Chama cha Democrasia na Maendeleo (CDM) kina kila sababu sasa kuhakikisha kina azisha kituo cha TV, ili kuondoa hujuma tunazo zishuhudia katika TV yetu ya umma TBC dhidi ya kile kinachoonekana dhahiri kuziminya habari za chama hiki na wakati mwingine kutokukipa muda wa kutosha ukilinganisha na CCM.
Wote tunaelewa kuwa chama hiki kimeonesha kukubalika na wengi hasa vijana wengi wao wakiwa mijini,nadhani hapa jitihada za makusudi zinahitajika zifanyike ili elimu ya mabadiliko ifike mpaka vijijini ambako CCM bado imepafanya kama mtaji wa chama.so nafikiri,kama cdm tv itaanzishwa na ikawa na uwezo wa kuchana mawimbi nchi nzima basi moja kwa moja CCM ijiandae kuzikwa rasmi 2015.
Wito wangu kwa viongozi wa CDM kuandaa mkakati kabambe wa kitaifa waje nao kwa wapenzi na wanachama wote wa CDM bila kuwasahau hata wasiokuwa na chama ili kuendesha mchango wa fedha nchi nzima wa kuanzishwa kwa tv chadema je tuko tayari?.lakini nikileta hoja hii kwenu naomba pia nijulishwe je mamlaka ya anga hapa TZ ina kizuizi kisheria juu ya jambo hili kufanyika? Naomba kuwasilisha.