CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

Kwani kutupa karatasi dhambi? watu wanatupa kond..... mbona hawaulizwi bana?

Kwani wale wazee wa mabwepande wameiona!
 
mimi ni mwana ccm wa kudumu. nashangaa chama chetu kinachukiwa kana kwamba ni chama cha kighaidi wakati ndio chama kilichotuletea uhuru toka kwa mkoloni. naona kujua sababu kuu zinazoifanya chama mama kuchkiwa kiasi hiki na wananchi hasa vijana? nawasilisha.
 
Ufisadi,uzembe,uzinzi,wizi,ushenzi,ujinga,ulimbukeni,uzandiki,uharamia,ubabe,kiburi,ushetwani,ukahaba,uchawi,dhuruma,ghilba,shirki,dharau, uganga uganga, ujanja ujanja, utapeli,ulimbukeni,uhasherati,fitna,majungu,uongo,ulevi,ulafi,uroho,ulaghai, udhiafu na kulindana kwa wazi kunakofanywa na viongozi kiasi cha kusababisha kuwa na tofauti kubwa sana ya kimaendeleo ya kiuchumi kati ya wanasiasa na wananchi wa kawaida, zaidi ni kauli za kebehi zinazotolewa na viongozi wa ccm pale wanapohojiwa juu ya namna wanavyoendesha nchi.

Hii inasababisha chuki kubwa sana hasa baada ya wananchi kutambua kwamba ni wao ndio wenye maamuzi ya mwisho juu ya chama hiki kuendelea kuongoza dola yetu au la!
 
tena nikiona jina lake tu napata allergy haraka mwili mzima! plz sema magamba at least, usikitaje kabisa, nakichikiajeeeeee?? uwiiiiiiiii cjui kitatoka lini madarakani, hiyo siku SITALALA!! NITASHINDA KANISANI KUIMBA NYIMBO NA MASIFU KUMSIFU MUNGU! I HATE CCM! PERIOD!
 
mimi ni mwana ccm wa kudumu. nashangaa chama chetu kinachukiwa kana kwamba ni chama cha kighaidi wakati ndio chama kilichotuletea uhuru toka kwa mkoloni. naona kujua sababu kuu zinazoifanya chama mama kuchkiwa kiasi hiki na wananchi hasa vijana? nawasilisha.

Kwa sababu Watanzania wengi wanafahamu fika kwamba matatizo mengi ya nchi yetu yanasababishwa na magamba kwa kudai nchi yetu ni maskini, kitu ambacho si kweli na pia kuendeleza ngojera zao "Serikali haina uwezo" huku wao wakiendeleza matanuzi ya kufa mtu mwaka nenda mwaka rudi.
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana Chama chetu tawala na vyama vya upinzani. Watanzania tuna wakati mgumu kuliko tunavyofikia kwasababu kubwa mbili :

(1) CCM ina watu wengi wasio na uzalendo wala sera: CCM wana viongozi wengi sana waliozoea utamaduni wa kwenda kwenye madaraka kwasababu ya kujinufaisha kibinafsi. Pamoja na kupelekwa mahakamani tumeendelea kuona mawaziri wakitafuta kila njia kutumia pesa za budget za maendeleo ya wananchi kila mara. Hili jambo lilikuwa kuanzia wakati wa Mwinyi hadi sasa. CCM kitu kimoja kikubwa wana tatizo ya kutokuwa na mawazo mapya hasa ya vijana na kutokuwa na uzalendo. Kwa hili ni vigumu kupata mabadiliko CCM. Kikubwa hawana hata sera nzuri.
(2)Upinzani hauna sera: Tanzania tuna upinzania wenye mwamko mkubwa lakini sijawahi kusikia sera za maana za maendeleo zenye kubadilisha nchi. Ndiyo rushwa ni sababu kubwa sana ya kukokuwa na maendeleo lakini kuna vitu vingi sana ambavyo upinzania ingeweza kuonyesha kama sera. Nilijaribu kuwasikiliza vijana wenzangu wa Chadema wakina Mwanyika na Zitto nata wa CCM Nape na Makamba sijawahi kusikia sera hata moja ya maana ni ushabiki tu. Mfano Zitto alikuwa anasema walimu waongezewe mshahara nikaanza kumuuliza unataka pesa itoke wapi kwenye budget, Je utabadilisha vipi mfumo wa sasa na akanikimbia kwenye hili. Tatizo ni kwamba hawa vijana wote wa CCM na upinzania hawana uzoefu wa sera zaidi ya kusoma vitabu na historia. Mimi kijana ambaye ni msomi na nimepigika huku USA na nimefanya kazi kwenye sehemu tofauti ninaweza kuwa na Mawazo ya kutatua mfumo kuliko mwanasiasa wa Tanzania lakini hawaweza kunisikiliza kwasababu mimi sijulikani na sio mshabiki.

Mfano wa elimu:
Nilishawahi kuongea na Zitto miaka iliyopita kuhusu mfumo wa elimu ya sekondari Tanzania. Mimi nikauliza inawezekanaje shule ambayo inafelisha kila mwaka Div 4 na 0 inaruhusiwa kuendelea kufundisha na kutoza ada kwa Wazazi wa Kitanzania? Je ni kwanini kama ni Tatizo la kifetha au walimu tusiweke Utaratibu wa Vijana wa Chuo kufundisha kwa miezi sita kabla ya kupewa vyeti na kulazimisha hizo shule zinazofelisha kutumia kiwango kidogo kuwalipa hao wanavyuo kama Training fees.

Zitto alikubaliana na mimi lakini hajazoea sera tofauti na anavyofikiria! kitu tofauti kidogo. Volevile kwenye swala la Afya nilishauri tuweke utaratibu wa kuwa na Mobile Hospital ambazo zinatembea kila kijiji na wilaya na kutoa elimu ya Afya, Chanjo n.k Gharama itakuwa chini kwasababu Dr watakuwa wachache, hunahaja ya kujenga hospitali kila mahali, utapunguza msongamano kwenye hospitali za mikoa na rufaa n.k lakini hawakujua nina maana gani naposema Mobile Hospital.

Nimebahatika kukutana kwenye mkutano wa Diaspora na wakuu wa NSSF, BOT, TRA, TIB, Chambers of Commerce n.k. Ukiuliza Gavana je ni kwanini Interest Rate ziko 20% anasema tatizo ni hatuna ID. Nikamuuliza je umefanya nini kuchangia kutatua tatizo hilo? hana jibu, je umemueleza raisi kuhusu tatizo hilo ma mathara ya nchi? hana jibu? Nikauliza NSSF je nyumba mnazojenga zinapanda kwa thamani gani kwa mwaka? hawanajibu? sasa kama hamjui mnatoa wapi plan zenu za ujenzi na uwekezaji bila kujua thamani halisi ya majengo unayojenga? hawanajibu?. Nikawauliza TRA je Gari moja Tanzania linaingiza kodi kiasi gani kwa miaka kumi kwenye mafuta, spare, kodi ya barabara, matairi n.k je hamuoni kama mkiweka kodi kubwa sana na kufanya watu wasilete magari mnakosa pesa nyingi kuliko mngeshusha kodi na magari kuwa mengi? hawana jibu.

Hawa ndiyo watu wanaoendesha nchi yetu lakini hawajui njia mpya za kutatua matatizo na nyia zilizopo sasa hazifai.

Hivyo sijaona upinzani ukijaribu kuja na sera mpya.
 
Kamundu,

Kuhusu swala la Elimu nchini lazima tukubali kwamba sisi wenyewe ndio sababu ya watoto hawa kuwa failures na kila mwaka tunaendelea kufundisha Ujinga kwa wajinga hivyo kuunda Taifa la wajinga..Umeuliza swali zuri sana kuhusu shule zinazotoa watoto division 4 kila mwaka.. tatizo kubwa ni kwamba shue hizo toka mwanzo huchukua watoto walioshindwa mtihani wa darasa la saba. Tena wengine hawajui hata kusoma wala kuandika ila wameweza kumaliza darasa la saba..

Sasa hawa vijana baba zao hujikomba na kibindo chake kidogo kuhakikisha mwanaye amepata shule ya sekondari kumbe kapeleka Kabuntas ambaye katoka na F.. mfululizo. Sisi zamani ukipata C tu ktk mtihani au somo unajisikia vibaya sana lakini siku hizi mtoto akikomba C anajiona kashinda vibaya sana. Hivyo hata standard zetu ziko chini sana na hatuwezi kupandisha maana kama sikosei mwaka 2010 walioshinda Division 1 form iv niliambiwa walikuwa 24 au 26 Tanzania nzima (kaa sikosei).

Kwa hiyo inatakiwa sana marekebisho makubwa sana na sidhani kama tupo tayari kufanya marekebisho hayo kutokana na Uhaba wa kila kitu. Our problems are manmade! Na kuhusu Credit rates mkuu wangu hilo mtaji mkubwa sana kwa banks ambazo lengo lake kubwa ni biashara yenye faida kubwa na hawawezi kushusha rates kuwasaidia watu ikiwa soko lipo (wahitaji) na wanatengeneza vibaya sana. Hiyo sababu ya Vitambulisho ni kukutoa nje tu, ama hawaelewi undani wa janga hili maana banks wenyewe wanaelewa kuwa Wafanyabiashara wengi nchini wanachukua mikopo at that rate na maombi yamejaa makabatini. Na hata wakipandisha zaidi watu watakwenda kuchukua zaidi na zaidi isipokuwa wanachokitaka ni rehani hasa ya kiwanja, nyumba au shamba..

Watu wanachukua mikopo kufanya biashara haramu iwe kununua na kuuza Unga au kwenda China na kununua vitu feki iwe madawa au households ambavyo huja nyumbani na kuvbiuza kwa faida ya mara 10 au 5 amekosa sana..Hakuna mtu anayechukua mkopo wa asilimia kubwa kufanya kitu halali haiwezekani utarudisha vipi mkopo na kujenga faida?. Na Utashindwa vipi kurudisha mkopo wa asilimia 20 wakati umetengeneza profit ya 500 to 1000%..Again tunakuta ni swala la VIWANGO kwa mali zinazoingiza au biashara tunazochagua. Zote hazijengi uchumibali zinajenga maradhi na ujambazi - Shida juu ya shida..

Kwa hiyo kwa kuanzia tu swla la VIWANGO linatakiwa sana kutazamwa upya, iwe malizinazoingia nchini, Elimu, Afya, Maji, Umeme vitu vyote hivi viwango tunavyoweka ndivyo sababu ya kushindwa kwetu. How in the hell nchi nzima inagawa umeme for only 15% na the rest wako ktk kusubiri maombi yao au wakiambiwa hakuna miti unless utoe kitu kidogo utavutiwa...Kwa kila hali sisi wenyewe tuna create scarsity, tunaunda fitna na shida kwa waanchi ili walipe zaidi kama nchi ya Vita.. Ukienda Kongo leo unaambiwa kilo ya Sukari ni karibu dollar 10, sababu kuna vita lakini sisi WaTanzania inakuwaje hatuwezi kabisa kukidhi mahitaji yetu badala yake tuna create uhaba zaidi.. Ukimwaga sukari nchi nzima wenye maduka watazichimbia ktk maghala yao na kutoa kidogo kidogo to keep demand iliyopo high. Nadhani unakumbuka wakati wa Sokoine ilikuwa swala ni ufichaji bidhaa ili kusababisha shida na bei kupanda, mchezo huu upo hadi leo. Sii bank, majumbani, shule, Afya hadi miundombinu..

Kwa hiyo mkuu wangu kazi kubwa sana inatakiwa kwanza ni kuwabadilisha wananchi kifira, kuweka sheria mbele ya kila kitu na adhabu kali kwa wenye kukiuka, na tatu kuweka malengo yetu high ktk viwango na ku aim higher..bila haya tutakuwa tunacheza ndongolo tu, kukata viuno kaa Shakila..Haya mambo hayahitaji eimu ya darasani bali elimu kama msingi na ujanja wa Mujini kuwasoma WATU na MAZINGIRA yake ili upate ukuyafumbua..
 
Last edited by a moderator:
hongera Uzi wako unaishi, but leo haina ubishi CHADEMA wamejipanga na kujiimarisha zaidi ya ilivotegemewa na CCM imeporomoka kwa kasi ya ajabu, Now Kuna M4C Everywhere
 
Chaguzi za jana, zinaendelea kudhihirisha uliyoyasema baada ya uchaguzi mkuu.
 
Chaguzi za jana, zinaendelea kudhihirisha uliyoyasema baada ya uchaguzi mkuu.

Mimi naamua kuungana na Mzee Mwanakijiji, kwa kumpelekea kuni za mti wa mpingo, ili kukoleza moto kwenye lile tanuru na kuwapitisha humo viongozi wa Chadema, wataopita salama, watakuwa chuma cha pua, wale dhaifu, watateketea na kubaki majivu!.

Tanzania ni shamba letu sote, tukiendelea kuwachekea nyani, for sure 2015 tutavuna mabua!.

Nimeusoma ule uzi wako wa kizungu, nitachangia baada ya kupata ile dikishenari yangu.!.
 
Kwa jinsi upepo unavyoenda CDM wasipobadili mbinu na kujipanga upya,ni dhahiri 2015 pumzi inaweza kuwa imepungua na kushindwa kuhimili vishindo.Ni jambo la busara sana unaposhauriwa kujaribu kutafakari na kuyafanyia kazi yale yanayoonekana ni ya msingi.
Ubishi wa kila mara hauna tija yoyote.
 
Mkuu Pasco aliliona tatizo la CDM kila alipojaribu kuliaddress alizomewa akapachikwa majina mabovu uchaguzi wa udiwani Pasco ni mshindi CDM wamebeba aibu.
 
Last edited by a moderator:
Pasco, binafsi nadhani bado haumtendei haki Dr. Slaa. Sisi tuko mezani tunasubiri chakula, Dr. Slaa yuko jikoni, kuchelewa kufika kwa chakula haina maana kuwa ametunyima nafasi ya kula. Alishaongea kuwa kuna data anakusanya. Several times mwenyewe amesema si mtu wa kukurupuka bali huja na facts mkononi. Hebu tuwe wavumilivu tumpe nafasi.
Sorry Mkuu Superman, nilikuwa napitia tuu baadhi ya threads za zamani, nikakutana na hii kitu, japo ni issue ya siku nyingi three years back, bur its still valid, mimi ni mtu wa on off hapa nyumbani naweza kuwa nilipitwa!, hivi kile chakula tuliokuwa tunakisubiria mezani, wakati kilipokuwa kinapikwa, kiliiva?, kilipakuliwa? na kililiwa?.

Kwa vile ni cha zamani, huna haja ya kujibu kwa haraka ili kupata muda wa kutosha kukusanya kumbukumbu.
Pasco.
 
Mkuu Pasco aliliona tatizo la CDM kila alipojaribu kuliaddress alizomewa akapachikwa majina mabovu uchaguzi wa udiwani Pasco ni mshindi CDM wamebeba aibu.
Mkuu Ngongo, kupasi mtihani wowote kunategemea maandalizi!, na ushindi katika uchaguzi wowote kunategemea kujipanga!, concentration ya wengi ni kwenye uchaguzi mkuu wa 2015, ambao tutapata, rais wabunge na madiwani, lakini kabla ya uchaguzi mkuu, tunauchaguzi wa serikali za mitaa 2014!, huu ni uchaguzi muhimu kuliko uchaguzi mkuu kwa sababu ndio unaoweka grass root level ya uongozi kunyooshea mapito ya wanao kuja!. Kitu kinachoichoitwa "Diverting Attention na Delaying Tactics" pia ni mbinu za medani kwenye uwanja wa vita vya kisiasa, kumkeep busy adui yako kwa issues zozote ambazo zita divert attention yake kwa jambo muhimu lililopo mbele yake, ili muda wa ku stike ukifika, unafanya surprise attack (ambush) kwa kushutukiza, hivyo kumkuta adui hajajiandaa, na kumpiga hadi kumshinda kiulaini!.

Hili la kujipanga, kiukweli bado ni tatizo, na sasa hizi kesi mahakamani ambazo Chama kimejitolea kukubali kusimama nazo as if ni kesi za chama na sio kesi za watu, bila kujijua, wanampatia adui yao kile anachokitaka!. Kwa mwenendo wa kesi za Tanzania zilivyo, this will drag on for sometimes, hivyo diverting the attention, likimalizika moja, litaibuliwa lingine, mpaka kukosekana kabisa muda wa kujipanga!, kufunga na kufungua, ni uchaguzi wa serikali za mitaa, usipochukua landslide huku, ni aghlabu sana kuchukua lanslide kule!.
Sisi wengine kazi yetu ni kuona tuu na kusema, tutaitwa kila aina ya majina, ila mwisho wa siku, matokeo ya mwisho, yatathibisha tuliona nini na tulisema nini!.
Pasco.
 
Wanabodi,

Nikiwa hapa Dom, nimebahatika kukutana baadhi ya wabunge wapya wa CCM na wa kambi ya upinzani, kujaribu kufahamiana, sio siri, baadhi yao hawana hata substance ya ni nini kilichowafanya washinde,

Nilipoongea na baadhi ya wale makamanda waliokata magogo kanda ya ziwa, nimewaona ni wa kawaida tuu, hivyo nimefikia jibu moja la uhakika, kuwa CCM katika baadhi ya maeneo, imechokwa mpaka basi!, upinzani hata ungesimamisha jiwe, lingechaguliwa!


Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga.
Nimeikumbuka hii, miliisema 2010, leo ni 2013, bado naisema tena!.
Nimesoma thread ya mmoja wa wabunge wa Chadema humu jf!, kiukweli ukiwa makini, vichwa vitupu utavitambua tuu, hata kama vimelishwa maneno!.

Chadema jipangeni!, time is not on your side anymore!, by the time mnaamka, it might be too little too late!.
Pasco.
 
Wanabodi,
Dawa pekee ya kuitibu CCM, ni kuirevamp CCM completely, task nambari moja ni Makamba should go first with his old guards team. Msisubiri mpaka uchaguzi mkuu wa chama chenu, miaka miwili ijayo (2012), itakuwa too late. If you are to du anything, doi it now and fast!. Leteni fresh blood kina January type, Kippi, Nape type and the like ambao wanaweza siasa za kisasa za dot com type.

Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.

Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa kwenye Usukani, Katibu Mkuu mpeni Zitto, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, ili Walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kuwapigia kura 2015.

Kitendo cha kuihodhi kambi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani, Chadema peke yenu hamuwezi!.

Kama CCM iko ICU na Chadema haijajipanga, spika ndio huyo mama ma over confidence na over reaction, 2015 tutegemee nini?.
Niliwahi kusema Chadema haijajipanga!, sasa nafuatilia kwa makini jinsi inavyojipanga kuelekea 2015!.
Pasco.
 
Hii niliisema mara tuu baada ya uchaguzi wa 2010!. Leo ni 2014, Matokeo ya uchaguzi wa udiwani ni uthibitisho kuwa Chadema bado haijajipanga!. Base ya ushindi wa uchaguzi mkiuu wa 2015, ni ushindi wa kishindo uchaguzi wa serikali za mitaa baadae mwaka huu!. Kwa matokeo haya, na kinachoendelea sasa ndani ya Chadema, I doubt kama time is in your side!, by now its already late!, 2015, time will be too little too late!.

Naomba Chadema msilie, as if hamkujua!, tuliwaambia!, na tunaendelea kuwaambia!.
Pasco.
 
Back
Top Bottom