KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 86
Mkuu Wangu kitila,
Heshima mbele, katika ishu inayoniudhi sana kuliko zote katika siasa, ni unazi wa kitoto tena kwenye uwanja mkubwa kama huu wa JF,
Juzi niliona chama changu kikiitwa chamcha malaya, leo cha mafisadi, no way mkuu, tutofautiane ki-hoja, ila viroja hatuhitaji hapa,
Tukubalinae kutokubaliana lakini tuheshimiane, mafisadi 10 ndani ya serikali hawatufanyi wanachama wote wa CCM kuwa mafisadi, kama vile viongozi watano, wa chama chako kuwa kabila moja haiwafanyi owte muwe hilo kabila, hivi kuna mtu anahitaji kuelimishwa hilo hapa?
Wewe mkuu tunakuaminia kuwa siku moja uwe mwenyekiti wa huko upande wa pili, lakini na wewe umeshaanza kuwa na makengeza yale yale, CCM inapoitwa chama cha mafisadi kuoni, lakini kukiguswa uoande wa pili tu here you are!
Wakuu tukate hoja hapa, unazi hauna nafasi kwenye taifa, nilisema huko nyuma kuwa nenda Magomeni pale bondeni Jangwani asubuhi uone wananchi wakiteremka bonde kwa mguu kwenda kazini kwa kukosa nauli ya basi, I bet you some of them yaani wananchi walalahoi are CCM na wengine ni upinzani, na viongozi wetu wa pande zote mbili they could careless, maana hutawakuta wakienda kwenye biashara zao kwa miguu!
Sasa tunakuja kujaza unazi hapa, huku kina Cheyo wako Ikulu kwenye tafrija za taifa, tuache unazi hapa!
safi sana ! am working on this thing about ccm na nadhani itakuwa vizuri nikishare na wanaJF ! nikimaliza kuiandika nitaitundika hapa !