CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

Pamoja na kwamba Mwanzilishi wa thread hii ameforge na Kuchakachua ni dhahili kwamba Watanzania wamekomaa Kisiasa. Swala hapa Si CHADEMA wala CUF Kuwachukuwa Madiwani waliofukuzwa CCM , issue hapa ni kwamba Watu wamechoka , na hata ndani ya CCM kwa sasa wameamua kusema "Liwalo na Liwe" Maana "hamna Namna nyingine ya Kupambana na dhuruma ya CCM". Madiwani hao Wameonyesha Ujasiri Mkubwa na inabidi iwe mfano wa kuingwa kwa almashauri zingine zenye matendo ya Kifisadi. Kwa MaCCM ukizigatia upepo wa Kisiasa nchini naweza sema kwao hii ni Political Miscalculation kwani kwa kuiga CHADEMA's political strategy ya walivyowa fukuza Madiwani wao jijini Arusha, Itawagharimu Asilani. Swali ni Je CCM wakiingia Kwenye Uchaguzi leo hii Watavirudisha Viti hivyo???? na Je Madiwani waliotimuliwa wana support ya wapiga kura kwa kile walichokisimamia hadi wanafukuzwa Chamani???, Mwisho kabisa Uchaguzi Ukifanyika leo na ikatokea CCM Imeshindwa Kuvirudisha Viti hivyo vya Madiwani waliowatimua basi Watanzania Watakuwa Wamepata Somo zuri nalo ni "Ukiwapinga waziwazi na ukapambana na Mafisadi & Ufisadi ndani ya CCM ni dhambi Kubwa kama ugojwa wa Ukoma, baba wa taifa.

Ni kweli kwa sasa ni wananchi tu ndiyo wameshikilia power ya kutokomeza tabia za kifisadi kwa kuamua haki ndani ya masanduku ya kura.

Kuhusu hii ya CCM kufukuza madiwani, naona ni kosa baya sana. Na usishangae wakaamua kutoitisha uchaguzi tena. Vinginevyo kupoteza kuko wazi. Hata hivyo hiki wanachofanya mi hakijanistua. Kwa kawaida hata mchawi akiroga sana hufikia wakati akasahau mchana na usiku na akatoka kuwanga mchana kweupe. Ndilo lililowakuta CCM
 
Si kawaida yenu lakini kuwapokea wanao fukuzwa chama kikuu? Slaa, mke wake, kina Lusinde, Chriss huyu anae wapa shida humu ndani etc. Waamue tu wenyewe kutojiunga il nyie kama nyie mnawapenda sana.
 
kwa Mungu yote yanawezekana karibuni cdm.
 
unajua ccm wanacheza ngoma wasiyoijua na waache kuiga maana unawafukuza madiwani wazarendo na kuukumbatia usaliti na ufisadi, kweli hizi akili ndogo katu haziwezi kutawala akili kubwa! Hizo kata zote zitaenda kwa CDM.

Sio akili tena pale, ni njaa na tamaa tu na roho mbaya. Mwiteni HAMY-D aje atoe msimamo wa chama chake..
 
Last edited by a moderator:
Hivi wakifakuzwa hoja yao na meya inakuwa ndio imekufa? au waliobaki wanaweza kuuendeleza?
 
[font=&quot]ni baada ya vikao na majadiliano ya muda mrefu yaliyofanywa kwa usiri mkubwa na viongozi wa chadema taifa kwa kushirikana na viongozi wa chadema mkoa wa kagera kwa lengo la kuwashawishi madiwani wa ccm kuendelea na mgomo wao dhidi ya vitisho wa wakuu wa ccm huku lumumba kwa kuwaahidi kuwapokea na kuwapa nafasi ya kugombea kata husika ikiwa watafukukuzwa ndani ya ccm.kwa mujibu wa nyaraka zilizopatikana madiwani hao wameagizwa kutoyakatia rufaa maamuzi ya ccm mkoa ya kuwavua uanachama mahakamani au ngazi za juu za ccm kwa luwa watapewa nafasi za kugombea kata husika bila kipingamizi.[/font]
[font=&quot]hili linakuja baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu kati ya madiwani 8 wa ccm walioamua kuuasi uongozi wa ccm huko kagera na kuamua kuungana wa wapinzani yaani cuf na chadema kupinga mipango ya ufisadi inayoratibiwa na meya wa manispaa ya bukoba akishirikianna na baadhi ya viongozi wa ccm mkoa na taifa wenye masilahi katika ufisadi huo kwa kutumia kampuni nyingi zilizoibuliwa kama uyoga kwa ajli ya kula fedha za manispaa.[/font]
[font=&quot]kinachoendela kwa sasa ni kuwa kuna mkurugenzi mmoja wa chadema aliyetumwa kagera kwa ajili ya kukamilisha mpango huo mapema usije ukatekwa nyara na cuf. [/font]
[font=&quot]mpango huu umelenga kuiangamiza ccm ndani ya kanda ya ziwa kuelekea uhaguzi mkuu 2015.tusubiri tuone[/font]

Sasa kama una uhakika kuna nyaraka zimepatikana kwa nini hii uiite tetesi? Unge comfirm tu na kutuwekea hizo nyaraka hapa. Otherwise mii nauita huu ni UMBEA
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera, leo kimewafukuza madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kupitia chama hicho na kufutwa nyadhifa zao za udiwani kutokana na mgogoro uliokuwa ukiendelea


Waliofukuzwa ni:


  1. Richard Gaspar (Miembeni )
  2. Murungi Kichwabuta (Viti maalum)
  3. Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe)
  4. Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai)
  5. Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga)
  6. Robert Katunzi (Hamugembe)
  7. Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na
  8. Dauda Kalumuna (Ijuganyondo)
 
CCM wakiacha mambo yewe hivihivi watapoteza viti vyote
Kama wakishindwa kusimamia maamuzi yao kama CHADEMA walivyofanya Arusha,basi CCM itakuwa imeonyesha udhaifu wa hari ya juu!
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera, leo kimewafukuza madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kupitia chama hicho na kufutwa nyadhifa zao za udiwani kutokana na mgogoro uliokuwa ukiendelea


Waliofukuzwa ni:


  1. Richard Gaspar (Miembeni )
  2. Murungi Kichwabuta (Viti maalum)
  3. Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe)
  4. Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai)
  5. Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga)
  6. Robert Katunzi (Hamugembe)
  7. Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na
  8. Dauda Kalumuna (Ijuganyondo)
Nimependa heading yako
 
katibu wa ccm mkoa wa kagera bw avelin mushi amemaliza press conf hivi punde na kufafanua kuwa kikao cha halmasahuri kuu ya mkoa wa kagera imemaliza kikao chake hivi punde na kuamua madiwani 8 wa manispaa ya bukoba kufukuzwa katika chama na kufutiwa nyadhifa za udiwani kutoka na mgogoro uliokuwa ukiendelea.

waliofukuzwa ni:

1. Richard gaspar (miembeni )

2. Murungi kichwabuta (viti maalum)

3. Alexander ngalinda ambaye pia ni naibu meya (buhembe)

4. Yusuf ngaiza ambaye pia ni mwenyekiti wa ccm wa wilaya (kashai)

5. Deusdedit mutakyahwa (nyanga)

6. Robert katunzi (hamugembe)

7. Samwel ruhangisa (kitendaguro) na

8. Dauda kalumuna (ijuganyondo).

Katibu huyo ameongeza kuwa madiwani hao wanaweza kukata rufaa kwa ngazi za juu za chama wakiona hawakutendea haki na kuwa ngazi ya mkoa ina mamlaka ya kufanya hivyo kwa madiwani wa ngazi hizo.

Aidha amesema kwa bw yusuph ngaiza amabye ni mwenyekiti wa ccm bukoba,nafasi yake hiyo inasubiriwa ngazi za juu amabazo ndizo zenye mamlaka juu yake(kwa cheo hicho)

manispaa ya bukoba ina kata 14 na kati ya hizo kata 4 zinaongozwa na cdm(2) na cuf(2) hivyo kwa bukoba mjini ccm imebakiza madiwani 3 tu wa kuchaguliwa .kama ifuatavyo
1.kashai-amefukuzwa
2. Miembeni-amefukuzwa
3.miembe-amefukuzwa
4.nyanga-amefukuzwa
5.hamugembe-amefukuzwa
6.kitendaguro-amefukuzwa
7.ijuganyondo-amefukuzwa
8.(1)kagondo-amebaki (ccm) (meya amani)
9.(2)nshambya-amebaki(ccm)
10.(3)kahororo-amebaki(ccm)
11.bilele-amebaki(cuf)
12.kibeta-amebaki(chadema)
13.bakoba-amebaki(cuf)
14.rwamishenye-amebaki(chadema)
xxxxxxxxxxxxx

kujua historia ya chanzo cha yote hapa fungua hapa chini.
historia ya mgogoro wa kisiasa bukoba manispaa


baadaye nitaingiza video.
sikio lakufa
 
Utaratibu huu ni angamizo la Demokrasia na ni Jeneza la CDM. Sipenda CDM kuruhusu tena Mateja kama Shibuda. Naamini CDM ina watu wengi wazuri wakuchukua nafasi hizo na Ukatumika utaratibu mzuri wa kuwapata wagombea wasio kuwa na tabia za PANYA, Baba mwizi, mama mwizi, mtoto mwizi, Panya wote wezi, achaneni na tabia hii mbovu ya kuokota MAKOMBO ya ccm. Sipendi kuona CDM ikichukuwa viongozi toka ccm. HAKUNA KIONGOZI ccm alie SALAMA wote wameathirika na VIRUSI vya UFISADI

wazo lako ni zuri, ila kwa upande mwingine ukirudi kwa hawa madiwani ni kwamba wao wanajiamini kuwa wana support kubwa ya wananchi na ndio maana wakakomaa mpaka wamefukuzwa uanachama.kuwaacha bila kuwapa a second chance iwe CDM au chama kingine itakuwa siyo kuwatendea haki. ni vizuri wakawaeleze wananchi ni nini walichokuwa wanapigania na waombe nafasi ya kuchaguliwa tena ili wakakamilishe kazi walioianza ya kupambana na ufisadi.

Napenda kuwapongeza madiwani hawa wa CCM kwa maamuzi yao ya kupinga vitendo vya onyonyaji wa mali za umma, Heko kwao sana. Taifa hili tungekuwa na watu kama hawa tangu mapema kwa kila chombo cha maamuzi/utawala Nchi hii ingekuwa imepiga hatua kubwa. Kuoneana aibu kwa maan ya kubebana / kulindana ndiyo yanayotusumbua sasa!

Nyote hapo juu mawazo yenu ni sahihi. Mimi ningependekeza kuwa kwa vile katiba mpya inayoruhusu mgombea binafsi bado haijawa tayari, ni busara kuwapa nafasi madiwani hawa ili wapate kumalizia kipindi chao cha miaka mitano. Lakini pia tukiangalia mifano ya wenzetu Kenya ukiona chama ulichonacho mambo yake yanakwenda kinyume na maadili unuhuru wa kujiengua na kujiunga au kuacha siasa. Vivyo hivyo kwenye nafasi za kuteuliwa kushika madaraka serikalini au taasisi nyingine muhimu.

Wito wangu kwa watanzania wote, ifike mahali tuseme kuwa ukiona mambo hayaendi kama unavyoona inafaa using'ang'anie, ng'atuka! Kwa nini uvumilie maovu! Uongozi bora ni pamoja na kujiuzuru! Hii ni indicator nzuri kwa akina Sita, Mwakyembe, Magufuri. Msing'ang'anie hata pale maamuzi yenu mazuri kwa taifa mnapoona yanapingwa hata hadhalani, achia madaraka utakuwa shujaa zaidi!
 
Uroho wa pesa umewaponza wanatumiwa tu kama wajinga waende hai sasa wakamsaidie mbowe.
 
It is very very interesting kwamba kwa CCM wanaopinga ufisadi ndio hufukuzwa katika chama lakini yale mafisadi, majambazi, majangili, na mauza unga yaliyokubuhu ndio kwanza yanaachwa na hata kupewa nafasi za juu za uongozi katika chama, serikalini, na bungeni.

Hili linashangaza sana! Hivi CCM wanaweza kuwaeleza wananchi sababu ya msingi na inayoingia akili ya kuwafukuza hao madiwani zaidi ya bla bla za kisiasa za akina Nape?

Unanikumbusha kinachomsibu Deo Haule Filikunjombe jembe la Ludewa.

kwa maneno mengine CCM na ufisadi ni damu damu kama yule msanii na mabinti
 
Napenda kuwapongeza madiwani hawa wa CCM kwa maamuzi yao ya kupinga vitendo vya onyonyaji wa mali za umma, Heko kwao sana. Taifa hili tungekuwa na watu kama hawa tangu mapema kwa kila chombo cha maamuzi/utawala Nchi hii ingekuwa imepiga hatua kubwa. Kuoneana aibu kwa maan ya kubebana / kulindana ndiyo yanayotusumbua sasa!

Nyote hapo juu mawazo yenu ni sahihi. Mimi ningependekeza kuwa kwa vile katiba mpya inayoruhusu mgombea binafsi bado haijawa tayari, ni busara kuwapa nafasi madiwani hawa ili wapate kumalizia kipindi chao cha miaka mitano. Lakini pia tukiangalia mifano ya wenzetu Kenya ukiona chama ulichonacho mambo yake yanakwenda kinyume na maadili unuhuru wa kujiengua na kujiunga au kuacha siasa. Vivyo hivyo kwenye nafasi za kuteuliwa kushika madaraka serikalini au taasisi nyingine muhimu.

Wito wangu kwa watanzania wote, ifike mahali tuseme kuwa ukiona mambo hayaendi kama unavyoona inafaa using'ang'anie, ng'atuka! Kwa nini uvumilie maovu! Uongozi bora ni pamoja na kujiuzuru! Hii ni indicator nzuri kwa akina Sita, Mwakyembe, Magufuri. Msing'ang'anie hata pale maamuzi yenu mazuri kwa taifa mnapoona yanapingwa hata hadhalani, achia madaraka utakuwa shujaa zaidi!
Wale hawakuwa na chochote cha maana zaidi ya kutumiwa na upinzani kuivuruga ccm wao ndiyo wachafu na mafisadi wakubwa leo wanasema walikuwa wanazuia wizi,wizi gani huo kama siyo wehu tu wanasiasa wa namna hii hawana msaada kwa watu.
 
Hawa wote waamie CHADEMA kwani ndiko kunakowastahili. Ukiwa CCM ukapinga ufisadi unajenga uadui na viongozi wako kama tunavyojionea kila mahali. Ukiwa CHADEMA unakuwa huru kuikosoa CCM.
 
Back
Top Bottom