CHADEMA kuchukua nchi ni baadae sana

CHADEMA kuchukua nchi ni baadae sana

SABABU ZA CHADEMA KUSHIKA DOLA -2015

na Mwandishi wako:Technician


CHADEMA
Ina nafasi ya kushinda uchaguzi 2015, ninayasema
haya baada ya kufanya utafiti wangu
mdogo kuhusu mlolongo wa chaguzi mbalimbali zilizopita
tangu kuanza kwa chaguzi za vyama vyingi hapa Tanzania.
Kinachohitajika hapa ni Msukumo kidogo tu kwenye ELIMU ya
URAIA Na Ushawishi wa kushiriki kupiga Kura.

Mwaka 1995 waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 8,929,969
na waliojitokeza kupiga kura ni watu 6,846,681 sawa na 76.7%
ya watu wote waliojiandikisha.CCM ilishinda kwa kupata kura
4,026,422 sawa na 61.82%.Watu 2,083,288 sawa na 23.3%
Hawakupiga kura.

Mwaka 2000 waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 10,088,484
na waliojitokeza kupiga kura ni watu 8,517,598 sawa na 84.4%.
CCM Ilishinda kwa kura 5,863,201 sawa na 71.74%.Watu 1,570,886
Sawa na 15.6% hawakupiga kura.
Mwaka 2005 waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 16,401,694
na waliojitokeza kupiga kura ni watu 11,875,927 sawa na 72.4%.
CCM Ilishinda kwa kura 9,123,952 sawa na 80.28%.Watu 4,525,767
Sawa na 27.6% Hawakupiga kura.

Mwaka 2010 waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 20,137,303
na waliojitokeza kupiga kura ni watu 8,626,283 sawa na 42.83%.
CCM Ilishinda kwa kura 5,276,827 sawa na 62.8%.Watu 11,511,020
Sawa na 57.17% Hawakupiga kura.

Kimsingi Rais wa Tanzania alichaguliwa na watu 5,276,827
kati ya watu 20,137,303 waliojiandikisha kupiga kura sawa na 26.2%.
Kuna kundi la watu wasiopungua 14,860,476 sawa na 73% ambao
hawakumchagua mgombea wa CCM na ni miongoni mwa waliojiandikisha
kupiga kura,na hawakupiga kura kwasababu mbalimbali.

JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI
Jumla ya wananchi waliojiandikisha kupiga kura jimboni Arumeru mashariki
mwaka 2010 ni zaidi ya 127,000,waliojitokeza walikuwa wananchi 55,698
sawa na 43.86%,Mgombea wa CCM alishinda kwa kupata kura 34,661 sawa
na 62.23% ya waliojitokeza kupiga kura naKuna idadi ya wapiga kura kama
71,302 sawa na 56.14% ambao hawakujitokeza kupiga kura.Mgombea wa
CHADEMA alipata kura 19,123 sawa na 34.33% ya kura za waliojitokeza
kupiga kura.Uamuzi wa nani awakilishe jimbo la Arumeru mashariki uko
kwenye hili kundi la watu 71,302(56.14% ya waliojiandikisha kupiga kura
Arumeru Mashariki).

Wasiliana na mimi kwa:Technician@jamiiforum.com




 
Rejea moja ya thread ya zamani ya Ndugu yetu M.M Mwanakijiji yenye kichwa cha habari kinachosomeka "the triangle of political success" utapata majibu!
 
Pamoja na utafiti wako mkuu, bila tume huru ya uchaguzi hakuna litakalowezekana kuifanya ccm iachie dola. Kuna hatari kwenye katiba mpya ccm wakafanya juu chini ili utaratibu wa kupata tume ya uchaguzi uwe ni wa kuwanufaisha wao na kuwasaidia wasiondoke madarakani kwa aibu.
 
Wanabodi,

Baada ya ushindi wa tsunami huko Arumeru, jee hii ndio dalili ya "the wind of change is sweeping across Tanzania kiasi kwamba 2015 Chadema kuchukua nchi?!.

Nawashauri wale wabunge wa maeneo yenye changanoto ama wajiunge Chadema sasa ili kuyatetea majimbo yao, au wajiandae kuanguka na CCM yao!.

Ushindi huu wa Arumeru anawaweka wanasiasa ambao vuguvugu ambao sio moto wala sio baridi kuchagua upande rasmi au moto wa Chadema au baridi ya CCM!.

Mwaka huu pia kunauwezekano wa kufanyika chaguzi nyingine ndogo 2 kanda hiyo ya Kaskazini hivyo kulikomboa karibu kanda nzima!.

Ushauri kwa Ole Sendeka, Ole Medeye na wabunge wengine wa kanda hiyo, don't wait too long to take sides, after all kwenye politics hakuna permanent friends or permanent enemies, there is only common interest!. The time its now or never!.

Chadema kazi ya grooming makamanda watakaoshika majimbo ianze mapema, this time sio kusubiri CCM tena bali huko huko kwenye majimbo yanayoshikiliwa na CCM, pelekeni makamanda kuanzisha mchaka mchaka wa kuipekeka CCM puta ikose pa kupumulia na pa kutokea just ijifie kwa suffocation!.

Nawasilisha.

Pasco.

NB. Ukumbi wa jf ambao ulikuwa ment kwa ma great thinkers wenye great mind wanao duscuss ideas umegubikwa na low thinkers wenye simple minds ambao kazi yao ni kudiscuss people!.

Ukishasoma thread hii kama hujaona any idea ya kuchangia nakushauri usichangie!. Ukijiona huna na kuchangia kwenye hoja iliyoko mezani au mchango wako unataka kuchangia kumhusu mleta hoja Pasco badala ya kuchangia hoja yake, nakushauri bora jinyamazie tuu, tunataka michango ya great mind to discuss ideas not simple minds ambao kutwa kucha wanajadili watu!.

Pasco.
 
Ushauri kwa Ole Sendeka, Ole Medeye na wabunge wengine wa kanda hiyo, don't wait too long to take sides, after all kwenye politics hakuna permanent friends or permanent enemies, there is only common interest!. The time its now or never!.
Hata wewe pokea ushauri wako huohuo...kibaraka mkubwa wa CCM...!
 
unavyoona Lowasa bado atakuwa na pumzi ya kusimama 2015?
 
Mtaarifu kabisa Lowasa asijisumbue kutumbua mafao yake atadondokea pua kama alivyo lizwa huko kwa mkwewe
Mwache kwanza mzee apumzike machungu ya mkwe kukosa ubunge pamoja na jitihada zake zote za hali na mali za kumsaidia.
 
Pasco CCM 2015 ina hali mbaya sana. Kwa nini?

1.0 Vijana wengi hawajiandikisha kwa sababu hawakujua kuwa CDM ingekuwa mtetezi wao na wanajutia sana hilo. Hivyo 2015 vijana wengi watajiandikisha na hao ndiyo watakaoizika CCM.

2.0 CCM na ndoto za tume ya uchaguzi. CCM imekuwa kama muumini anaamini katika Mungu kuwa kila jambo linawezekana. Sasa CCM imekuwa ikiamini kuwa NEC itaibeba kwenye chaguzi wakisaidiwa na watu wa TISS!!!! Huwezi amini mpaka jana kuna baadhi ya watu wa system walikuwa wana imani ya kuchakachua kupitia techinique ambazo ni zilipendwa!!!!! Ni imani hiyo inayoifanya CCM isiwajibike kwa wananchi na kushindwa kujibu hoja ikijua itapita pasipo kupingwa.

3.0 Uelewa wa wada zote za watu umebadilika. Hata akina mama, wazee wameanza kuyaona machungu ya maisha ambayo hawajawahi kujaona. Katika hilo CDM wanawaaminisha watu mchawi ni CCM!!!! Imani hii imepata mapokeo chanya na sumu yake inatambaa mbaya kabisa.

4.0 Fashion. Katika siku za hivi karibuni imekuwa kama fashion kuwa chama cha upinzani hasa kwa vijana.

Anyway kila kitu kina huzaliwa, kukua na kufa. CCM saizi imezeeka na hivyo inajingoja taratibu kaburini.
 
Pasco,

Ushauri mzuri sana huu.Sasa hivi wabunge wa CCM wanaishi kwa wasiwasi mno na wanatamani 2015 isifike

Chadema tunaendelea kubadili fan base iwe loyal base.Uchaguzi wa Arumeru umekuwa pigo kubwa kwa Lowassana kundi lake.Najua baadhi ya makada wa CCM wanachekelea.

Najua uchaguzi mwingine mdogo makada wa CCM watasukumana nani aende.Wasianze kunyoosheana vidole tu sasa
 
Wanabodi,

Baada ya ushindi wa tsunami huko Arumeru, jee hii ndio dalili ya "the wind of change is sweeping across Tanzania kiasi kwamba 2015 Chadema kuchukua nchi?!.

Nawashauri wale wabunge wa maeneo yenye changanoto ama wajiunge Chadema sasa ili kuyatetea majimbo yao, au wajiandae kuanguka na CCM yao!.

Ushindi huu wa Arumeru anawaweka wanasiasa ambao vuguvugu ambao sio moto wala sio baridi kuchagua upande rasmi au moto wa Chadema au baridi ya CCM!.

Mwaka huu pia kunauwezekano wa kufanyika chaguzi nyingine ndogo 2 kanda hiyo ya Kaskazini hivyo kulikomboa karibu kanda nzima!.

Ushauri kwa Ole Sendeka, Ole Medeye na wabunge wengine wa kanda hiyo, don't wait too long to take sides, after all kwenye politics hakuna permanent friends or permanent enemies, there is only common interest!. The time its now or never!.

Chadema kazi ya grooming makamanda watakaoshika majimbo ianze mapema, this time sio kusubiri CCM tena bali huko huko kwenye majimbo yanayoshikiliwa na CCM, pelekeni makamanda kuanzisha mchaka mchaka wa kuipekeka CCM puta ikose pa kupumulia na pa kutokea just ijifie kwa suffocation!.

Nawasilisha.

Pasco.

NB. Ukumbi wa jf ambao ulikuwa ment kwa ma great thinkers wenye great mind wanao duscuss ideas umegubikwa na low thinkers wenye simple minds ambao kazi yao ni kudiscuss people!.

Ukishasoma thread hii kama hujaona any idea ya kuchangia nakushauri usichangie!. Ukijiona huna na kuchangia kwenye hoja iliyoko mezani au mchango wako unataka kuchangia kumhusu mleta hoja Pasco badala ya kuchangia hoja yake, nakushauri bora jinyamazie tuu, tunataka michango ya great mind to discuss ideas not simple minds ambao kutwa kucha wanajadili watu!.

Pasco.

Pasco,

Huu ni ushauri mzuri sana. Na jambo kubwa ni kuwatoa wananchi woga. Jinsi CHADEMA itakavyoweza kuhamasisha wananchi kwenye majimbo mengi ndivyo vitisho vya polisi vitapungua kwani hawatakuwa na uwezo wa kupeleka polisi na magari ya kumwaga maji kama walivyofanya Arumeru. Kazi kwa CHADEma sasa ni kumarisha nguvu kanda ya ziwa na kanda ya nyanda za juu. Pia kufanya opresheni maalumu ya kuwainua waliolala kanda ya kati, pwani na kusini.
 
ni pongezi kubwa sana kwa CDM kwa juhudi ya kuifanya nchi hii iendee kwenye uhuru wa kweli. naomba wongeze nguvu katika maeneo fulani ya nchi hasa kusini mwa TZ ili watu watambue vzr CDM wanafanya nn. Hongera sana CDM, wazee wa Makamanda!!!!!
 
....Pasco ni kama jani la mti, ukitaka kuufahamu mueleko wake angalia mwelekeo wa upepo, you should do better than this bro...

...Uchaguzi huu ni pigo kubwa sana kwa CCM-Lowassa,na ni siku ya furaha sio kwa CHADEMA tu bali pia kwa wapinzani wa Lowassa ndani ya CCM, ni dhahiri sasa kuliko ilivyokuwa jana kuwa kumbe Lowassa-Asiyeshindwa ni SImba tu wa kuchorwa asiye na uwezo na ushawishi wowote ata kwenye uwanja wake wa nyumbani-Arusha, leo ingekuwa ni siku ya heri sana kwa Lowassa kama CCM ingelikata jina la Sioni ili wafuasi wake na UVCCM-Arusha wapate hoja ya hasira za wananchi juu ya siasa za majitaka dhidi ya Lowassa ndani ya CCM...

...Lakini pia hii ni onyo kwa CCM kwa ujumla, kuwa muda wa kuwachukulia wananchi for granted umekwisha, jana maeneo ambayo yalikuwa ni ngome za CCM kama Rungwe-Mbeya wameongea, Songea pia wameongea, hii ni wake-up call kwa CCM, ni either chama kifanye mabadiliko seriously au la majuto anaweza akawa ni mjukuu muda mchache ujao...
 
baada ya matokeo ya igunga, baadhi yetu tulitoa verdict ya 2015. kwamba igunga ilikuwa ndio mwanzo wa mwisho wa ccm na uwezekano mkubwa wa opposition (i.e chadema) kushika madaraka.

nilikuwa na wasiwasi sana kuwa ccm wangefanya rafu kubwa arumeru, hususani ukizingatia kuwa tangu day 1 ya kampeni tayari rafu zilianza kuchezwa kupitia mkapa. nilikuwa nime-predict chadema kushinda lakini mgombea wa ccm angetangazwa mshindi kwa mizengwe (rigging).....lakini kumbe nilifanya kosa la kuwa-underrate watu wa arumeru katika ku-prevent rigging, which is commendable na jambo la kuigwa kwenye constituencies zingine zote.

the ccm gang is now heading down the drain, and the pace is not slow!
 
Mtaarifu kabisa Lowasa asijisumbue kutumbua mafao yake atadondokea pua kama alivyo lizwa huko kwa mkwewe
song3.jpg
 
2015 Mbona Mbali. We kaa kitako uone mechi inavyochezwa.. Ukishagundua maficho ya Kunguni huwezi subiri tena.. Ukisema tungojee hadi 2015 kamsemo ka Chukua Chako Mapema watakabadilisha na kuwa Chukua Chako Na Chao Mapema..
Hata Kama CDM haitasimamisha wagombea ila CCM hakuna sehemu itapata hands tena.. Watu watakipa Chama chochote mbali Na CCM.
 
Mwache kwanza mzee apumzike machungu ya mkwe kukosa ubunge pamoja na jitihada zake zote za hali na mali za kumsaidia.
aliporudi toka Ujerumani akase..''NIMERUDI NIKO FITI KWA MAPAMBANO...''

Wanaomjua wakashaurina kumwambia.....''USIENDE ARUMERU AFYA YAKO BADO WATAKUONGEZEA MATATIZO..''

aakfikiria mwisho akaamua kwenda kwani lengo lilikuwa kumsaidia Mkwewe wenye busara wakaliona na kusema

UNAKWENDA KUJIBOMOA ZAIDI ''Dr Slaa aliwahi kisema Uchafu uliona hakuna Maji wala sabuni ya kuutakatisha..''
 
Pasco, with all due respect, I do not believe for a minute you are qualified enough to judge who is a great thinker or a 'low thinker'. Your recent contributions in this forum has been for most part full of errors if not mis-leading. You have taken upon yourself a role of political analyst with cheap spinnning tactics. And for you come here and tell people what they can or cannot say is rather disturbing and worse against the fundemental principles of this forum! So, get real and spare us from this phoney prophesy mkakati.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom