CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

Wakisikia hivo watakuja kukanusha kwamba hawajafukuza madiwani wao
 
itakuwa vizuri wakija chadema na kuwapa nafasi ya kugombea
 
Watashindana lakini hawata shinda, wameanza kutimuana wao kwa wao,
 
Utaratibu huu ni angamizo la Demokrasia na ni Jeneza la CDM. Sipenda CDM kuruhusu tena Mateja kama Shibuda. Naamini CDM ina watu wengi wazuri wakuchukua nafasi hizo na Ukatumika utaratibu mzuri wa kuwapata wagombea wasio kuwa na tabia za PANYA, Baba mwizi, mama mwizi, mtoto mwizi, Panya wote wezi, achaneni na tabia hii mbovu ya kuokota MAKOMBO ya ccm. Sipendi kuona CDM ikichukuwa viongozi toka ccm. HAKUNA KIONGOZI ccm alie SALAMA wote wameathirika na VIRUSI vya UFISADI
 
Mhhh!!!! Hawa si ndio watiifu kwa Kagasheki?!!! Na Kagasheki si ndiye mpinanzani mkuu wa CDM jimboni hapo?!!! Hapanahisi tunataka kuandaa 'mashibuda' wengine nane... Hata kama watahamia CDM, mi napendekeza wawe wanachama tu wa kawaida, na wasipewe nafasi za ugombea. Probably CDM walikuwa na mtaji wao huko wa kutosha, wautumie huo huo...
 
- Habari yako mkuu haiko sawa, CCM Mkoa wa Bukoba kwa katiba ya CCM Taifa haina Mamlaka ya Kumfukuza Diwani ni Kamati Kuu ya CCM tu ndiyo yenye huo uwezo, Mkoa unaweza kuwasimamisha tu na kusubiri maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM kama kusimamisha huko ni kwa halali su sio halali, lakini kufukuza ni Kamati Kuu tu ndio yenye huo uwezo, so hii habari haiko sawa.

- Madiwani hao 8 tayari wameshaandika kwa CCM Taifa kuiomba itengue uamuzi huo ambao umefanywa na Viongozi walio upande mmoja wa Vita kubwa ya kisiasa ambayo imekuwa ikiendelea katika Manispaa na jimbo la Ubunge la Bukoba Mjini.

- My Take ni CCM Mkoa wamekurupuka na kujidhalilisha sana na this ishu, kwa sababu bado Madiwani wanaweza kwenda Mahakamani na kubaki na Udiwani wao, uwezekano wa Madiwani hao kufukuzwa na Kamati Kuuu sidhani hata kama upo, kwa kuzingatia sababu za msingi zilizowapeleka CCM Mkoa kuwasimamisha, ni aibu sana kwa Viongozi wa Mkoa wa CCM, tena mmoja Katibu Mkuu wa Mkoa akiwa ni rafiki yangu wa karibu sana, ameniskitisha sana na this!!

Le Mutuz

Le Mutuz bila Shaka Bukoba ni mkoa mpya bila Shaka
 
Kagasheki amechangia sana kudumaza maendeleo ya huko, na hao madiwani bila aibu wakashiriki kum-support kwa kutoshiriki vikao vya maamuzi ya maendeleo kwa ujira wanaoujua wao. Acha wavuliwe uanachama tu, hawakuwa na msaada kwa Kagera.

Unazidi kunishawishi kuwa Kagasheki akiwa mmoja wao nae ni lazima afukuzwe kama kweli wako fair!
 
Hatimaye Bkb tumetoa kishindo na makamanda wote karibuni CDM ili tukawatumikie wanabukoba ,nasema hivi kwani naamini mnayo nia ya dhati ya kuwatumikia watu wenu na kwasababu mmefukuzwa kutokana na kusimamia haki basi furahini katika Bwana make watetea haki wako CDM na CDM iko kwa ajiri yenu

Najiandaa mwezi ujao kurudi home kusaidia harakati hizi mpaka CCM izikwe pale pale Rweru Sea.
 
Hapo kwenye red; sidhani kama kile chama mfu cha Sheikh Ponda kina jeuri hiyo.
upogo wa udini wakati mwingine huwa mnajikuta mnawaharibia wengi...mimi ni CDM lakini huwa sipendezwi na propaganda zenye element za udini ...
 
Unataka kutuambia Ponda ndo Chairman mtarajiwa wa cuf?
 
Hatimaye Bkb tumetoa kishindo na makamanda wote karibuni CDM ili tukawatumikie wanabukoba ,nasema hivi kwani naamini mnayo nia ya dhati ya kuwatumikia watu wenu na kwasababu mmefukuzwa kutokana na kusimamia haki basi furahini katika Bwana make watetea haki wako CDM na CDM iko kwa ajiri yenu

Najiandaa mwezi ujao kurudi home kusaidia harakati hizi mpaka CCM izikwe pale pale Rweru Sea.
 
Thread hii ya kweli, kama ccm inatenda haki, na haitaki kuaminisha watu kuwa inaonea wanyonge, kikao husika kumchukulie hatua Kagasheki pia.
 
Ama kweli tofauti haipo kati ya waliomo madarakani na wanaoyataka madaraka! Siasa imekuwa profession ambaye utaweza kuajiriwa popote. nikifikiri siasa ni utaratibu wa sera na imani ya mtu kwa sera fulani kumbe ni sawasawa na soka unaweza kutoka klabu moja ukaingia nyengine hapo hapo!
 
Habari zilizotufikia punde toka Bukoba zinasema Chama cha Mapinduzi-CCM Mkoani Kagera kimewafukuza madiwani wanane wa chama hicho na kuwavua nyadhifa zote walizokuwa nazo. --- (ITV)

-------------

Katibu wa CCM mkoa amemaliza press conference hi vi punde na kufafanua kuwa Halmashauri Kuu ya Mkoa imemaliza kikao chake hivi punde na kuamua madiwani nane wa manispaa ya Bukoba kufukuzwa katika chama na kufutwa nyadhifa zao za udiwani kutoka na mgogoro uliokuwa ukiendelea.

Majina ya madiwani hao nane waliofukuzwa ni haya yafuatayo:-


  1. Richard Gaspar (Miembeni )
  2. Murungi Kichwabuta (Viti maalum)
  3. Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe)
  4. Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai)
  5. Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga)
  6. Robert Katunzi (Hamugembe)
  7. Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na
  8. Dauda Kalumuna (Ijuganyondo)
Matias Byabato, Chanel TEN, Bukoba --- (BukobaWadau blog)

------------

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera Avelin Mushi, imesema kuwa uamuzi huo umechukuliwa kutokana na chama kujali maslahi ya wananchi tofauti ya watu binafsi.

Mushi amesema kuwa kufukuzwa kwa madiwani hao ni kutokana na mgogoro ulidumu kwa muda mrefu juu ya Mbunge na Meya ambapo Rais Kikwete akiwa ziarani Kagera alitoa agizo la wanachama hao kutoendelea na mgogoro huo lakini maagizo hayo yalipuuzwa.

Pia, amesema kuwa vikao vya chama vimekuwa vikiendelea kwa kufuata kanuni na taratibu kwa kuwaonya juu ya kuhujumu serikali ya CCM kwa kushirikiana na madiwani kambi ya upinzani kutotekeleza maendeleo ya wananchi lakini wahusika wote wamekuwa wakikahidi maagizo ya kuitwa kwenye vikao. (CCM Chama blog)​

Source: CCM-Kagera yawafukuza Madiwani 8 wa manispaa ya Mji wa Bukoba - wavuti.com
 
Kweli jambo usilolijua ni sawa na usiku wa kiza! Tutashuhudia stori nyingi sana za hawa "masalia" wa CCM endapo watajiunga CDM!
 
Ngazi za juu ccm watawalamba miguu, watawaomba wajifanye kukata rufaa nao watawasamehe kwa ahadi yakuwa watambadilisha meya kwa uchaguzi kurudiwa upya nao watakubali baada ya kuombwa sana.....CCM hawana ubavu wakuruhusu hayo, hawana ubavu wa kurudi kwenye uchaguzi mwingine sasa hivi
 
Back
Top Bottom