Chadema hawajakiuka maadili?

Chadema hawajakiuka maadili?

167109_175117322524527_135719259797667_317209_3652943_n.jpg
 
Muongo mchungu hii mada yako haina kichwa wala miguu tumekushtukia kua wewe ni mamluki wa chama cha majambazi wa demokrasia!
 
Sijui kama hizo taratibu unazoziongelea ni absolute. Lakini unanishangaza pia kwa maelezo yako yanayojichanganya "Lkn chadema wameuweka mwili wa madhehebu ya kiislam siku 6 sawa na madhehebu mengine jambo ambalo ktk mtazamo wa kiislam sio nadra kutokea labda patokee dharura.jee chadema hawakukiuka maadili?hawakuona haja ya kuuzika mapema?" neno sio nadra maana yake ni ya kawaida. Ukisema isipokuwa kama kuna dharura, ni dharura gani hiyo? Labda ungesema kama kungekuwapo na sababu maalum. Kama ndio ulitaka kusema, ndio sababu maalum iluikuwapo, sio chadema tena bali kwa uchunguzi wa serikali yenyewe. Hakuna anayependa kukaa na mwili wa marehemu kwa muda mrefu bila kuwapo na sababu. Kwa maoni yangu umeshajijibu mwenyewe. Ningeungana nawe ungeuliza iwapo serikali ilifuata utaratibu. Hata hapo sioni jibu sahihi kwani muuaji ana utaratibu wa kwa kufuata utaratibu wa mazishi?
 

Haksante Mzito Kabwe, hili sasa kwa watu wenye hekima na akili(sio Bwn Makamba)liwe fundisho. Wajifunze kuheshimu watu, wasifanye vituko kama vya Kandhahari, wajue watu si wanyama kama nguruwe, hata nguruwe huwezi kuwapiga mpaka watokwe ngeu. Ni bora IGP na RPC washitakiwe waweze kujibu asili ya unyama huu. This is total violation of human rights, tunao wanasheria wetu they can present a very strong case. Nadhani msg imefika kwa mheshimiwa mkuu wa boma.WATU WAMECHOKA MBAYA.
 
View attachment 20160
Usiku wa Septemba 25 mfalme Hussein wa Jordan alifariki na 26 akazikwa kwa kuwa muislam.
Pia mauji ya Pemba watu waliofariki walizikwa siku inayofuata kwa kuwa wote waliofariki ni madhehebu ya kiislam.
Unapokuwa karibu na waumini wa kiislam wanakwambia, kitu cha kwanza kufanyiwa baada ya kukamilika taratibu zote ni kupelekwa mahala pake pa milele yaani kaburini, ndio maana hata viongozi wakuu wa madhehebu hayo mara tu akifa hakai siku nyingi huzikwa
Kwa upande wa madhehebu mengine kama baba wa taifa alikaa muda wa 2 week.
Lkn chadema wameuweka mwili wa madhehebu ya kiislam siku 6 sawa na madhehebu mengine jambo ambalo ktk mtazamo wa kiislam sio nadra kutokea labda patokee dharura.
jee chadema hawakukiuka maadili?hawakuona haja ya kuuzika mapema?
Wewe Mhogo Mchungu bado umelala ebu amka!!!!!!!!! Hujui kwamba kulikuwa na taratibu za kufuata????????????? Hata hivyo umetoa majibu mwenyewe angalia nyekundu hapo juu. Tuliza kichwa kaa sawa!!!!!!!!!
 
Huyu ni fara tuu, hajui analoliandika. Hapa si udini ndugu yangu
 
Muhogo mchungu umekosa cha kuandika??? Mimi nadhani tafakari na chukua hatua acha unafiki wa kichama! Kidini! kiitikadi! Unaonyesha hauna hoja ya msingi bali unataka tu watu wajue na wewe kuwa umo!
 
Natamani nikuone Muhogomchungu nikutandike risasi ya kichwa!
 
Hata mimi naungana na wewe!

sio kuwagombanisha. hoja kuna haja gani chadema kuweka mwili wa marehemu ambae imani yake inakataza kuweka kama sanamu wakati ameshafariki? kwani kwa upande wa dini nyengine hilo la kawaida
 
Chicken IQ!

Bw. Muhogomchungu umeleta hoja ya kipuuzi kabisa. Nyie ni wale mnaotaka kuleta migogoro ya kidini kwenye jamii.

Hii case ya marehemu waliokufa kwenye sakata la mauaji yaliyofanywa na Polisi kwenye maandamano ya Wana-chadema ni a very special case it must be treated differently. Lazima ujue kuwa hata muislamu akiuwawa kwenye hali za utata kama kupigwa risasi,kunyongwa,kunywa sumu na vitu kama hivyo lazima kuna taratibu za Polisi za kufanya postmortem ili kubaini kama marehemu aliuwawa na kitu gani.It can take day,two,three even a week kutegemea na mazingira.

Kwa hiyo kuzika siku hiyo hiyo au kesho yake marehemu tangu afariki is IMMATERIAL!
Kuna matukio ya ajali huwa yanatokea kama kuzama baharini na maiti inatafutwa hata kwa wiki 2 je, hapo wafanyaje na sharia yako ya KUZIKA CHAP CHAP??????????

Acha hizo bana! Crap.


jee hii kwa chadema tu?
 
View attachment 20319

Kawaida ya waumini wa kiislam baada ya mazishi siku ya 3 hufanyika kisomo ili kumuombea dua marehemu.
Kwa kuwa aliokufa kishujaa amezikwa kwa heshima za chama . jee chadema itakuwa na jukukumu la kuandaa dua ya marehemu ambae ametangualia?
kwani Hata Cuf yalipotokea mauji ya wafuasi wao tulishuhudia viongozi wao wakuu wakishiriki kikamilifu katika kisomo hicho? jee Chadema wanajukumu la kuandaa kisomo kama walivyoandaa mazishi ya Shujaa wetu au ni jukumu la Familia?
 
Ataandaliwa na familia yake, CUF waliandaa kwa vile ni tawi la msikiti.
 
Chadema sio chama cha kidini. Ningeshauri Mzee Omar, baba yake marehemu Ishmael atumie michango iliyotolewa na wana-Chadema na marafiki zao(e.g. Sabodo), kuandaa hicho kisomo.
 
View attachment 20319

Kawaida ya waumini wa kiislam baada ya mazishi siku ya 3 hufanyika kisomo ili kumuombea dua marehemu.
Kwa kuwa aliokufa kishujaa amezikwa kwa heshima za chama . jee chadema itakuwa na jukukumu la kuandaa dua ya marehemu ambae ametangualia?
kwani Hata Cuf yalipotokea mauji ya wafuasi wao tulishuhudia viongozi wao wakuu wakishiriki kikamilifu katika kisomo hicho?
 
Back
Top Bottom