujua kama Chadema walifanya Controlled Conflict na Wangwe ili CCM wamsogelee na yeye awarekodi na baadaye KUMWAGA siri UMAFIA wa CCM. CCM Mafia walipojua nini kinaendelea, wakafanya vitu vyao na KUCHUKUA PESA ZILIZOKUWA KWENYE KOTI MKONO WA KUSHOTO/KULIA???
Hii iwe WARNING. Ukicheza na CCM ..................... Sijui kama Wangwe alijua hili.

NB:- Kama CHADEMA wangelitaka kumuua basi si wangelimuacha NDANI ya chama kama kiongozi na kujifanya CONFLICT zimeisha na hapo ndipo mnamrudi. Huwezi kumuuwa mtu huku mko kwenye conflict. SIdhani kama CHADEMA ni WABOVU kiasi hicho.
 
Mk,

haya yametoka CCM imetoka wapi tena?mie nilikuwa naomba uweke yale maneno yako uliyosyasema katika ile thread ya kumkashfu wangwe baada ya kusimamishwa na CHADEMA,uliongea maneno mengi sana na mojawapo ni la RA kukutana na Marehemu chacha..

Embu tueleze waliongea nini
Kuhusu kuwa Prof.alikuwa na ushawishi kwa mdogo wake sio kweli kwani walikuwa na ugomvi wao na walikuwa hata hawasalimiani.

Una uhakika walikuwa hawasalimiani?MK wewe ulimkandia sana Marehemu chacha kipindi kile cha azimio la Moshi,sasa uliwezaje kujua ya Chacha na samwel?
 
Msisahau taarifa zilizosema marehemu lionekana akiingia katika chumba cha Rostam Aziz kwa mazungumzo yasiyofahamika mpaka sasa.

there is someone here can tell us about the whole story..i think it is the time for him to lets us know the whole story
 
Mk,

haya yametoka CCM imetoka wapi tena?mie nilikuwa naomba uweke yale maneno yako uliyosyasema katika ile thread ya kumkashfu wangwe baada ya kusimamishwa na CHADEMA,uliongea maneno mengi sana na mojawapo ni la RA kukutana na Marehemu chacha..

Embu tueleze waliongea nini

Nilishasema kama unataka kukumbuka rudi kwenye mada ile na utaweza kukumbuka nilichosema .

Sikuwahi kuwa na thread ya kumkashifu wangwe, na jua kuwa wewe tangia jana uanze malumbano yako na Kiranja na hata kukiri kuwa wewe ni mtu wa CCM ila sio mtu wa ROSTAM ,huku mwenzio Kiranja akisisitiza kuwa wewe ni mtu wa ROSTAM , sioni haya ya kuendeleza mijadala isiyokuwa na tija kwa taifa letu.
 
Hii kali, yaani kuna watu wa CCM na watu wa ROSTAM? Naomba ufafanuzi..
 
nimesoma raia mwema ni kweli alikuwa anataka kuhamia ccm, hilo halina ubishi, na kufeli kwa mipango hiyo ndo kunawapagaisha ccm.
 
Mk,

haya yametoka CCM imetoka wapi tena?mie nilikuwa naomba uweke yale maneno yako uliyosyasema katika ile thread ya kumkashfu wangwe baada ya kusimamishwa na CHADEMA,uliongea maneno mengi sana na mojawapo ni la RA kukutana na Marehemu chacha..

Embu tueleze waliongea nini


Una uhakika walikuwa hawasalimiani?MK wewe ulimkandia sana Marehemu chacha kipindi kile cha azimio la Moshi,sasa uliwezaje kujua ya Chacha na samwel?

Azimio la MOSHI NI LIPI? mimi silijui.

Kuhusu kuwa walikuwa na ugomvi nimesema kuwa hata wakati wa kupiga kura za mbunge wa E.A Assembly,wangwe alitoka nje ya ukumbi wa bunge ili asishiriki kumpigia kura ndugu yake. sasa wewe unaweza kuona extent ya ugomvi wao.

Jua pia huyu Prof.alienda Tarime kwa ajili ya kampeni za kumpinga wangwe akishirikiana na mdogo wa marehemu aliyekuwa mwenyekiti wa halimashauri ya Tarime kwa wakati huo.
 
Back
Top Bottom