CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

GS, ngoja nikae chini na kuchanganua matatizo ya sera za CHADEMA na ni kwanini ni kinyume na zile za CCJ. Kuamini vitu vile vile au kwa karibu haina maana mtatumia njia zile zile kwa sababu yote uliyoyasema kuhusu imani za Chadema yaweza kuwa ni imani ya CCM vile viile!

Utatumia nguvu nyingi sana kuchanganua tofauti ya itikadi katika vyama vyetu, na unaweza usifanikiwe. Muhimu zaidi, kufikiri kwamba matatizo yetu yanatokana na itikadi mbaya au kutokuwa na itikadi inaweza ikawa very simplistic, na tunaweza tukawa tunajaribu kutibu malaria kwa tumia panadol, hatutapona!!
 
Mkuu hayo maswali yako yanachanganya kwa sababu wewe hutaki kusema malengo yako isipokuwa ya wengine. Sema wewe malengo ya CCJ kisha tuone kama kuna watu hawakubaliani nayo..Nijuavyo tunakubaliana na hoja zetu kama tunavyokubaliana na hizo za Chadema - REFORM inahitajika..Na sote hapa tumefikia kutoa ushauri wetu ni kwa sababu tunaamini katika vyama vyote wapo wananchama na watu wanaotaka mageuzi (changes) ambayo ndio msingi wa muungano huu.

Kuna mambo ambayo ni ya msingi karibu vyama vyote vinakubaliana; hata hayo ambayo wanasema Chadema ni ya kwao utaona kwa karibu CCM inayakubali in principle. Kwa hiyo siyo katika malengo bali katika mbinu za kuyafikia malengo hayo vile vile.

Hebu tuangalie kama malengo na imani za Chadema ni kinyume na imani za CCM au zinafanana:

Chadema inasema:

Falsafa ni fikra na mtazamo wa Chama ambayo ni kuamini katika “Nguvu na Mamlaka ya Umma” (The People’s Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasilimali, uchumi na siasa ya nchi yao

CCM inasema:

Lengo la Ujamaa na Kujitegemea ni kuhakikisha kuwa uchumi wa Tanzania unamilikiwa na kuendeshwa na wananchi wenyewe kwa njia mbalimbali.

Chadema inasema:

Nguvu na Mamlaka ya Umma” ndiyo msingi na chimbuko la kuundwa dola ya nchi, na kuwa, Umma ndiyo wenye madaraka ya mwanzo na ya mwisho katika kuamua hatima ya nchi na taifa pasipo kuingiliwa, kudanganywa au kughilibiwa na viongozi, watawala au wageni.
Ujenzi na udumishaji wa Demokrasia na Maendeleo nchini vitatokana na Nguvu na Mamlaka ya Umma wa Watanzania. Nguvu na Mamlaka ya Umma itabainishwa, kuainishwa na kulindwa katika Katiba ya nchi na Umma ndiyo utakuwa chimbuko la Katiba hiyo.

CCM inasema hivi:


Dhana ya Sekta Binafsi ina maana pana zaidi kuliko ilivyo dhana ya
ubinafsishaji. Kimsingi ni dhana inayomaanisha kuwapa watu binafsi, yaani wananchi walio wengi fursa ya kumiliki na kuendesha uchumi moja kwa moja badala ya kupitia sekta ya dola.

ukiangalia mambo ambayo Chadema inasimamia utaona kuwa hayapingani kabisa na yale ambayo CCM inasimamia hasa ukisoma nyaraka zao.

Sasa kama kuangalia malengo peke yake ndio sababu ya kuungana au kushirikiana ni wazi kuwa Chadema inakubaliana zaidi na CCM kuliko CCJ! Wao wangefanya jitihada ya kutafuta ushirikiano na CCM kama malengo yao yanafanana.

Kama nilivyosema hapo awali hakuna chama Tanzania chenye itikadi, ila ni mawazo ya kutuwezesha kutoka ktk Umaskini. Mapungufu ya CCM sii mapungufu ya chama ila makosa ya viongozi wake wameshindwa kutuondoa ktk Umaskini..Navyojua mimi hili ndio chimbuko la vyama vyote vya Upinzani nchini kuzaliwa kwake.

Kama hili ni kweli viongozi wa Chadema wahamie CCM ili kukipa uongozi unaohitajika.

Mzee Mtei kutokubaliana na Nyerere na Ujamaa haina maana ilikuwa itikadi ya kisiasa ila dhidi ya mfumo wa Uchumi. Mrema na NCCR haikuwa kupinga Ubepari bali kupinga mfumo wa Uongozi ktk kukuza uchumi wetu kwa kutumia wageni (Wakaburu). Hivyo hiyvo vyama vyote vimeundwa kwa kutazama zaidi mapungufu ya Uongozi na sio mapungufu ya Itikadi kwani hatujawahi kutumia itikadi yoyote kiutawala toka tumeacha Ujamaa.

Hilo ni kweli na ndio sababu ya CCJ kutaka kulisahihisha. Chadema kiitikadi haina tofauti na CCM.

Nadhani utarurahishia sote ukiweka malengo ya CCJ hapa ukumbini na vizuri zaidi ikiwa malengo hayo yatazungumzwa na wahusika (vyama vingine) zaidi yetu sisi kwani huko ndiko utapata majibu yenye kuthibitisha muungano huu utakuwa wa aina gani. Mkubaliane msikubaliane swala la ushindi dhidi ya CCM ni lazima kuwepo na UMOJA wenu ktk hatua za awali, kinyume cha hapo itakuwa kazi kubwa sana kuushawishi Umma ikiwa vyama vyote vinahadithia hadithi ile ile...Utawala wa CCM ni Mafisadi!

Umoja unaofanana kimalengo na CCM ni umoja wa namna gani huu. Ni bora tupiganie turudi kwenye chama kimoja kwa sababu vyama vyote kwa kuangalia malengo tu vinafanana.
 
Really? This is certainly big news to me. I have to revisit my ideological class!!

You will have to if to you "ujamaa" I'm talking about is the same as the classical socialism of Marx and Lenin.. I'm not. My definition of Ujamaa is fundamentally that is more conservative and based mostly on Nyerere's understanding of Ujamaa. So, I would suggest you read "Nyerere's Ujamaa" to get a glimpse of what I'm talking about because I'm quite sure this "ujamaa" is not being taught in our schools anymore.
 
MMM
Kuhusu hiyo hoja hapo juu, kuachiana majimbo ni kutathmini kila chama kinaelewa maeneo ambayo kinakubalika zaidi hivyo basi ni budi kuongeza juhudi huko kuliko kwenda kwenye majimbo ambayo chama kinajua wazi kuwa uwezo wa kushinda ni mdogo. Makubaliana hayo ni juu ya viongozi wa vyama husika kuamua ndio kukomaa kisiasa huko na mojawapo ya njia za kuwatoa CCM, as is now ni kuwa na uroho wa kisiasa yaani ni wazi majimbo mengine wanajua wazi kuwa CCM iko mbele na wanaona ni bora wote wakose...Kanuni za makubaliano ni wazi lazima waangalie nani zaidi ama kwa kutumia opinion polls au historical voting patern za maeneo husika. Ni lazima viongozi wakubali kuwa ili mabadiliko ya kweli yaje Tz ni muhimu kuwa na aina moja au nyingine ya ushirikiano kwenye upinzani, jinsi ilivyo sasa kwa upinzani kushika mamlaka ya dola ni kujidanganya tu na kuota ndoto za alinacha.

Kuhusu swala lako hapo juu ni wazi kuwa kama kungekuwa na chama kimoja cha upinzani chenye nguvu ni bora zaidi ya utitiri wa vyama bungeni hiyo ni wazi angalia Marekani (mainly 2 political parties )au hata UK (mainly 3 parties). Sasa hapa kwetu kweli inaumiza kichwa. Kama mtu unataka mageuzi (ng'oa CCM) halafu siku ya uchaguzi unapatwa na mchecheto nani niwape kura yangu CUF, Chadema, UDP au CCJ?
 
Hivi vyama vyetu vingi unaweza kusema kuwa ni centrist rather than left or right. In the Us same story Democrats they are not a leftist party bu any means more centre left like the labour party in UK. On the other side Republican like the tories in the UK are centre right.

Ukweli ni kuwa their differences kiitikadi ni ndogo sana same goes with Chadema na CCM kama ilivyoanishwa vyema hapo juu.

Kuhusu Nyerere na itikadi yake ya ujamaa hii wasomi wengi na modern historian wanakubaliana kuwa alikuwa heavily influenced na Kibbutzism from Israel especially kwenye suala la vijiji vya ujamaa na sera nzima ya kujitegemea rather than Marxist or Leninist ideology. Lakini hii ni nadharia kivitendo hatujawahi kujitegemea hata enzi hizo Nyerere was still stretching the begging bowl left, right and centre, kama ilivo sasa au hata kama chama kingeni kikichukua madaraka.
 
MMM
Kuhusu hiyo hoja hapo juu, kuachiana majimbo ni kutathmini kila chama kinaelewa maeneo ambayo kinakubalika zaidi hivyo basi ni budi kuongeza juhudi huko kuliko kwenda kwenye majimbo ambayo chama kinajua wazi kuwa uwezo wa kushinda ni mdogo. Makubaliana hayo ni juu ya viongozi wa vyama husika kuamua ndio kukomaa kisiasa huko na mojawapo ya njia za kuwatoa CCM, as is now ni kuwa na uroho wa kisiasa yaani ni wazi majimbo mengine wanajua wazi kuwa CCM iko mbele na wanaona ni bora wote wakose...Kanuni za makubaliano ni wazi lazima waangalie nani zaidi ama kwa kutumia opinion polls au historical voting patern za maeneo husika. Ni lazima viongozi wakubali kuwa ili mabadiliko ya kweli yaje Tz ni muhimu kuwa na aina moja au nyingine ya ushirikiano kwenye upinzani, jinsi ilivyo sasa kwa upinzani kushika mamlaka ya dola ni kujidanganya tu na kuota ndoto za alinacha.

Hili halijajaribu hata chembe kujibu maswali yangu; umerudia rudia kile ambacho kimesharudiwa mara nyingi tangu mfumo wavyama vingi urudishwe tena.


Kuhusu swala lako hapo juu ni wazi kuwa kama kungekuwa na chama kimoja cha upinzani chenye nguvu ni bora zaidi ya utitiri wa vyama bungeni hiyo ni wazi angalia Marekani (mainly 2 political parties )au hata UK (mainly 3 parties). Sasa hapa kwetu kweli inaumiza kichwa. Kama mtu unataka mageuzi (ng'oa CCM) halafu siku ya uchaguzi unapatwa na mchecheto nani niwape kura yangu CUF, Chadema, UDP au CCJ?

Sasa u nafikiria kuwa na chama kimoja chenye nguvu kutawezekana kama msingi wa muungano ni kutokuunganisha vyama kabisa kuunda chama kimoja?
 
Hili halijajaribu hata chembe kujibu maswali yangu; umerudia rudia kile ambacho kimesharudiwa mara nyingi tangu mfumo wavyama vingi urudishwe tena.




Sasa u nafikiria kuwa na chama kimoja chenye nguvu kutawezekana kama msingi wa muungano ni kutokuunganisha vyama kabisa kuunda chama kimoja?

Basi labda la msingi kwa vile uundwaji wa chama kimoja au viwili vya upinzani umeshindikana ni kusubiri hivi vilivyopo vife natural death hadi hapo kimojawapo au viwili vibakie, yaani survival of the fitest, how long this will take? only time will tell. Tumeshaona jinsi NCCR na TLP vimeisha nguvu hivo basi niaka ijayo nayo labda chadema, cuf na ccj vitakufa taratibu na kimojawapo kuibuka kidedea. Tatizo la hilo ni kuwa itachukua muda and time is not on our side.

Wewe ushauri wako ni upi ili tuwe na upinzani ulio imara na wa kweli katika chaguzi zetu? Mimi nimeshatoa maoni yangu
 
Wewe ushauri wako ni upi ili tuwe na upinzani ulio imara na wa kweli katika chaguzi zetu? Mimi nimeshatoa maoni yangu

NI kuwa na chama kimoja chenye nguvu na kinachokubalika kisiasa na chenye uwezo wa kuwa mbadala wa chama tawala. Aidha vyam vikubwa vya upinzani vikubali kufa ili kuunda chama hicho au chama kimoja kikubali kwenda kivyake vyake na kujaribu kujijenga hivyo.
 
Okay,W e got that advertisement.So what I need to know,The place where I can get the CcJ MEMBER CARD?
 
Mzee Mwanakijiji,
Mifano yako haina sura mkuu wangu. Usitumie mifano isiyowezekana ktk mazingira ambayo unajua fika kwamba haijawahi kutokea na haitokea. Hili la mgombea wa Chadema kuwa na asilimia 40 na CUF 40 halafu CCM 20 hakuna. Ni mfano ambao haupo na kama ungekuwepo usingetusikia hapa tukibwabwaja..Kila jimbo la Ubunge ugonvi mkubwa ni CCM na Wapinzani. Kila ushindi wa jimbo ni kutoka CCM sio vyama vya upinzani.

Nijuavyo mimi kila jimbo kuna chama kilichoweza kuwavuta wananchi kuliko CCM hushinda, au karibu sana chama hicho hushika nafasi ya pili (chini ya CCM) kile cha tatu siku zote huachwa nyuma vibaya..aghalab kutokea upinzani kwa upinzani kugombea jimbo, kisha CCM asichukue kiulainiii...na hata kama imetokea ni jimbo moja au mawili tu. Na kikubwa zaidi kutazama mfumo mzima wa uchaguzi usitegemee mahala kiongozi wa CCM anapopata asilimia 80 au zaidi, hawa wapinzani wakaweza kupata ushindi kwa asilmia hizo ktk majimbo ni vigumu sana..
Kila jimbo lililomchagua Kikwete limemchagua pia mbunge wake, na wabunge wengi kama sii wote wa Upinzani waliopita uchaguzi hata Kikwete alifanya vibaya majimbo hayo. Hii ndio reality pamoja na kwamba demokrasia ya kura za maarufu (popular vote) huchezea na akili za watu kufikiria inawezekana pasipo wezekana.

Na kuhusu Bunge, mkuu wangu mbunge ni mwakiklishi wa wananchi na sio mwakilishi wa chama bungeni. Naona kama unalenga kuleta ushindani Bungeni, badala ya bunge kuwakilisha wananchi tulowachagua. Kwa ujumla wetu mkuu wangu, wananchi wote tunataka Uhuru wetu urudishwe, katiba kuandikwa upya, mfumo wa uongozi ufanyiwe marekebisho, miiko na maadili ya uongozi zirudishwe, nguvu ya kiutawala ifanyiwe marekebisho makubwa toka ngazi ya Rais, Makamu, Rais wa Zanzibar,Waziri mkuu, Mawaziri,Wakuu wa mikoa wilaya na kadhalika..Haya ni mageuzi ya mwongozo wa utawala ambao hivi sasa hauna dira...Tunapuyanga tu.

Hivyo hata ukiwa na Wabunge wengi wa CCJ bungeni kama hamna kiti cha rais, upinzani wa CCM na vyama vingine vitawazuia kupitisha maazimio. Hata iweje tuwape kila la kheri CCJ...wameshinda sana CCJ inaweza kupata asilimia 40, CCM 30, CUF 10 na vyama vingine 20.
Now, tuzame kwenye reality ya siasa za Bongo, CCM ana uwezo wa kubadilisha kura za wajumbe wa upinzani kuwa nao kuliko CCJ kuwavuta hawa kwa sababu kwanza ujio wa CCJ ni kikwazo kwao zaidi ya CCM. Hizi ndio siasa za Bongo ukishindwa kuliona hilo basi kazi kubwa mnayo.

Kwa kuongezea tu zile quotes ulizoweka za Chadema hapo juu nadhani ndicho nilichosema hapo awali..Reformist ni mageuzi ya kurudisha mwongozo ambao hautumiki tena (utekelezaji). Nakuomba sana unipe hiyo Itikadi ya CCJ kama haikubaliki na Chadema au CCM..
 
Mkuu Mkandara wala usipoteze energy bure kwa huu wazimu sijui CCJ, sijui chama kingine kipya!!

Sisi watanzania tuliozaliwa kabla ya 1990 ni majuha na machizi, hivyo tuombe mungu kizazi hiki kipya kiwe na hekima.

Haiingii akilini kuwa kwenye kila jimbo on average CCM 50% na wasioipenda CCM ni 50%, sasa wale wasioipenda CCM wanavurugwa na utitiri wa vyama angalau 10, so at the end CCM on average wanashinda kwenye 90% ya majimbo.

Mchezo ungekuwa mzuri kama kuna chama kimoja tu cha upinzani, hivyo almost kila jimbo lingekuwa toss up, oooh no kwa wazimu wetu na kujifanya tunajua sana sijui itikadi, mara sera tuna vyama kama 10.

Issue namba moja ni CCM kushindwa kwanza, then in the future ndio mambo ya itikadi, sijui sera sijui wazimu upi mpya yaje. Sasa hivi ITIKADI NA SERA should be NGOA CCM, hakuna zaidi ya hapo.
 
Wajomba sikilizeni, the issue here is very simple

Regardless of the Chama kimoja, vingi, itikadi, malengo n.k Kikubwa ni kwamba, Tanzania kwasasa tunahitaji kiongozi SHUPAVU ambye atarekebisha mambo till upatikane muelekeo, maaana kwa sasa Tz tume-loose Identity yetu. A question for ourselves "Is do we real have a STRONG leader to lead the country!!!?
Nionavyo mimi Tanzania hatujapata kiongozi bado, Tuna majuha tu. Ndio maana Chama kama chama kinaweza kuwa na wriitten documents nzuriiii sana lakini muweke kiongozi wake hapo mbele akupangie hoja na malengo yake..... Kituko!

Tanzanaia we are after Sera zinazotekelezeka, We are after Real Leaders who can stand strong for the battle from the start to the end. Naunga mkono Mgombea binafsi. Strong, wise tena mwenye utiisho, asiye banwa na chama wala wanachama, mwenye uchungu na uhusiano wa moja kwa moja na raia.

Then later ndio tutahitaji chama na mfumo fula ni wa uongozi
 
Firstcollina,
Mkuu katika nchi ya Demokrasia haiwezekani kabisa kumpata kiongozi toka kwa Wagombea binafsi. Hii ni sawa na kufungiwa mbuzi ndani ya gunia au wazungu wanasema - Life is a box of chocolates, you never know what you're gonna get. Hivyo ni muhimu wakati kama huu kutambua tunachonunua.

Umesema nchi yetu haijapata kiongozi shupavu, hapana mkuu wangu wote waliopita ni mashupavu na ndio maana wameweza kuchukua Ikulu mahala ambapo sii pa lelemama. Pressure of the national circumstances were different toka Nyerere hadi Kikwete na sidhani kama unaweza kutuambia ushupavu ulotakiwa wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa hadi huyu Kikwete ulikuwa upi.

Binafsi naamini hakuna psychological characteristics za kiongozi bora akiwa nje ya Ikulu zinaweza kutupa picha ya kiongozi bora ni lazima mtu atinge kwanza kiti cha Ikulu ndipo tutajua.Hata hayo mataifa makubwa kama Marekani kwa miaka zaidi ya 100 wana marais shupavu wachache wala hawajai mkononi, wabovu ndio usiseme wengi wao hata hawajulikani kabisa kwawamerekani wenyewe kwamba waliwahi kuwa marais wa nchi hiyo..lakini siku zote America imesimama on top of the world kama Taifa bora na tajiri kwa sababu wenzetu wana DIRA.

Mimi sidhani kama tatizo letu ni Kikwete au alikuwa Nyerere,Mwinyi au Mkapa ila tatizo ni sisi wenyewe wananchi. Ebu fikiria hapa tupo kijiweni tu tumeshindwa kufikia maamuzi ya busara hali tukijua wazi kwamba CCM ndiye tatizo letu sii Kikwete. CCM ndio wametawala nchi yetu kwa miaka 49 (by the way next year Uhuru wetuutakuwa miaka 50) na hakuna mafanikio kabisaaa, yet kwa kutambua hivyo bado tunashindwa kukubaliana tatizo ni kitu gani na jinsi gani tunaweza kuondokana nalo. Na kila mwaka wa uchaguzi huzuka mtu anajua zaidi na matokeo yake tunaishia kugonga Ukuta.

Jamani mweeee, kama alivyosema Moelex23 tatizo ni CCM hakuna jinsi kwani JK mwenyewe alijaribu kufikiria mageuzi toka mwaka 2000 akidhani kazi itakuwa rahisi. Alipoingia Ikulu alijikuta mdogo kanywea kwani madudu alokuwa nayo yeye pekee yangemmaliza..
Hivi jamani hamsikii viongozi wote toka Kikwete, Malecela, Pinda, Hosea wote wanadai kwamba tukijaribu kusimamisha sheria nchi yetu haitakuwa salama. Nakumbuka Pindaalifikia kusema ni bora ahukumiwe yeye.. Haya Lowassa mwenyewe alisema amejiuzuru ili kukiokoa chama..wakuu zangu hizi lugha bado mnafikiria kwamba CCM sio tatizo letu kubwa.
Kama kweli mtaji tulokuwa nao ndio huu basi mimi nadhani CCM sio problem ila sisi wenyewe watawaliwa...(nchi ya WAJINGA na MALIMBUKENI)
 
Haiingii akilini kuwa kwenye kila jimbo on average CCM 50% na wasioipenda CCM ni 50%, sasa wale wasioipenda CCM wanavurugwa na utitiri wa vyama angalau 10, so at the end CCM on average wanashinda kwenye 90% ya majimbo.


Ukiwa na hekima kwa vile umezaliwa kabla ya 1990 (na mimi ni wakundi hilo) huwezi kusema such a definitive statement without backing it up with some form of evidence. How on earth did you come up with those numbers?
 
Mkuu Mkandara wala usipoteze energy bure kwa huu wazimu sijui CCJ, sijui chama kingine kipya!!

Sisi watanzania tuliozaliwa kabla ya 1990 ni majuha na machizi, hivyo tuombe mungu kizazi hiki kipya kiwe na hekima.

Haiingii akilini kuwa kwenye kila jimbo on average CCM 50% na wasioipenda CCM ni 50%, sasa wale wasioipenda CCM wanavurugwa na utitiri wa vyama angalau 10, so at the end CCM on average wanashinda kwenye 90% ya majimbo.

Mchezo ungekuwa mzuri kama kuna chama kimoja tu cha upinzani, hivyo almost kila jimbo lingekuwa toss up, oooh no kwa wazimu wetu na kujifanya tunajua sana sijui itikadi, mara sera tuna vyama kama 10.

Issue namba moja ni CCM kushindwa kwanza, then in the future ndio mambo ya itikadi, sijui sera sijui wazimu upi mpya yaje. Sasa hivi ITIKADI NA SERA should be NGOA CCM, hakuna zaidi ya hapo.


Kweli wewe ni wa mwaka 1990! Hivi ukishaing'oa CCM bila kuwa na mpango wowote zaidi ya hapo nchi utaiendeshaje?
 
Hivi mwenzetu unajua TANU walipomng'oa mkoloni walikuwa na mpango gani zaidi?

walikuwa wamejipanga kuongoza taifa; lengo lao halikuwa kumng'oa mkoloni tu halafu mambo mengine yaje mbele ya safari. Walijua wanataka kufanya nini kuhusu elimu, miundombinu, barabara, afya n.k na mara baada ya kupata uhuru walianza kutekeleza mipango hiyo. Kweli unaamini walikuwa wanataka kumuondoa mkoloni ili aondoke tu halafu mengine watayarifikiria baada ya kumng'oa mkoloni?
 
Ama kweli watu wanapenda debate. Mwanakijiji hiyo 50/50 ni maono tu ya juu juu nikimaanisha kuna watu wengi wameichoka CCM, lakini wanaona hakuna possibility ya kuingoa so at the end wanaipigia CCM kura shingo upande au hawapigi kura kabisa, kungekuwa na viable option ungeshaa lakini sitaki discussion ya nuts & bolts issue ni NGOA CCM.

Boramaisha, unauliza ukiingoa CCM, nchi utaendesha vipi?? What?? Hapa tulipo nchi inakwenda tu yenyewe bila muendeshaji, so anything else itakayofuata tu sheria say Watu walipe kodi, rushwa iondolewe, watu wawe appointed on merits, kipaumbele cha vitendo (ie budget) kwenye kilimo, Afya, elimu itakuwa step in the right direction.

Kujifanya wajuaji sijui ooh tunamipango hii sera hiii, itikadi hii ndio tutaishia humu humu kubishana na CCM kupiga magoli milele.

Haiwezekani kijiji kinashambuliwa na Simba hatari wanaokula mifugo na watu, badala ya issue kuwa namna ya kuua simba, wanakijiji wanakaa kubishana simba wakishauliwa mifugo itagawanjwa vipi au njia mpya za ufugaji, UA KWANZA SIMBA, mengine yatafuata.
 
Okay,W e got that advertisement.So what I need to know,The place where I can get the CcJ MEMBER CARD?

Kama uko dar unaweza kwenda Lumumba! ila uwe mwangalifu, wewe uliza wapiganaji ukioneshwa basi unamuuliza kadi, wanatembea nazo ili watakapopata tu usajiri waweze kuanza Charm Offensive na kutufundisha itikadi ya ujamaa (mlengo wa kulia) na kuchukua nchi kwa sababu chadema na vyama vin ginene havina itikadi -Did I say that?
 
Ama kweli watu wanapenda debate. Mwanakijiji hiyo 50/50 ni maono tu ya juu juu nikimaanisha kuna watu wengi wameichoka CCM, lakini wanaona hakuna possibility ya kuingoa so at the end wanaipigia CCM kura shingo upande au hawapigi kura kabisa, kungekuwa na viable option ungeshaa lakini sitaki discussion ya nuts & bolts issue ni NGOA CCM.

hata maono ya juu juu yana masingi siyo kupenda debate. Kama hutaki kumaanisha kitu basi unaweza qualifiers fulani lakini wewe umezungumza with authority kuwa "kila"... halafu ukaweka na figures kabisa. Sasa hiilo si tatizo kwani yaweza kuwa kweli lakini at least ungedokeza kuwa msingi wa "maono tu ya juu juu" ni nini? vinginevyo usingebeza wengine pasipo kuwa na msingi wa ubezaji huo. Hata sasa bado unazungumza with authority kuwa "wengi" na kuwa "wanapigia kura kwa shingo upande".. how do you know. Hivi umemuona mwana CCM anayeenda kupiga kura huku analia kwa uchungu?

Boramaisha, unauliza ukiingoa CCM, nchi utaendesha vipi?? What?? Hapa tulipo nchi inakwenda tu yenyewe bila muendeshaji, so anything else itakayofuata tu sheria say Watu walipe kodi, rushwa iondolewe, watu wawe appointed on merits, kipaumbele cha vitendo (ie budget) kwenye kilimo, Afya, elimu itakuwa step in the right direction.

Right.. hata CCM wnasema hayo hayo, kodi inakusanywa, rushwa inaondolewa, watu wanachaguliwa on merits or vinginevyo, bajeti ya kilimo imeongezwa, afya ndio wanajenga hadi taasisi ya moyo, elimu watakuonesha UDOM.. halafu utasema hawafanyi kitu? Watanzania wanaona hayo yote na hata kama siyo superb lakini wanaridhika. Sasa mtu mwingine aje na mapendekezo ya kufanya hivyo hivyo? Tofauti itakuwa nini?
Kujifanya wajuaji sijui ooh tunamipango hii sera hiii, itikadi hii ndio tutaishia humu humu kubishana na CCM kupiga magoli milele.

a typical Tanzanian sentiment.. mtu akizungumza na kung'ang'ania anaitwa "mjuaji" na ndivyo walivyomuita Mwalimu kuwa "haambiliki"; ukijenga hoja dhaifu itaoneshwa kuwa ni dhaifu na huko siyo kujifanya kujua. Ukitaka kushawishi basi jaribu kujenga hoja yenye nguvu ambayo si rahisi kupanguliwa na hoja nyingine nzito.

Haiwezekani kijiji kinashambuliwa na Simba hatari wanaokula mifugo na watu, badala ya issue kuwa namna ya kuua simba, wanakijiji wanakaa kubishana simba wakishauliwa mifugo itagawanjwa vipi au njia mpya za ufugaji, UA KWANZA SIMBA, mengine yatafuata.

Mfano wako kuhusu Simba au wengine wanatumia nyoka ni mzuri.... ukihusu nyoka siyo wanasiasa na hatima ya taifa zima. Tumeshaona yaliyotokea Kenya, Ukraine, na hivi karibuni Krzygstan... haitoshi tu kuindoa serikali madarakani ati ilimradi tumeiondoa halafu mengine tutayafikiria mbele ya safari. Isn't that what CCM is doing?

Wanaotaka kuingia madarakani ni lazima waje na wawe na sera na mipango inayoeleweka. Siamini kabisa katika muungano wa kutaka CCM iondoke madarakni bila wanaotaka kuiondoa kujulikana mipango yao nini kwa taifa na wataifanyaje? Wanasema the devil is in the detail. Obama hakusema tumuondoe tu Bush halafu tutajua cha kufanya mbele ya safari, Wamarekani wangemuona mzugaji. Aliwaambia kabisa atakachofanya na atakifanya vipi na kwa muda gani. Huo ndio msingi wa kuiondoa serikali iliyoko madarakani, siyo kusema tuiondoe tu alimradi turuke ruke mitaani kushangilia "CCM imeng'oka".. sasa mumuue Simba halafu mkaribishe CHui!? Well.. mtashangilia mmeua simba, lakini mtakuwa mmeondoa tatizo?
 
Back
Top Bottom