CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

Yes! hii nimeipenda Magamba wameiga kunya kwa Tembo acha wapoteze viti 8. jeuri ya kuvitetea Magamba hawana tena.
 
Madiwani 8 ni mtaji tosha!!!

Lakini tuache utani kufukuza madiwani 8 si jambo dogo!! Kwa mara nyingine siasa zinaenda kutuingiza katika gharama za kijinga kabisa!!
Kaka mkubwa kuliko pesa zetu kutumika kununua makahaba Dodoma ni bora zitumike kukuza demokrasia...hizo ndizo gharama na changamoto zenyewe za demokrasia
 
Mkuu Ritz, ina sikitisha kuona chama kikuu cha upinzani nchini (CHADEMA) kuwa na makao makuu kwenye nyumba ya kupanga ila viongozi wake kutembelea mashangingi (VX V8) kwa pesa ya chama.
Mmeshikwa pabaya jibuni hoja iliyopo kwanza baadae tutahamia kwenye hiyo nyumba mnayodhani ni issue.kuitetea ccm ni lazima uwe na akili za maiti.
 
Huu hapa ndiyo UFISADI wa MEYA ANATORY:
CCM na tabia ya kuabudu miungu watu!!

Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na taarifa mbalimbali za mzozo kati ya meya huyu na mbunge wa jimbo la bukoba mjini Balozi Khamis Kagasheki.

Kwa ambao hawajui sababu ,chanzo undani wa mgogoro huu wa kisiasa sasa kupitia thread hii watajua kila kitu,siasa za bukoba kuelekea 2015 na mambo kadha wa kadhaa kuhusu wanasiasa hawa lakini hasa huyu ANATORY AMAN ni nani?.


Baadaye nitakuwekea historia yake kuanzia alikozaliwa,alikosoma,amefanya nini mabaya na mazuri yake lengo kuu ni kutaka kuweka kumbukumbu sawa kwa wale ambao wanajifanya kuchambua siasa za huyu bwana.

Kupitia hii thread nitachambua na kuweka hapa mambo yafuatayo:

i)Alivyo FISIDI Mradi wa viwanja Bukoba
ii)Alivyo FISIDI Mradi wa Soko Bukoba
iii)Alivyo FISIDI Mradi wa ujenzi wa stendi kuu ya mabasi bukoba mjini
iv)Mengine kuhusu Anatory Aman.
v)kuweka nyaraka mbalimbali hapa JF

i)Alivyo FISIDI Mradi wa viwanja Bukoba
Kwanza mapema kabla ya uongozi wa Anatory aman ,Halmasahuri ya Manispaa ya Bukoba iliandaa mradi wa kupima viwanja vya wananchi wa manispaa ya bukoba vipatavyo elfu 5 .Halmashauri iliomba fedha kutoka wizarani kutekeleza mradi huo lakini wizara haikuwa na fedha.Mradi huu ulipanga kutumia sh 2.6 bilioni.

Baada ya meya kuingia madarakani mwaka 2010 mchakato ulibadilika kwani yeye aliamua kutafuta mtu wa kuwapatia fedha kutekeleza mradi huo kama ilivyokuwa imepangwa lakini safari hii aliomba mkopo kutoka TIB ambapo katika kikao kimojawapo cha madiwani alidai kupata mtu wa kuisaidia manispaa kupima viwanja hivyo kwa sh 2:4 bilioni kwamba itasaidia kuokoa sh milioni 200 iwapo wangetumia wizara.

Lakini baadaye bila maandishi alidai kwenye kikao cha madiwani kwamba TIB wameomba ziongezwe kutoka 2.4 bilioni hadi 2.9 bilioni na kuwa TIB walitaka walipwe sh 3.5 bilioni baada ya kumaliza kazi ya kupimisha viwanja na kuuza.
Hapa milioni 500,000 hazijukani zilipo

Viwanja vya kupima mali ya nani?
Kwa kuwa manispaa ya bukoba haikuwa na viwanja MEYA Anatory aman aliamua kuanza kununua viwanja na mashamba ya wananchi kwa gharama ya sh 300-400 kwa square meter moja.Kwa mtindo huo walinunua viwanja vya wananchi kwa makubaliano kwamba katika mchakato wa kuvobresha kwa kuweka barabara ,umeme na maji basi wangewauzia wananchi hao hao kwa riba kidogo,wananchi walikubali.

Baada ya kununua viwanaj vyao sasa halmshauri imepima viwanja kwa kushirikiana na TIB lakini inauza square meter moja kwa sh kati ya 3500 na 4000 hivyo waliofanikiwa kununua viwanja hivi ni matajiri na watu wenyer kipato cha wastani.

Bei ya kushika kiwanja ilikuwa ni sh 210,000 hadi 510,000 na iwapo mhusika angepata basi wakati wa kuilipa zinakatwa depost zake.hapa halmshauri iliingiza wastan wa jumla ya sh 170 milioni (kwa walilipia sh 350,000) tu ambazo MEYA Anatory aman aliziingiza katika account t(fixed account) ya kuzaa katika benki moja nchini.fedha hizi zimekaa humo kwa miezi mitano kabla ya kuanza mchakato wa kuanza kugawa viwanja hadi sasa nusu ya fedha hizi bado ziko kwenye hiyio account na taarif ya meya ni kuwa waliiomba waendelee kusubiri mchakato mpya unaoendelee.HAPA FEDHA YA WANANCHI INAENDELEA KUZALISHWA TU.



Ngoja nipumue kidogo naendelee…………………..



Nb:Anatory Aman ni mmojwapo wa member humu JF hivyo nafikiri atajitokeza kujibu baadfhi ya hoja hapa ili watanzania wajue mbivu na mbichi.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
ah ah kwa raha, na ninavowajua wahaya huwa hawatikisi masikio na watafanya kweli kwa kuikataa ccm hadharani

Mchezo unaisha magoli ni 8-0

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Kwa kweli CCM inabidi waishukuru sana CHADEMA, ndio wamewafundisha mambo haya ya kufukuzia mbali wanachama ambao hawana tija kwa chama hata wakiwa viongozi. Anyway, ninawapongeza CCM kwa ukomavu na uthubutu huu, you are growing now!
 
Kwenye sakata hili kuna pande mbili kila moja likituhumu lenzake:

1. Upande mmoja ukiongozwa na Kagasheki na hao wabunge waliofukuzwa wakiwa wafuasi wake pamoja na mbunge wa viti maalum Chadema, na baadhi ya madiwani wa kuteuliwa chadema na Cuf

2. Ukiongozwa na Meya Amani akiungwa mkono mkono na madiwani nane wa CHAMA CHA MAPINDUZI, madiwani wawili wa CHADEMA, diwani mmoja wa CUF, wabunge wawili wa viti maalum CHAMA CHA MAPINDUZI, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Viongozi wa juu wa mkoa CHAMA CHA MAPINDUZI na baadhi ya viongozi wa CHAMA CHA MAPINDUZI wilaya!

Who are the real fisadis in this saga? Na kundi lipi liko sahihi?


WEL SPOKEN, UYU NDO ANAJUA NI NINI KIMEFANYIKA BUKOBA, APO BABITO KAGASHEKI IMEKULA KWAKE, KWANI HAO NI WAFUASI WAKE, SASA NI MUDA MUAFAKA HII FAMILIA YA KAGASHEKI IKAHAMIA CHADEMA, KWANI KAGASHEKI NI MTU SAFI KATIKA BWAWA LA WAUAJI ccm. KAGASHEKI KARIBU CHADEMA TUIOKOE BUKOBA YETU
 
Kwa kweli CCM inabidi waishukuru sana CHADEMA, ndio wamewafundisha mambo haya ya kufukuzia mbali wanachama ambao hawana tija kwa chama hata wakiwa viongozi. Anyway, ninawapongeza CCM kwa ukomavu na uthubutu huu, you are growing now!


Kama kuwafukuza wanaopinga ufisadi na kuwaacha mafisadi ndani ya chama ndio ku-grow, it's better to shrink!
 
Badala ya kufukuza fisadi meya moja eti wanafukuza madiwani nane wapigania utawala bora. Pambafu kweli! Eti kosa lao kuunga hoja ya wapinzani badala wangeegemea kuona kama meya hajatumia madaraka yake vibaya. Inji hii bana wacha tu; sasa imekua inaongozwa na fisadis na vipepari uchwara ambavyo ni just thieves. Ngojeni sasa wahamie cdm kama ulimi haujawatoka.
 
Tunaenda tena kwenye Uchaguzi wa Udiwani wa kata 8.
Huu mgogoro nilishausahau, ulikuwa kama Episode au Tamthilia.

- Habari yako mkuu haiko sawa, CCM Mkoa wa Bukoba kwa katiba ya CCM Taifa haina Mamlaka ya Kumfukuza Diwani ni Kamati Kuu ya CCM tu ndiyo yenye huo uwezo, Mkoa unaweza kuwasimamisha tu na kusubiri maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM kama kusimamisha huko ni kwa halali su sio halali, lakini kufukuza ni Kamati Kuu tu ndio yenye huo uwezo, so hii habari haiko sawa.

- Madiwani hao 8 tayari wameshaandika kwa CCM Taifa kuiomba itengue uamuzi huo ambao umefanywa na Viongozi walio upande mmoja wa Vita kubwa ya kisiasa ambayo imekuwa ikiendelea katika Manispaa na jimbo la Ubunge la Bukoba Mjini.

- My Take ni CCM Mkoa wamekurupuka na kujidhalilisha sana na this ishu, kwa sababu bado Madiwani wanaweza kwenda Mahakamani na kubaki na Udiwani wao, uwezekano wa Madiwani hao kufukuzwa na Kamati Kuuu sidhani hata kama upo, kwa kuzingatia sababu za msingi zilizowapeleka CCM Mkoa kuwasimamisha, ni aibu sana kwa Viongozi wa Mkoa wa CCM, tena mmoja Katibu Mkuu wa Mkoa akiwa ni rafiki yangu wa karibu sana, ameniskitisha sana na this!!

Le Mutuz
 
KITU ccm kinaenda anticlockwise ...
wakati sisi tunapinga UFISADI,wenzetu wanawakingia kifua mafisadi....what a hell?
 
Last edited by a moderator:
Inawezekana uchaguzi usifanyike mapema ili kuinusuru ccm kipigo cha man u kwa Arsenal ile 8-0. Nadhani tume itawabeba ccm kuchelewesha uchaguz kwa makusudi...sidhani kama madiwani hawa wana kosa lolote...nawapongeza hawa madiwani wa ccm kuonesha kuwatetea wanachi ila magamba hawataki hcho kitu kbs
 
Mkuu, Nashukuru kwa ufafanuzi mzuri,
maana Chaguzi hizi zinamaliza pesa tunazolipa kodi.
Nimekusoma pia kwenye Blog yako ya " Le Mutuz".


- Habari yako mkuu haiko sawa, CCM Mkoa wa Bukoba kwa katiba ya CCM Taifa haina Mamlaka ya Kumfukuza Diwani ni Kamati Kuu ya CCM tu ndiyo yenye huo uwezo, Mkoa unaweza kuwasimamisha tu na kusubiri maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM kama kusimamisha huko ni kwa halali su sio halali, lakini kufukuza ni Kamati Kuu tu ndio yenye huo uwezo, so hii habari haiko sawa.

- Madiwani hao 8 tayari wameshaandika kwa CCM Taifa kuiomba itengue uamuzi huo ambao umefanywa na Viongozi walio upande mmoja wa Vita kubwa ya kisiasa ambayo imekuwa ikiendelea katika Manispaa na jimbo la Ubunge la Bukoba Mjini.

- My Take ni CCM Mkoa wamekurupuka na kujidhalilisha sana na this ishu, kwa sababu bado Madiwani wanaweza kwenda Mahakamani na kubaki na Udiwani wao, uwezekano wa Madiwani hao kufukuzwa na Kamati Kuuu sidhani hata kama upo, kwa kuzingatia sababu za msingi zilizowapeleka CCM Mkoa kuwasimamisha, ni aibu sana kwa Viongozi wa Mkoa wa CCM, tena mmoja Katibu Mkuu wa Mkoa akiwa ni rafiki yangu wa karibu sana, ameniskitisha sana na this!!

Le Mutuz
 
[font=&quot]ni baada ya vikao na majadiliano ya muda mrefu yaliyofanywa kwa usiri mkubwa na viongozi wa chadema taifa kwa kushirikana na viongozi wa chadema mkoa wa kagera kwa lengo la kuwashawishi madiwani wa ccm kuendelea na mgomo wao dhidi ya vitisho wa wakuu wa ccm huku lumumba kwa kuwaahidi kuwapokea na kuwapa nafasi ya kugombea kata husika ikiwa watafukukuzwa ndani ya ccm.kwa mujibu wa nyaraka zilizopatikana madiwani hao wameagizwa kutoyakatia rufaa maamuzi ya ccm mkoa ya kuwavua uanachama mahakamani au ngazi za juu za ccm kwa luwa watapewa nafasi za kugombea kata husika bila kipingamizi.[/font]
[font=&quot]hili linakuja baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu kati ya madiwani 8 wa ccm walioamua kuuasi uongozi wa ccm huko kagera na kuamua kuungana wa wapinzani yaani cuf na chadema kupinga mipango ya ufisadi inayoratibiwa na meya wa manispaa ya bukoba akishirikianna na baadhi ya viongozi wa ccm mkoa na taifa wenye masilahi katika ufisadi huo kwa kutumia kampuni nyingi zilizoibuliwa kama uyoga kwa ajli ya kula fedha za manispaa.[/font]
[font=&quot]kinachoendela kwa sasa ni kuwa kuna mkurugenzi mmoja wa chadema aliyetumwa kagera kwa ajili ya kukamilisha mpango huo mapema usije ukatekwa nyara na cuf. [/font]
[font=&quot]mpango huu umelenga kuiangamiza ccm ndani ya kanda ya ziwa kuelekea uhaguzi mkuu 2015.tusubiri tuone[/font]
 
mimi nawashauri hawa madiwani wasiende mahakamani waje CHADEMA wajiunge waende kuchukua kata zao tena warudi kuwafukua mapanya buku hapo halmashauri haraka sana
 
Sijui kwanini hawajamfukuza Sitta mpaka sasa... kila kukicha anakiponda chama chake ...
 
Back
Top Bottom