CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

Ndio utamu wa siasa unapoanzia ....

Arusha matokeo yalikuwa Four o'clock

Kagera je?
 
Mliofukuzwa msikate tamaa endeleeni kupigania haki za wananchi! Na waelimisheni wananchi kujua haki zao za kikatiba.
 
good maamuzi magumu hyo ndio tuna itaji lakini yasiishie hapo hata wle wakubwa wchukulieni maamuzi Kama hayo
 
Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Bw Avelin Mushi amemaliza Press Conf hivi punde na kufafanua kuwa kikao cha Halmasahuri Kuu ya mkoa wa Kagera imemaliza kikao chake hivi punde na kuamua madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kufukuzwa katika chama na kufutiwa nyadhifa za udiwani kutoka na mgogoro uliokuwa ukiendelea.

Waliofukuzwa ni:

1. Richard Gaspar (Miembeni )

2. Murungi Kichwabuta (viti maalum)

3. Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe)

4. Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai)

5. Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga)

6. Robert Katunzi (Hamugembe)

7. Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na

8. Dauda Kalumuna (Ijuganyondo).

Katibu huyo ameongeza kuwa madiwani hao wanaweza kukata rufaa kwa ngazi za juu za chama wakiona hawakutendea haki na kuwa ngazi ya mkoa ina mamlaka ya kufanya hivyo kwa madiwani wa ngazi hizo.

Aidha amesema kwa Bw Yusuph ngaiza amabye ni mwenyekiti wa CCM bukoba,nafasi yake hiyo inasubiriwa ngazi za juu amabazo ndizo zenye mamlaka juu yake(kwa cheo hicho)

Manispaa ya Bukoba ina kata 14 na kati ya hizo kata 4 zinaongozwa na CDM(2) na CUF(2) hivyo kwa Bukoba mjini CCM imebakiza madiwani 3 TU wa kuchaguliwa .kama ifuatavyo
1.Kashai-Amefukuzwa
2. Miembeni-Amefukuzwa
3.Miembe-Amefukuzwa
4.Nyanga-Amefukuzwa
5.Hamugembe-Amefukuzwa
6.Kitendaguro-Amefukuzwa
7.Ijuganyondo-Amefukuzwa
8.(1)Kagondo-Amebaki (CCM) (Meya Amani)
9.(2)Nshambya-Amebaki(CCM)
10.(3)Kahororo-Amebaki(CCM)
11.Bilele-Amebaki(CUF)
12.Kibeta-Amebaki(CHADEMA)
13.Bakoba-Amebaki(CUF)
14.Rwamishenye-Amebaki(CHADEMA)
XXXXXXXXXXXXX

Kujua historia ya chanzo cha yote hapa fungua hapa chini:

Historia ya mgogoro wa kisiasa Bukoba manispaa

Kama ni hivyo inaonesha nguvu ya Kagasheki ndani ya CCM - Bukoba ni questionable na hii ni indicator kuwa mambo yanaweza kumuwia vigumu kurejea katika kati chake mwaka 2015 kupitia ndani ya CCM.
 
Hii inazidi kudhihilisha kuwa katika CCM ukipinga ufisadi wewe ni muasi, umeasi. Hivyo CCM = UNYONYAJI (UFISADI) + KULINDANA. Mifano iko mingi kudhilisha hili na ndiyo maana CCM haijawahi kuchukua hatua dhidi ya wala rushwa na mafisadi. CCM iliwahi kuja na mikakati ya kujivua gamba lakini mkakakati huu haukuchukua hata miezi mitatu na hakuna lolote lililofanyika kukomesha rushwa na ufisadi si tu kwenye chama bali pia katika serikali yake. Gamba limekaukia kwenye mwili. CCM bila Unyonyaji itakufa! ni sawa na kupe bila kunyonya damu hukauka hivyo chama hiki huchukua tahadhari kwa gharama yoyote kulinda ufisadi na rushwa kwa sababu ndiyo roho yake!
 
tatizo wamepingana na kauli ya kikwete, kwani jamaa ni dikteta na wasipokua makini atawapoteza ile mbaya
 
CCM mmeiga kunya kwa tembo (CDM, mtapasuka msamba. hiyo ni BK, wamewakorofisha nshomile mtapata funzo. Amani na Kagesheki wanaogombana hawakufukuzwa, mnawafukuza wasiogombana!
 
Copy, HAMY-D , Njiwa , chama , Chris Lukosi , Ritz, Simiyu yetu

Karibu wakuu kujionea madiliko ya kweli, yanaenda na wakati.

Wakati ni ukuta ukipigana nao utaumia mwenyewe, Tafadhali msipingane na matakwa ya wakati.

Hao jamaa wamekunywa maji ya bendera sidhani kama wanakuelewa ila kwa sababu umesema ukweli hapo chini nadhani watakusikia when it is too late
 
Bila UFISADI CCM Itakufa. Itapata wapi fedha ya kunua khanga, kofia ,chumvi, sukari, pombe za kienyeji, kusafirisha wapiga debe, etc?
 
Kama wakishindwa kusimamia maamuzi yao kama CHADEMA walivyofanya Arusha,basi CCM itakuwa imeonyesha udhaifu wa hari ya juu!

Mkuu maamuzi gani?
Maamuzi yametolewa na ngazi ya Mkoa, wahusika wanafasi ya kukata rufaa ngazi za juu na Chama kikiona kuna namna nyingine ya kutatatua tatizo zaidi ya kuwafukuza kinaweza kubatilisha maamuzi....thats demekrasi
 
Ccm hata ukitangazwa uchaguzi leo wanashinda hilo halina shaka.
 
ccm kwisha habari mnaiga chadema arusha ngoja tuone
 
Hapa CCM wanajaribu kuwatisha hao madiwani wao lakini kwa uhakika kabisa hawana ubavu wa kuwafukuza! Kinachofanyika hivi sasa ni kuwavunja nguvu ili warudi kuomba msamaha na kurudishiwa uanachama wao kwa masharti!!! na ndiyo maana katibu huyo amehitimisha kwa kusema wanayohaki ya kukata rufaa ngazi ya juu!!. Hali ya kisiasa kwa sasa haiwapi jeuri CCM kufukuza madiwani 8 hata kidogo!!. Stay tuned!

100% sure Mkuu! Hii ni janja ya kuwatisha ili walegeze msimamo na ninavyowajua mwisho wa siku wataongea lugha moja, kumbuka kampeni ya kuvuana magamba iliishia wapi?
 
Chama cha mapinduzi kimewafukuza madiwani wake bukoba. Hili ni pigo kwani ninaamini hili litawagharimu utakapo itishwa uchaguzi mdogo lazima chadema watachukua baadhi ya kata na hivyo hasira ya mkizi nafuu ya mvuvi, kimsingi madiwani walikua wanasimamia haki je kuungana na chadema na cuf kudai haki ndio wamefanya kosa bila shaka yoyote chadema watachukua madiwani wengi uchaguzi mdogo utakapoandaliwa labda kipofu ndo hawezi kuliona hili. Mtu anatetea haki unamfukuza unataka atetee ufisadi hapa ccm mmechemka sana mtakuja kukumbuka maamuzi mabovu kama haya
 
Kuna habari kwamba Ccm Lumumba wamesitisha uamuzi wa mkoa na sasa wanajiandaa kutoa tamko,
Machale yamewacheza, na pia siyo kawaida kwa Ccm kuwajibishana
 
Back
Top Bottom