CHADEMA kuna tatizo kama ni kweli

CHADEMA kuna tatizo kama ni kweli

Kumekuwa na shutuma nyingi sana juu ya uongozi wa juu wa chama.

Shutuma za ubadhilifu wa rasilimali fedha ndani ya chama.

Huu ni ushuhuda kutoka kwa mmoja wa viongozi wa chama mkoa wa Kilimanjaro.

Tujadili wana Jf

View attachment 3624857

---------------

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Mwanga, Mkoani Kilimanjaro Lembrus Mchome ametoa tuhuma dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, John Heche, akidai kuwa amekuwa akikusanya fedha kutoka kwa wadau, wafanyabiashara na mashirika mbalimbali kwaajili ya shughuli za chama lakini fedha hizo hazijafikishwa kwenye mifuko rasmi ya chama.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mchome amedai kuwa suala hilo lilijadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na kusababisha mvutano miongoni mwa viongozi, akimpongeza Godbless Lema kwa kile alichodai kuwa ni alisimama kidete kutaka fedha hizo ziwekwe wazi na kuwajibishwa kwa waliohusika.

"Tumekuwa na Makamu Mwenyekiti ambaye amekuwa akichukua fedha kutoka kwa wadau mbalimbali lakini zimekuwa hazifiki ndani ya chama. Ndio maana juzi kwenye Kamati Kuu wamegombana. Nimpongeze sana Godbless Lema kwani alisimama kidete kutaka fedha hizi zirudi, lakini haikuwezekana kwani Makamu Mwenyekiti alidai kuwa ameshazitumia na nyingine amenununulia vyombo vya muziki vya chama," alisema Mchome.

Mchome amebainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliowasiliana na Uongozi wa Chadema kupitia Kamati kuu iliyoketi Mkoani Kigoma walithibitisha kuwa walitoa michango kwa Heche kwaajili ya kukisaidia chama. Pia alidai Heche alisafiri hadi Afrika Kusini kwa lengo la kupokea fedha kutoka kwa wadau, akitoa rai ya wanachadema kumshinikiza Heche kujiondoa kwenye uongozi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo.

"Sasa niwaombe wanachama wa Chadema tushikamane kumtaka John Heche atupishe kwanza kwaajili ya uchunguzi. Chama hiki kinaamini katika misingi ya haki na kupinga ufisadi, kwa hiyo kwanini leo tumfumbie macho Heche?" alisema Mchome.

Katika hatua nyingine Mchome amemtuhumu Heche kunufaika kisiasa na hali ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu kuwa gerezani, akisema amekuwa akijijenga kisiasa pamoja na kutumia mwanya huo kuweza kufanya ubadhirifu kwa


Chanzo: Michuzi TV
Tukisema 'kafika bei', tutakuwa tunakosea?

Kwa nini huyu amwage mtama hadharani kwa mambo yao ya ndani?

Mambo ya Lissu kugoma kununulika ili kukiuza chama kwa maridhiano haramu, yeye kayajuaje?

Kumbe bado kuna mamluki wengi sana Cdm!
 
Tukisema 'kafika bei', tutakuwa tunakosea?

Kwa nini huyu amwage mtama hadharani kwa mambo yao ya ndani?

Mambo ya Lissu kugoma kununulika ili kukiuza chama kwa maridhiano haramu, yeye kayajuaje?

Kumbe bado kuna mamluki wengi sana Cdm!
Yote yanawezekana mkuu
 
Mnatumika kijinga kweli kweli.

Kwahiyo Heche alienda SA kuchukua/kubeba hela kwenye sandarusi au shangazi kaja? Ina maana chama hakina banki akaunti au yeye Heche hana akaunti ya banki?

Kama hao 'Wafanyabiashara' walimpa Heche hela, halafu hakuzifikisha chamani, unawezaje kuthibitisha hilo??
 
Chadema ina maadui wawili ambao inatakiwa kujidhatiti kukabiliana nao kuwashinda.

1. Mbowe na minions wake ambao alikuwa anagawana nao maokoto. Hawa hawajakubali kabisa kuwa chadema sio chama chao binafsi bali ni taasisi ya kijamii ambayo inahudumia jamii na sio kikundi cha wala rushwa na wapenda pesa za bure kilichokuwa hosted na kulelewa na macho manne a.k.a Mbowe.

2. CCM hawa ni wazi kuwa ni adui namba moja wa chadema ya sasa kwasababu kwanza chadema imebadili mfumo wa zamani wa ubadhirifu na uongozi wa undumila kuwili uliokuwa unaigiza uzalendo kumbe jioni wanagonga glass na vigogo hao hao na kugawana posho za udhalimu wao.

Kila siku ccm wanajaribu ku infiltrate ndani ya CHADEMA ili kuleta migogoro na kuharibu utaratibu wa ndani. Hii si sawa nyakati hizi za kujenga siasa safi ya kuimalisha democratic leadership.

Kama CHADEMA wanafanya uhujumu then utaratibu ni simple,fanya inquiry for financial reports and records halafu uje hapa utuonyeshe mapato na matumizi ya CHADEMA plus utuonyeshe hayo magepu ya wizi wa pesa yapo wapo na ututajie majina ya wadokozi ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Kwa taarifa yako tu, vyama vya siasa huwa navyo vinapewa hati safi au chafu za mahesabu baada ya ukaguzi.

Je ,wewe unaweza kutuletea ushahidi wa hati chafu yenye ushahidi wa ubadhirifu ndani ya CHADEMA?

If so then you have every right kuwashambulia viongozi waliochezea pesa.

Kwaiyo Adui namba 1 ninani 👈

sasa mana umeweka Mzee mbowe na CCM wote namba 1 sawa ??
 
Mana umbeya umeniponyoka kidogo nimeshindwa kupiga
kinyaa🤣🤣🤣
 
Kumekuwa na shutuma nyingi sana juu ya uongozi wa juu wa chama.

Shutuma za ubadhilifu wa rasilimali fedha ndani ya chama.

Huu ni ushuhuda kutoka kwa mmoja wa viongozi wa chama mkoa wa Kilimanjaro.

Tujadili wana Jf

View attachment 3624857

---------------

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Mwanga, Mkoani Kilimanjaro Lembrus Mchome ametoa tuhuma dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, John Heche, akidai kuwa amekuwa akikusanya fedha kutoka kwa wadau, wafanyabiashara na mashirika mbalimbali kwaajili ya shughuli za chama lakini fedha hizo hazijafikishwa kwenye mifuko rasmi ya chama.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mchome amedai kuwa suala hilo lilijadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na kusababisha mvutano miongoni mwa viongozi, akimpongeza Godbless Lema kwa kile alichodai kuwa ni alisimama kidete kutaka fedha hizo ziwekwe wazi na kuwajibishwa kwa waliohusika.

"Tumekuwa na Makamu Mwenyekiti ambaye amekuwa akichukua fedha kutoka kwa wadau mbalimbali lakini zimekuwa hazifiki ndani ya chama. Ndio maana juzi kwenye Kamati Kuu wamegombana. Nimpongeze sana Godbless Lema kwani alisimama kidete kutaka fedha hizi zirudi, lakini haikuwezekana kwani Makamu Mwenyekiti alidai kuwa ameshazitumia na nyingine amenununulia vyombo vya muziki vya chama," alisema Mchome.

Mchome amebainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliowasiliana na Uongozi wa Chadema kupitia Kamati kuu iliyoketi Mkoani Kigoma walithibitisha kuwa walitoa michango kwa Heche kwaajili ya kukisaidia chama. Pia alidai Heche alisafiri hadi Afrika Kusini kwa lengo la kupokea fedha kutoka kwa wadau, akitoa rai ya wanachadema kumshinikiza Heche kujiondoa kwenye uongozi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo.

"Sasa niwaombe wanachama wa Chadema tushikamane kumtaka John Heche atupishe kwanza kwaajili ya uchunguzi. Chama hiki kinaamini katika misingi ya haki na kupinga ufisadi, kwa hiyo kwanini leo tumfumbie macho Heche?" alisema Mchome.

Katika hatua nyingine Mchome amemtuhumu Heche kunufaika kisiasa na hali ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu kuwa gerezani, akisema amekuwa akijijenga kisiasa pamoja na kutumia mwanya huo kuweza kufanya ubadhirifu kwa


Chanzo: Michuzi TV

Huyu si alifukuzwa kitambo sana tangu apangishiwe chumba na msajili? Amekuwaje tena kiongozi? Uhawara na mutungi uliisha kwani kawa huru apate bwana mpya? Hata biblia ilisema huwezi kuwatumikia mabwana wawili wakuu...
 
Majeraha ya uchaguzi wa ndani yamegoma kupona!😁

Katika mazingira tuliyopo,ni shirika/mfanyabiashara gani ana ubavu wa kuipa pesa CDM?

Si atazongwa na kesi za kutakatisha fedha!
 
Si kweli wala hakuna ukweli. Nyumba ya jirani imeungua tayari, maridhiano hayatakuwepo wanatapatapa.
 
Thread nyingine hazina kichwa wala miguu, inakuwaje tunajadili thread ya mtu aliyekwishatimuliwa chadema halafu gafla leo anaibuka kusema kana kwamba yeye bado ni kiongozi ndani ya chadema...kwa akili ya kawaida, hauoni kuna jambo ovu dhidi ya chadema na hasa uongozi huu wa sasa linapikwa hapo??
 
Kumekuwa na shutuma nyingi sana juu ya uongozi wa juu wa chama.

Shutuma za ubadhilifu wa rasilimali fedha ndani ya chama.

Huu ni ushuhuda kutoka kwa mmoja wa viongozi wa chama mkoa wa Kilimanjaro.

Tujadili wana Jf

View attachment 3624857

---------------

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Mwanga, Mkoani Kilimanjaro Lembrus Mchome ametoa tuhuma dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, John Heche, akidai kuwa amekuwa akikusanya fedha kutoka kwa wadau, wafanyabiashara na mashirika mbalimbali kwaajili ya shughuli za chama lakini fedha hizo hazijafikishwa kwenye mifuko rasmi ya chama.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mchome amedai kuwa suala hilo lilijadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na kusababisha mvutano miongoni mwa viongozi, akimpongeza Godbless Lema kwa kile alichodai kuwa ni alisimama kidete kutaka fedha hizo ziwekwe wazi na kuwajibishwa kwa waliohusika.

"Tumekuwa na Makamu Mwenyekiti ambaye amekuwa akichukua fedha kutoka kwa wadau mbalimbali lakini zimekuwa hazifiki ndani ya chama. Ndio maana juzi kwenye Kamati Kuu wamegombana. Nimpongeze sana Godbless Lema kwani alisimama kidete kutaka fedha hizi zirudi, lakini haikuwezekana kwani Makamu Mwenyekiti alidai kuwa ameshazitumia na nyingine amenununulia vyombo vya muziki vya chama," alisema Mchome.

Mchome amebainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliowasiliana na Uongozi wa Chadema kupitia Kamati kuu iliyoketi Mkoani Kigoma walithibitisha kuwa walitoa michango kwa Heche kwaajili ya kukisaidia chama. Pia alidai Heche alisafiri hadi Afrika Kusini kwa lengo la kupokea fedha kutoka kwa wadau, akitoa rai ya wanachadema kumshinikiza Heche kujiondoa kwenye uongozi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo.

"Sasa niwaombe wanachama wa Chadema tushikamane kumtaka John Heche atupishe kwanza kwaajili ya uchunguzi. Chama hiki kinaamini katika misingi ya haki na kupinga ufisadi, kwa hiyo kwanini leo tumfumbie macho Heche?" alisema Mchome.

Katika hatua nyingine Mchome amemtuhumu Heche kunufaika kisiasa na hali ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu kuwa gerezani, akisema amekuwa akijijenga kisiasa pamoja na kutumia mwanya huo kuweza kufanya ubadhirifu kwa


Chanzo: Michuzi TV
Ya lini hayo, kwani huyu ni mwana chadema bado, upuuzi tu.
 
Mtoa mara katika Moja na mbili

Uzuri JF never forgets
Amesema kipi kibaya? Hajasema amejitoa Chadema bali ametoa tahadhari kwa viongozi wa sasa wa chama chake wawe makini na yanayo endelea. Hiyo nayo imekuwa dhambi?

Sana sana kinachoonekana hapa ni kuwa sio mnafik na yuko tayari kutoa ushauri mchungu kwa chama chake.

Amandla...
 
Amesema kipi kibaya? Hajasema amejitoa Chadema bali ametoa tahadhari kwa viongozi wa sasa wa chama chake wawe makini na yanayo endelea. Hiyo nayo imekuwa dhambi?

Sana sana kinachoonekana hapa ni kuwa sio mnafik na yuko tayari kutoa ushauri mchungu kwa chama chake.

Amandla...

Tangu mwanzo ameonesha yupo Kinyume na Uongozi huu. Sio mtu mwema Kwa CHADEMA. Post zake kadhaa amekuwa akiwatukana Viongozi wa sasa wa CHADEMA.

Huwezi kuwa unatukana Viongozi Kisha ukasema upo nao pamoja. Yupo kwenye rekodi akitaka Lissu afungwe maisha. Je, huyu Mmawia anaitakia mema CHADEMA?
 
Tangu mwanzo ameonesha yupo Kinyume na Uongozi huu. Sio mtu mwema Kwa CHADEMA. Post zake kadhaa amekuwa akiwatukana Viongozi wa sasa wa CHADEMA.
Kwani kipimo cha kuwa mwema kwa Chadema ni kukubaliana na uongozi uliopo? Ingekuwa hivyo basi wakina Lissu, Lema na wengine hawana sifa za kuwa wana Chadema kwa sababu walionyesha wazi kuwa hawaendani na uongozi uliopita.þ
Huwezi kuwa unatukana Viongozi Kisha ukasema upo nao pamoja. Yupo kwenye rekodi akitaka Lissu afungwe maisha. Je, huyu Mmawia anaitakia mema CHADEMA?
Inategemea tafsiri ya tusi. Msiwe kama CCM ambapo kila ukosoaji wa uongozi unaitwa tusi.
Alisema Lissu afungwe maisha kwa kosa gani?
Hilo la kuitakia mema CDM ya sasa siwezi kujibu maana mimi sio Mmawia. Lakini inawezekana kabisa kuwa anaikosoa CDM kwa sababu anaitakia mema. Chadema haihitaji machawa.

Amandla....
 


Hapa ndio utamsoma vizuri mtoa mada
Namjua vizuri sana huyu Mmawia si tu kwa hii nickname yake bali kwa jina lake halisi, anapoishi, shughuli yake na role yake ndani ya CHADEMA

Huyu ni TEAM FREEMAN MBOWE 100% na mpaka sasa hawaamini kuwa walishindwa kwenye uchaguzi wa 21/1/2025

Ni wazi kuwa harakati za kisheria kupitia mahakama kwa usaidizi wa serikali haramu chini ya Samia Suluhu Hassan na CCM yake kuifanya CHADEMA a toothless dog zimeshagonga mwamba. Sasa wanajaribu kuisambaratisha from outside kwenda inside...

Hii kizungu inaitwa Sabotage. Wanafikiri wanaweza kuu - sabotage uongozi wa Mwenyekiti Tundu Lissu na hivyo kukirudisha chama mikononi mwao ili waanze kupiga hela toka kwa watawala waovu...

Tundu Lissu, John Heche na John Mnyika wameshategeshewa mabilioni ya shilingi ili wasalitiane. Tundu Lissu awasaliti wenzake na John Mnyika na Heche wamsaliti Mwenyekiti wao, IMESHINDIKANA...!!

Kiongozi wa kizazi hiki kilichojaa tamaa na ulafi wa pesa kukataa pesa chafu za damu nyingi kiasi hicho ambazo angekula miaka na miaka na familia yake, ni kiongozi muhimu na anayestahili Kulindwa sana na ofcoz hawa tayari wako chini ya ulinzi dhabiti wa Mungu Yehova mwenyewe..!
Kiongozi kwanza Nashukuru sana kwa kufuatilia Mada yangu.

Pili nikujulishe tu kuwa mimi ni Kati ya waasisi wa CDM,kubakia kataa.

Binafsi sina tatizo na uongozi wa CHADEMA kabisa.
Nikichokifanya ni kuweka Hilo bandiko kwa Umma ili kama Kuna Hilo tatizo liwe hadharani ili lijulikane na kwa kufanya hivyo wale watuhumiwa watarudi nyuma kwa kuogopa nguvu ya Umma.

By the way nimekubaliana na ulivyo nihukumu kiongozi ila sipo huko ulipo nipangiq kwa mtazamo wako.
Sawa Mmawia..

Na pole sana kwa fimbo hizi. Mwana mpotevu na aliyekengeuka lazima apate kibano kidogo ili kumrejesha katika mstari...

Na honestly, mnafanya mambo yenu kienyeji sana...

Mnafanya makusudi ku - sabotage mapambano dhidi ya dhuluma, uonevu na mauaji yanayofanywa na watawala dhalimu wasio na ridhaa ya wananchi kuongoza nchi na taifa hili...

Deep ndani kabisa toka ktk moyo wako, Heche huyu anayewindwa na watawala ktk kila hatua ili auwawe na ikishindikana la kumuua ingalau abambikiwe kesi mbaya isiyo na dhamana anaweza vipi kufanya kosa la kijinga hivi kujichafua ili nyie wahuni mpate sababu ya kumshitaki? Ona tu, juzi wamemuua dereva wake masikini. Lakini Ukweli, aliyekuwa anatafutwa ni yeye..!!

Mimi Mtumishi wa Yesu Kristo aliye hai, ninawashauri tafuteni njia nyingine halali za kujipatia pesa za kutunza familia zetu na mahitaji ya starehe zenu binafsi..

Kukubali kupokea pesa za damu kutoka kwa watawala hayawani wa serikali hii dhalimu na haramu walioua maelfu ya ndugu zetu ni kujichumia laana, mabalaa na mikosi isiyo na sababu kabisa bali kwa kujitakia kwa sbb ya tamaa zenu..
 
Back
Top Bottom