Mkandara kwenye suala la Mama Ntilia nadhani kauli yako hii hakutaka iiche pasipo kuiangalia kwa ukaribu kwa sababu imedai "Ukweli" kuondoa ukweli mwingine wote:
Kwa kuongezea tu nitakupa ukweli ambao wengi hatupendi kuuweka maanani leo hii. Waislaam waliutaka Uhuru wa Tanzania mapema lakini wasingeweza kufanikiwa pasipo support ya Wakristu. Ndipo walipokuja na plan ya kuwavuta Wakristu na mwalimu akapewa Uenyekiti.
Kwa mtu yeyote ambaye ameisoma kauli yako ilikuwa inataka kusema kuwa
a. Waislamu walitaka Uhuru wakristu walikuwa hawataki - ndio maana ya kutumia neno "mapema"
b. Wasingeweza kufanikiwa wenyewe - sielewi msingi wa hili ni nini, kwa sababu wangeweza kupata uhuru lakini sijui kama ungekuwa ni waislamu peke yao na wakristu wangeendelea kuw wakoloni au walitaka uhuru wa Watanzania wote kwani wote walikuwa chini ya mkoloni?
c. Walihitaji support (kuungwa mkono) na Wakristu - kana kwamba Wakristu wao hawakuwa na maslahi katika uhuru huo.
d. Waislamu walilpoona (a-c)wakabuni mpango wa kuwavuta Wakristu - kwa maneno mengine kabla yake wakristu hawakuwa katika mpango huo na wao walikaribishwa kutoa support
e. Mwalimu alipewa Uenyekiti kwa sababu ya Ukristu wake (ukizingatia d). Yaani, walimpa hivyo bila kujali uwezo wa kuongoza, uwezo wa kushawishi au yeye mwenyewe kutaka uhuru wa Tanganyika vile vile. Kama Mkristu inaonekana Nyerere hakutaka Uhuru wa TAnganyika hadi alipokutana na Waislamu wa Dar ambao kama wengine huko nyuma wamewahi kudai (kimzaha au ukweli) alifundishwa kuvaa kaptula - kana kwamba alipokuwa anaishi Butiama alikuwa anavaa manyasi.
Ni kutokana na hilo ndio mama Ntilie amekuja na jibu lake hilo. Hii haiondoi hata kidogo mchango wa Watanganyika wa awali katika kupigania uhuru bila ya kujali dini zao, au hadhi zao kwani hoja yako ikikubaliwa kama ulivyoiweka awali inaashiria (na mara nyingine imesikika hivyo inapotolewa na watu wengi) kuwa waislamu ndio wana haki zaidi na Tanganyika kwa sababu "walitaka uhuru wa tanganyika mapema").
Kwenye suala la umoja, huu umoja unaoupendekza msingi wake uwe ni nini? NI vitu gani ambavyo tunaweza kusema 1, 2, 3, 4, 5 na 6 tunakubaliana na hivyo tuunde umoja. Sidhani kama unataka watu waungane tu kwenye jina au chama kimoja for the sake of being able to say "we are united". Ni lazima kuwe na mambo fulani ya kuunganisha. Zaidi ya kuondoa CCM madarakani ni vitu gani vinapaswa viwe msingi wa muungano wa upinzani Tanzania?