Mwanakijiji na Shalom CHADEMA sio chama cha kiribelari..Soma hapa Falsafa na Itikadi ya CHADEMA..Huu ndio mtazamo wetu.
- Falsafa ni fikra na mtazamo wa Chama ambayo ni kuamini katika "Nguvu na Mamlaka ya Umma" (The People's Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasilimali, uchumi na siasa ya nchi yao.
- Aidha falsafa ya "Nguvu na Mamlaka ya Umma" ndiyo msingi na chimbuko la kuundwa dola ya nchi, na kuwa, Umma ndiyo wenye madaraka ya mwanzo na ya mwisho katika kuamua hatima ya nchi na taifa pasipo kuingiliwa, kudanganywa au kughilibiwa na viongozi, watawala au wageni.
- Ujenzi na udumishaji wa Demokrasia na Maendeleo nchini vitatokana na Nguvu na Mamlaka ya Umma wa Watanzania. Nguvu na Mamlaka ya Umma itabainishwa, kuainishwa na kulindwa katika Katiba ya nchi na Umma ndiyo utakuwa chimbuko la Katiba hiyo.
- Historia inaonyesha kuwa "UMMA" wa Watanzania haujawahi kuwa na sauti, mamlaka na madaraka juu ya maamuzi ya hatima ya maisha ya watu. Uhuru, nguvu, mamlaka na madaraka wakati wote, tokea enzi za ukoloni mpaka leo, vimekuwa vikihodhiwa na kumilikiwa na watu wachache ambao wana mamlaka ya kuongoza SERIKALI na kuwakandamiza wananchi.
- CHADEMA tunaamini kuwa mifumo na miundo ya utawala wa nchi yetu havijawapo kwa ajili ya kuutumikia umma, bali umma ndiyo huzitumikia serikali hizo ambazo ni mali ya watu wachache wanaopoka "Nguvu ya Umma". Sambamba na hilo, umma wa Watanzania umekuwa hauna mamlaka ya mwisho ya kuhoji maamuzi ya serikali yanayowaathiri watu, na hivyo kujikuta hauna mamlaka juu ya rasilimali, sheria, utawala, na uendeshaji wa nchi. Aidha, Katiba ya Nchi imekuwa miliki ya Serikali kwa kutumia Bunge ambalo linatawaliwa na mawazo kongwe ya ukiritimba wa enzi za mfumo wa Chama kimoja cha siasa nchini.
- CHADEMA tunaamini na kutambua kuwa "kuchaguliwa" kuunda utawala wa kuongoza nchi hakumaanishi wachaguliwa kujitwalia mamalaka ya UMMA na kisha kuyatumia mamlaka hayo kuwakandamiza "waliowachagua" kwa sababu tu ya kutetea maslahi binafsi badala ya maslahi ya umma.
- Hivyo basi, falsafa ya "Nguvu na Mamlaka ya Umma" ndiyo njia ya msingi ya kubadilisha fikra na uongozi unaokandamiza umma, ili kuibua fikra mpya na kuweka uongozi unaoweza kumilikiwa, kuhojiwa, na kuwajibishwa na umma kwa kutumia vyombo vilivyopatikana kwa utashi wa wengi kupitia chaguzi huru na za haki.
- Falsafa ya "Nguvu na Mamlaka ya Umma" inalenga kuwaamsha, kuwahamasisha, kuwaelimisha, kuwashawishi na kuwaandaa Watanzania wachukue hatua ya kuimiliki, kuitawala, kuilinda na kuifaidi nchi yao tofauti na kipindi cha miaka mingi chini ya mfumo wa chama kimoja cha siasa na miaka kumi na nne ya mwanzo ya mfumo wa vyama vingi.
- CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI (center party).
- CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.
- CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.
- CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.
- CHADEMA inaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri.
- CHADEMA inaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo za haki.
- CHADEMA inaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa.
- CHADEMA inaweka umuhimu wa pekee katika familia kama moja ya taasisi muhimu ya kijamii.
- CHADEMA inaamini katika umuhimu wa uhuru wa kuamini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola.
- CHADEMA inaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu.
- CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.
- CHADEMA inaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake.
Bibi Ntilie,
Mkuu hayo yote tuyaache nyuma tugange yaliyopo na yajayo maanake mzigo huu unatuelemea sote.
Kama Chadema ni chama cha CENTRAL, meaning a Reform Party sijui Mwanakijiji na hao CCJ wao wanakuja na itikadi gani tofauti...
Nijuavyo mimi Central party mara zote huundwa kwa sababu ya haikubaliani na uongozi mzima wa serikali unavyoendeshwa.. Mara nyingi ni pale nchi inapokotoka ktk dira au inapokosa DIRA, mambo yanaendeshwa KIUTAWALA zaidi ya KUONGOZA kwani Kutawala huhitaji dira wala idiology isipokuwa deceitful and control ya Utawala wako, usokuwa na Uhuru.
Hivyo kiitikadi Chadema wanataka ku reform serikali kuu, kurudisha Haki ya wananchi, kurudisha uhuru wao ili waongozwe na sii kutawaliwa kufuatana na dira ya taifa na kikubwa zaidi wananchi wawe ndio wenye control ya serikali kuu kwani hiyo ndio maana halisi ya wananchi walio UHURU..as to say Chadema noble cause ni true reform of the government..
Hii lugha naisikia tena CCJ! - what's up yaani tuna cenral party ngapi maanake nasikia hata Mtikila anajiiweka central..
Hapa ndipo napopigwa bao na siasa za Bongo maanake kila mtu ni reformist, ebu nitafutie mtu au kiongozi yeyote toka chama chochote Tanzania asome ya Chadema kisha anambie wapi anapingana na Itikadi ya Chadema! sidhani kama utampata...Kifupi Tanzania hatuna chama chochote chenye itikadi zaidi ya porojo..hakuna kitu Iitikadi za Kushoto wala Kulia, ila ni mapana ya fikra ktk muundo wa HAKI za jamii baada ya matokeo ndani ya nchi huru badala ya - Itikadi kuwa biblia ya mfumo wa maisha yao - way of life...
Utunzi wa Itikadi kidogo unafanana na Imani ya dini zetu ambazo kimsingi binadamu wote tunatafuta kutoingia motoni..Sasa hizi imani ziwe ni hadithi au kuna ukweli ndivyo siasa za Itikadi zinavyoaminiwa pia...Kila dini imetupa dira ya kuishi ili upate uzima wa milele, na tumepewa pia mamlaka ya kuchagua imani na umayoiamini wewe na haki ya kuyaendesha maisha yako kufuatana na imani ulokuwa nayo. Mwisho wa siku mhukumiwa ni wewe mmoja. Tofauti baina ya dini, Demokrasia huja na mfumo wa itikadi (Biblia) ambayo tunapewa dira ya kwenda sote peponi (maendeleo) na mamlaka ya sisi kuchagua itikadi gani tutaifuata kwa kupiga kura zetu haki ya wengi ktk ushindi hupewa nafasi ya kutuongoza, na sote tunafuata dira hiyo kuelekea huko kuzimuni.
Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa, Chama CCM wawe na Katiba yao ambayo CUF,NCCR au CCJ wakiisoma wanaona hakuna maendeleo kama tutafuata path hiyo.. CCM vile vile wakisoma za wenzao.. wapo wengine wanaweza kubaliana na nguzo za itkadi lakini kuna vipengele ambavyo havikubaliki na ndipo hujitenga na kuunda Central Right au Left. Ni kama kama dini moja ilojitenga ktk dhehebu fulani....
Ukija kwetu hakika sisi tumeuvaa mkenge, tumevamia mfumo huu Demokrasia kwa sababu Uongozi bora na mbaya kwa nchi zetu ni Mtawala mwenyewe...Aidha ana sifa za Dikteta, Corrupt, Kiongozi asiyependa madaraka ya kiutawala ila a kuongoza umma wake (hawa ni aghlabu kuwapata) but all of them huchaguliwa regardless of Idiology kwa sababu hatuna kitu hicho ila tunzi za haki za binadamu waliokuwa huru..Sawa na kuwa na Biblia au Kuran mkononi lakini sifa ya maisha ni kubembea kwa sana..