Chadema hawajakiuka maadili?

Shehe wa Msikiti wa Bondeni, Shaaban Juma, alisema familia hiyo haina haja ya kuomba radhi, kwa kuwa alishirikiana nayo kwa hali na mali, lakini akashangazwa alipoambiwa na mmoja wa wanafamilia, aondoke kwenye chumba cha maiti na angempigia simu baadaye, kwa kuwa suala hilo lilikuwa likiihusu familia pekee.

Alisema kamwe hawezi kuiomba radhi familia hiyo wala kutoa msamaha yeye, kwani familia imemkosea Mwenyezi Mungu na si Waislamu, kwa kukiuka misingi na taratibu za dini hiyo na iwapo iliona inazidiwa nguvu, ilipaswa kukabidhi jukumu hilo kwa viongozi wa kiislamu ili walisimamie.

"Mbali na Qur'an na Hadithi za Mtume kukataza, lakini kitendo cha kumpeleka marehemu wa
kiislamu uwanjani pale, ambao uligubikwa mapambio ni kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu na ni moja ya sababu iliyosababisha yeye asihudhurie maziko hayo," alisema Shehe Shaaban.

Juzi Chadema iliendesha ibada maalumu ya kuaga miili ya marehemu wawili waliopoteza maisha katika mapambano baina ya wafuasi wa Chadema na Polisi kutokana na kufanya maandamano yaliyozuiwa kwa kuhofia uvunjifu wa amani ambapo watu watatu walipoteza maisha.

SOURCE: Habari Leo

Watu wanacheza na Mungu
 
Hii yote ni njia serikali kutaka kuonyesha ya kwamba kuna udini. Mungu tunakuomba tunusuru tanzania na hali hii mbaya, hatujui tuendako.
 
Kwa kiasi kikubwa CHADEMA wamefanikisha sana mazishi yale kwa heshima zote. Hivyo ujinga kama huu wa HabariLeo tuliutarajia.
 
If it is a fact kuwa CHADEMA iliishurutisha familia kukiuka taratibu za kidini katika mazishi ya kijana wao! WALIKOSEA SANA! Tujifunze kukubali makosa!
 
Katika harakati za kushugulikia mazishi ya alieuliwa Arusha, Chadema kimetumia mabavu na vitisho kwa familia ya marehemu ili maiti hiyo ipelekwe ktk maonyesho na maombelezo huko uwanjani NMC Arusha, kinyume na matakwa ya familia ya marehemu!

Hii habari imekaaje? soma hapa: HabariLeo | Chadema kwenye kashfa ya maiti

Kadogoo bado unasoma magazeti ya chama cha CCM? What do you expect? that is total Craaap! Neeext?
 
Katika harakati za kushugulikia mazishi ya alieuliwa Arusha, Chadema kimetumia mabavu na vitisho kwa familia ya marehemu ili maiti hiyo ipelekwe ktk maonyesho na maombelezo huko uwanjani NMC Arusha, kinyume na matakwa ya familia ya marehemu!

Hii habari imekaaje? soma hapa: HabariLeo | Chadema kwenye kashfa ya maiti
Hakuna cha kujadili kwani chanzo cha habari ya hayo magazeti inajulikana kwani ndugu yake gazeti lingine la Uhuru pia ameandika hivyoivyo so wanatumika kupotosha jamii.
 
Wana JF

Katika Nchi yetu Tumepata Msiba, Msiba katika Jamii ya Kiafrika tunaomboleza ili kuonyesha mshikamano na hisia zetu juu ya mambo yaliyotokea na ni muda muafaka wa kujifunza.

Arusha yametokea yaliyotokea, Lakini Cha kushanganza Mkuu wa Kaya kakaa kimya kana kwamba hao walokufa sio watanzania, Sasa anaanza kuwatumia waandishi wa magazeti kuwasilisha hisia Zake. JK Jitokeze hadhara na utueleze WaTZ umeguswa vipi na janga hilo la Arusha.

JK uongozi sio kukaa kimya, au Nchi haina Kiongozi, Iga angalau Mifano ya Viongozi wenzio, angalizo, uhai wa Raia mmoja wa TZ unathamani kubwa sana lakini JK hilo halioni na wala haoni umuhimu wa kutoa kauli yake itakuwa na maana zaidi kwa sasa kuliko kukaa kimya na kutoa nafasi kwa Mapolisi kuanza kuchanganya habari, na Kunyoosheana Vidole.

Nashauri JK atoe kauli na Hisia zake Juu ya yaliyotokea Arusha Otherwise The Leadership in ou Country is at stake
 
Wakuu hebu someni hiyo habari hapo chini kutoka huko huko habari leo utaona jinsi walivyokuwa wanataka ku-invent kitu ambacho hata hakikuwepo. Yaani ni ushabiki mtupu.

Cha ajabu hata polisi wenyewe hawajamshtaki Dr. Slaa kwa makosa ambayo habari leo walitaka wananchi wayaamini!


ARUSHA KWALIPUKA

Imeandikwa na John Mhala, Arusha; Tarehe: 5th January 2011

Source: Hapa

WABUNGE wanne wa Chadema wamesekwa rumande katika kituo kikuu cha Polisi mjini hapa baada ya kukaidi amri ya Polisi ya kuacha maandamano.

Mbali ya wabunge hao kutiwa ndani pia mke wa Katibu Mkuu wa Chadema Willibrod Slaa, Josephine Mushumbusi, naye amekamatwa na kutiwa ndani huku akiwa na majeraha ya kupigwa na polisi.

Pia wafuasi watatu wa chama hicho walijeruhiwa kwa risasi za moto na polisi waliokuwa wakidhibiti maandamano ya wafuasi hao.

Kabla ya matukio hayo, tangu jana asubuhi hadi mchana ulinzi wa polisi uliimarishwa karibu kila kona za Jiji, lakini wafuasi wa Chadema walikaidi amri ya Mkuu wa Polisi, IGP Said Mwema ya kutofanya maandamano.

Badala yake, wafuasi hao walitii mwito wa Dk. Slaa aliyetangaza kupitia vyombo vya habari kuwa wataandamana licha ya amri halali ya Jeshi la Polisi ya kutoandamana.

Wafuasi hao ambao wote walikuwa na vitambaa vyeupe kichwani na vingine vikubwa vilivyoandikwa ujumbe, mabango na wengine wakiimba nyimbo za kumtukuza Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, waliandamana wakielekea uwanja wa NMC.

Katika hoteli ya kitalii ya Mount Meru ambako ndiko viongozi wa juu wa Chadema walikofikia, polisi walilazimika kutumia maji ya kuwasha kutawanya wafuasi hao.

Mbali ya hilo katika Kata ya Sombetini, wafuasi hao waliokuwa na vitambaa vilivyosomeka ‘Meya wa Jiji la Arusha wa CCM ni wa kuchongwa’, mengine yakisomeka: 'Tunataka uchaguzi wa Meya urudiwe’, walitawanywa kwa nguvu.

Hata hivyo polisi, mgambo na askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) walidhibiti kwa asilimia kubwa maandamano hayo licha ya kwamba wengine waliandamana kwa magari yenye bendera za chama hicho ili kuchelea kibano.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobis Andengenye, alipoulizwa kwa njia ya simu kama ana taarifa juu ya matukio hayo, alijibu kwa kifupi kuwa yuko kwenye kikao hivyo hawezi kutoa maelezo hadi baadaye.

Hata hivyo, katika mkutano wa hadhara ambao Slaa alianza kuhutubia saa 6 mchana, aliwataja kwa majina wabunge waliokamatwa, kuwa ni pamoja na wa Hai, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Dk. Slaa aliwataja wengine kuwa ni Joseph Selasini wa Rombo, Lucy Owenya wa Viti Maalumu na wa Arusha Mjini Godblles Lema ambao wote wako ndani katika kituo kikuu cha Polisi.

Katibu huyo alisema pia kuwa vijana watatu wa chama hicho walijeruhiwa kwa risasi na waliswekwa rumande walipokwenda kituoni hapo kutaka kuchukua fomu namba tatu ya matibabu - PF3.

Dk. Slaa aliwahamasisha wananchi waliofurika katika mkutano huo kuwa iwapo polisi watagoma kuwaachia huru wabunge, mkewe na vijana waliojeruhiwa, atawaachia wafuasi wa chama hicho mjini hapa, kuamua cha kufanya kwani yeye hatahusika kwa lolote.

“Ninawapa muda polisi kuwaachia viongozi wote wa Chadema walioko ndani na ikishindikana umma wa wakazi wa Arusha utaamua la kufanya na mimi sitahusika na lolote,’’ alisema.

Baadaye amri hiyo ilitolewa na wafuasi hao kuelekea kituo cha Polisi ambako walikumbana na mabomu ya kutoa machozi.

Dk. Slaa alifikia hatua hiyo baada ya kuona hakuna uwezekano wa kuwaachia viongozi hao bila masharti ili warudi kuhutubia wananchi juu ya mustakabali wa kwa nini Jiji la Arusha lina Meya wa CCM.

Baada ya kauli hiyo umati ulielekea katika kituo cha Polisi wakitii amri ya kiongozi wao, lakini ghafla Polisi ilionesha ubavu wake na kumimina mabomu huku mamia ya wafuasi hao wakionesha hofu na kutawanyika hovyo mitaani.

Hali hiyo pia iliwakuta pia waandishi wa habari. Hata hivyo habari zilisema waandishi wanne wanashikiliwa na Polisi kwa kilichoelezwa na Jeshi hilo kuwa ni kushabikia Chadema.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wamesema hatua ya Dk. Slaa kuruhusu wafuasi wake kuvamia kituo cha Polisi ili kuwatoa watuhumiwa ni uchochezi usiovumilika, ambao unaweza kuhatarisha maisha ya watu na amani ya nchi kwa jumla.

Hata hivyo, wengine wameomba suluhu ya kudumu ipatikane ili kuepusha umwagaji damu mkoani humo ambao unachochewa na tofauti za itikadi za kisiasa lakini na uchochezi wa wanasiasa.

Wakati huohuo, katika hali isiyotarajiwa, Diwani wa Sombetini kwa tiketi ya CCM, Alphonce Mawazo, alimkana Rais Jakaya Kikwete mbele ya umati mkubwa wa watu kuwa hakumpigia kura bali alimpigia Dk. Slaa.

Mawazo ambaye aliibuka ghafla kwenye mkutano huo na kulazimishwa kupanda jukwaani, alisema yeye ni mwanamageuzi wa kweli na anaikubali Chadema kwa asilimia kubwa na ndiyo maana katika kura ya urais aliipigia Chadema.

Diwani huyo alisema hayo jukwaani alipokaribishwa na Dk. Slaa na kupewa kipaza sauti na kutamka kuwa yeye ni Chadema ‘damu damu’ ndiyo maana alikuwa hapo kusikiliza mkutano huo na kushukuru kupewa nafasi na kueleza azma yake.

Chadema imekuwa ikidai kupitia kwa Dk. Slaa, kwamba halmashauri za majiji ya Mwanza na Arusha; Hai na Kigoma Ujiji, uchaguzi wa mameya ulivurugwa katika mazingira yanayoashiria kuwapo maelekezo kutoka ngazi za juu.

Hivyo chama hicho kutoa masharti kwamba usifanyike uchaguzi wowote wa mameya au wenyeviti wa halmashauri Mwanza, Kigoma/Ujiji, Arusha na Hai.

Pia Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha ajiuzulu kwa madai ya kukiuka kanuni za halmashauri na kusimamia uchaguzi kinyume na taratibu, vilevile kinalalamika kwamba uongozi wa TAMISEMI uliingilia uchaguzi hasa Kigoma/Ujiji, hivyo wahusika wote wachukuliwe hatua.

Chama hicho pia kinaitaka Serikali imchukulie hatua Ofisa Upelelezi wa Arusha kwa madai ya kuingia na kumkamata mbunge ndani ya kikao halali kinyume na kanuni za uendeshaji wa halmashauri, hivyo kinataka ofisa huyo ajiuzulu au aondolewe.

Chadema pia inadai kuwa polisi ni watuhumiwa katika matukio ya Arusha, hivyo kama hakutakuwa na maridhiano Serikali itakuwa imewalazimisha kuchukua hatua.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha chini ya mwezi, kwa wafuasi wa Chadema kukabiliana na Polisi, mara ya kwanza ikiwa ni Desemba 18 Polisi ilipokabiliana na vurugu zilizoongozwa na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema.

Katika ghasia hizo, Lema alipigwa na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kwa matibabu, kabla ya hapo Polisi ilishatumia maji ya kuwasha na mabomu ya kutoa machozi kutawanya wafuasi hao waliokuwa wamezingira Ofisi ya Manispaa ya Arusha.

Vurugu hizo zilitokana na Chadema kususia uchaguzi wa meya na hivyo CCM na TLP kuendelea nao na kumchagua Diwani wa Olorien, Gaudence Lyimo akisaidiwa na Michael Kivuyo wa TLP, ambaye ni Diwani wa Sokoni.


Lets face the truth! Dr. Slaa una la kusema juu ya tuhuma hizo? damu za hao marehemu umesababisha wewe zimwagike? kama sivyo please respond! kimya chako tangu hili litokee na kutokuwapo kwenye mazishi kuna leta maswali mengi hasa ukisoma those red lines above zinafanana na ukweli. please come out. remmember the body count is now two (2), and the counter is on.
 
Gazeti hilo linakosa mwelekeo na mauzo yao yakishuka sijui watamlalamikia nani! Ukiisoma kwa undani habari yenyewe haiko balanced na zaid inawaachia maswali mengi wasomaji na hivyo kupoteza maana ya habari (information)
 
Ni suala lililo wazi kuwa viongozi wa cdm walitumia msiba wa Watanzania wenzetu kujinufaisha kisiasa.
Kwanza ni cdm waliosababisha vifo vyao, kisha wanatumia miili yao kisiasa kinyume cha matwaka ya wanandugu.
Aibu kubwa iliyoje hii!!!
Nani aliwaambia kuwa siasa zinaendeshwa hivi??
Huu ni uhuni na ulimbukeni wa kisiasa. Hata Jumuia ya Kimataifa inashangazwa na ushenzi huu.
SHAME ON YOU.
 
Jamani hiyo habari si ya kweli nafikiri ni mkono wa ccm kwa kuifua Chadema.Mimi mmoja wapo nilioudhulia mazishi ya huyo kijana na pia niliishi na familia ya marehemu tukiwa majirani kwahiyo mimi nawafahamu vizuri sana hawawezi kutoa tamko hilo pia mimi naishi Usa river sasa na madai yakutolipa si kweli maana pesa za rambirambi zilitolewa na wananchi wengi tu hapa usa river palipatika kiasi kikubwa cha fedha zingeweza kulipia hata kama hilo jeneza lingekuwa linanunuliwa kwa laki tano.Huo ni ucochezi wa dini pia hata mimi ni mwislamu lakini hiyo haipo kwani marehemu alifikishwa nyumbani na kulifanyika taratibu zote za dini na tulimaliza kuzika saa mbili na dakika tano usiku tukiwa na viongozi wa chadema kwa kweli nawapongeza vijana wa chadema katika kupeleka mwili wa marehemu kaburini maana kulikuwa na matope sana lakini hawakujali hilo na kweli mazishi yalifanikiwa kwa asilimia mia.Mpaka vijana wa ccm wengi walijikuta wakiona aibu kuhusu mambo yanaongelewa na viongozi wao wengi wao wamebadilisha msimamo wao wa kukipenda ccm na kubadilika sasa wao ni wanachadema.wadau nitawajuza mengi kuhusu kijana Ismail aka Tumaini.
 
Hivi palestina wale waliokufa kwa kupigwa risasi mbona huwa wanabeba jeneza kwa kuandamana mitaani au wao ni wakristo???
 
Jamani hiyo habari si ya kweli nafikiri ni mkono wa ccm kwa kuifua Chadema.Mimi mmoja wapo nilioudhulia mazishi ya huyo kijana na pia niliishi na familia ya marehemu tukiwa majirani kwahiyo mimi nawafahamu vizuri sana hawawezi kutoa tamko hilo pia mimi naishi Usa river sasa na madai yakutolipa si kweli maana pesa za rambirambi zilitolewa na wananchi wengi tu hapa usa river palipatika kiasi kikubwa cha fedha zingeweza kulipia hata kama hilo jeneza lingekuwa linanunuliwa kwa laki tano.Huo ni ucochezi wa dini pia hata mimi ni mwislamu lakini hiyo haipo kwani marehemu alifikishwa nyumbani na kulifanyika taratibu zote za dini na tulimaliza kuzika saa mbili na dakika tano usiku tukiwa na viongozi wa chadema kwa kweli nawapongeza vijana wa chadema katika kupeleka mwili wa marehemu kaburini maana kulikuwa na matope sana lakini hawakujali hilo na kweli mazishi yalifanikiwa kwa asilimia mia.Mpaka vijana wa ccm wengi walijikuta wakiona aibu kuhusu mambo yanaongelewa na viongozi wao wengi wao wamebadilisha msimamo wao wa kukipenda ccm na kubadilika sasa wao ni wanachadema.wadau nitawajuza mengi kuhusu kijana Ismail aka Tumaini.

thx 4 info.
 
FAMILIA ya marehemu Ismail Omari (25) aliyeuawa katika vurugu za kisiasa zilizotokea Januari 5 mwaka huu mkoani hapa, imedai kushinikizwa na Chadema kumpeleka marehemu wao katika uwanja wa NMC kuagwa kinyume na maamrisho ya dini yao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, baba mzazi wa marehemu huyo Omar Juma,
alisema shinikizo lililowafanya kukubali kitendo hicho lilitolewa juzi usiku baada ya msemaji wa familia yake, Nyerere Kamili, kupokea simu kutoka kwa mmoja wa viongozi wa Chadema; Diwani wa Elerai, John Bayo, kuwa iwapo hawatakubali kupeleka mwili wa ndugu yao kwenye uwanja huo, chama chake kitajitoa kushughulikia mazishi.

Alidai mbali na shinikizo hilo, pia juzi wakiwa chumba cha maiti, katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru, kuchukua mwili huo, walikuta mazingira yasiyo mazuri kwao kugomea kupeleka mwili huo wakihofia kudhuriwa na wafuasi wa Chadema, ambao walikuwa wamefurika eneo hilo wakitaka miili yote ipelekwe uwanjani kuagwa.

Alisema kutokana na sababu hizo, pia alilazimika kuwapigia simu viongozi hao wa Chadema na alikutana nao siku hiyo, wakakubaliana kuupeleka mwili huo uwanjani hapo, ili kupata msaada wa chama hicho wa mazishi kwa kuwa hawana uwezo wa kuendesha mazishi hayo.

“Sasa baada ya sisi kupokea simu hiyo, tulilazimika kuwapigia simu ili kupata msaada, maana vifo vimetokana na mkutano wao, sasa uwezo hatuna na hali ilivyokuwa pale, tungeweza kupigwa hata mawe na wafuasi wao kwa hiyo ilikuwa hivyo,” alisema Omar.

Pia alisema kutokana na shinikizo hilo, liliipa wakati mgumu familia yake baada ya Waislamu kuchukizwa na kitendo hicho hadi kufikia kunyimwa jeneza la kubebea maiti hali iliyowalazimu kuhangaika katika zaidi ya misikiti mitatu bila mafanikio.

Aliongeza kuwa baada ya hali hiyo, alikwenda kuchukua jeneza kwenye msikiti wa hospitali ya Mount Meru akikodi kwa Sh 5,000 ambayo hadi jana walikuwa wakidaiwa kutokana na kushindwa kulipa.

Kwa hali hiyo na kutambua kuukosea Uislamu na Waislamu kwa jumla, aliwaomba viongozi kuisamehe familia yake kwa kuwa haikuwa dhamira yao kufanya hivyo, bali kwa shinikizo la Chadema.

Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Baraza la Wazee wa Chadema wa Mkoa wa Arusha, Haruna Fundikira, alipoulizwa kuhusu suala hilo alikiri na kusema hata yeye aliungana na familia ya marehemu, kuwa suala la kupeleka maiti katika uwanja huo halikuwa sahihi kulingana na maamrisho ya dini.

Alisema walichokubaliana ni kupata japo picha ya marehemu Ismail ili ioneshwe uwanjani hapo, lakini maiti achukuliwe na kupelekwa kwa maziko Usa River, lakini alishangazwa na taarifa kuwa mwili huo ulipelekwa uwanjani hapo.

Alisema siku moja kabla ya maziko, alikwenda kwa familia ya marehemu kupanga mipango ya maziko hayo na walipokubaliana juu ya taratibu hizo, aliahidi kutoa sanda, lakini alilazimika kuahirisha kuitoa, baada ya kuona utaratibu tofauti na aliokubaliana na familia hiyo.

"Mimi jana sikwenda uwanjani hapo, nilikuwa na mgeni nyumbani, lakini nilichosikia ni kwamba walipeleka mwili huo uwanjani tofauti na nilivyokubaliana nao na sikutoa tena sanda, maana walikuwa na uamuzi wao kama familia,” alisema Fundikira.

Aliongeza kuwa, baada ya kuahirisha kutoa sanda, alipokea simu kutoka kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akisema ameshakubaliana na familia kuhusu taratibu zote za maziko na asihangaike kutoa sanda, kwani chama kitatoa.

Shehe wa Msikiti wa Bondeni, Shaaban Juma, alisema familia hiyo haina haja ya kuomba radhi, kwa kuwa alishirikiana nayo kwa hali na mali, lakini akashangazwa alipoambiwa na
mmoja wa wanafamilia, aondoke kwenye chumba cha maiti na angempigia simu baadaye, kwa kuwa suala hilo lilikuwa likiihusu familia pekee.

Alisema kamwe hawezi kuiomba radhi familia hiyo wala kutoa msamaha yeye, kwani familia imemkosea Mwenyezi Mungu na si Waislamu, kwa kukiuka misingi na taratibu za dini hiyo na iwapo iliona inazidiwa nguvu, ilipaswa kukabidhi jukumu hilo kwa viongozi wa kiislamu ili walisimamie.

“Mbali na Qur’an na Hadithi za Mtume kukataza, lakini kitendo cha kumpeleka marehemu wa
kiislamu uwanjani pale, ambao uligubikwa mapambio ni kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu na ni moja ya sababu iliyosababisha yeye asihudhurie maziko hayo,” alisema Shehe Shaaban.

Juzi Chadema iliendesha ibada maalumu ya kuaga miili ya marehemu wawili waliopoteza maisha katika mapambano baina ya wafuasi wa Chadema na Polisi kutokana na kufanya maandamano yaliyozuiwa kwa kuhofia uvunjifu wa amani ambapo watu watatu walipoteza maisha.

Katika hatua nyingine mwili wa marehemu Denis Shirima, nao ulihamishwa kutoka sanduku ambalo lilionekana kuwa duni na kuingizwa katika sanduku la kifahari, ambalo lilinunuliwa na Chadema.

Awali marehemu alikuwa kwenye sanduku la kawaida la rangi nyeupe wakati mwili ukiwa hospitalini tayari kupelekwa kwenye uwanja wa NMC kuuagwa, lakini baadaye ukabadilishiwa kwenye sanduku hilo jipya na la zamani haikujulikana lilikopelekwa.

Source Habari Leo
 
Ni suala lililo wazi kuwa viongozi wa cdm walitumia msiba wa Watanzania wenzetu kujinufaisha kisiasa.
Kwanza ni cdm waliosababisha vifo vyao, kisha wanatumia miili yao kisiasa kinyume cha matwaka ya wanandugu.
Aibu kubwa iliyoje hii!!!
Nani aliwaambia kuwa siasa zinaendeshwa hivi??
Huu ni uhuni na ulimbukeni wa kisiasa. Hata Jumuia ya Kimataifa inashangazwa na ushenzi huu.
SHAME ON YOU.
indeed!
 
Na huyu mzee kahongwa pesa chafu za CCM kama baba wa mzee aliyeuwawa na Ditopile? CCM ni kawaida yao kuuwa na kutoa hongo kwa wazee, penye nuru giza linajitenga, uozo wa CCM uko wazi sana hata wakitumia magazeti na TBC haitoleta tofauti, Watanganyika tuzidishe mapambano tusihamishwe akili zetu na "cheap arguments" za CCM, Mapambano yanaendelea mbele mpaka kieleweke! Makamba, JK muda wa blahblah umekwisha prepare to hand over Tanganyika 2015
 
kwa ujinga wenu mumesabaisha vifo kwa vijana wetu na msiaze kuwapamba kwa kuwaita mashujaa! Kawaiteni mama zenu masjuaaa!
 
Back
Top Bottom