JK namfagilia kiasi fulani, kwani CCM kipindi hiki kinataka kiongozwe na watu wa kutumia mabavu kama Mukama, muda wa longo longo haupo tena. CDM wakimwaga mboga CCM imwage ugali hapo KITAELEWEKA! Suala la kuajiri watu wa kwao si tatizo ili mradi wawe na uwezo, asiwe kama Makamba kujaza wasambaa akiwemo Tambwe Hiza bila ya kujali uwezo wake. Sifa ya ziada ya Mukama ni kujenga hoja na mzungumzaji mzuri katika mdahalo! Hivyo Dr. Slaa ajiandae kwa mdahalo CCM sasa hivi ina katibu mkuu msomi sio Makamba mkimbia midahalo
Mbano hukutupa jibu kuhusu Ufisadi wa Kutoa Ukusanyaji wa Ushuru katika Kituo cha Ubungo kwa kampuni yenye uhusiano na familia ya Kingunge alipokuwa kuwa Mkurugenzi wa Jiji?