CHADEMA kuna tatizo kama ni kweli

CHADEMA kuna tatizo kama ni kweli

CHADEMA itakutesa sana . Mlisema bila ruzuku haitafika mahali ila Sasa mmebadilisha Tena usemi mnadai ubadhirifu wa pesa baada ya kuona haitetereki.
Mkuu hujui kuwa mti wenye matunda ndiyo upigwao mawe siku zote?
 
Tena ni wapumbavu mamluki wa ccm waliokosa soko baada ya kagenge kao ka chaumma kubuma kama yale manguruwe ya Samia yanayoshangilia ushindi wa asilimia 98 lakini kichwani Yana depression.
Duuuu ,hatari sana
 
unataka watu wajadili udaku.
leo hii mtu x atajirekodi huko uchochoroni na kusema Mmawia ni choko, unataka ndugu zako waichukulie habari hiyo seriously?
haujui kwamba watu wanaweza kuandika au kuongea chochote wanachojisikia hata kama ni cha uongo.
Unatumia nguvu nyingi kuongea na mpuuzi??? Mbona haongelei riport ya CA G na maandamano ya Jana??
 
Wangefuata ahadi ya uwazi waliyotoa haya yote yasingetokea. Siri siri ndio zinaibua maneno haya.

Amandla...
Uwazi upi?. Leo mnalilia uwazi. Si nyie mlisema ruzuku ndio imewafanya muhamie chaumma?. Kwamba CHADEMA haiwezi kudumu bila ruzuku. Mmeona michango ya raia mmeanza kelele. CHADEMA kwa Sasa ni Mali ya wananchi.
 
Sasa mbona hamuishi kumfuata fuata? Pambaneni na hao mnaowaita vijana wake, muache mjumbe wenu wa kudumu wa Kamati Kuu aliye mmoja wa waasisi wa CDM aendelee na maisha yake bila kumbughudhi. Kama hamu mmiss mpotezeeni.

Amandla....
Nani anammiss huyo tapeli? Aje achukuwe mamluki wake aondoke nao. Very stupid
 
Kumekuwa na shutuma nyingi sana juu ya uongozi wa juu wa chama.

Shutuma za ubadhilifu wa rasilimali fedha ndani ya chama.

Huu ni ushuhuda kutoka kwa mmoja wa viongozi wa chama mkoa wa Kilimanjaro.

Tujadili wana Jf

View attachment 3624857

---------------

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Mwanga, Mkoani Kilimanjaro Lembrus Mchome ametoa tuhuma dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, John Heche, akidai kuwa amekuwa akikusanya fedha kutoka kwa wadau, wafanyabiashara na mashirika mbalimbali kwaajili ya shughuli za chama lakini fedha hizo hazijafikishwa kwenye mifuko rasmi ya chama.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mchome amedai kuwa suala hilo lilijadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na kusababisha mvutano miongoni mwa viongozi, akimpongeza Godbless Lema kwa kile alichodai kuwa ni alisimama kidete kutaka fedha hizo ziwekwe wazi na kuwajibishwa kwa waliohusika.

"Tumekuwa na Makamu Mwenyekiti ambaye amekuwa akichukua fedha kutoka kwa wadau mbalimbali lakini zimekuwa hazifiki ndani ya chama. Ndio maana juzi kwenye Kamati Kuu wamegombana. Nimpongeze sana Godbless Lema kwani alisimama kidete kutaka fedha hizi zirudi, lakini haikuwezekana kwani Makamu Mwenyekiti alidai kuwa ameshazitumia na nyingine amenununulia vyombo vya muziki vya chama," alisema Mchome.

Mchome amebainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliowasiliana na Uongozi wa Chadema kupitia Kamati kuu iliyoketi Mkoani Kigoma walithibitisha kuwa walitoa michango kwa Heche kwaajili ya kukisaidia chama. Pia alidai Heche alisafiri hadi Afrika Kusini kwa lengo la kupokea fedha kutoka kwa wadau, akitoa rai ya wanachadema kumshinikiza Heche kujiondoa kwenye uongozi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo.

"Sasa niwaombe wanachama wa Chadema tushikamane kumtaka John Heche atupishe kwanza kwaajili ya uchunguzi. Chama hiki kinaamini katika misingi ya haki na kupinga ufisadi, kwa hiyo kwanini leo tumfumbie macho Heche?" alisema Mchome.

Katika hatua nyingine Mchome amemtuhumu Heche kunufaika kisiasa na hali ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu kuwa gerezani, akisema amekuwa akijijenga kisiasa pamoja na kutumia mwanya huo kuweza kufanya ubadhirifu kwa


Chanzo: Michuzi TV
Rubbish......yaani huyu ndio nani vile. Wewe na nani ? Moto umekuwa mkali na bado
 
Kwa faida ya watanzania wote hasa hasa wapenda siasa za mageuzi
Anayeweza thibitisha ubadhirifu ni CAG tu kupitia taarifa zake za ukaguzi, pia Financial intelligence Unit etc

Sasa kaguzi ya mwaka jana tu sijaona hizi query za wizi au ubadhirifu je nyie mnatoa wapi hizi taarifa? Mchome ni wazi ni mpinzani wa uongozi mpya hawezi kuwa credible source ya kuibua shutuma na zikaaminika.

Kubalini tu majira yamebadilika, chadema mpya ni ya moto sana na ndio wananchi wanaiunga mkono. Hivyo mjiunge mapema au mwende chaumma mkapotee kisiasa
 
itakuwaje wamuondoe kwenye uenyekiti wa CDM mtu ambae wanajua ni mwanachama wa Chaumma? Tafuteni uongo mwingine.

Jibuni shutma za mwanachama wenu. Chaumma wana matatizo yao na haya ya mwanachama wa CDM hayawahusu.

Amandla...
Soma hilo T-shirt kabla ya kukometi
 

Attachments

  • Screenshot_20260708-105028.png
    Screenshot_20260708-105028.png
    1.3 MB · Views: 10
Waliokuwa G55 walikuwa wanachama wa Chadema. Kuvaa t shirt hiyo hakuna maana zaidi ya kuwa alikuwa anawaunga mkono. Kuwaunga kwake mkono hakumaanishi kuwa aliunga mkono uamuzi wa baadhi yao kujiunga na Chaumma.

Amandla...
 
Kwa faida ya watanzania wote hasa hasa wapenda siasa za mageuzi
Tangu lini Mchome akawa ni kiongozi CHADEMA ?
Huyu sio mwanachama... Alishirikiana na Ofisi ya Msajili kusema Katibu Mkuu Mnyika hakuchaguliwa kihalali..

Msajili akamzuia Katibu mkuu, bahati nzuri Mahakama ikaona ni ulimbukeni

Sasa Leo kapewa Hela ndio umuamini huyu limbukeni ?
 
Pia nasikia Heche kakimbilia Ubelgiji na pia twaomba ufafanuzi kwa hili.kwanini akimbilie ubelgiji na je anaenda huko kufanya nini?
Yule aliyeenda kumtembelea mjane leo siyo heche kumbe
 
Kama ni hivyo ni rahisi kusema ngapi zimekusanywa na zimetumika vipi. Aidha, kinachokaguliwa ni kilichoingizwa kwenye akaunti, sio fedha taslimu zilizokusanywa kwenye mikutano n.k.

Heche, hata Lissu hawawezi kukiuza chama kwa mtu yeyote. Kinachotakiwa hapa ni uadilifu na si kinginepo. Kama hamna ubadhirifu (au harufu yake) uliotokea, chama kiseme hivyo. Wakifanya hivyo watakuwa wamemsafisha Heche na kuonyesha kuwa ni chama ambacho hakiogopi kukoselewa.

Amandla...
Kuna utaratibu wa ripoti za mahesabu hata kwenye kikoba huwezi kusonewa TU

Isitoshe Kila mkoa walikuwa WANASOMA jumla
 
Back
Top Bottom