CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

Timu zinashambuliana kwa vipindi, dakika kama 15 za mwanzo za kipindi ccha pili Zanzibar walikua wanashambulia sana...
Lakini sasa ni zamu ya Stars kuwapeleka puta Heroes...
Dk 70. Mrisho Ngassa anakosa goli la wazi baada ya kukosa kuunganisha mpira wa chini toka kwa John Bocco
 
Mkuu, football ni mchezo wa makosa, tuhuma kama hizi siyo nzuri bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwamba alikula mlungula kutoka Kenya.
mkuu hata watangazaji wa super sport walimuongelea na kuwa na mashaka nae, hasa pale wakati wa kupiga penalt madini kila penalt aliyokua anapigiwa kabla ya penalt kupigwa alikua anaonesha mkono wa kulia na kuunyosha kulia ili lumuonesha mpiga penalt mkenya kuwa nalala kulia funga kushoto,na hivyo ndio ilivyokua,je umeiona mechi mkuu,,nina uhakika ninachoongea ni taarifa zilizotoka ktk kambi ya timu ya zenj huko kampala.
 
Dk 72. Zanzibar kwa mara nyingine wanakosa goli baada ya shuti la mchezaji mmoja(nadhani Mcha Hamis) kuishia mikononi mwa Kaseja
 
Dk 74. Zanzibar wanafanya mabadiliko... Abdalla Othman anaingia badala ya Abdallah Gulamu
 
Dk 76. John Bocco anaumia, Kim Poulsen kocha wa Kili stars anautumia muda huo kutoa maelekezo
Zanzibar wanafanya mabadiliko tena, anaingia Ally Twaha badala ya Selembe Kassim
 
mkuu hata watangazaji wa super sport walimuongelea na kuwa na mashaka nae, hasa pale wakati wa kupiga penalt madini kila penalt aliyokua anapigiwa kabla ya penalt kupigwa alikua anaonesha mkono wa kulia na kuunyosha kulia ili lumuonesha mpiga penalt mkenya kuwa nalala kulia funga kushoto,na hivyo ndio ilivyokua,je umeiona mechi mkuu,,nina uhakika ninachoongea ni taarifa zilizotoka ktk kambi ya timu ya zenj huko kampala.

Mkuu mechi niliiona hadi mwisho, nadhani Mwadini hakuwa kwenye 'form'.
 
Dk 78. Zanzibar wanakosa nafasi ya wazi mpira uliopigwa na Chollo unagonga mwamba wa juu, Zanzibar wanashindwa kufanya collection ya rebound


Dk 79. Kevin Yondan aningia matatani baada ya kufanya undava anapewa kadi ya njano
Ilitokea tafrani kati ya wachezaji, na Zanzibar wanapiga freekick....ni kama mita 22...mpira huooo unapaa goal kick
 
Dk 81. Kili stars wanafanya mabadiliko anatoka John Bocco anaingia Aboubakar Salum "Sure Boy"

Dk 82. Zanzibar wanakosa goli shuti lililopigwa linanyakwa na Kseja
 
Kama nilivyoandika hapo awali, kipindi cha pili timu zinashambuliana kwa vipindi...naona mabadiliko waliyofanya Zanzibar Heroes yanawasaidia na sasa wasaishambulia sana Kilimanjaro Stars

Dk 85. Zanzibar wanasawazisha ni Abdalla Othman
 
Kama nilivyoandika hapo awali, kipindi cha pili timu zinashambuliana kwa vipindi...naona mabadiliko waliyofanya Zanzibar Heroes yanawasaidia na sasa wasaishambulia sana Kilimanjaro Stars

Dk 85. Zanzibar wanasawazisha ni Abdalla Othman
Inamaana hata mshindi wa tatu tunaelekea kukosa....Tenga lazima uondoke...
 
Back
Top Bottom