CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

Watanzania hatuwezi tawaliwa na nyoka ni mdudu hatari sana!kwa nini tusitawaliwe na tembo twiga ngombe maana hata kwenye vitabu vitakatifu biblia,quran, nyoka amelaaniwa!
 
Kwani wananchi walikuwa wamekerwa na gamba la huyo nyoka (ccm) au tabia yake?
 
Kwa falsafa na uelewa wa ccm, jibu ni ndio. Kisayansi jibu ni hapana.

Kujivua gamba ni msemo mpya (nionavyo) ambao una lengo la kuwasilisha hoja fulani za ccm kwa manufaa ya kisiasa. Ni ujinga kwao kutumia paronamasia by merely playing with empty words.

Kazi yao kwisha.
 
Wakati tunafurahia ccm "kujivua gamba" pengine tujiulize ina maana gani hasa.

Kama tunatumia mfano wa nyoka kujivua gamba basi naona tunakosea kuamini kwamba ccm imebdalika. Kwa sababu nyoka anapojivua magamba hubaki kuwa ni nyoka yule yule kwa tabia, aina na sifa zake zote. Tena kama ni nyoka wa hatari au wa sumu hubaki kuwa hivyo hivyo.

Walichofanya ccm ni kama mtu kubadili gari tu. Gari jipya (au kuukuu kama Mukama) halibadili chochote katika tabia na sifa za mwenye gari. Lakini walichofanya hakileti mabadiliko yoyote kwa sababu viongozi wakuu wamebaki kuwa wale wale wa tangu enzi za TANU na Afro Shirazi. Mawazo na uwezo wao pia ni wa karne hiyo.

Wazee wanang'ang'ania madaraka hata pale wanapoona wameshindwa kabisa!

Hivi ni kuwa hatuelewi kweli au tumeamua tu kuwa na nongwa? 'Kujivua gamba' ni kujihuisha au 'rejuvinate'. Ni zoezi la kawaida kabisa duniani kufanywa na vyama vya siasa. Kule Uingereza kuna 'New Labor' na 'New Conservative'. Hapa nyumbani CHADEMA miaka michache iliyopita ilijivua gamba ktk mkutano wake mkuu, wakanadlsha bendera yao wakaachana na ile ya blue bahari ya kina mzee Mtei na Makani, wakarasimisha combart kuwa vazi la chama, wakabadilisha katiba, wakaja n falsafa ya CHADEMA ni tawi etc. Baada ya hapo, CHADEMA. Imeendelea kuwa CHADEMA, likewise CCM itaendelea kuwa CCM. Muhimu ni kuwa vyama vinajihuisha kuendana na wakati.

Ukiachana na kujadili mantiki na kutaka kukebehi tu, basi mtu pia aweza kusema kuwa hata baada ya mabadiliko yale ktk chadema kimeendelea kuwa chama cha wachaga na kaskazini, wakristo, na kinachoendeshwa kifamilia.

Sio nia yangu kukebehi, mimi ni mtanzania nisiye na chama, napenda vyama vyote, nchi ni yetu sote, ikituharibikia tutaumia sote. Tuache hii dhana ya kubeza beza kila kitu. Haijengi.
 
yangu nyoka akivua gamba na kuwa na ngozi laini kuliko ile aliyokuwa nayo kabla ya kuvua gamba la awali nyoka huwa very active, speedy, productive, fierce, na mengine mengi aliyokuwa nayo kabla. Sasa CCM wako katika kuvua gamba hivi karibuni watakuwa wapya kwa muonekano. Kama ilivyotabia ya nyoka ambaye huwa very active nao pia watakuwa very active katika kutenda mambo yao yakiwamo yale ya ufisadi. Nasema hivi kwa kujiamini kabisa kwani kama ni kupambana na ufisadi wangewalengo watuhumiwa moja kwa moja. Kinachofanyika ni kunoa kucha zao watufinye zaidi. Natamani wavue magamba yao mpaka wachanike, walemae wasiwe kama walivyokuwa. Nawasilisha hoja japo kwa hofu ya kudumu miaka mingine 50 maana hadi waje kuhitajika kujivua gamba mimi nitakuwa "KWETU"
 
Kwa falsafa na uelewa wa ccm, jibu ni ndio. Kisayansi jibu ni hapana.

Kujivua gamba ni msemo mpya (nionavyo) ambao una lengo la kuwasilisha hoja fulani za ccm kwa manufaa ya kisiasa. Ni ujinga kwao kutumia paronamasia by merely playing with empty words.

Kazi yao kwisha.

Mambo ya kuwakumbuka wenyeviti wa CCM:
Falsafa ya Mwenyekiti wa TANU: Ujamaa na Kujitegemea
Falsafa ya Mwenyekiti wa I wa CCM: Mapinduzi (Kilimo, Elimu, siasa ya Ujamaa na Kujitegemea)
Falsafa ya Mwenyekiti wa II wa CCM: Ruksa, utandawazi

Falsafa ya Mwenyekiti wa III wa CCM: Uwazi na Ukweli?, utandawazi?

Falsafa ya Mwenyekiti wa IV CCM: Ari mpya, Nguvu mpya, Kasi mpya -> ya nini?
Falsafa ya Mwenyekiti wa IV CCM: Ari zaidi, Nguvu zaidi, Kasi zaidi -> ya nini?
Falsafa ya Mwenyekiti wa IV wa CCM: Chama kujivua Magamba => CCM ni joka? kama viongozi wake ni magamba, CCM mwenyewe anayebaki ni nani? Sera na imani za chama sio! Na wanachama ni nini kwenye hii model ya nyoka? Na wananchi ni nani!
 
Mimi nadhani suala hapa ni "MFANO WA NYOKA" Nyoka ni nyoka tu hata iweje. Kujitoa gamba ni sehemu ya kukua kimwili tu. Kujitoa gamba hakumfanyi nyoka ageuke kuwa Mjusi au Kenge. Uwezo wake katika kutoa sumu ndo kwanza unaongezeka; kwahiyo madhara yake huwa makubwa zaidi. Ingekuwa jambo jema kwa CCM kutoutumia mfano huu wa NYOKA ili kuondoa utata uliopo sasa.

Ingefaa waseme chama kimejiosha; kwa maana ya kuwaondoa mafisadi na watendaji wabovu kama akina Makamba, Rostamu na wengine wanaofanana na hao. Mtu akioga huwa safi na hubadirika kimwili na kiakiri. Lakini nyoka akijivua gamba habadiliki kamwe; hubaki kuwa yule yule tena mwenye madhara makubwa sana.

Hata hivyo CCM wamefanya vizuri sana kuupunguza uozo uliokithiri kwenye chama chao. Ingawa sielewi kunanini kati ya JKM na Mama Zakia Mejgh. Naona amemng'ang'ania sana kila kona anae tu. Mh!
 
nakumbukia hadithi ya mjomba wangu kule longido aliyesema wanasiasa ni kama manyani tu.

Wote ni wala mahindi.hata kama ametokea songea au mpanda. Tunabadilisha aina ya nyani ila bado tunaendela kupanda mahindi. Watayala tu hawa.
 
Nyoka huyu(ccm) tumemzowea takribani miaka 50 sasa. Na kawaida ya nyoka baada ya muda ni lazima ajivue magamba,lakini nyoka ni yule yule. Hawana jipya ccm
 
hii falsafa ya kutumia picha ya nyoka kwa watu waliosoma kiswahli kwenye fasih andish kpengele cha fani matumiz ya lugha ya pcha pale anapotajwa nyoka ujue ni hatari tupu hapa kaliki hapana amani wala mshkmano sasa ccm wanapojifananisha na nyoka kwa kujivua gamba manake wanahatarisha amani kama afanyavyo nyoka tafadhali ccm kama hakuna wanafalsafa kwenu naomba mje chadema tuwape falsafa za kutumia ukiacha hii tunayotumia sasa zpo nyingne kbao ccm pga namba hii peoples, power . na upate falsafa
 
It is hard to let old beliefs go. They are familiar. We are
comfortable with them and have spent years building systems
and developing habits that depend on them. Like a man who has
worn eyeglasses so long that he forgets he has them on, we
forget that the world looks to us the way it does because we
have become used to seeing it that way through a particular
set of lenses. Today, however, we need new lenses. And we need
to throw the old ones away.
 
Hivi mafisadi bado wamo CCM? pamoja na shutuma zote bado CCm inawakumbatia,sasa naanza kuona njia ya CHADEMA nyeupe na mtaji uwe ni kupambana na mafisadi tu,tunataka CHADEMA kikishika nchi mafisadi wafanywe kama wanavyofanywa China
 
MABADILIKO YALIYOFANYWA NA CCM NI KUONDOA GAMBA LA KICHWANI TUU NA HUKU MWILI WOTE UKIBAKI NA GAMBA LA ZAMANI

NI UJINGA NA DANGANYA TOTO NYINGINE WATANZANIA TUSIRUDI NYUMA SISI NA CHADEMA CHADEMA NA SISI


mpaka kieleweke
 
Wadau naweka hoja jamvini kufuatia yaloyijiri huko dodoma kataika kikao cha nec-ccm kwa kujivua gamba.

Kwa mtazamo wangu hakuna gamba lolote walilojivua ccm na wote waliochaguliwa ni wafuasi wazuri wa lowassa na rostam azizi

1. January makamba - ni mfuasi mzuri wa lowassa na rostam

2. Mwigulu - ni mfuasi mzuri wa lowassa

3. Abdallah kigoda - dalali wa rasilimali zetu ndio aliye binafsisha mashirika pasipo kuwa na maslahi ya taifa

4. Zakhia meghji - amepoteza rasilimali nyingi za taifa hili akiwa waziri wa maliasili - fedha

5. Wassira - asiyejali maslahi ya taifa wala wananchi bali yake na ma boss zake tuu, hana mapenzi ya dhati na chama bali maslahi tuu
 
Nyoka ni nyoka tu, whether atajivua gamba au kubaki alivyokuwa!
Kilichotakiwa kufanywa ni kubadili software na hardware, na si hardware tu!

Usaniii huu!
 
Mimi nimewapenda CCM, wamempooza makamba kwa kumpa kikombe mtoto JM, na wamemkumbuka mzee wangu mnauye kwa kusaidia familia. hapa zinalipwa fadhila na fadhila zinatakiwa back. sasa kama JK alilipa fadhila kwa kumwachia RA na EL kula kama nchi ni shamba la bibi je hawa vijana watalipa nini kwa waliowaweka.?????????????/ Jibu subiria uone.
 
Na Nova Kambota,

Hakuna ubishi kuwa kauli yenye utata ya mwenyekiti wa CCM JakayaKikwete ya kukitaka chama chake kufanya kile kinachoitwa ‘kujivua gamba’ inazidi kukibomoa chama hiko kikongwe zaidi nchini, naaita kauli yenye utata kufuatia tafsiri isiyoeleweka ya kauli hiyo ambayo kwa wachambuzi wengi wa kisiasa wanadai kuwa iwe kwa kutoelewa au kwa kudhamiria watu mbalimbali ndani ya chama hiko wanaataka kuitumia kauli hiyo kupakanaa matope kama sio kufanyiana michezo ya kimafia ya siasa za majitaka.
Baada ya kauli hiyo ilifuatiwa na tamko la UVCCM mkoa wa Pwani ambapo kati ya mambo yalitamkwa ni kuwa viongozi wastaafu yaani Sumaye na Lowassa waache rafu zao za kuutaka urais, akisoma tamko hilo Abdalah Ulega hakusita kkubainisha kuwa vigogo hao wasahau ndoto ya urais kwa madai kuwa tayari Kikwete ana jina la mrithi wake, baada ya hilo Umoja wa vijana taifa chini ya Benno Malissa nao ukakaa na kupigilia msumari kwenye lakini katika hiko kikao tunaelezwa kuwa mjumbe mmoja kutoka Arusha Bw Mrisho Gumbo aliweka wazi kuwa ni lazima wale wote wanaohusika na tuhuma za ufisadi wang’olewe kwenye chama.
Ndani ya mbilinge hii pia akaibuka Fredrick Sumaye akajibu mapigo akiwataka vijana hao kuacha kutumiwa, wakati huhuo huko Tabora lingine likazuka la Robert Kamoga mwenyekiti wa UVCCM mkoani humo kumng’oa mlezi wao Bw Samwel Sitta lakini wenzake wakajitokeza na kupinga uamuzi huo, kabla hali ya mambo haijakaa sawa UVCCM Arusha wakatangaza kumwondoa Mrisho Gumbo ambaye na yeye hata hivyo ameongea kwa msisitizo kuwa UVCCM Arusha hawana ubavu huo na huko Iringa nako kumeibuka kundi lingine la UVCCM linalotaka viongozi wa umoja huo taifa wang’olewe kwa madai kuwa hawana mwelekeo na hawana msaada kwa chama chao., hii ndio hali ya UVCCM kwa sasa.
Hii ina maana gani katika zama hizi za CCM kujivua gamba? Hakika ni vigumu hata kubaini haswa gamba analozungumzia mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete ni lipi? Ndani ya CCM kuna makundi yanasigana huku moja likiwa linapinga ufisadi na lingine ingawa halijatamka wazi kuwa linaunga mkono ufisadi lakini kwa jinsi lisivyokemea ufisadi tafsiri yake ni kuwa linaunga mkono ufisadi. Kwa mantiki hii sasa ni kuwa Kikwete anaposema kujivua gamba kila kundi linatafsiri yake, kwa kila kundi linaamini kuwa kundi pinzani ndio gamba linalotakiwa kuvuliwa nah ii ndio imepelekea vuguvugu hili kuikumba hata UVCCM nah ii ni lele tu ngoma yenyewe inakuja kwani kuna kila dalili kuwa hali hii itavamia hata umoja wa wanawake wa chama hiko na pia jumuia ya wazazi wa chama hiko nko huko kote hali inatajwa kuwa si punde itakuwa ni mwendo wa kujivua gamba kama ilivyo UVCCM.
Kwangu mimi na imani kuwa ni vigumu kusema gamba ni nani ndani ya chama hiko? Kama ni mafisadi sasa mbona hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi ni wanachama watiifu wa CCM? Tena baadhi yao wapo kwenye kamati kuu ya chama hiko? Na kama ni wapinga ufisadi mbona baadhi yao ni mawaziri? Tena nao ni wajumbe wa kamati kuu? Kwa muktadha huu ni sahihi kusema kuwa gamba limeshikamana na ngozi je wataweza kujivua? Lakini tukigeukia upande wa pili ambao ni UVCCM nao kwa mbali naona kuwa wamejiingiza kwenye mgogoro usiowahusu, kwangu mimi UVCCM ni sehemu muhimu ya CCM, tofauti na wachambuzi wengine wanaodai kuwa UVCCM haina chochote ni jumuia tu naomba nitofautiane nao ni kweli UVCCM ni jumuia tu lakini sio huko walipotoka kina Kikwete au Sumaye enzi hizo ikiitwa TANU youth League? Kwa maana nyingine UVCCM ni chombo na kiungo muhimu kwa uhai wa CCM na ndio maana hata wanaotaka kuupata urais wameanza na UVCCM kabla ya jumuia nyingine ndani ya chama hiko.
Lakini swali la msingi ni je UVCCM ni gamba au ngozi? Kama gamba basi ivuliwe na kama ngozi itunzwe, pia ni vigumu kusema moja kwa moja kuwa UVCCM ni ngozi au gamba. CCM wakifumba macho na harakaharaka tu wakadai kuwa UVCCM ni gamba basi ivuliwe naomba niwape angalizo kuwa sio kila anayevaa shati la kijani anakipenda chama hiko na sio kila mwanaUVCCM kweli yupo tayari kudhalilika kwa hoja ya uamuzi wa chama wasije kujidanganya kwa kuifuta jumuia hiyo kirahisirahisi,napenda kuwaonya kuwa baadhi yao vijana hao watageuka wapinzani wakubwa wa CCM hakuna ubishi kuwa hata Makamba na Kikwete wanafahamu siri nzito za chama walizonazo vijana hao kwenye mioyo yake na bila shaka kwa mantiki hii CCM wanaweza kukisia athari za vijana hao kugeuka wapinzani na hata mkurugenzi wa propaganda wa CCM Tambwe Hizza anaweza kubashiri kitakachowapata chama chake 2015 kama vijana hao watageuka wapinzani!
Na iwapo CCM wakajifanya kufumba macho kwa kulea kinachoendelea ndani ya UVCCM na kuifananisha jumuia hiyo na ngozi hivyo kuitunza tu bila shaka watakuwa wanajidanganya, itakuwa ni kama kujipalia makaa ya moto kwani hakuna ubishi kuwa UVCCM haijui majukumu yake na haijui ifanye nini, imechoshwa na makundi na minyukano ya kisiasa, imepigwa ikapigika sasa imeamua kuishi kwa mwongozo wa vigogo na sio kwa katiba inayoongoza jumuia hiyo kwa maana nyingine haileleki hata kidogo kwa mazingira ya sasa hivyo si sahihi pia kuiita ngozi basi UVCCM ni nini?
Kwa jinsi hali ilivyo na ikizingatiwa umuhimu mkubwa wa jumuia hiyo kama nilivyoeleza hapo awali basi ni sahihi sasa kusema kuwa UVCCM sio ngozi bali ngozi yenye chunusi na mabaka, sasa nini kifanyike ili kutibu chunusi na mabaka haya kuifanya ngozi hiyo kuwa nzuri, jibu ni rahisi ila kutimiza mahitaji ya jibu si jambo rahisi, CCM haipaswi kukaa kimya katika timbwili hili ni laziima ionyeshe ubaba wake na ni lazima ionyeshe kuwa UVCCM ipo chini ya CCM na siyo CCM chini ya UVCCM lakini hili sifanyike kwa nia ya kuonyeshana ubabe bali lifanyike kwa busara kubwa tena kwa uadilifu ili lizae matunda hakuna ubishi kuwa imefika wakati sasa viongozi wote wa UVCCM waliotekwa na makundi wapigwe chini ! na kuwekwa vijana wanaojua jukumu lao kubwa ni kuisaidia CCM kwa mema siyo kwa mabaya kama kuunga mkono ufisadi, imefika sehemu ya kufumba macho na kuinua panga kukata kidole kilichoanza kuoza maana kikiachwa mkono wote utaoza.
Na hili halipaswi kuishia ndani ya UVCCM bali liende mpaka huko CCM kwenyewe kwa maana haiingii akilini kuona UVCCM inasafishwa halafu CCM inaendelea na mwenendo wake ambao si salama hata kidogo, CCM inapaswa ijipambanue iwapo inaunga mkono ufisadi kwa maana hao ndio wenye hela wanaweza kuwa wafadhili wazuri na wakubwa au pia ijipambanue kuwa inapinga ufisadi na kwa hapa kabla hawajaamua niwakumbushe kuwa wananchi wanapinga ufisadi na zaidi wananchi ndio wapiga kura hivyo kwangu mimi naona ni busara na salama kwa chama hiko kujipambanua kimaneno na kimatendo kuwa kinapinga ufisadi kwa kuwaengua kabisa wahusika wote wa ufisadi na hapo ndio haswa CCM itakuwa imejivua gamba kinyume na hili ni porojo na makidamakida tu….Tafakari!





Nova Kambota ni mwandishi mpya kijana wa Makala wa Gazeti hili la Dira , ni mchambuzi na mtafiti wa maswala ya kisiasa pia ni mwanaharakati wa vijana anapatikana kwa anwani ya barua pepe; novakambota@gmail.com au tembelea blog yake ; www.novatzdream.blogspot.com
Au mpigie kwa namba 0717-709618 au 0766-730256.

 
Back
Top Bottom