CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

Kwa mtu yo yote mwenye ufahamu wa kawaida anajua kuwa, Nyoka akijivua gamba hawi Chura au Mjusi, kama anasuma wala sumu yake haipungui makali. Sana sana anajipanga kutenda yale yale ya siku zote kwa kasi zaidi.Habadili chakula, wala habidili tabia, umri wa kuishi au kitu chochote. Ni yule yule Nyoka hata jina lake halibadiliki. Kilichobadilika ni ngozi tu imekuwa nzuri zaidi, mpya zaidi inayovutia.

CCM wamebadilisha sura za secretariet, wamebadili pia baadhi ya wajumbe wa kamati kuu. Hivi kumweka mkama nafasi ya makamba kunaleta nafuu gani kwa watazania? Hawa wote walikuwa ni viongozi wa CCM na Serikali yake kabla ya uteuzi wa jana. Mkama alikuwa katibu wa wizara ya afya miaka kadhaa akikumbwa na tuhuma kibao zilizohusu dawa ya ukimwi. Magazeti yaliandika sana tu. Chiligati alikuwa waziri wa ardhi. Hakufanya lolote zaidi ya kuharibu na kurudisha nyuma kazi nzuri aliyoanzisha magufuli katika wizara ile. Je, kubadili secretariet inawafaidije watanzania? Au itawasaidiaje CCM? Ina punguzaje mikataba ya feki kama IPTL. Je, itaibuka na kauli ya kutokulipa Downs? Itatoa tamko la kuridhia mabadiliko makubwa ktk mswada wa mabadiliko ya katiba yanayopigiwa kelele kila kona wakati mkiti wake ni Rais JK aliyeuleta mswada huo? Au kumtosa Fisadi mkubwa kuliko wote RA kwenye CC wakati mfanyakazi wake wa zamani/Swahiba wake ni waziri wa Nishati na Madini (Ngeleja) kwa kupigiwa debe na RA mwenyewe kunaleta jipya gani?
HII ni danganya toto, tatizo la CCM ni la kimfumo, halibadiliswi kwa kubadili sura za watedaji.
My take,
Maisha bora hayawezi kuletwa na Chama kile kile, chenye sera zile zile kikiongozwa na Kikwete yule yule aliyeleta ombwe la uongozi ktk nchi yetu, eti kwa kubadili nafasi za baadhi ya viongozi na kuwa hadaa wananchi kuwa kimejivua gamba CCM kingali na sumu ile ile ya Ufisadi
 
Nyoka akijivua gamba atahitaji kula zaidi,maana katika kujivua gamba anatumia nguvu nyingi.so tutarajie maumivu zaidi.
 
JOKA ni joka tu........ kama alivyo Paka ni paka, hata apewe nini lazima atakula panya . CCM ni CCM tu hata ijipake mafuta kwa nje , ni mafisadi na vilaza watupu walioshindwa kuongozi nchi. Period
 
CCM yote, pamoja na UVCCM sio gamba tu bali ni ukurutu na ukoma, ngozi yabisi, ngozi ya chui. Kobe ukimvua gamba unamuua, nyoka anajivua gamba lakini anabaki sumu yake. Tiba ya CCM ni kuondoka, ibakie benchi kwa miaka angalau 50 hivi, mpaka kizazi kilichopo cha mafisadi na wanafiki kiyeyuke kabisa.
 
<table align="left" border="0" cellpadding="0" cellspacing="0" width="100%"><tbody><tr bgcolor="#ffffff"> <td class="kaziBody" align="left" bgcolor="#ffffff" valign="middle">
</td> </tr> <tr bgcolor="#ffffff"> <td class="kaziBody" bgcolor="#ffffff">Wednesday Apr 13, 2011
</td> </tr> <tr bgcolor="#ffffff"> <td class="kaziBody" bgcolor="#ffffff">
04_11_2e4gww.jpg
</td> </tr> <tr bgcolor="#ffffff"> <td class="kaziBody" bgcolor="#ffffff">HERE I AM: The new CCM Secretary General, Mr Wilson Mukama, acknowledges cheers from the party’s headquarters staff in Dodoma after being introduced by the National Chairman, President Jakaya Kikwete (third left), on Tuesday. Others in the picture are Deputy Secretary General (Zanzibar), Mr Vuai Ali Vuai, CCM Vice-Chairman (Mainland), Mr Pius Msekwa and Deputy Secretary General (Mainland), Mr John Chiligati. (Photo by Freddy Maro)</td></tr></tbody></table>
 
CCM deludes herself that a reluctant change of guard will redeem her political fortunes...............................well not that easy......................and for obvious reasons....life is a tough business...........................
 
kuna updates nimepewa na watu wanaomfahamu katibu mkuu mpya wa chama cha magamba na kuambiwa nae ni gamba tu linalostahili kuvuliwa.
kwa wale wanaomfahamu na tuliowahi kusikia mkataba wa kifisadi wa ukusanyaji ushuru pale Ubungo Bus Termninal ni huyu bwana mkubwa ndio aliouidhinisha kwa nguli wa siasa Kingunge N. Mwiru, ni huyu ndio alio idhinisha mkataba wa ukusanyaji ushuru wa car parking jijin DSM mikataba yote hii ilikuwa haina faida kwa jiji wala serikali bali hela nyingi zilirudi mifukoni mwao wenyewe na kupeleka ushuru kidogo kwa jiji, haya yamefanyika wakati bwana mkubwa huyu akiwa mkurugenzi wa jiji la Dar Es Salaam

Akiwa katibu mkuu wa wizara ya afya bwana mkubwa wakati wa mgomo wa madaktari kudai maslahi zaidi huyu bwana mkubwa aliwatimua wote nakutoa maneno mengi ya dhihaka na kupeleka wanajeshi wakagange watu pale National Hospital

mwenye data za zaidi ziweke mezani tafadhali
 
Huyu amelipwa fadhila na Kingunge wala hana jipya tofauti na Makamba kuwa hana uwezo wa kukariri vifungu vya biblia na qurani
 
halipo kuwa jiji aliajiri watu kutoka musoma tu , na kupa spendo ya ukabila
 
Siku zote moja ya vipimo vya appointing authority ni watu anaowateua. Huyu mjita Mkama ni kama Makamba sema yeye hatukani hovyo, ila matendo yake ni matusi tu. JK na CCM ni sikio la kufa lisilo na dawa.
 
JK namfagilia kiasi fulani, kwani CCM kipindi hiki kinataka kiongozwe na watu wa kutumia mabavu kama Mukama, muda wa longo longo haupo tena. CDM wakimwaga mboga CCM imwage ugali hapo KITAELEWEKA! Suala la kuajiri watu wa kwao si tatizo ili mradi wawe na uwezo, asiwe kama Makamba kujaza wasambaa akiwemo Tambwe Hiza bila ya kujali uwezo wake. Sifa ya ziada ya Mukama ni kujenga hoja na mzungumzaji mzuri katika mdahalo! Hivyo Dr. Slaa ajiandae kwa mdahalo CCM sasa hivi ina katibu mkuu msomi sio Makamba mkimbia midahalo
 
alipokuwa wizara ya afya ziliwahi kuagizwa air condition special kwa ajili ya theaters muhimbili...very expensive units. zilipofika dar port upon physical inspection zikakutwa na split units kama ziuzwazo pale JM Mall!!! hakukuwa na hata haja ya kuziagiza. na hizo split units wala hazifai kwa matumizi ya chumba cha upasuaji!! wadanganyika once...wadanganyika forever!!!
 
Hivi karibuni chama cha mapinduzi katika mkutano wake uliofanyika mjini dodoma walifanya mabadiliko katika safu zao za uongozi wa juu wa chama hicho katika kile kinachoonekana ni kujivua gamba kama nyoka afanyavyo anapozeeka! Hatua hii imepokelewa kwa hisia tofauti na wadau mbali mbali, wengine wakipongeza hatua hii na wengine wakiiponda na kuona hawajafanya lolote. Kwa mtazamo wa kisosholojia ni kwamba hakuna walichokifanya baada ya kushindwa kujua tatizo ni nini. Tatizo la ccm sio watu(japo huenda watu wakawa ni tatizo) tatizo ni mfumo wa maingiliano baina(interaction system) na sera (policy) za chama cha mapinduzi! Wao wanatibu observable object/figure by using observable object kitu ambacho sio sahihi! Observable object hutibiwa by change of relation and interaction form in the party. Kwa kubadilisha watu lakini forms of interaction and policy remains the same bado hawajatibu tatizo coz hata wao walioingia mfumo huo utawaharibu na kuwa kama waliotoka! Hivyo basi gamba la ccm bado lipo pale pale bado hawajalivua! Kama kweli wamekusudia kukiimarisha chama chao iko haja ya kujingalia upya hilo gamba lao na kulivua!. Kwa wadau wote nawasilisha.
 
Back
Top Bottom