Maneno yako sawa kabisa mkuu wangu isipokuwa unasahau kwamba hawa Wabunge wa Zanzibar walipewa maagizo hayo kuhusiana na jambo moja tu - Wamchague nani kuwa Spika for the interest ya CUF na WaZanzibar , kwani kupitia CCM ndio wamepata huo ulaji wa kuunda kwa serikali ya mseto. Na Yawezekana hofu yao kubwa wakimchagua spika wa Chadema anaweza kuwakwamisha ktk baadhi ya makubaliano walofanya na CCM kuhusiana na mabadiliko yaliyokwisha tangulia iwe muundo wa serikali, katiba na mengine tusoyajua. Kifupi, tumeona CUF wakiwapa support CCM ktk swala linalogusa maslahi ya Zanzibar na utetezi wa makubaliano haya wameujengea ukuta kumchagua Spika wa CCM. Na ndio maana nikasema tusiwaliaumu sana CUF kwani wao sasa hivi wanatafuta Ulaji ingawa picha nzima inaonyesha wajiunga na CCM kwa maslahi ya Wazanzibar.Ndugu Mkandara,
siamini kuwa wabunge wa CUF wa Zanzibar wanaweza wakatengana na wenzao wa Bara; hili jamani tuwe realistic. Yaani ni kuunda kambi ambayo unajua haitkuwa na mwelekeo ili mradi tu huko nje uonekane umeungana? Wabunge wa CUF kutokea Zanzibar ndo wanaoifanya CUF iwe na nguvu ndani ya Bunge la jamhuri ya muungano. Wabunge wa bara ni wawili tu!! Sasa Chadema iungane na CUF kwenye kambi ya upinzani wakati CUF wameshapewa maelekezo kutoka Zanzibar kuwa waiunge mkono CCM. Yaani Chadema iseme, aaa unajua ninyi CUF ni upinzani, hata kama mnaiunga mkono CCM, tuwe kambi moja halafu wale wabunge wenu wawili wa bara ndo wasiwe wanaiunga mkono CCM! Kweli unaamini hii ni practical? Yaani wabunge wa CUF wana maelekezo kutoka kwenye chama chao yanayowataka waiunge mkono CCM, halafu bado unaona kuna hoja, kwa mfano ya katiba, ambayo unaamini CUF wataiacha CCM waiunge mkono Chadema.
Ohh, as much as tunapenda kuona nguvu ya upinzani ikiongezeka, tuwe wakweli na tuangalie mambo kwa hali halisi. CCM wameshanusa harufu ya kushindwa, wako tayari kutoa sacrifice, na sacrifice hiyo ni kuwa embrace baadhi ya wapinzani. Haikuwa rahisi kwa Mahafidhina wa uingereza kukubali kuungana na waliberali. Lilikuwa jambo gumu, lakini when madaraka is at stake, lolote laweza kutokea! CUF wameambiwa kutoka Zanzibar (ilipo ngome yao) kuwa waiunge mkono CCM; kwa hivyo voting zao zote itakuwa ni pro CCM. Itakuwa ni kujaribu kuzoa maji yaliyomwagika kwa Chadema kujaribu kuwang'ang'ania CUF. Hata mie sioni haja ya kufanya hivyo, unless Chadema nayo ikubali kuwa itapiga kura zake kuiunga mkono CCM. Hapo tutakao umia ni wapiga kura, kwani mtawala atakuwa amejihakikishia kutawala bila hata kelele.
Kwa numbers zilivyo huko bungeni, bado upinzani ni noise tu kwa hapa Tanzania. CCM bado wanaweza wakafanya chochote bila kuhitaji mpinzani yeyote. Lakini noise zikiwa genuine, itakuwa ngumu kwa CCM kutawala kwa mtindo ule ule wa business as usual. Tumeona mfano wa mambo ya EPA na Richmond. Ingawa bado wahusika wakubwa wako at large, lakini noise za wapinzani zilisaidia angalau kuwafunua macho wabongo walio usingizini. Kwa hiyo, tunahitaji upinzani genuine, hata kama utakuwa na wabunge wachache, cha muhimu uwe upinzani wa kweli usio na chembe au ukakasi wa kushirikiana na utawala. Only then nguvu ya hoja itasimama. Upinzani nusu, utawala nusu (Status ya CUF leo) haiwezi kuwa kitu tunachotamani kuona wengi.
Sasa yapo maswala ya msingi na ya kimuungano ambayo wao wanaweza kusimama nasi kwa kupata maagizo hayo hayo. Ifahamike tu kwamba miaka mitano iliyopita Chadema ilikuwa na wabunge wangapi?. Kwa nini wao wasijiulize maswali kama haya hali Chadema haina mbunge hata mmoja zanzibar au ndio tunarudi palepale kwamba wao hawakuwa na hesabu ya wabunge wa kutosha kuunda kambi ya Upinzani.. Na kama ndivyo hivyo basi wangeacha kabisa kusiwekpo na kambi ya Upinzani maadam wao hawataki kuwa na Chadema ambao muda wote wamekuwa wapinzani wa Tanzania au Zanzibar kujiunga na OIC.
Lakini haikuwa hivyo, waliunda kambi hiyo kwa maslahi ya Watanzania na Chadema wakapata mahala pa kujivunia masifa ambayo ndio sababu kubwa ya leo chama hiki kuwa hapa kilipo. Wangetaka wangempiga chini Dr.Slaa au Zitto kutokuwa wasemaji wa Upinzani na wakaweka watu wao. Na wakati wote huo CUF haikuwa na mbunge hata mmoja toka bara kama sikosei kwa hyo hawakuwa na sababu ya kujali kabisa maslahi ya Chadema kama chama.
Tena basi CUF hawakunufaika na lolote zaidi ya kuona maswala yao mengi yakitupwa nje na hata hapa JF tumekuwa wapinzani wakubwa ktk maswala mengi ya CUF kuhusu matakwa ya WaZanzibar na yanayohusu muungano. Hivyo inawezekana pia kuwa hizi ndio sababu zilizowasukuma CUF kujiunga na CCM ili wapate japo ulaji maana wameshindwa kupewa ushindi walostahili toka mwaka 1995.
Na tumejenga uhasama mkubwa kiasi kwamba Bara na Zanzibar zimekuwa nchi mbili tofauti kabisa inapofikia maswala mengi ya muungano japokuwa Chadema kama chama inawaunga mkono lakini wananchi wengi wa bara hawakubaliani na matakwa ya CUF kuhusiana na Zanzibar.
Kweli kabisa Tanzania leo hatuna Upinzani na CCM wataendelea kufanya wanayotaka kufanya ikiwa Upinzani hauwezi kujijenga lakini kumbuka tu moja ya njia bora ya kujenga Upinzani huanzia ktk ushirika unaojengwa na sio ushirika unaovunjika. Leo hii Upinzani wapo mbali zaidi kuliko mwaka jana au juzi kwa sababu tumevunja ushirikiano nje ya Bunge na sasa tumevunja bungeni hivyo safari ya kupata Upinzani wa kweli inazidi kuwa ndefu zaidi. Kwa mafanikio ya Chadema tunasahamu kwamba hata CUF wameongeza viti bungeni pia na vyama vingine vimepata kiti bungeni hali bunge lililopita walikuwa hawana kitu, kifupi kila chama kimegain kutoka CCM baada ya kushuka toka asilimia 80 hadi 61. Kila chama cha Upinzani kinajiona kimeongeza nguvu zake mwaka huu.
Na kibaya zaidi kutokana na kiburi cha Watanzania kila chama kitajiona wao wanaweza kufika mahala pasipo mwingine na hakika watakao umia zaidi ni wananchi. Haya nimesikia Mafisadi wanarudi kupitia viti maalum, hivi kweli kuna tegemeo lolote ambalko wewe una hakika Chadema watafanikiwa bungeni.. Watapiga kelele zipi ikiwa maswala yote yatafagiliwa uvunguni? kwenye magazeti na vyombo vya habari ambayo CCM wanaweza wafungia na wakapoteza biashara zao!
Ni wapi sauti ya mwananchi itasikika kesho? Aaaah mkuu wangu nitaonekana mbishi sana hivyo tuyaache kama yalivyo lakini kumbuka tu nachoweza kusema ni kwamba Upinzani bungeni siku zote hauna maana mtakubaliana kwa kila kitu baina yenu wenyewe. Kila mmoja wenu ndani ya Upinzani ana agenda zake kuwakilisha wananchi wake na sio lazima nyote mpigiane kura isipokuwa mnaunda Upinzani against chama tawala na yapo maswala Chadema inaweza kuwa against CUF kama ilivyotokea ktk swala la Spika lakini kipaumbele ni kuweka Upinzani kwa chama tawala kwa manufaa ya wnaanchi.