CHADEMA vs CCM: Nani Mbabaishaji?

CHADEMA vs CCM: Nani Mbabaishaji?

Watu wengi wanaoeneza udaku na uzushi huwa wanasema ulichosema hapa. Chambiri ana matatizo yake mengi tu kiuchumi na kisiasa Tarime, mambo ya kutaka kumtoa kafara kwa yaliyotokea Tarime ni uonevu mkubwa sana ambao sio tu unaonyesha rangi halisi za mtoa udaku, bali pia unajaribu kushusha hadhi ya jamii forum.

Ushahidi wa hao wengi? Hakuna aliyemtoa kafara Chambiri. Na haya tunayoyatoa hapa ni maoni yetu binafsi mimi na wewe. Yanaishusha vipi JF?
MK, una undugu wowote na akina Chambiri?
 
Ushahidi wa hao wengi? Hakuna aliyemtoa kafara Chambiri. Na haya tunayoyatoa hapa ni maoni yetu binafsi mimi na wewe. Yanaishusha vipi JF?
MK, una undugu wowote na akina Chambiri?

Anayeleta udaku na uzushi hapa kuwa Chambiri aliihujumu CCM Tarime kwa kutoa pesa kwa wananchi wa Tarime na CHADEMA ili CCM ishindwe kwenye jimbo la Tarime anajaribu kumtoa Chambiri kafara kwa yaliyoipata CCM Tarime.

Habari za udaku na uzushi kama unazojaribu kuziweka hapa huku ukiziita facts zimezoeleka kwenye magazeti ya udaku ya shigongo na wenzake. Ukiziendeleza hapa basi nia yako inaweza kuhesabika kama ya kutaka kuipeleka JF kuwa kama moja ya magazeti ya Shigongo.

No, sina undugu wowote na kina Chambiri ila nimecheza makopolo na michezo mingine yote ya kitoto na watoto wa Kisyeri na Mwita.
 
Naona wandugu hapa kwetu bongo siasa zinaelekea kuwashinda watatwala wetu kwani sasa hawajibu hoja badala yake wanajibu vioja.

Pili nimeshangazwa na CCM kujibu tamko lililoelekezwa kwa rais na CHADEMA badala ya habari maelezo kufanya hivyo je?hii ni kulinda mzee asiumbuliwe?

Naweka tamko la CHADEMA hapa na mwenye la CCM tafadhali aliweke hapa pia ili tuweze kujadili kwa kina.
CCM hawana akili
 
Back
Top Bottom