CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

Nobody knows what actually will ensue in October, but one of the above two guys will fulfill the reality. Right now we can keep on speculating through powers of our beliefs, imagination and theories. So keep on the discussion and I am enjoying it. However, I want to see CCJ given its permanent registration because there is no limit of number of political parties required by the law. On the other hand I want the opposition parties to unite if they can agree on the right and workable policy to facilitate for a stronger union.

very good indeed; that is why it is paramount that CCJ gets full registration soon so it could participate in the General Elections. To condemn it and deny it without giving it opportunity to present its policies as proposals to the nations ni kuonesha tu kuwa watu wanakiogopa.
 
Pasco...........

Katiba inasemaje juu ya chama kujiunga na kusimamisha mgombea mmoja.....Je wanaweza kuungana na kufanya 'rainbow' coalition kama ilivyokuwa Kenya(inaruhusiwa?,ama wakiungana inabidi waisajili upya hiyo coalition yao.......Ikoje hii?

Ama wanaweza kuwa na muungano usio rasmi...kwamba wote wanaamua let say kuiunga mkono CHADEMA katika uchaguzi(sijui kama litawezekana hili,kwa Tanzania)

unajua kuungana wala kushirikiana siyo kazi ni jambo rahisi sana; lakini ni muungane au ushirikiano wa nini? Kwanini vyama vingine kwa mfano viiunge mkono Chadema na si TLP.. well wengine wanasema ili vishinde uchaguzi na kuiangusha CCM. Kwa haraka hilo linaonekanaa ni "bright idea" lakini ukiisigolea kwa karibu inabidi ujiuliza waiangushe CCM ili kiwe nini? ili nani kati yao atawale, kwa misingi gani, kwa sera zipi, na mgawanyo wa madaraka utakuwa vipi n.k Hamuwezi kuungana ili kuiangusha CCM tu itoke madarakani halafu that would automatically become a panacea of our woes!
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu nakuomba unielewe kwamba situkani mtu ila nazungumza ukweli ambao wakati mwngine unauma..the good thing is, I have said so kuliko kukubeba kwa shangwe hali nakung'ong'a.
Nimekusoma na naendelea kukusoma lakini kusema kweli unashangaza sana, labda nikwambie tu kwamba haya mawazo yako unayoamini wewe hayana mvuto hadi sasa acha hiyo Itikadi ya CCJ. Ikiwa unashindwa kuwashawishi watu hapa hali unaona kila kitu sawa utaweza vipi kuona mapana ya idiologia kuweza kuvuta wananchi. Hapo nyuma kuna ndugu yangu kaweka bayana kabisa nachozungumza mimi na kisha kaweka mawazo yako wewe vizuri tu. Na hakika ndivyo nilivyokuelewa mimi na kwa bahati mbaya umeshindwa kunivuta.

Na pengine huwezi kuamini maneno yangu..ila nakuomba sana weka Mada ambayo inauliza watu uwezekano wa CCJ kushawishi watu Ushindi 2010 ikiwa wataungana nao ktk mapambano yao wakiwa solo..Na waulize wananchi wa hapa JF tena wanaoamini ushindi hauwezi patikana pasipo muungano wa vyama vya Upinzani (wanachama) pengine utaweza kushawishika. Nitarudia kusema itikadi za chama sio solution ya kumwondoa CCM ila dhumuni liwe kuunganisha nguvu za kura za wananchi kupitia vyama vilivyosajiliwa tayari. Vyama hivi kwa mujibu wa sheria ndivyo vyenye kuwakilisha watu ktk imani za kiitikadi tofauti ktk uchaguzi mkuu.

Ni sawa na Bunge letu lenye mamlaka ya kutunga sheria, kama tunaona kuna Upotoshaji wa haki za binadamu na tunataka sheria fulani ipite ni muhimu Umoja wa wabunge wetu pasipo kujali itikadi zao maadam wanaamini haki hiyo ni lazima isimame. Lengo la muungano wa wabunge hawa wa vyama tofauti ni kupitisha sheria itakayoleta haki kwa raia wake na sio mashindano ya itikadi au kwa nini swala hili Wabunge wa zamani hawakuliona wakaungana isipokuwa baada ya mbunge wa chama fulani kulileta kama Muswada. Hapa tutakesha na sheria haitapata kura za Wabunge wengi wasipokuwa na lengo moja.

Pasco,
Mkuu nakumbuka huko nyuma ulitoa shukran kwa kukupa taarifa ya mpango wa waislaam kumvuta mwalimu ili kutuwezesha kupata Uhuru..Kisha akafuatia Bibi Ntilie na hoja yenye nukuu za mkutano wa 1954, nilimwelewa vizuri na nikamjibu vizuri sana kiasi kwamba hakurudi kuuliza zaidi aidha alielewa au bado alikuwa akitafuta hoja zaidi. Hoja ya Ntilie ilihusu zaidi uuwiano wa waislaam na Wakristu ktk mkutano wa mwaka 1954 na kuuliza mbona walikuwa wajumbe sawa pande zote mbili? na nikamjibu kwamba mwaka 1954 ilikuwa ni miaka miwili baada ya Mwalimu kujiunga na TAA, hivyo ushawishi mikoani tayari ulikwisha anza na hakika watu hawajui kazi kubwa ya ushawishi aloifanya mwalimu kwa muda wa miaka miwili tu kufikia kuundwa kwa TANU ktk mkutano huo wa 1954.

Hata hivyo, harakati za Uhuru wetu na wanaTAA zilianza mapema na wapiganaji wetu walipokuwa India..Kwa bahati kubwa sana nimewahi kuzungumza na Mzee Ally Sykes kwa mapana zaidi. Nakumbuka aliniuliza kama najua kuwa Ule wimbo wa Taaanzaniiia - Tanzania, nakupenda kwa moyo woote - waliutunga wao wakiwa kambini India..Nilibakia domo wazi nikifikiria uchungu waliokuwa nao hawa watu wakiwa vitani tena nchi za wageni.
Lakini hata yeye niliweza kuchambua pumba toka ktk maelezo yake alipodai baadhi ya vitu kwa lengo la Ubinafsi zaidi... nikaweza kujumlisha mengi hata kuelewa pengine hizi ndio sababu zinazofanya historia hii isipate kuwekwa wazi kwani itakuwa na madhara yake, madhara kama haya hapa JF tunavyoyaona...

Nashindwa kumwelekeza Mwanakijiji mambo muhimu kwa sababu tayari kisha ingia uchungu wa kidini akifikira kwamba maadam Waislaam ndio walianza mapema basi ina maana Wakristu walikuwa hawautaki Uhuru. Nimemwambia sio kweli bado hataki kuelewa - Jazba!

Kuna historia mbili ambazo Tanzania hatutaki kuzizungumzia ama kuziwekea maanani (kumbukumbu) kwa sababu maalum....1. Harakati za Uhuru wa Bara na 2. Mapinduzi ya Zanzibar.

Katika historia hizi, ukweli utabakia ukweli hata kama Historia haikubaliki ktk umma wa leo. I bet U mkuu hakuna mtu humu anajua historia ya TAA iliyoanzishwa mwaka 1929 Nyerere akiwa na umri wa miaka 7 kuja hadi kufikia 1953 kwa undani zaidi.. hakuna na kama wapo ni wachache sana..Na bahati mbaya wengi wetu hatupendi kutafuta ukweli wa historia yetu.
 
Pasco,
Mkuu nakumbuka huko nyuma ulitoa shukran kwa kukupa taarifa ya mpango wa waislaam kumvuta mwalimu ili kutuwezesha kupata Uhuru..Kisha akafuatia Bibi Ntilie na hoja yenye nukuu za mkutano wa 1954, nilimwelewa vizuri na nikamjibu vizuri sana kiasi kwamba hakurudi kuuliza zaidi aidha alielewa au bado alikuwa akitafuta hoja zaidi. Hoja ya Ntilie ilihusu zaidi uuwiano wa waislaam na Wakristu ktk mkutano wa mwaka 1954 na kuuliza mbona walikuwa wajumbe sawa pande zote mbili? na nikamjibu kwamba mwaka 1954 ilikuwa ni miaka miwili baada ya Mwalimu kujiunga na TAA, hivyo ushawishi mikoani tayari ulikwisha anza na hakika watu hawajui kazi kubwa ya ushawishi aloifanya mwalimu kwa muda wa miaka miwili tu kufikia kuundwa kwa TANU ktk mkutano huo wa 1954.

Hata hivyo, harakati za Uhuru wetu na wanaTAA zilianza mapema na wapiganaji wetu walipokuwa India..Kwa bahati kubwa sana nimewahi kuzungumza na Mzee Ally Sykes kwa mapana zaidi. Nakumbuka aliniuliza kama najua kuwa Ule wimbo wa Taaanzaniiia - Tanzania, nakupenda kwa moyo woote - waliutunga wao wakiwa kambini India..Nilibakia domo wazi nikifikiria uchungu waliokuwa nao hawa watu wakiwa vitani tena nchi za wageni.
Lakini hata yeye niliweza kuchambua pumba toka ktk maelezo yake alipodai baadhi ya vitu kwa lengo la Ubinafsi zaidi... nikaweza kujumlisha mengi hata kuelewa pengine hizi ndio sababu zinazofanya historia hii isipate kuwekwa wazi kwani itakuwa na madhara yake, madhara kama haya hapa JF tunavyoyaona...

Nashindwa kumwelekeza Mwanakijiji mambo muhimu kwa sababu tayari kisha ingia uchungu wa kidini akifikira kwamba maadam Waislaam ndio walianza mapema basi ina maana Wakristu walikuwa hawautaki Uhuru. Nimemwambia sio kweli bado hataki kuelewa - Jazba!

Kuna historia mbili ambazo Tanzania hatutaki kuzizungumzia ama kuziwekea maanani (kumbukumbu) kwa sababu maalum....1. Harakati za Uhuru wa Bara na 2. Mapinduzi ya Zanzibar.

Katika historia hizi, ukweli utabakia ukweli hata kama Historia haikubaliki ktk umma wa leo. I bet U mkuu hakuna mtu humu anajua historia ya TAA iliyoanzishwa mwaka 1929 Nyerere akiwa na umri wa miaka 7 kuja hadi kufikia 1953 kwa undani zaidi.. hakuna na kama wapo ni wachache sana..Na bahati mbaya wengi wetu hatupendi kutafuta ukweli wa historia yetu.
.
Mkandara, kadri siku zinavyokwenda ndivyo ninavyozidi kuisoma na kuielewa baadhi ya misimamo ya baadhi yetu humu JF as members. Kuna members ambao its true ni much know lakini wana impaired vision au myopic view kwenye baadhi ya issues, hao wanaona upande mmoja tuu ule wanaaona wao kwa kuamini there is on one way which is the is the right way and all other ways ni wrong way, na hawatoi option ya njia mbadala in case their way is a wrong one wakijiaminisha is the right way, hawa siku zote huishia kutahayari kwa defeat!.

Hili la historia ya TAA, TANU na harakati za uhuru, ziliandikwa vizuri sana kwenye kijitabu fulani kilichoandikwa na hayati Robert Makange na Bagdelalah. Hakuna aliyesema Wakristu hawakutaka kudai uhuru, infact wakina Kaaya huko Kanda ya Kaskazini walianza harakati mapema hata kabla ya kuzaliwa kwa TANU, ila ni ukweli mchungu Wakristu wasomi enzi zile, walikuwa benefisharies wa utawala wa Mkoloni ndio Maana Mangi Mkuu, Thomas Marealle alipingana na Mwalimu, na Nyerere akawaachia laani nchi hii, kamwe haitakuja kutawaliwa na Mchagga!.

Mtu yoyote anayetaka kupingana na historia, apinge kwa kupresent hard facts na sio insunuitions za mawazo yake ambayo hayoko backed by facts.

Mzee Mwanakijiji ni great author nadhani hata orator kama kungekuwa na uwanja wa kusimuliana hadithi, lakini kwenye hili debe la CCJ, kwamba itasisima yenyewe, he is dam wrong ana kama kweli huo ndio msimamo wa CCJ, then down the drain watazama na CCJ yao!.

Wewe Mkandara na wengine wote wenye kuitakia mema nchi hii kwa ukombozi wa kweli, tuendeleze kuzamisha the sense of 'united we stand against the common enemy' mpaka izame ndani ya vicvhwa vyao vigumu!.
 
Mkuu pasco,Nimekupata hata mimi sielewi kwa nini haya yanatokea. Eti mtu anakuja na sababu kuwa chadema ni mabepari na ccj ni wajamaa. Halafu hao hao wajamaa wanategemea majitu kutoka chama kisicho hata na itikadi wala aibu lazima umtilie shaka. Mwaka huu tunaweza kushindwa vita lakni askari wa kukodi wote lazima wawekwe kweupe
 
CCJ mmepoteza mwelekeo
ban.mtazamo.jpg


Irene Mark


HIVI karibuni, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, alikaririwa na vyombo vya habari akiueleza umma kwamba kwa sasa ofisi yake haina fedha za kuhakiki majina ya wanachama wa Chama Cha Jamii (CCJ).
Kauli hiyo ya Tendwa, ilikuja siku moja baada ya viongozi wa muda wa CCJ, kuwasilisha mafaili yenye majina ya wanachama 2,000 kila mkoa kwa mikoa 10 Tanzania Bara na Visiwani.
Hiyo ilikuwa hatua ya mwisho ya CCJ katika kuomba usajili wa kudumu ili nayo iingie kwenye mchakato wa kupata wawakilishi (madiwani, wabunge ama rais), wa wananchi kupitia sanduku la kura zitakazopigwa nchi nzima Oktoba 31, mwaka huu.
Ni hatua nzuri yenye kustahili pongezi. Ndiyo, wanafaa kupongezwa maana ni kawaida ya waungwana kukosoa na kupongeza panapobidi. Nami nafanya hivyo.
Kama ilivyo ada kwa waungwana, na ndivyo ilivyo kwamba kila kizuri kina ubaya wake. Leo nitajadili pia mabaya ya viongozi wa CCJ na safu nzima ya chama hicho kilichojipambanua mwanzoni mwa mwaka huu na kufanikiwa kukitikisa chama kikongwe nchini yaani, Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Wakati wa mchakato wa kuomba usajili wa muda, waandishi wa habari, nikiwemo, walikuwa watu muhimu kwa viongozi hao. Ilifika wakati hata kabla ya kufanya jambo ilibidi wawafuate waliowaamini na kuomba ushauri.
Kwangu hilo ni jambo jema sana. Hali iliendelea hivyo mpaka siku walipoitwa rasmi kwenda kupokea cheti cha usajili wa muda pale kwenye ofisi za msajili katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Waandishi tulitimiza wajibu wetu. Umma ukahabarika, wapenda mageuzi wakajitokeza kwa wingi kiasi chao kwenda kushuhudia ujio wa chama kilichonadiwa kufanya mapinduzi ya fikra kwa Watanzania.
Wachache walioisikia CCJ walitamani kujua historia za waasisi wake (kisiasa zaidi) ambao walitajwa sana kwa nafasi ya uenyekiti na ukatibu. Kwa bahati mbaya, ni sura ngeni mno kwenye medani ya siasa.
Viongozi hao wakatokea kukubalika (kwa kipindi kile), wakapokelewa kwenye jamii kwa msaada wa vyombo mbalimbali vya habari. Misukosuko waliyoipata ilikemewa na waandishi wa habari, ukawa urafiki mwema kati ya viongozi wa muda wa CCJ na wahabarishaji wa umma.
Wapo waliokitilia hofu chama hicho kipya kwa madai ya kuwepo kwa kazi maalum ya kuuvuruga upinzani nchini, hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu. Nilitafakari kwa kina na kuandika kwenye safu hii nikiwauliza; ‘CCJ mmetumwa kutuvuruga?'
Hii ni baada ya wao kuanza kupanga ratiba za kesho… kesho pindi walipotaka kuzungumza na waandishi wa habari ili kueleza mkakati wao wa kuyapata majina 2,000 kila mkoa kwa mikoa 10 na mipango yao ya baadaye katika kufikia vigezo vya kupata usajili wa kudumu. Hapo ni baada ya kujiridhisha kwamba watapata usajili wa muda.
Kilichonisukuma kuandika mtazamo wangu ni hali ilivyobadilika punde baada ya kupata usajili wa muda ambapo viongozi hawa na wengine ndani ya CCJ walianza kususurika. Ushirikiano mwema kati yao na wanahabari ukaota ‘mbawa'.
Kumbukumbu zangu zinanilazimisha kunukuu baadhi ya maneno ya waandishi ‘marafiki' wa CCJ kwamba uongozi mzima wa chama hicho ni wa ‘kisanii', viongozi wote ni wasemaji wa chama hicho, matokeo yake wanaupotosha umma. Ndiyo, kwa takribani juma zima lililopita vyombo mbalimbali vya habari hususan magazeti, viliripoti kwamba chama hicho kingetoa tamko lao kuhusu kauli ya msajili kukosa pesa za kuhakiki majina yao ili kuharakisha mchakato wa kukipatia usajili wa kudumu. Sasa jamii imechoka kusikia simulizi za CCJ. Swali na mshangao vinabaki ni kwanini wasemaji wake wanatofautiana? Ni kweli kimepoteza mwelekeo? Kwanini mnatoa taarifa zisizo rasmi? Nawashauri, msipojipanga vema jamiii itawatenga na imani yao kwenu itapotea.
 
Mzee Mwanakijiji ukiwa kama Mmoja wa waanzailishi wa CCJ bado natatizwa na haizi kauli zako

Kama Katiba yao ndivyo ilivyo, I can say with absolute confidence; CCJ is nothing but a disappointment in the making.

Nyingine hii hapa

mkuu.. you might be very right.. wakati mwingine ili kujua maji ya moto kiasi gani inabidi utumbukize mkono. CCJ ilivyo na itikadi yake haijatoa sababu ya kwanini inataka kuwa chama kipya! Karibu malengo, nia, madhumuni, muundo na mfano ni carbon copy ya CCM tofauti ni herufi tu "J" na "M".. wao wameelezea yale yale yaliyoelezewa na CCM kwa maneno mengine!Labda ningependa kujua zaidi ni ajenda yao hasa ni nini?

Na mwisho kabisa ukatoa angalizo hili hapa

Binafsi ningemshauri mtu yeyote anayetaka kujiunga na CCJ kufikiria kwanza.


Kwenye page ya 5 tano ya topic hii hapa chini

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/50507-chama-kipya-ccj-na-hatima-ya-ccm-lisemwalo-5.html

Haya yangu Mache na Masikio tu
 
Mkuu nakumbuka huko nyuma ulitoa shukran kwa kukupa taarifa ya mpango wa waislaam kumvuta mwalimu ili kutuwezesha kupata Uhuru..Kisha akafuatia Bibi Ntilie na hoja yenye nukuu za mkutano wa 1954, nilimwelewa vizuri na nikamjibu vizuri sana kiasi kwamba hakurudi kuuliza zaidi aidha alielewa au bado alikuwa akitafuta hoja zaidi. Hoja ya Ntilie ilihusu zaidi uuwiano wa waislaam na Wakristu ktk mkutano wa mwaka 1954 na kuuliza mbona walikuwa wajumbe sawa pande zote mbili? na nikamjibu kwamba mwaka 1954 ilikuwa ni miaka miwili baada ya Mwalimu kujiunga na TAA, hivyo ushawishi mikoani tayari ulikwisha anza na hakika watu hawajui kazi kubwa ya ushawishi aloifanya mwalimu kwa muda wa miaka miwili tu kufikia kuundwa kwa TANU ktk mkutano huo wa 1954.

Mkuu Mkandara sikurudi tena sio kwa sababu ulizozitaja na hoja kwenye masuala kama haya huwa zinakuja automatic nikitafuta ni vibwagizo vingine tu. Anyway, msema kweli mpenzi wa Mungu, sababu ya kutojibu ni kwamba mie ni 'mstaafu' natumia internet nyumbani kwa kununua vocha za TTCL kwa hiyo kuingia kwenye internet kila wa leo sina uwezo huo. Nadhani wewe mwenzangu ni rahisi kwako maana huenda uko kazini ama kama ni 'mstaafu' basi ustaafu wako una afueni!! Leo nimepita kwenye ofisi za watu nikaomba kuchungulia JF kulikoni nikakuta unanisengenya!! Naomba nikujibu lile bandiko lako ifuatavyo:
Bibi Ntilie,
Sielewi lengo la swala hili kama ni kuthibitisha kwamba maneno yangu hayana ukweli au unachambua historia kwa kutafuta mikutano ya chama wa mwaka 1954 wakati Nyerere ali join chama hicho miaka miwili kabla, sasa sijui unajaribu ku prove kitu gani kwa kuorodhesha wajumbe wa mkutano huo hali wakati huo azma wa waanzilishi ipo ktk hatua ya utekelezaji wake. Je, unaweza kunambia hesabu ya wajumbe Wakristu ktk TAA before say in 40s au kufikia mwaka 1952 kabla ya mwalimu kujiunga?

Lengo ni kuonyesha kwamba baadhi ya uliyoandika yanaweza kuwapotosha wasioelewa historia wakadhani kwamba ni kweli kama ulivyoandika upo "ukweli ambao wengi hatupendi kuuweka maanani leo hii" kwamba "Waislamu waliutaka Uhuru wa Tanzania mapema lakini ….. Ndipo walipokuja na plan ya kuwavuta Wakristu na Mwalimu akapewa uenyekiti."

Hii statement inaweza ikampotosha msomaji ambaye hajawahi kusikia kilichojiri kuhusu historia ya chama cha TAA na hatimaye Mwalimu kuchaguliwa kuwa kiongozi. Mtu akisoma ulichoandika atadhani ni kweli wakati huo Waislamu walikuwa na mwamko wa siasa kuwashinda Wakristu kwa hiyo Wakristu walivutwa tu. Pia ataamini kwamba kulikuwa na ‘plan' maalum ya Waislamu kuwavuta Wakristu.

Kama ni suala la kuutaka Uhuru wa Tanzania, ni wananchi wa Tanganyika kwa pamoja (Waislamu, Wakristu, Wapagani n.k.) walioutaka huo Uhuru. Watafiti wanatuambia kwamba vyama vyote vilivyokuwepo tangu miaka ya 1940 vilikuwa ni vyama vidogo vidogo vilivyokuwa na malengo tofauti tofauti. Hatimaye katika miaka ya 1950 likawepo vuguvugu la wananchi kuelewa umuhimu wa kuutafuta Uhuru na kwamba wangeliweza kuvitumia vyama hivyo na kuleta muungano ambao utakuwa na nguvu ya kupambana na Mkoloni. Maelezo ya Utafiti niliyoyabandika yanadhihirisha kwamba TAA iliyomteua Mwalimu kuwa kiongozi wa kupigania Uhuru ilitokana na muungano wa vyama hivyo vidogo vidogo nchini na ni dhahiri likiwemo tawi la TAA Dar es Salaam ambalo Mwalimu alijiunga nalo.

Naweza kuelewa na kuona mantiki endapo statement yako ingelikuwa kama ile ya watafiti kwamba Waislam Wasomi wa Zanzibar waliwavuta Wakristu kuungana nao kwa sababu Visiwani Zanzibar idadi kubwa ya wakazi visiwani humo ni Waislamu. Pia naamini kwamba kwamba maelezo hayo yalitolewa kuelezea hali halisi ilivyokuwa na si kwa misingi ya "unafsi" uliouonyesha kwa kuweka maneno ya "wengi hatupendi kuuweka maanani".

Je ulitegemea mkutano wa mwaka 1954 uwe na wajumbe Waislaam wengi kuliko Wakristu hali lengo kubwa la waasisi wa TAA mpya iliyozaa TANU kina Abdul Wahid Sykes na Hamza Mwapachu ilikuwa kuunganisha nguvu za Watanzania iweje tena hawa watu wapunguze nguvu za ushiriki wa wakristu ktk kikao kikubwa kama hicho!

Aliyeleta suala na Waislamu na Wakristu ni wewe sio mimi. Nilichojaribu kufanya ni kuonyesha jinsi ambavyo hoja yako haina mashiko. Ni wengi wepi ambao hawapendi kuuweka maanani ‘ukweli' uliouzungumzia?

Pili, ulivyoelewa wewe walipoandika hivi:- Huko mikoani Chama TAA kilitokana na vyama vidogo vidogo ina maana kwamba hao ndio wanzilishi au waliojiunga na chama kilichokwisha anzishwa!..

Kama umenielewa hivyo basi this was a slight technical error na naweza kujitetea kwamba wakati na-'peruse' waliyoandika watafiti na kukujibu ilikuwa saa 8 usiku!! Lakini vyovyote vile ilivyokuwa opening statement yako has a lot to be desired! Ninavyoelewa mie Chama cha TAA (muungano wa vyama hivyo vidogo vidogo pamoja na hilo tawi la TAA Dar es Salaam walilokuwemo Sykes et al) ndicho kilichozaa TANU. Na kwa kuelewa kwangu hivyo, ni kwamba Mkutano, wa chama cha TAA (proper), ndio ulikuwa na wajumbe walioorodheshwa na ndio uliomchagua Mwalimu Nyerere kuwa kiongozi wa TAA na hatimaye TANU bila ya msingi wa Waislamu wengi kuwavuta Wakristu wachache.

Mkandara, kwa kuwa unaelewa mengine ambayo sie hatuyajui kuhusu TAA unayoijua wewe, tunaomba uandike kitabu kwa manufaa yetu na ya vizazi vijavyo. Ili kama kuna mahali umedanganya ama umeegemea zaidi kwenye "unafsi" basi waliokuwepo ama wanaojua upande mwingine waweze kukukosoa. Unajua nilipoisoma statement yako kichwani mwangu nikakupiga picha kwamba wewe ni 'Muislamu Msomi'. I admire your contributions though.

Leo hii CCJ imeanzishwa na kina Mwanakijiji umuhimu wa kupata wanachama na kufungua Ofisi zao mikoani wanaweza kutumia jumuiya zozote zile kwa malengo waliyokusudia wao. CCJ wanavyodai wao ni chama pekee kilichokuja na Itikadi tofauti na pinzani ya chama CCM....Could be true or not but the history will tell. Lakini nachoweza kusema ni ufanisi wa malengo yao kiitikadi ndiyo yatakayo onyesha tofauti hizo.

On the other hand, mimi najaribu kumuomba sana Mwanakijiji na wanachama wote wa Upinzani waunde UMOJA wa vyama lakini yeye na CCJ wanazo njia zao za kuunda UMOJA huo bila kuunganisha nguvu ya wanachama wa vyama vya Upinzani. Lakini let's say kama wao watakuwa wa kwanza kuwezesha umoja huu naozungumzia mimi (hypothetically).
Kujiunga kwa vyama, wanachama, vikundi vya jumuiya na kadhalika ktk umoja huu hakuwezi kubadilisha maana kwa kutazama Uuwiano wa wajumbe wa mkutano mkuu mwaka kesho..Tena ukiona uuwiano mkubwa wa wanachama wenye itikadi tofauti hii itakuwa ishara nzuri kwamba lengo la CCJ limekamilika zaidi kuliko tukiona wajumbe wa CCJ ndio wamejaa mkutano mkuu. Au nakosea bibie?

Mkandara, you are too obvious kwamba una 'unafsi' dhidi ya Mwanakijiji na pia nadhani mabandiko yako dhidi ya CCJ yana "unafsi" pia ndani yake. Una tatizo gani na CCJ, if I may ask? Kama huoni sababu wala mantiki ya ujio wake then let CCJ be. Kama wewe ni CHADEMA ama TLP you had your oportunity and chances kuunganisha vyama vyote vilivyopo nchini humu. Miaka 15 na hamkuweza kufanikiwa kuifanyia nchi hii yaliyotakikana wala hamkuona kwamba kuungana ni jambo muhimu sana mpaka CCJ kilipojitokeza ndio mnauona umuhimu wake na ku-amplify! Najua wewe binafsi umekuwa ukilipigia kelele jambo hili muhimu. Lakini ni juhudi zipi ulizozionyesha wewe kama wewe nje ya JF kufanikisha au ni michango ya hoja kali ndani ya JF tu? Kama kweli nia yako ni kuona vyama vinaungana basi ungana na Mwanakijiji (anayefanya kweli) kujaribu upya, huenda this time CCJ wanaweza kula mfupa uliomshinda fisi. Who knows!
 
Mkuu Mkandara, you are too obvious kwamba una 'unafsi' dhidi ya Mwanakijiji na pia nadhani mabandiko yako dhidi ya CCJ yana "unafsi" pia ndani yake. Una tatizo gani na CCJ, if I may ask? Kama huoni sababu wala mantiki ya ujio wake then let CCJ be. Kama wewe ni CHADEMA ama TLP you had your oportunity and chances kuunganisha vyama vyote vilivyopo nchini humu. Miaka 15 na hamkuweza kufanikiwa kuifanyia nchi hii yaliyotakikana wala hamkuona kwamba kuungana ni jambo muhimu sana mpaka CCJ kilipojitokeza ndio mnauona umuhimu wake na ku-amplify! Najua wewe binafsi umekuwa ukilipigia kelele jambo hili muhimu. Lakini ni juhudi zipi ulizozionyesha wewe kama wewe nje ya JF kufanikisha au ni michango ya hoja kali ndani ya JF? Kama kweli nia yako ni kuona vyama vinaungana basi ungana na Mwanakijiji (anayefanya kweli) kujaribu upya, huenda this time CCJ wanaweza kula mfupa uliomshinda fisi. Who knows!
.
Bibi Ntilie, tusiupersonalize huu mjadada ukafikia kiwango cha kuonekana ni Mkandala vs Mwanakijiji. Hapo tunabishana kwa hoja, tena ni hoja muhimu sana kwa mustakabali wa taifa letu. Hoja ya Mwanakijiji kuwa CCJ peke yake wanaweza, na hoja ya Mkandala CCJ peke yenu hamuwezi, nami kwa upande wangu, ninasimama na hoja ya Mkandala kuwa CCJ peke yenu hamuwezi hata kwa dawa.

Hoja ya harakati za kupigania uhuru tangu TAA mpaka TANU imeibuliwa na lengo la kusisitiza umuhimu wa ushirikiano na umoja ni nguvu ikijumlisha 'managing divesity' towards the common enemy, ndipo ilipokuja hoja kwanini Julius alipewa ukuu TAA na Hatimaye TANU.

Kuna mambo mengi kwenye historia hayajaandikwa na hayajasemwa hadharani. Hakuna ubishi kuhusu uwezo wa Mwalimu kwenye tasnia ya uongozi, ila wengi wanaamini ni Mwalimu kwa utashi wake mwenyewe, sio wengi wanaojua kuwa Mwalimu alishawishiwa na kupatiwa ahadi fulani ndipo akakubali.

Sio wengi wanaofahamu kuwa Mwalimu alipotoka Pugu, alikuwa hana pa kuishi, bali alifikia moja kwa moja nyumbani kwa kina Sykes pale Ilala Boma, wakati huo John Rupia tayari akiwa ni mmiliki wa yale maghorofa yote matatu yanayozunguka Uhuru Round About. Hakuna watu wanaofahamu Mama Maria alifanya biashara ya kuuza mafuta ya Taa na alifundishwa kupika Chapati na Vitumbua na Mama Sykes for survival.

Pamoja na hitaji la kuutumia uwezo wa Mwalimu, pia umuhimu wa kuutumia Ukristo wake, Ukatoliki kwenye kuwavuta Wakristo pia ulizingatiwa (Rupia ni Anglicana). Hoja hii ndio iliyoingizwa sentments za kidini na kunyumbulishwa, kupinduliwa na kugeuzwa kuwa Wakristu hawakudai uhuru, hoja hapa sio nani alidai uhuru, hoja hapa ni need ya wapinzani kufanya kazi pamoja towards common enemy.

Mwanakijiji anaheshima yake kwa jamii kutokana na maandishi yake, ana nguvu kubwa ya ushawishi, hivyo kitendo tuu cha Mzee Mwanakijiji, kujitanabaisha hadharani kuwa ni miongoni mwa CCJ, kumeleta tumaini jipya kwa watu kama mimi kuwa kama hata Mzee Mwanakijiji anaweza kujiunga CCJ na kupigia debe, then CCJ ni substance is not nothing. Kwangu mimi hata Mpendazoe ni Nothing lakini Mzee Mwanakijiji ni something, ndio maana nikaunga mkono juhudi za Mkandala kumuelimisha Mwanakijiji umuhimu wa 'United we Stand' na akatolea mifano ya kushindwa kwa wapinzani kwenye chaguzi za huko nyuma.

Bibi Ntilie mimi nakusoma kwa great interest haswa unavyokwenda Sambamba na Mwanakijiji in Mwanakijiji Syle " Kama kweli nia yako ni kuona vyama vinaungana basi ungana na Mwanakijiji (anayefanya kweli) kujaribu upya, huenda this time CCJ wanaweza kula mfupa uliomshinda fisi. Who knows!". Ni CCJ gani hiyo inayoweza kuula mfupa uliomshinda fisi ili hali hiyo CCJ hata meno hayajaota, unless otherwize itaota meno ya chuma, hivyo na uchanga wake ndipo ifanikishe huo ufupa uliomshinda fisi, ila kumbuka fisi hawindi mwenyewe, hata simba ambaye ni mnyama mwenye nguvu, hukaa kwa makundi.

Jamani jamani, lets work together, CCJ peke yenu hamuwezi?.
 
.
Bibi Ntilie, tusiupersonalize huu mjadada ukafikia kiwango cha kuonekana ni Mkandala vs Mwanakijiji. Hapo tunabishana kwa hoja, tena ni hoja muhimu sana kwa mustakabali wa taifa letu. Hoja ya Mwanakijiji kuwa CCJ peke yake wanaweza, na hoja ya Mkandala CCJ peke yenu hamuwezi, nami kwa upande wangu, ninasimama na hoja ya Mkandala kuwa CCJ peke yenu hamuwezi hata kwa dawa.

Hakuna anaye-upersonalize mjadala as you put it. Kama mabishano ya hoja bin hoja why mention names in a personal manner badala ya kihoja? Mkandara alikuwa na maana gani kumwambia Mwanakijiji: "Wee nani kusoma vichwani mwa watu? Labda unataka kunambia Bibie Ntilie ni wewe mwenyewe.." Hii ni lugha ya kujenga hoja kweli?

Hoja ya harakati za kupigania uhuru tangu TAA mpaka TANU imeibuliwa na lengo la kusisitiza umuhimu wa ushirikiano na umoja ni nguvu ikijumlisha 'managing divesity' towards the common enemy, ndipo ilipokuja hoja kwanini Julius alipewa ukuu TAA na Hatimaye TANU.

Sawa. Lakini kuibuliwa huko kumeleta mushkeli wa kuona kuna elements za kutaka dini moja ionekane kuwa ndiyo iliyovuta dini nyingine jambo ambalo si kweli na sidhani kwamba hilo lilikuwa ndio lengo la akina Mzee Sykes enzi hizo.

Kuna mambo mengi kwenye historia hayajaandikwa na hayajasemwa hadharani. Hakuna ubishi kuhusu uwezo wa Mwalimu kwenye tasnia ya uongozi, ila wengi wanaamini ni Mwalimu kwa utashi wake mwenyewe, sio wengi wanaojua kuwa Mwalimu alishawishiwa na kupatiwa ahadi fulani ndipo akakubali.

Ndio maana nimemwambia Mkandara naye aandike kitabu kuhusu anayoyajua. Mimi nimetoa nukuu kutoka kwenye kitabu kilichoandikwa na Wasomi waliofanya utafiti kuhusu chama cha TAA na TANU. Kama watafiti hao hawakuandika yote, basi tuleteeni yale mnayoyajua nyie kwamba ndiyo hasa yaliyotokea lakini si kutuambia kwamba Waislamu waliwavuta Wakristo kujiunga na TAA; ipi?

Pia hili la kwamba "ila wengi wanaamini ni Mwalimu kwa utashi wake mwenyewe, sio wengi wanaojua kuwa Mwalimu alishawishiwa na kupatiwa ahadi fulani ndipo akakubali" Nalo naliona lina mushkeli. Nadhani hapa watu wanataka ku'water down' good intentions za Mwalimu kutaka kuingia kwenye siasa bila ushawishi wa aina yoyote ile. Ushawishi gani waliompa? Kwamba akikubali kujiunga nao atakuwa kiongozi wao? Kwa vyovyote vile angelikuwa kiongozi wao tu maana walimuona ana akili ya kuweza kuongoza!

Sio wengi wanaofahamu kuwa Mwalimu alipotoka Pugu, alikuwa hana pa kuishi, bali alifikia moja kwa moja nyumbani kwa kina Sykes pale Ilala Boma, wakati huo John Rupia tayari akiwa ni mmiliki wa yale maghorofa yote matatu yanayozunguka Uhuru Round About. Hakuna watu wanaofahamu Mama Maria alifanya biashara ya kuuza mafuta ya Taa na alifundishwa kupika Chapati na Vitumbua na Mama Sykes for survival.

Hii sio ‘breaking news'. Imo kwenye vitabu walivyoandika watu na hata Mwalimu alikuwa akieleza mara nyingi kwenye hotuba zake. Tatizo ni kwamba Watanzania tu wavivu kusoma mambo yaliyoandikwa na wenzetu huko nyuma tunadhani tukishapata digirii, masters na maPhd basi ndio tumemaliza kila kitu! Twendeni kwenye Taasisi mbalimbali na kwenye Maktaba tusome waliyoandika watu makini juu historia ya nchi yetu. Mkandara anatuambia hatujui yaliyojiri mwaka 1929. Hatuyajui labda kwa sababu hayakuwa na impact ya kutosha kuweza kuwekwa kwenye kumbukumbu!

Pamoja na hitaji la kuutumia uwezo wa Mwalimu, pia umuhimu wa kuutumia Ukristo wake, Ukatoliki kwenye kuwavuta Wakristo pia ulizingatiwa (Rupia ni Anglicana). Hoja hii ndio iliyoingizwa sentments za kidini na kunyumbulishwa, kupinduliwa na kugeuzwa kuwa Wakristu hawakudai uhuru, hoja hapa sio nani alidai uhuru, hoja hapa ni need ya wapinzani kufanya kazi pamoja towards common enemy.

I think you do not get my point. Mkandala hakuwa na sababu ya kuleta hiyohoja in the first place na kudai kwamba wengi hawaupendi ukweli huo. Ukianza kuleta mambo yanayohusiana na dini tupo akina sie ambao hatutaelewa unachotaka katika society ambayo kwa miaka nenda rudi tumekuwa hatuangalii masuala ya dini kwenye siasa. What is the big deal about ukatoliki na u-anglican wa Rupia ama uislamu wa Sykes na Mwapachu? Wote walikuwa ni Watanganyika ambao walikuwa na nia moja ya kutaka kumng'oa mkoloni ili Waafrika wajitawale wenyewe. Hilo ndilo la msingi kulijua kwa nini iwe hoja kutakiwa tujue kwamba Waislamu waliwavuta Wakristu?

Mwanakijiji anaheshima yake kwa jamii kutokana na maandishi yake, ana nguvu kubwa ya ushawishi, hivyo kitendo tuu cha Mzee Mwanakijiji, kujitanabaisha hadharani kuwa ni miongoni mwa CCJ, kumeleta tumaini jipya kwa watu kama mimi kuwa kama hata Mzee Mwanakijiji anaweza kujiunga CCJ na kupigia debe, then CCJ ni substance is not nothing. Kwangu mimi hata Mpendazoe ni Nothing lakini Mzee Mwanakijiji ni something, ndio maana nikaunga mkono juhudi za Mkandala kumuelimisha Mwanakijiji umuhimu wa 'United we Stand' na akatolea mifano ya kushindwa kwa wapinzani kwenye chaguzi za huko nyuma.

Pasco, nakubaliana nawe kuwa Mwanakijiji ana heshima yake kwa jamii kutokana na maandishi yake na nguvu ya ushawishi aliyonayo ambayo nadhani inatushawishi mimi na wewe! Lakini sikubaliana nawe kwa msimamo wako huo wa kusema so and so is something and another one is nothing. Kwa mtazamo wangu kila mtu hata yule aliyeko kijijini asiyejua kusoma wala kuandika, asiyejua tofauti ya CCM na CHADEMA ama NCCR ni something when it comes to mustakabali wa Taifa letu kwa sababu chochote kile kinachoandikwa na Mwanakijiji watu wakakipokea na kukikubali na kinachosemwa na Mpendazoe (uliyemtolea mfano) na watu wakakipokea kwa msingi huo huo kinakuwa na impact kwenye mustakabali wa Taifa letu. Kwa kweli nashindwa kukuelewa unaposema "Mpendazoe is nothing" wakati ndani ya Bunge amekuwa mstari wa mbele kuzungumzia bila woga juu ya uozo ulio ndani ya Serikali ya CCM. Halafu miongoni mwa wanaoitwa vigogo ni yeye aliyesimama ahesabiwe kwamba amechoshwa na yanayoendelea CCM wakati hakuna mwingine yoyote mpaka sasa aliyeweza kuonyesha ujasiri wa aina ya Mpendazoe.

Bibi Ntilie mimi nakusoma kwa great interest haswa unavyokwenda Sambamba na Mwanakijiji in Mwanakijiji Syle " Kama kweli nia yako ni kuona vyama vinaungana basi ungana na Mwanakijiji (anayefanya kweli) kujaribu upya, huenda this time CCJ wanaweza kula mfupa uliomshinda fisi. Who knows!". Ni CCJ gani hiyo inayoweza kuula mfupa uliomshinda fisi ili hali hiyo CCJ hata meno hayajaota, unless otherwize itaota meno ya chuma, hivyo na uchanga wake ndipo ifanikishe huo ufupa uliomshinda fisi, ila kumbuka fisi hawindi mwenyewe, hata simba ambaye ni mnyama mwenye nguvu, hukaa kwa makundi.

Sioni popote ninapokwenda "sambamba ya Mwanakijiji in Mwanakijiji style" zaidi ya kueleza yale ninayoyaona na kufikiria. Mwanakijiji simjui hanijui zaidi ya kukutana humu JF. Je nawe niseme unaenda sambamba na Mkandara style? Kama ilivyo kwa Mkandara, michango yenu ndani ya JF ni ya maana sana maana naamini inatolewa kwa nia njema kabisa kutaka tufike huko tunakotarajia kwenda kwa mustakabali mwema wa taifa letu. Lakini kosa mnalofanya ni kuanza kuweweseka sana na kuhangaika na speculations juu ya chama ambacho wala hata hakijapata usajili wa kudumu na huenda kisipate.

Jamani jamani, lets work together, CCJ peke yenu hamuwezi?.

Umesema kwamba CCJ hakina meno ya kuweza kula mfupa. Lakini je unakubaliana nami kwamba vyama vya upinzani vilivyopo mpaka sasa vimeshindwa ku-deliver? Pia sidhani kwamba kuna anayepinga umuhimu wa vyama kuungana ama kudai kwamba CCJ peke yao wanaweza. Ninachosema mie ni kwamba waacheni CCJ nao wafanye kile watakachoweza. Wakipata usajili wa muda na kuingia kwenye ulingo wa siasa za nchi wanaweza kutoa mchango mkubwa katika kufanikisha kuunganisha vyama vya upinzani! Who knows…..!

Pasco, tatizo lenu mnataka mjue kila kitu kinachohusu CCJ wakati chama chenyewe kama ulivyosema mwenyewe - hata meno hayaanza kuota!
 
Mkandara, you are too obvious kwamba una 'unafsi' dhidi ya Mwanakijiji na pia nadhani mabandiko yako dhidi ya CCJ yana "unafsi" pia ndani yake. Una tatizo gani na CCJ, if I may ask? Kama huoni sababu wala mantiki ya ujio wake then let CCJ be. Kama wewe ni CHADEMA ama TLP you had your oportunity and chances kuunganisha vyama vyote vilivyopo nchini humu. Miaka 15 na hamkuweza kufanikiwa kuifanyia nchi hii yaliyotakikana wala hamkuona kwamba kuungana ni jambo muhimu sana mpaka CCJ kilipojitokeza ndio mnauona umuhimu wake na ku-amplify! Najua wewe binafsi umekuwa ukilipigia kelele jambo hili muhimu. Lakini ni juhudi zipi ulizozionyesha wewe kama wewe nje ya JF kufanikisha au ni michango ya hoja kali ndani ya JF tu? Kama kweli nia yako ni kuona vyama vinaungana basi ungana na Mwanakijiji (anayefanya kweli) kujaribu upya, huenda this time CCJ wanaweza kula mfupa uliomshinda fisi. Who knows!

Hapa kina Mkandara tupo wengi sana....CCJ!!! Mhhhh

omarilyas
 
Ninaamini CCJ itapata usajili wa Kudumu na itashirikiana na vyama vingine japo kuongeza idadi ya Wabunge wa kambi ya Upinzani ndani ya Bunge, naamini kuna maeneo itakubalika na kuna maeneo haitakubalika sana, jambo la msingi ni kupata bungelitakalokuwa na uwezo wa kutengeza Msingi wa Mabadiliko katika Mfumo Mzima wa Taifa hili. Bila Bunge Imara kulibadili hili taifa ni vigumu sana. Cha Msingi CCJ ijitengenezee mazingira Mazuri ya kuaminika na kuweza kushirikiana na vyama vilivyopo. Hapa sizungumzii Chama kimoja kukiunga mkono chama kingine la hasha bali vyama kutambua ni wapi kila kimoja kina nguvu na wapi kingine kina nguvu ili viweze kuachiana majombo
 
.
Bibi Ntilie, tusiupersonalize huu mjadada ukafikia kiwango cha kuonekana ni Mkandala vs Mwanakijiji. Hapo tunabishana kwa hoja, tena ni hoja muhimu sana kwa mustakabali wa taifa letu. Hoja ya Mwanakijiji kuwa CCJ peke yake wanaweza, na hoja ya Mkandala CCJ peke yenu hamuwezi, nami kwa upande wangu, ninasimama na hoja ya Mkandala kuwa CCJ peke yenu hamuwezi hata kwa dawa..

Inategemea wanaweza nini na kwa manufaa ya nani na kwa muda gani......Hata mtandao wameweza kufanikisha yale mapinduzi ya chimwaga 2010....lakini jee kwa ajili gani na kwa faida ya nani?

omarilyas
 
Hebu tukubaliane kwa sekunde chache kuwa CCJ haiwezi, haipaswi kuweza na haitoweza hata "kwa dawa". Nani anaweza? Tunaambiwa kuwa muungano wa vyama vya upinzani peke yake utaweza. Hii ina sauti nzuri na inavutia hisia kwa sababu haina lengo la kusema ukweli. Tunatakiwa kupendekezewa kuwa ati vya vikiungana ndio itawezekena really?

a. Kwa miaka 15 haja ya muungano wa vyama vya upinzani imekuwepo na wengine tulikuwa nayo vile vile lakini kwa miaka 15 huu muungano haujafanikiwa. Ndugu zetu watetezi wa muungano huu wa upinzani hawawajaribu kutuambia kwa kina kwanini umeshindikana lakini sasa hivi unawezekana.

b. Tangu vyama vingi virejee nchini kumekuwepo na uchaguzi, 1995, 2000, na 2005 katika chaguzi hizo zote wimbo wa "wapinzani waungane" umerudiwa na kuwa kibwagizo cha kisiasa nchini na kama muziki usio na ala wapinzani wameshindwa kuungana. Hatuambiwi kwanini ila katika uchaguzi huu 2010 ati muungano utakuwa ni bora na unafaa na utawezekana.

c. Najua hoja nyingi zinazotolewa juu ya kushindikana kwa muungano zinakimbilia kudai ni "ubinafsi wa viongozi" kwani kila kiongozi wa upinzani "anataka kuwa yeye". Jibu laweza kuvuta hisia lakini halina msingi katika uhalasia. Na watu hawataki kukubali kuwa kuna makubwa zaidi ya ubinafsi. Watetezi hawa wa muungano wanataka tuamini kuwa sasa hivi huo "ubinafsi" mwaka huu umeisha. Kwamba mwaka huu kwa sababu watu wameamka na kujua zaidi basi muungano utafanikiwa. Tunawauliza huo ubinafsi umeisha lini?

Sasa licha ya hayo yote hapo juu watetezi wetu wa muungano "usio na msingi" wanataka upinzani uungane ili tu uing'oe CCM. Kwa haraka na kwa wengi hili ni lengo zuri, lakini ni lengo hafifu na lisilo na msingi wa kusimamia. Ati "kuindoa CCM madarakani" ndio liwe lengo la msingi vinginevyo itaendelea kutawala. Well.. kwa haraka na kwa wenye hisia hili ni jambo jema. Lakini tukiliangalia kwa ukaribu tutaona hatari yake na ni kwanini ni jambo la kuepuka.

- Huwezi kuunganisha vyama kwa lengo la kuondoa chama kingine madarakani wakati vyama hivyo vina tofauti za itikadi na sera. Vikishinda vitaongoza kwa sera za chama gani?
- Huwezi kuunganisha watu wenye malengo tofauti yanayotokana na vyama vyao huku vikiwa vimeahidiana nafasi mbalimbali halafu vikiingia madarakani baada ya kuiangusha CCM vianze kuulizana na kudaiana na baadaye kuvutana huku Watanzania wanaanza kulalamika tena kwanini "wapinzani hawapatani". Muungano wa kuindoa CCM ni muungano hatari.
- Huwezi kuunganisha vyama vyenye mitazamo tofauti na sera tofauti za kushughulikia matatizo ya nchi ukatarajia ati vikiingia madarakani vitapatana jinsi ya kufanya hivyo. Hii ni kuwa naive. Nchi huongozwa kwa sera na sera hujenga sheria na sheria hujenga maamuzi mbalimbali ya kiutendaji. Sasa mnapokuwa na vyama vyenye sera tofauti wakati mmekiondoa chama chenye sera moja hivyo vyama vitaweza vipi kutawala taifa huku kimoja bado kikiwa na malengo na sera zake?

Lakini zaidi cha kushangaza ambacho watetezi hawa wa muungano wanashindwa kutuambia ni kuwa haya "maslahi ya taifa" ya taifa yatakayotokana na kuondolewa CCM madarakani na kuingia kwa muungnao wa upinzani usiokuwa na madhumuni, sera, malengo, au njia wanazokubaliana kutawala taifa ni maslahi yapi? Haiwezekani kusema ati kuondoka CCM madarakani ndio "maslahi ya taifa". Hizo ni semantics mumbo jumbo! Maslahi ya taifa ni mambo mema ambayo yatatokea kwa CCM kutoka madarakani siyo CCM KUTOKA MADARAKANI. Naomba watetezi wa muungano mtuanishie maslahi ya taifa ambayo yatatokea kwa CCM kuondolewa madarakani na muungano ambao haujaunganisha malengo, madhumuni, itikadi, sera wala mwelekeo wa taifa:

Sasa, binafsi nilishaandika huko nyuma vile vile kuwa Chadema isiungane na chama kingine. Kanuni ile ile ndio imeniongoza wakati huu. Kinachohitajika nchini dhidi ya CCM ni chama kingine chenye nguvu, chenya sera inayokubalika, maono ya kitaifa, uongozi uliokomaa, na mwelekeo usio na shaka. Chama hicho kingetumia muda kujijenga peke yake kingeweza kabisa kuiangusha CCM. Hata hivyo siyo chadema wala cuf wala tlp ambavyo vimetaka kutumia muda uliopita kujijenga kuweza kushika uongozi wa taifa. Wote wana malengo ya kuindoa CCM madarakani na hawaoni tatizo la kifalsafa la mawazo hayo.

KUONDOLEWA CCM MADARAKANI ni lazima kuwe ni MATOKEO na siyo LENGO la chama cha upinzani. Kwamba, kutokana na kukubalika kwa sera, mipango, uongozi, siasa na mapendekezo ya kushughulikia matatizo ya wananchi na kujenga taifa basi wananchi wanaamua kuchagua chama hicho kingine na kwa kufanya kwao hivyo wanajikuta wameiondoa CCM madarakani. Hivyo, CCM itaondolewa kwa sababu wananchi wamepata kitu bora na cha kuwafaa kwa maisha yao; wamepata mbadala wa kweli wa kisiasa na kiuongozi na wakauchagua.

Naomba nieleweke vizuri. Kama CCJ itashindwa kupewa usajili wa kudumu au nafasi ya kushindwa kushiriki uchaguzi bado nitaunga mkono upinzani. Lakini sitounga mkono umoja wa upinzani usio na msingi. Nitachagua chama kingine ambacho naamini kinaweza kuja na sera, mikakati na itikadi inayolifaa taifa. SIWEZI kuunga mkono upinzani kwa minajili tu ya kuiangusha CCM; huo ni mtazamo wa hatari. Siwezi kuunga mkono upinzani ilimradi nionekane niko kinyume na CCM wakati sikubaliani na sera, mikakati au itikadi zao; siwezi kuunga mkono upinzani kwa sababu ati nachukia CCM. Muungano wa chuki hauwezi kudumu kwa sababu chuki kama chuki inatabia ya kumtafuna mwenye nayo.

Sasa, naomba nitoe changamoto kwa watetezi wa muungano wa upinzani; NAOMBA mchague mambo matano tu ya msingi ambayo yawe sababu ya vyama vya upinzani kukubaliana kuungana na mambo hayo yakigombaniwa kwa pamoja yatasababisha wananchi wauchague umoja wa upinzani na kwa kufanya hivyo watakuwa wameichagulia CCM kuondoka madarakani. Katika mambo hayo matano - KUINDOA CCM MADARAKANI kusiwe mojapo. Yaani, mambo matano ambayo wapinzani wakikubaliana kuhusu muundo wa serikali yao, kuhusu namna ya kutawala, kuhusu kugawana madaraka kati yao, kuhusu sera za elimu, afya, miundo mbinu, kilimo, sayansi na teknolojia, na kuhusu mambo ya uongozi wa juu wa taifa. Naomba mnipe mambo MATANO TU ambayo yaweza kuwa msingi wa ushirikiano au muungano wa upinzani ambayo yanaweza kusababisha CCM itolewe madarakani kwenye sanduku la kura.

Msiendelee kuniimbia wimbo kuwa hakiingii kichwani, au kichwa changu kigumu, au ni mdini au maneno mengine yoyote ya kushambulia nafsi yangu badala ya hoja. JENGENI HOJA YA MSINGI WA USHIRIKIANO WA UPINZANI AMBAYO INAWEZA KUSABABISHA CCM KUONDOLEWA MADARAKANI. Msiimbe tu "tuungane tuungane" maana kama ingekuwa rahisi hivyo na muhimu hivyo kwanini vyama vilivyopo sasa vimeshindwa kuungana hadi hivi sasa? Kwanini hata kwenye chaguzi ndogo ambapo ingekuwa rahisi zaidi kama kule Mbeya Vijiji walishindwa kuungana? Kwanini hata kama wameshindwa kuungana Tanzania nzima wameshindwa kuungana Jiji la Dar tu au Arusha au Mwanza kuiangusha CCM kwenye maeneo hayo?

Watetezi hamtaki kujua sababu?
 
Mkuu Mwanakijiji Kimsingi nakubaliana na Hoja zako nyingi, napingana na wewe kama msimamo wako ni kwamba Vyama viende kwenye Uchaguzi kila mtu kivyake hapana mkuu hilo litakuwa ni kosa kubwa sana, mimi naomba niwe kati kati yaani napenda kuwe na Partial Muungano hasa katika Nafasi Za Ubunge. Mimi naungalia Uchaguzi huu kama Msingi wa Kuleta Mabadiliko makubwa katika kipindi cha 2010/2015. Na Mabadiliko hayo hayawezi kuwepo kama tutaruhusu Kamati ya CCM ( Namaanisha bunge lililosheheni CCM) itutungie sheria katika kipindi hicho. Ni Lazima tukubali kwamba tunahitaji bunge lenye nguvu ili tuweke bases kuelekea Mabadiliko ya Kimfumo tunayoyahitaji na hilo halitowezekana kwa Vyama vya Upinzani kwenda man to man katika Majimbo yote si CHADEMA si CUF si CCJ watakaoweza kupata wabunge wengi bila ya KUACHIANA MAJIMBO. Mkuu Nataka USHIRIKIANO na SI KUUNGANISHA vyama ili tuwe na Uwakilishi wenye Nguvu
 
Kinachohitajika nchini dhidi ya CCM ni chama kingine chenye nguvu, chenya sera inayokubalika, maono ya kitaifa, uongozi uliokomaa, na mwelekeo usio na shaka. Chama hicho kingetumia muda kujijenga peke yake kingeweza kabisa kuiangusha CCM. Hata hivyo siyo chadema wala cuf wala tlp ambavyo vimetaka kutumia muda uliopita kujijenga kuweza kushika uongozi wa taifa. Wote wana malengo ya kuindoa CCM madarakani na hawaoni tatizo la kifalsafa la mawazo hayo.

Na pindi hilo likitokea vyama vingine vitajifia kifo cha kawaida, mbona hatujiulizi pamoja na uwepo kwa vyama 18 bado vyama hivyo havina athari yoyote katika kupunguza kura za CUF Zanzibar?wananchi wa tanzania bara bado hawakiona chama cha kukiamini na wala tatizo sio uwingi wa vyama.
 
Hebu tukubaliane kwa sekunde chache kuwa CCJ haiwezi, haipaswi kuweza na haitoweza hata "kwa dawa". Nani anaweza? Tunaambiwa kuwa muungano wa vyama vya upinzani peke yake utaweza. Hii ina sauti nzuri na inavutia hisia kwa sababu haina lengo la kusema ukweli. Tunatakiwa kupendekezewa kuwa ati vya vikiungana ndio itawezekena really?

a. Kwa miaka 15 haja ya muungano wa vyama vya upinzani imekuwepo na wengine tulikuwa nayo vile vile lakini kwa miaka 15 huu muungano haujafanikiwa. Ndugu zetu watetezi wa muungano huu wa upinzani hawawajaribu kutuambia kwa kina kwanini umeshindikana lakini sasa hivi unawezekana.

b. Tangu vyama vingi virejee nchini kumekuwepo na uchaguzi, 1995, 2000, na 2005 katika chaguzi hizo zote wimbo wa "wapinzani waungane" umerudiwa na kuwa kibwagizo cha kisiasa nchini na kama muziki usio na ala wapinzani wameshindwa kuungana. Hatuambiwi kwanini ila katika uchaguzi huu 2010 ati muungano utakuwa ni bora na unafaa na utawezekana.

c. Najua hoja nyingi zinazotolewa juu ya kushindikana kwa muungano zinakimbilia kudai ni "ubinafsi wa viongozi" kwani kila kiongozi wa upinzani "anataka kuwa yeye". Jibu laweza kuvuta hisia lakini halina msingi katika uhalasia. Na watu hawataki kukubali kuwa kuna makubwa zaidi ya ubinafsi. Watetezi hawa wa muungano wanataka tuamini kuwa sasa hivi huo "ubinafsi" mwaka huu umeisha. Kwamba mwaka huu kwa sababu watu wameamka na kujua zaidi basi muungano utafanikiwa. Tunawauliza huo ubinafsi umeisha lini?

Sasa licha ya hayo yote hapo juu watetezi wetu wa muungano "usio na msingi" wanataka upinzani uungane ili tu uing'oe CCM. Kwa haraka na kwa wengi hili ni lengo zuri, lakini ni lengo hafifu na lisilo na msingi wa kusimamia. Ati "kuindoa CCM madarakani" ndio liwe lengo la msingi vinginevyo itaendelea kutawala. Well.. kwa haraka na kwa wenye hisia hili ni jambo jema. Lakini tukiliangalia kwa ukaribu tutaona hatari yake na ni kwanini ni jambo la kuepuka.

- Huwezi kuunganisha vyama kwa lengo la kuondoa chama kingine madarakani wakati vyama hivyo vina tofauti za itikadi na sera. Vikishinda vitaongoza kwa sera za chama gani?
- Huwezi kuunganisha watu wenye malengo tofauti yanayotokana na vyama vyao huku vikiwa vimeahidiana nafasi mbalimbali halafu vikiingia madarakani baada ya kuiangusha CCM vianze kuulizana na kudaiana na baadaye kuvutana huku Watanzania wanaanza kulalamika tena kwanini "wapinzani hawapatani". Muungano wa kuindoa CCM ni muungano hatari.
- Huwezi kuunganisha vyama vyenye mitazamo tofauti na sera tofauti za kushughulikia matatizo ya nchi ukatarajia ati vikiingia madarakani vitapatana jinsi ya kufanya hivyo. Hii ni kuwa naive. Nchi huongozwa kwa sera na sera hujenga sheria na sheria hujenga maamuzi mbalimbali ya kiutendaji. Sasa mnapokuwa na vyama vyenye sera tofauti wakati mmekiondoa chama chenye sera moja hivyo vyama vitaweza vipi kutawala taifa huku kimoja bado kikiwa na malengo na sera zake?

Lakini zaidi cha kushangaza ambacho watetezi hawa wa muungano wanashindwa kutuambia ni kuwa haya "maslahi ya taifa" ya taifa yatakayotokana na kuondolewa CCM madarakani na kuingia kwa muungnao wa upinzani usiokuwa na madhumuni, sera, malengo, au njia wanazokubaliana kutawala taifa ni maslahi yapi? Haiwezekani kusema ati kuondoka CCM madarakani ndio "maslahi ya taifa". Hizo ni semantics mumbo jumbo! Maslahi ya taifa ni mambo mema ambayo yatatokea kwa CCM kutoka madarakani siyo CCM KUTOKA MADARAKANI. Naomba watetezi wa muungano mtuanishie maslahi ya taifa ambayo yatatokea kwa CCM kuondolewa madarakani na muungano ambao haujaunganisha malengo, madhumuni, itikadi, sera wala mwelekeo wa taifa:

Sasa, binafsi nilishaandika huko nyuma vile vile kuwa Chadema isiungane na chama kingine. Kanuni ile ile ndio imeniongoza wakati huu. Kinachohitajika nchini dhidi ya CCM ni chama kingine chenye nguvu, chenya sera inayokubalika, maono ya kitaifa, uongozi uliokomaa, na mwelekeo usio na shaka. Chama hicho kingetumia muda kujijenga peke yake kingeweza kabisa kuiangusha CCM. Hata hivyo siyo chadema wala cuf wala tlp ambavyo vimetaka kutumia muda uliopita kujijenga kuweza kushika uongozi wa taifa. Wote wana malengo ya kuindoa CCM madarakani na hawaoni tatizo la kifalsafa la mawazo hayo.

KUONDOLEWA CCM MADARAKANI ni lazima kuwe ni MATOKEO na siyo LENGO la chama cha upinzani. Kwamba, kutokana na kukubalika kwa sera, mipango, uongozi, siasa na mapendekezo ya kushughulikia matatizo ya wananchi na kujenga taifa basi wananchi wanaamua kuchagua chama hicho kingine na kwa kufanya kwao hivyo wanajikuta wameiondoa CCM madarakani. Hivyo, CCM itaondolewa kwa sababu wananchi wamepata kitu bora na cha kuwafaa kwa maisha yao; wamepata mbadala wa kweli wa kisiasa na kiuongozi na wakauchagua.

Naomba nieleweke vizuri. Kama CCJ itashindwa kupewa usajili wa kudumu au nafasi ya kushindwa kushiriki uchaguzi bado nitaunga mkono upinzani. Lakini sitounga mkono umoja wa upinzani usio na msingi. Nitachagua chama kingine ambacho naamini kinaweza kuja na sera, mikakati na itikadi inayolifaa taifa. SIWEZI kuunga mkono upinzani kwa minajili tu ya kuiangusha CCM; huo ni mtazamo wa hatari. Siwezi kuunga mkono upinzani ilimradi nionekane niko kinyume na CCM wakati sikubaliani na sera, mikakati au itikadi zao; siwezi kuunga mkono upinzani kwa sababu ati nachukia CCM. Muungano wa chuki hauwezi kudumu kwa sababu chuki kama chuki inatabia ya kumtafuna mwenye nayo.

Sasa, naomba nitoe changamoto kwa watetezi wa muungano wa upinzani; NAOMBA mchague mambo matano tu ya msingi ambayo yawe sababu ya vyama vya upinzani kukubaliana kuungana na mambo hayo yakigombaniwa kwa pamoja yatasababisha wananchi wauchague umoja wa upinzani na kwa kufanya hivyo watakuwa wameichagulia CCM kuondoka madarakani. Katika mambo hayo matano - KUINDOA CCM MADARAKANI kusiwe mojapo. Yaani, mambo matano ambayo wapinzani wakikubaliana kuhusu muundo wa serikali yao, kuhusu namna ya kutawala, kuhusu kugawana madaraka kati yao, kuhusu sera za elimu, afya, miundo mbinu, kilimo, sayansi na teknolojia, na kuhusu mambo ya uongozi wa juu wa taifa. Naomba mnipe mambo MATANO TU ambayo yaweza kuwa msingi wa ushirikiano au muungano wa upinzani ambayo yanaweza kusababisha CCM itolewe madarakani kwenye sanduku la kura.

Msiendelee kuniimbia wimbo kuwa hakiingii kichwani, au kichwa changu kigumu, au ni mdini au maneno mengine yoyote ya kushambulia nafsi yangu badala ya hoja. JENGENI HOJA YA MSINGI WA USHIRIKIANO WA UPINZANI AMBAYO INAWEZA KUSABABISHA CCM KUONDOLEWA MADARAKANI. Msiimbe tu "tuungane tuungane" maana kama ingekuwa rahisi hivyo na muhimu hivyo kwanini vyama vilivyopo sasa vimeshindwa kuungana hadi hivi sasa? Kwanini hata kwenye chaguzi ndogo ambapo ingekuwa rahisi zaidi kama kule Mbeya Vijiji walishindwa kuungana? Kwanini hata kama wameshindwa kuungana Tanzania nzima wameshindwa kuungana Jiji la Dar tu au Arusha au Mwanza kuiangusha CCM kwenye maeneo hayo?

Watetezi hamtaki kujua sababu?

Mwanakijiji nakubaliana na wewe na baadhi ya hoja zako..Vyama kushindwa kuungana huko nyuma hakumaanishi ndio kushindwa leo,inawezekana ilishindikana huko nyuma lakini leo ikawezekana siasa haina fomula wala kanuni..Natambua kwa muda uliobaki hili practically haliwezekani..Hoja yangu ni kuwa muda umebaki mchache na CCJ bado haijui hatima yake.Mimi ningeshauri vigogo wanaounda CCJ basi wawe na alternative ya nini cha kufanya ili wasikose haki yao ya kuongoza taifa hili kwa kiwango cha uwajibikaji wa kweli kwenye uchaguzi wa mwaka huu..Muda umeisha they have to decide now..Dalili zinaonyesha mambo sio marahisi kama ilivyotarajiwa
 
Mkuu Mwanakijiji Kimsingi nakubaliana na Hoja zako nyingi, napingana na wewe kama msimamo wako ni kwamba Vyama viende kwenye Uchaguzi kila mtu kivyake hapana mkuu hilo litakuwa ni kosa kubwa sana, mimi naomba niwe kati kati yaani napenda kuwe na Partial Muungano hasa katika Nafasi Za Ubunge.

NyU, sawa tukubaliane wanasimamisha mgombea mmoja wa Ubunge kwa mfano jimbo la Ilala. Je atakuwa ni mgombea wa chama kipi, anapatikana vipi na akishinda anatekeleza sera zipi au kwa vile ameshinda ndio utakuwa mwisho - maana wa CCM atakuwa ameangushwa! Wakishapata hicho kiti inakuwaje? Je anapolipwa mshahara na marupurupu vyote vinakwenda kwenye chama chake au anagawia kidogo vyama vilivyokubali kumsimamisha?


Mimi naungalia Uchaguzi huu kama Msingi wa Kuleta Mabadiliko makubwa katika kipindi cha 2010/2015. Na Mabadiliko hayo hayawezi kuwepo kama tutaruhusu Kamati ya CCM ( Namaanisha bunge lililosheheni CCM) itutungie sheria katika kipindi hicho. Ni Lazima tukubali kwamba tunahitaji bunge lenye nguvu ili tuweke bases kuelekea Mabadiliko ya Kimfumo tunayoyahitaji na hilo halitowezekana kwa Vyama vya Upinzani kwenda man to man katika Majimbo yote si CHADEMA si CUF si CCJ watakaoweza kupata wabunge wengi bila ya KUACHIANA MAJIMBO.

Hili si tatizo kuachiana majimbo. Sasa wakishaachiana majimbo na wakajazana Bungeni watunge sheria sivyo? Wanafuata sera za nani na zipi katika kutunga sheria hizo? Je watatakiwa kusikiliza vyama vyao? Itakuwaje kama kwenye sheria vyama vinapinganawakati vina wabunge wa kutosha nini kitazuia baadhi yao kupiga kura na CCM?

Mkuu Nataka USHIRIKIANO na SI KUUNGANISHA vyama ili tuwe na Uwakilishi wenye Nguvu

Sawa.. sasa mtakuwa mnawakilisha nini? kuiondoa CCM?
 
Mwanakijiji nakubaliana na wewe na baadhi ya hoja zako..

Ni baadhi ya hoja zipi unakubaliana nazo? Binafsi kama Chadema inataka kwenda ilivyo (endapo CCJ itanyimwa) niko tayari kuinga mkono lakini siwezi kuiunga mkono kwa lengo la kuiondoa CCM madarakani kwani ni msingi mbovu wa kuchagua watu. Ni lazima uwe ni uungwaji mkono wa kukubaliana na sera na itikadi yao. Kwa sasa ni ngumu mno kufanya hivyo kwa sababu wao wana mwelekeo wa Kiliberali na mimi nina mwelekeo wa wa mrengo wa kulia.
 
Ni baadhi ya hoja zipi unakubaliana nazo? Binafsi kama Chadema inataka kwenda ilivyo (endapo CCJ itanyimwa) niko tayari kuinga mkono lakini siwezi kuiunga mkono kwa lengo la kuiondoa CCM madarakani kwani ni msingi mbovu wa kuchagua watu. Ni lazima uwe ni uungwaji mkono wa kukubaliana na sera na itikadi yao. Kwa sasa ni ngumu mno kufanya hivyo kwa sababu wao wana mwelekeo wa Kiliberali na mimi nina mwelekeo wa wa mrengo wa kulia.
Za kutounga mkono chama chochote cha upinzani kwasababu ya kuion'goa CCM madarakani kwani naamini lengo si kuwa madarakani tu.Mrengo wa CHADEMA ni Center Right....Ni vema vigogo wote wa CCJ wakaunga mkono CHADEMA kwakuwa vinafanana sana kimtazamo na hata kiitikadi..
 
Back
Top Bottom