Mzee Mwanakijiji,
Kwanza matumizi ya hili neno KULIA ktk elimu ya itikadi tulofundishwa au kupumbazwa nayo unalitumia vibaya kwa sababu hapa sii mahala pake pamoja na kwamba mimi nakuelewa where U come from..
Maadam neno hili linatumika vinginevyo na unapolibadilisha kutokana na mazingira yetu nina hakika utawachanganya wengi. Hakuna mahala panasema ni lazima KULIA iwe pinzani na UJAMAA lakini ndivyo inavyofahamika kwa watu wote kutokana na mfumo mzima wa Demokrasia. Na hakuna mtu who cares na hizi habari za KULIA au KUSHOTO - hakuna mkuu wangu, watu hapa hawana dini (siii kulia wala kushoto)kutokana na Njaa kali.
Pili, Katika kampeni zenu mnapotumia neno UJAMAA mnapoteza nguvu na maana halisi ya UJAMAA, kwa sababu watu wengi wanajua kwamba UJAMAA ni Ukomunist na usoshalist, pale serikali ku control watu na Uchumi, njaa zaidi na machungu yote waliyoyapata wakati wa mwalimu yatarudi vile vile kama ilivyokuwa mwaka 1982 hata kama lengo la itikadi yenu ni kulinda Uhuru na maslahi ya Taifa kwanza.
Hivyo unaposema UJAMAA watu wengi watakukimbieni pasipo kufikiria mara mbili. Ni muhimu kutafuta neno jingine ambalo kwao haliambatanishi UJAMAA na UKOMUNIST, hii ni nchi ya wajinga na wengi wataamini mnataka kurudisha hali ile ya Kutaifishaji, vijiji vya Ujamaa, foleni ya vyakula na kadhalika...It reminds them of hardship!
Na kuhusu Chadema mkuu umeshindwa kuelewa kwamba Unahitaji mageuzi ya serikali kuu kwanza na sio mageuzi ndani ya chama..Kwa wajinga wengi watasema mnabadilsiha chupa lakini mvinyo ni ule ule..besides njia hii huchukua nguvu na muda mrefu kusimama..Again nitakukumbusha tu kwamba CCJ imekataliwa au kucheleweshwa kusajiliwa na yaonyesha hakuna plan B, siku zinayoyoma na hadi sasa CCM mshindi kwa sababu hii ni nchi ya WAJINGA hamuwezi kupata support ya wengi inabidi mfikirie kama wanavyofikiria wao. By the way wanasema wao ni lengo wa kati (wasiofungamana na upande wowote) na mimi ni mfuasi wa KULIA lakini nakubaliana na mageuzi yao kutokana na Watu/Mazingira tuliyopo.
Hapo ndipo CCM huwapiga bao Wapinzani wote kwa sababu huzungumzia vitu vinavyoonekana kwao..Elimu, Afya, Barabara, maji, Mawasiliano, ajira na kadhalika hata kama hawawezi kuvileta kuliko kutumia hizi lugha za itikadi, sera na Ilani. Watu hawajali sana kusoma maelezo mareefu yasiyokuwa na tija kwao.
Mkuu sijui ulikuwa Bongo mara ya mwisho lini lakini Ukimuuliza Mdanganyika yeyote nini maana ya Itikadi basi katika kila 1000 utapata mmoja!..lakini muulize kama anataka CCM iondoke kwa sababu imeshindwa ku deliver maendeleo kwa wananchi, utapata kura za watu 999 na mmoja atakayekataa ni kiongozi wa chama. Hivyo babuu ni muhimu sana kujua Wadanganyika wanafikiri nini - Mwenye NJAA mwambie atakula wapi na sii siasa za Utampa kazi aje kesho..Kamba hizi wanazijua vizuri na hata wao huzitumia ktk maisha yao ya kila siku.