Wakati tunafurahia ccm "kujivua gamba" pengine tujiulize ina maana gani hasa.
Kama tunatumia mfano wa nyoka kujivua gamba basi naona tunakosea kuamini kwamba ccm imebdalika. Kwa sababu nyoka anapojivua magamba hubaki kuwa ni nyoka yule yule kwa tabia, aina na sifa zake zote. Tena kama ni nyoka wa hatari au wa sumu hubaki kuwa hivyo hivyo.
Walichofanya ccm ni kama mtu kubadili gari tu. Gari jipya (au kuukuu kama Mukama) halibadili chochote katika tabia na sifa za mwenye gari. Lakini walichofanya hakileti mabadiliko yoyote kwa sababu viongozi wakuu wamebaki kuwa wale wale wa tangu enzi za TANU na Afro Shirazi. Mawazo na uwezo wao pia ni wa karne hiyo.
Wazee wanang'ang'ania madaraka hata pale wanapoona wameshindwa kabisa!
Kwa falsafa na uelewa wa ccm, jibu ni ndio. Kisayansi jibu ni hapana.
Kujivua gamba ni msemo mpya (nionavyo) ambao una lengo la kuwasilisha hoja fulani za ccm kwa manufaa ya kisiasa. Ni ujinga kwao kutumia paronamasia by merely playing with empty words.
Kazi yao kwisha.