tayari hizo kata ni zetu kilainiiiii,M4C piga kambi huko mapema,ila hao madiwani ni wazalendo nashauri wajigeuze waje wavalishwe magwanda wagombee kwa tiketi ya chama chetu cdm,mnaonaje wadau?
ni baada ya vikao na majadiliano ya muda mrefu yaliyofanywa kwa usiri mkubwa na viongozi wa chadema taifa kwa kushirikana na viongozi wa chadema mkoa wa kagera kwa lengo la kuwashawishi madiwani wa ccm kuendelea na mgomo wao dhidi ya vitisho wa wakuu wa ccm huku lumumba kwa kuwaahidi kuwapokea na kuwapa nafasi ya kugombea kata husika ikiwa watafukukuzwa ndani ya ccm.kwa mujibu wa nyaraka zilizopatikana madiwani hao wameagizwa kutoyakatia rufaa maamuzi ya ccm mkoa ya kuwavua uanachama mahakamani au ngazi za juu za ccm kwa luwa watapewa nafasi za kugombea kata husika bila kipingamizi.
hili linakuja baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu kati ya madiwani 8 wa ccm walioamua kuuasi uongozi wa ccm huko kagera na kuamua kuungana wa wapinzani yaani cuf na chadema kupinga mipango ya ufisadi inayoratibiwa na meya wa manispaa ya bukoba akishirikianna na baadhi ya viongozi wa ccm mkoa na taifa wenye masilahi katika ufisadi huo kwa kutumia kampuni nyingi zilizoibuliwa kama uyoga kwa ajli ya kula fedha za manispaa.
kinachoendela kwa sasa ni kuwa kuna mkurugenzi mmoja wa chadema aliyetumwa kagera kwa ajili ya kukamilisha mpango huo mapema usije ukatekwa nyara na cuf.
mpango huu umelenga kuiangamiza ccm ndani ya kanda ya ziwa kuelekea uhaguzi mkuu 2015.tusubiri tuone
Mkuu adolay wameanza kufukuzana baada ya uwindaji wa tembo kuwa mgumu?
It is very very interesting kwamba kwa CCM wanaopinga ufisadi ndio hufukuzwa katika chama lakini yale mafisadi, majambazi, majangili, na mauza unga yaliyokubuhu ndio kwanza yanaachwa na hata kupewa nafasi za juu za uongozi katika chama, serikalini, na bungeni.
Hili linashangaza sana! Hivi CCM wanaweza kuwaeleza wananchi sababu ya msingi na inayoingia akili ya kuwafukuza hao madiwani zaidi ya bla bla za kisiasa za akina Nape?
Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Bw Avelin Mushi amemaliza Press Conf hivi punde na kufafanua kuwa kikao cha Halmasahuri Kuu ya mkoa wa Kagera imemaliza kikao chake hivi punde na kuamua madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kufukuzwa katika chama na kufutiwa nyadhifa za udiwani kutoka na mgogoro uliokuwa ukiendelea.
Waliofukuzwa ni:
1. Richard Gaspar (Miembeni )
2. Murungi Kichwabuta (viti maalum)
3. Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe)
4. Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai)
5. Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga)
6. Robert Katunzi (Hamugembe)
7. Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na
8. Dauda Kalumuna (Ijuganyondo).
Katibu huyo ameongeza kuwa madiwani hao wanaweza kukata rufaa kwa ngazi za juu za chama wakiona hawakutendea haki na kuwa ngazi ya mkoa ina mamlaka ya kufanya hivyo kwa madiwani wa ngazi hizo.
Aidha amesema kwa Bw Yusuph ngaiza amabye ni mwenyekiti wa CCM bukoba,nafasi yake hiyo inasubiriwa ngazi za juu amabazo ndizo zenye mamlaka juu yake(kwa cheo hicho)
Manispaa ya Bukoba ina kata 14 na kati ya hizo kata 4 zinaongozwa na CDM(2) na CUF(2) hivyo kwa Bukoba mjini CCM imebakiza madiwani 3 TU wa kuchaguliwa .kama ifuatavyo
1.Kashai-Amefukuzwa
2. Miembeni-Amefukuzwa
3.Miembe-Amefukuzwa
4.Nyanga-Amefukuzwa
5.Hamugembe-Amefukuzwa
6.Kitendaguro-Amefukuzwa
7.Ijuganyondo-Amefukuzwa
8.(1)Kagondo-Amebaki (CCM) (Meya Amani)
9.(2)Nshambya-Amebaki(CCM)
10.(3)Kahororo-Amebaki(CCM)
11.Bilele-Amebaki(CUF)
12.Kibeta-Amebaki(CHADEMA)
13.Bakoba-Amebaki(CUF)
14.Rwamishenye-Amebaki(CHADEMA)
XXXXXXXXXXXXX
Kujua historia ya chanzo cha yote hapa fungua hapa chini.
Historia ya mgogoro wa kisiasa Bukoba manispaa
Baadaye nitaingiza video.
Arusha ndio zilikuwa za kijinga kabisaMadiwani 8 ni mtaji tosha!!! Lakini tuache utani kufukuza madiwani 8 si jambo dogo!! Kwa mara nyingine siasa zinaenda kutuingiza katika gharama za kijinga kabisa!!
Minor Correction, ni CCM Mkoa wa Kagera kwani Bukoba ni makao makuu ya Mkoa wa Kagera- Habari yako mkuu haiko sawa, CCM Mkoa wa Bukoba kwa katiba ya CCM Taifa haina Mamlaka ya Kumfukuza Diwani ni Kamati Kuu ya CCM tu ndiyo yenye huo uwezo, Mkoa unaweza kuwasimamisha tu na kusubiri maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM kama kusimamisha huko ni kwa halali su sio halali, lakini kufukuza ni Kamati Kuu tu ndio yenye huo uwezo, so hii habari haiko sawa.
- Madiwani hao 8 tayari wameshaandika kwa CCM Taifa kuiomba itengue uamuzi huo ambao umefanywa na Viongozi walio upande mmoja wa Vita kubwa ya kisiasa ambayo imekuwa ikiendelea katika Manispaa na jimbo la Ubunge la Bukoba Mjini.
- My Take ni CCM Mkoa wamekurupuka na kujidhalilisha sana na this ishu, kwa sababu bado Madiwani wanaweza kwenda Mahakamani na kubaki na Udiwani wao, uwezekano wa Madiwani hao kufukuzwa na Kamati Kuuu sidhani hata kama upo, kwa kuzingatia sababu za msingi zilizowapeleka CCM Mkoa kuwasimamisha, ni aibu sana kwa Viongozi wa Mkoa wa CCM, tena mmoja Katibu Mkuu wa Mkoa akiwa ni rafiki yangu wa karibu sana, ameniskitisha sana na this!!
Le Mutuz
acha ukorofi usio na tijaHapo kwenye red; sidhani kama kile chama mfu cha Sheikh Ponda kina jeuri hiyo.
safi sana karibuni chadema na kata zenu ziko wazi
Oooh, Katonda! CCM yafwire nira. Byona bushai.