CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

hapana nawaongezea tu more possibilities ya vitu vya kuamini na sababu ya kuviamini.
Sina tatizo na vitu vya kuamini, ila bado natatizika the motive behind hizo sababu, yaani underlying facts zilizopelekea hata wewe kuiaminia CCJ.
Mimi bado ni Tomaso!.

Uwepo wako, au support yako kwa CCJ in apelekea to send signals that CCJ is something with a substance that is more that what we see ambacho ninyi wenzetu kama wewe umekiona, open our eyes na sisi tuone hicho unachokiona.
 
Sina tatizo na vitu vya kuamini, ila bado natatizika the motive behind hizo sababu, yaani underlying facts zilizopelekea hata wewe kuiaminia CCJ.
Mimi bado ni Tomaso!.

Uwepo wako, au support yako kwa CCJ in apelekea to send signals that CCJ is something with a substance that is more that what we see ambacho ninyi wenzetu kama wewe umekiona, open our eyes na sisi tuone hicho unachokiona.

here is the thing; kuna vitu unaweza kuangalia vinafanyika au unaweza kushiriki kuvifanya. Mimi kama wewe niliona upungufu wa upinzani ulivyo nchini. Na toka mwanzo niliona tatizo lililoko CCJ kwa sababu kilianzishwa out of spite and anger. Lakini hakikuwa na substance wala kujua mbele kitakuwaje. Kwa vile naamini mabadiliko siyo yale tunayoyangojea au yale tunayoyaombea nikaamua nishiriki baada ya kutafuta ukweli wote wa kutosha kunishawishi na mimi.

Ni baada ya kufanya hivyo na kujua mengine (ambayo hayako wazi sasa) nikaamua kutoa my full support. Sasa kwa wengine ni vizuri muendelee kusubiri kama Tomaso au mchukue hatua kama niliyochukua mimi ya kwenda kuutafuta undani badala ya kukaa pembeni kusubiri undani uletwe kwenu.

Kama CCJ haitakuwa ninavyotarajia itakuwa ni gharama ambayo niko tayari kuilipa. Lakini nitakuwa nimeshiriki kuifanya iwe ambavyo ningependa iwe. Mabadiliko ni yale tunayoyaleta.
 
here is the thing; kuna vitu unaweza kuangalia vinafanyika au unaweza kushiriki kuvifanya. Mimi kama wewe niliona upungufu wa upinzani ulivyo nchini. Na toka mwanzo niliona tatizo lililoko CCJ kwa sababu kilianzishwa out of spite and anger. Lakini hakikuwa na substance wala kujua mbele kitakuwaje. Kwa vile naamini mabadiliko siyo yale tunayoyangojea au yale tunayoyaombea nikaamua nishiriki baada ya kutafuta ukweli wote wa kutosha kunishawishi na mimi.

Ni baada ya kufanya hivyo na kujua mengine (ambayo hayako wazi sasa) nikaamua kutoa my full support. Sasa kwa wengine ni vizuri muendelee kusubiri kama Tomaso au mchukue hatua kama niliyochukua mimi ya kwenda kuutafuta undani badala ya kukaa pembeni kusubiri undani uletwe kwenu.

Kama CCJ haitakuwa ninavyotarajia itakuwa ni gharama ambayo niko tayari kuilipa. Lakini nitakuwa nimeshiriki kuifanya iwe ambavyo ningependa iwe. Mabadiliko ni yale tunayoyaleta.

Thanks for inspirational encouragement, kwa muda mrefu mimi nimekuwa mtu wa kukaa pembeni, sit and watch, nikisubiria changes I can believe in ziletwe na watu wengine, from now, with this little time left before October, I am now volunteered to step ahead and be part of that change, bringing about the changes I need. So from now, I'm part of the changes but in the doctrine ya 'together you can!' CUF peke yao hawawezi, Chadema peke yao pia hawawezi na nyinyi CCJ peke yenu hamuwezi! You must stand together as one, ndipo hili lidude likubwa li SISIEM, litang'oka, bila hivyo, tusubirie miaka 5 mingine!
 
Uwepo wako, au support yako kwa CCJ in apelekea to send signals that CCJ is something with a substance that is more that what we see ambacho ninyi wenzetu kama wewe umekiona, open our eyes na sisi tuone hicho unachokiona.
Kwa vile naamini mabadiliko siyo yale tunayoyangojea au yale tunayoyaombea nikaamua nishiriki baada ya kutafuta ukweli wote wa kutosha kunishawishi na mimi.

Ni baada ya kufanya hivyo na kujua mengine (ambayo hayako wazi sasa) nikaamua kutoa my full support. Sasa kwa wengine ni vizuri muendelee kusubiri kama Tomaso au mchukue hatua kama niliyochukua mimi ya kwenda kuutafuta undani badala ya kukaa pembeni kusubiri undani uletwe kwenu.
Mzee Mwanakijiji, hapa ndipo unatakiwa uje na huo 'ukweli wote wa kutosha kunishawishi na mimi'. mengine (ambayo hayako wazi sasa) ili uyatumie kuwashawishi na wengine.
 
Chama cha mwamko mpya wa ujenzi wa taifa CCJ kinaanza harakati za kukutana na kuzungumza na wananchi katika kujitambulisha zaidi kwa wananchi wakati kinaendelea kusubiri usajili wa kudumu. Hadi hivi sasa maelfu ya Watanzania wameamua kujiunga na chama hiki ambacho hakina "jina kubwa" na ambacho viongozi wake "hawana majina makubwa" katika medani za siasa nchini.

Katika siku chache zijazo CCJ itapita kusalimiana na kukutana (meet and greet tour) wananchi katika sehemu mbalimbali za Tanzania Bara na Visiwani.

Yawezekana una maswali mengi kuhusu CCJ ni yapi hasa na ungependa hasa kujua nini?

Asante sana MM. Hawa CCJ wanakuja na lipi jipya hasa ambacho Chadema, NCCR Mageuzi nk hawana? It was my thought that we need to strentghern existing political parties and enable then to have powers to Remove CCM from teh top seat!
 
Mzee Mwanakijiji,
Kwa kuongezea tu nitakupa ukweli ambao wengi hatupendi kuuweka maanani leo hii. Waislaam waliutaka Uhuru wa Tanzania mapema lakini wasingeweza kufanikiwa pasipo support ya Wakristu. Ndipo walipokuja na plan ya kuwavuta Wakristu na mwalimu akapewa Uenyekiti.
Pamoja na tofauti za kiimani, itikadi na malezi yao mwalimu alipokea kitu kicho akiwa pia na nia moja tu - kumwondoa mkoloni kwanza. Mwalimu aliweza kuwatumia waislaam na Wakristu kwa pamoja (umoja wao) kuleta Uhuru na kisha kuleta itikadi zake za Ujamaa na Kujitegemea, jambo ambalo kina Marealle na Mtenvu walishindwa kuliona - We should learn from Him..
.
Mkandara, nimekusoma muda mrefu unavyojaribu ku-inject sense ya 'umoja ni nguvu' into Mwanakijiji's head and it doesn't sink. Naomba usikate tamaa, ila hili la vyama kutoshirikiana ni tatizo ambalo hata mimi nimekuwa nikiliona kwa muda mrefu na kulinyamazia.
Kwa vile hawa viongozi wa upinzani ni wenzeni, tunakutana nao kila siku kwenye social interactions za hapa na pale, naomba try as much as you can to sink this into their hard heads kuwa yoyote kati yao, hawezi bila ya kuwashirikisha wengine.

Kati ya majimbo 9 ya uchaguzi mkoani Kilimanjaro, CCM ina walk over majimbo matatu tuu mawili kati yake ni ya Upareni. Majimbo sita yaliyobakia, CCM imeshinda 5 na Chadema 1. Majimbo yote hayo matano, CCM imeshinda less than 50% wapinzani wamezigawa kura za upinzani hali iliyopelekea CCM kuibuka kidedea. Mfano Moshi Vijijini, CCM imeshinda kwa only 27% na Chadema, NCCR na TLP wakagawana 73%. Hawa wasipokubaliana tena, CCM itashinda hivyo hivyo, only Jimbo la Ndesa, CCM haiwezi kushinda hata kwa dawa, labda kama wata dhikr ...bila nguo.

Kwenye pita pita zangu na kutana kutana na hawa wanasiasa, nimekuwa siku zote nikiwauliza hili viongozi wa vyama, Lipumba analielewa, ila kwenye CUF, Lipumba hana kitu zaidi ya Baraghashia yake, realy powes lies with Seif, ambao muungano wa wapinzani kwake hauna maslahi yoyote.

Dr. Slaa anasema hatuwezi kushirikiana na vyama mamluki, wao wanaushahidi kuna viongozi wakuu wa vyama wako kwenye payroll ya CCM.

Watu pekee wenye matumaini ni viongozi vijana kama Zitto na Jussa, hili wameliona na wamelikubali, tatizo ni wakuu wa vyama vyao sijui kamma watalielewa.

Kwa vile mimi binafsi sio mwanachama wa chama chochote ila ni mshabiki wa demokrasia ya kweli, nadhani umefikia wakati to play more active role. If there is anything anybody can do to inject the sense of 'united we stand', or 'together we can' kwa spirit ya 'umoja ni nguvu', uchaguzi wa mwaka huu, hata kama hawatachukua nchi, ila CCM wataitikisa na bungeni kwa wingi watatinga.
 
Pasco,
Kwanza mkuu wangu shukran sana kwa kunielewa. Mimi nimemsoma sana Dr. Slaa na hakika nimewahi kuongea hata na baadhi ya viongozi ingawa sii wote na hofu hii imekuwapo kiasi kwamba kila mmoja wao anamshuku mwenzie. Hapa ndipo CCM walipotupiga bao, wametumia njama ya mkoloni kutuweka ktk hali ya kutoaminiana hivyo utengano utaweza kutudhoofisha. Yawezekana kuna ukweli mkubwa ktk dhana hii lakini sisi binadamu tumeumbwa na akili sana kupita kiasi na vichwa vingi havikosi ufumbuzi.

Mimi nilikwisha kata tamaa kabisa baada ya Muungano ule wa kwanza kufa, na hakika ulikufa kwa sababu hawakuwa na agenda yoyote hasa baada ya kushindwa na CCM uchaguzi wa 2005. That was bad timing na hakika leo hii wapo bado viongozi ngazi za vyama hivi wanaamini ktk muungano..Nitarudia kusema Muungano wa vyama sii viongozi ila ni Wafuasi wa vyama. Chadema sii Mbowe Dr.Slaa au Zitoo hivyo hivyo CUF sii Sharif Hamad wala Lipumba na TLP,NCCR wote hawa wanajenga jina la chama kutokana na wanachama wake..

Sasa maadam hesabu kubwa ya wananchama wa vyama hivi wanataka kuunda nguvu kubwa ya pamoja kumshinda CCM isipokuwa baadhi viongozi wao wana ushawishi wa kuvunja nguvu hizi kumetokea kitu kingine hapa - UJIO wa CCJ...Hawa pia sii kitu pasipo wanachama wake Hivyo maadam hiki ni chama kipya chenye record ya Waasi ni vigumu wao kupokelewa kama mtu mmoja mmoja lakini kwa ujumla wao wakiomba kukutana na wananchi na ku extend their hand kuomba muungano kujenga Upinzani not politics za itikadis for now, wanachama wengi watawakubali na viongozi wale watakao kataa Umoja huo watajiengua wenyewe kwani Magazeti yote yatawasema wote waliojitokewza kuunga mkono Umoja huu.

Trust me, viongozi mapandikizi watashindwa kuingia chama na waasi.. na hata kama ni spies hawatakuwa na muda wa kujipanga zaidi ya kubabaika..Mchawi yoyote mtoe hadharani atanywea kama chatu. Hivi sasa mapandikizi wote wanatoa habari zinazoendelea ndani ya vyama vyao sasa mnapoogopa kuungana hali kikulacho kiinguoni mwako - what the hell!

Kibaya nachokiona hapa ni kwa CCJ kufikiria wanaweza kuvuta Umma wote wa watanzania pasipo msaada wawanachama wa vyama hivi vinginevyo. Sijui kwa jumla ya wanachama wote wa vyama hivi lakini naweza kusema kwamba wapowatu watakipigia kura Chadema, CUF, TLP au NCCR hata kama watasimamisha mbuzi. Hawa watu ndio huleta tofauti kubwa ktk kura hasa unapowaambia tuko chama moja. Mkuu mimi naweza sana kumpigia kura Salim lakini wapo wengi hawamkubali, hivyo hivyo Dr.Slaa na wengineo kwa sababu wakitazama nyuma yao hawaoni msululu wa makomandoo wapiganaji.. Lakini kama hawa watu watajipanga vizuri na kuchagua Wabunge wenye nafasi kubwa kushinda ktk kila jimbo pasipo kujali chama ila ushindi na kiti kikubwa akae mtu wa uhakika.. Amini maneno yangu JK atakuwa ktk hali ngumu sana.

Nje ya hapo CCJ ipigane toka ndani hawa wazee wanaweza kabisa kumchanganya JK toka ndani ifikapo uchaguzi kama watajitenga na kugawana majimbo wakitumia zidumu fikra za mwalimu..Huku nje kama unavyoona Mzee Mwanakijiji anataka kutufungia mbuzi ktk gunia..Yaani sisi wananchi tunaotakiwa kukijua chama ndio tumekuwa wataka cha Uvunguni..Badala ya chama kujitangaza na kuwa wazi wanaunauza nini wao wanaleta biashara ya baniani - Kama nataka nunua kama hutaki acha kushika shika mali. Kwa mtaji huo watakesha..
 
Pasco,
Kwanza mkuu wangu shukran sana kwa kunielewa. Mimi nimemsoma sana Dr. Slaa na hakika nimewahi kuongea hata na baadhi ya viongozi ingawa sii wote na hofu hii imekuwapo kiasi kwamba kila mmoja wao anamshuku mwenzie. Hapa ndipo CCM walipotupiga bao, wametumia njama ya mkoloni kutuweka ktk hali ya kutoaminiana hivyo utengano utaweza kutudhoofisha. Yawezekana kuna ukweli mkubwa ktk dhana hii lakini sisi binadamu tumeumbwa na akili sana kupita kiasi na vichwa vingi havikosi ufumbuzi.

Mimi nilikwisha kata tamaa kabisa baada ya Muungano ule wa kwanza kufa, na hakika ulikufa kwa sababu hawakuwa na agenda yoyote hasa baada ya kushindwa na CCM uchaguzi wa 2005. That was bad timing na hakika leo hii wapo bado viongozi ngazi za vyama hivi wanaamini ktk muungano..Nitarudia kusema Muungano wa vyama sii viongozi ila ni Wafuasi wa vyama. Chadema sii Mbowe Dr.Slaa au Zitoo hivyo hivyo CUF sii Sharif Hamad wala Lipumba na TLP,NCCR wote hawa wanajenga jina la chama kutokana na wanachama wake..

Sasa maadam hesabu kubwa ya wananchama wa vyama hivi wanataka kuunda nguvu kubwa ya pamoja kumshinda CCM isipokuwa baadhi viongozi wao wana ushawishi wa kuvunja nguvu hizi kumetokea kitu kingine hapa - UJIO wa CCJ...Hawa pia sii kitu pasipo wanachama wake Hivyo maadam hiki ni chama kipya chenye record ya Waasi ni vigumu wao kupokelewa kama mtu mmoja mmoja lakini kwa ujumla wao wakiomba kukutana na wananchi na ku extend their hand kuomba muungano kujenga Upinzani not politics za itikadis for now, wanachama wengi watawakubali na viongozi wale watakao kataa Umoja huo watajiengua wenyewe kwani Magazeti yote yatawasema wote waliojitokewza kuunga mkono Umoja huu.

Trust me, viongozi mapandikizi watashindwa kuingia chama na waasi.. na hata kama ni spies hawatakuwa na muda wa kujipanga zaidi ya kubabaika..Mchawi yoyote mtoe hadharani atanywea kama chatu. Hivi sasa mapandikizi wote wanatoa habari zinazoendelea ndani ya vyama vyao sasa mnapoogopa kuungana hali kikulacho kiinguoni mwako - what the hell!

Kibaya nachokiona hapa ni kwa CCJ kufikiria wanaweza kuvuta Umma wote wa watanzania pasipo msaada wawanachama wa vyama hivi vinginevyo. Sijui kwa jumla ya wanachama wote wa vyama hivi lakini naweza kusema kwamba wapowatu watakipigia kura Chadema, CUF, TLP au NCCR hata kama watasimamisha mbuzi. Hawa watu ndio huleta tofauti kubwa ktk kura hasa unapowaambia tuko chama moja. Mkuu mimi naweza sana kumpigia kura Salim lakini wapo wengi hawamkubali, hivyo hivyo Dr.Slaa na wengineo kwa sababu wakitazama nyuma yao hawaoni msululu wa makomandoo wapiganaji.. Lakini kama hawa watu watajipanga vizuri na kuchagua Wabunge wenye nafasi kubwa kushinda ktk kila jimbo pasipo kujali chama ila ushindi na kiti kikubwa akae mtu wa uhakika.. Amini maneno yangu JK atakuwa ktk hali ngumu sana.

Nje ya hapo CCJ ipigane toka ndani hawa wazee wanaweza kabisa kumchanganya JK toka ndani ifikapo uchaguzi kama watajitenga na kugawana majimbo wakitumia zidumu fikra za mwalimu..Huku nje kama unavyoona Mzee Mwanakijiji anataka kutufungia mbuzi ktk gunia..Yaani sisi wananchi tunaotakiwa kukijua chama ndio tumekuwa wataka cha Uvunguni..Badala ya chama kujitangaza na kuwa wazi wanaunauza nini wao wanaleta biashara ya baniani - Kama nataka nunua kama hutaki acha kushika shika mali. Kwa mtaji huo watakesha..
Mkandara, nimeipenda hii hoja yako ya ushirikiano. If there is anything you can do, please do!. Mwalimu aliwahi kusema mahali, "Umasikini mkubwa kabisa na mbaya zaidi, ni umasikini wa fikra". Viongozi wengi wa upinzani pia ni masikini wa fikra za ushirikiano. Hata mimi kama nisingekusomo humu, nisingeijua siri ya Julius kupewa usukani wa TANU enzi zile. Ukimwelimisha Mzee Mwanakijiji kuhusu somo hili, utakuwa umeielimisha CCJ, kazi ianze kwa man to man naamini eventually it will sink into their hard heads.
'It can be done play your part'
Thanks.
 
.
Mkandara, nimekusoma muda mrefu unavyojaribu ku-inject sense ya 'umoja ni nguvu' into Mwanakijiji's head and it doesn't sink.

Of course it doesn't sink! Huwezi kuwa na umoja katika udhaifu. Hauwezi kwa mfano kuungana kwa lengo la "kuiondoa CCM madarakani" huo utakuwa ni umoja wa Rainbow ya Kenya iliyoungana kuiondoa KANU na baada ya kufanikiwa wakajikuta wanachinjana wenyewe kwa wenyewe. NI lazima kuwe na msingi wa umoja. Kwa vile vyama vingine vya upinzani vimeshindwa kuleta umoja CCJ inataka kuweka msingi wa umoja katika nguvu ili vyama vingine vikubaliane nacho na kuwa tayari kuungana nacho.

Tatizo ninalo liona ni kuwa mnataka CCJ ndiyo isikubali kuwepo ili iungane na vyama vilivyopo; huu ni umoja katika udhaifu. - unity in weakness siyo endelevu.



Kwa vile mimi binafsi sio mwanachama wa chama chochote ila ni mshabiki wa demokrasia ya kweli, nadhani umefikia wakati to play more active role. If there is anything anybody can do to inject the sense of 'united we stand', or 'together we can' kwa spirit ya 'umoja ni nguvu', uchaguzi wa mwaka huu, hata kama hawatachukua nchi, ila CCM wataitikisa na bungeni kwa wingi watatinga.

hata wakiitikisa CCM na Bungeni wakatinga kwa wingi, watakuwa wanasimamia nini? Umoja wa wingi usio na msingi bado ni umoja wa udhaifu. Huwezi kuwakusanya nyuki, sisimizi, mchwa na siafu ati kwa sababu wote wanauma ukawaunganisha pamoja ili wamuue nyoka. Wakishamuua nyoka mchwa watawala sisimizi; sasa sisimizi hawezi kudai ati "tulikuwa na umoja kabla ya kuumua nyoka"! Na nyuki wakitaka kujenga mzinga ulipo mzoga wengine watasema nyuki anatumia nguvu zake zaidi!. You CAN NOT HAVE UNITY IN WEAKNESS. Hili naona ndio kwenu halizami kabisa. Nitaendelea kujitahidi hata hivyo.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu unapozungumzia Umoja wa Rainbow huwezi kuuhusisha na mauaji yaliyotokea Kenya. Hawa walkiungana wakamwondoa KANU baada ya hapo wakarudi ktkmakundi yao wakaanza kupingana wenyewe kwa makabila yao. Hapa tunaona makosa yao ambayo sidhani kama nyie mnaweza kuyafanya na pia WATU na MAZINGIRA yetu hayawezi kuruhusu Ukabila. Hakuna umoja unaweza kuwa weakness hata nguvu ya kidole kimoja haiwezi kuilinganishwa na vidole vitano vya mkono..no matter what. Ongezeko la kila kidole kwa nguvu tofauti zinakupa nguvu moja kubwa ya mkono mzima..Hapo hapo nguvu za mkono mzima zinaweza pungua na kuwa udhaifu kutokana na udhaifu wa kidole kimoja, still vidole vinne vina nguvu zaidi ya kimoja.
Tatizo ninalo liona ni kuwa mnataka CCJ ndiyo isikubali kuwepo ili iungane na vyama vilivyopo; huu ni umoja katika udhaifu. - unity in weakness siyo endelevu
Mkuu pengine huelewi kwamba tuna vyama 18 tayari wakigombania limited number za viti vya uongozi..Kuongezeka kwa CCJ ni kupunguza uwezekano wa ushindi nikiwa na maana kama tunatafuta Mbunge wa Kinondoni, nafasi ni moja tu ya mbunge. Kugombania watu 19 hali inawezekana kabisa kugombania watu 3 au 4 kwa nafasi hiyo moja ni kutojali gharama za matumizi ya kodi za wananchi maskini..Serikali itatakiwa kuvipa vyama 19 fungu kubwa la fedha kwa wagombea 19 tofauti na wagombea watatu au wanne. Na hata kama vyama hivyo 4 vitapewa fedha yote (mathlan), kila chama kitakuwa na mtaji tosha kujiendesha kuliko kugawana vyama 19 mtaji ule ule, unless tafsiri ya ushindani huu ni kugombania ruzuku moja ambayo ni pato la chama..

Mifano ni mingi sana tazama ushindani Zanzibar! kuna vyama viwili tu vinashindana haswa CUF na CCM na kutokana na hali hiyo CUF wana nafasi kubwa ya ushindi Zanzibar..Muhimu ni kuwepo kwa vyama viwili vya ushindani na sio upupu wa vyama visivyokuwa na malengo ila kutafuta Ubunge na ruzuku ambazo ni kodi ya wananchi.
hata wakiitikisa CCM na Bungeni wakatinga kwa wingi, watakuwa wanasimamia nini? Umoja wa wingi usio na msingi bado ni umoja wa udhaifu. Huwezi kuwakusanya nyuki, sisimizi, mchwa na siafu ati kwa sababu wote wanauma ukawaunganisha pamoja ili wamuue nyoka. Wakishamuua nyoka mchwa watawala sisimizi; sasa sisimizi hawezi kudai ati "tulikuwa na umoja kabla ya kuumua nyoka"! Na nyuki wakitaka kujenga mzinga ulipo mzoga wengine watasema nyuki anatumia nguvu zake zaidi!. You CAN NOT HAVE UNITY IN WEAKNESS. Hili naona ndio kwenu halizami kabisa. Nitaendelea kujitahidi hata hivyo
Mkuu mfano wako mzuri sana ikiwa tu hao wadudu wameamua kumuua nyoka kwa sababu huyo nyoka anawapa shida kubwa ktk maisha ya viumbe wote. Na itasherehesha zaidi ikiwa kati ya hao wadudu kuna mmoja wao anaweza kumuua huyo nyoka peke yake..lakini kama hakuna na kuna uwezekano wa hawa wadudu watatu kumuua nyoka ili kuboresha mazingira ya viumbe wote.. why not kwani siku zote Mchwa hula sisimizi hata pasipo kuwepo Nyoka. Na nyuki hawezi kujenga mzinga ulipo mzoga kwani asili ya asali haitaki mzoga karibu ila maua yanayonukia..

Mkuu wangu tatizo lako unatazama swala hili kwa picha fupi sana yaani unalitazama swala hili kama ni swala la CCJ against CCM hali Uokovu wa kumwondoa CCM ni kwa maslahi ya Taifa zima na sio CCJ. Ndivyo walivyokuwa wakifikiria CUF Chadema TLP na wengine wote..Mnarudia makosa yaleyale tuloyaona sisi wananchi. Huwezi kumshinda nyoka CCM kwa nguvu za nyuki anayeruka lakini hawezi kutambaa vichakani. Na ningekuelewa kama CCM ni tatizo la CCJ sio wananchi kwa ujumla wake, kwani silaha na nguvu ulizonazo wewe CCJ hana Chadema au CUF lakini pia walizonazo wao wewe huna. Ndio maana unaanza kutafuta kusajili na umeshindwa kupita hapo wakati wenzako wameisha kuwa na nguvu hiyo, bado unatafuta nguvu ya wanachama acha mbali Wapiga kura ambao within four month uwe tayari umewashawishi vya kutosha. Hizi ni weakness zako lakini ni plus ktk umoja wa vyama.

Hii mkuu wangu ni kuendeshwa na ego mkuu wangu badala ya kutazama ukweli halisi. Kwetu sisi walalahoi hili swala la uongozi bora sii swala la CCJ, Chadema wala CUF ila ni la kitaifa na maadam kuna utaratibu wa kumwondoa CCM kidemmokrasia hii ndio njia pekee ya kutuunganisha sote. Hakuna kitu UNITY in WEAKNESS pasipo kuwa na kipimo cha STRENGTH..
 
Mkandara, kwanini vyama vilivyoop vya upinzani visiungane au kwanini vimeshindwa kuungana? na kwanini bila ya CCJ haviwezi kuungana bado?
 
Mkandara, kwanini vyama vilivyoop vya upinzani visiungane au kwanini vimeshindwa kuungana? na kwanini bila ya CCJ haviwezi kuungana bado?
Mkuu nimekwisha kujibu swali hili huko nyuma. Ya kwamba, sababu za vyama hivi kutoungana ukweli sizijui kama nisivyojua sababu za CCJ...isipokuwa naweza ku speculate kwamba inatokana na ilee habari ya UJINGA (kutojua) na ULIMBUKENI (kujua) wakifikiri wao wanajua kumbe hawajui...na ndio shina la mti Ubinafsi kuunda matawi yake..

Pili, kutoelewa msingi wa kuwepo vyama vingi.. Demokrasia haimaanishi ni utengano baina ya watu kifikra ila ni umoja wenye itikadi (imani) tofauti. Politics zote za Bongo zinazungumzia Watu na Matukio, huu ndio muundo wa demokrasia yetu. Na huwezi kubadilisha tofauti hizi iwe kwa CUF, Chadema wala CCJ kwani wote pamoja na kuwa na itikadi zao bado wanaona hawana jukumu moja. Kila mmoja wao anafikiria yeye kuwa Mtawala kama yule Nyuki anayetaka kujenga mzinga karibu na mzoga. Sasa maadam silaha kubwa ya CCJ ni itikadi ambayo ndio wanajivunia hiyo itikadi haiwezi kufanya kazi ktk mfumo usiotambua tofauti hizi..Politics za Tanzania zinazungumzia sana WATU na MATUKIO yao..lacking insight of the all idea behind Politics

Mkuu wangu, CCM waliunda mfumo wa vyama vingi for their benefit and advantage. Kwanza ni Tanzania na uongozi wake kukubalika kama nchi ya demokrasia kuweza kupata mikopo na misaada. Na hivyo kufanya mfumo mzima wa demokrasia nchini kuwa fake hata kama kuna tofauti za Kiitikadi ambazo hazitumiki. Ni sawa na kuunda sheria lakini wapo watu ambao ni above the law, kisha mnaendelea kuongeza sheria zaidi pasipo kufuta mamlaka ya wale walioko juu ya sheria.

Sasa mkuu wangu mimi na wewe tusiwe kama wao, tufikirie tofauti na kuwakilisha mawazo yetu kwa Umma wa Watanzania ikiwa ni pamoja na viongozi wa vyama hivi. Tusiendelee kuunda vyama vingi ktk mfumo batili badala yake nguvu zetu ziwe ktk kubomoa muundo huo kwanza. Na hatuwezi kufanya hivyo pasipo ushindi dhidi ya CCM.. Kwangu mimi CCM ni sawa na mtawala mkoloni na aje huyo Kingunge aniulize kama namjua Mkoloni!..Na kumwondoa mkoloni kwanza unahitaji Uongozi safi, umoja na nguvu ya wananchi, siasa za Mapinduzi na mwisho master plan.
Tumechukua miaka kumsafisha Kikwete, chaguo lilikuwa la JK kutusikiliza au kutokutusikiliza maadam sisi tuliifanya kazi yetu kila tulipoona inahitajika lakini ktk akili za wanaojua kumbe hawajui walifanya wao wanayoyaona bora zaidi na tumefika hapa. . Na wewe Mwanakijiji pengine uliunda maadui kwa kufanya hivyo..lakini maadam ulikuwa na nia safi, lengo safi kwa maslahi ya taifa zima..Ujumbe wako wooote ulifika..
 
Mkuu nimekwisha kujibu swali hili huko nyuma. Ya kwamba, sababu za vyama hivi kutoungana ukweli sizijui kama nisivyojua sababu za CCJ...isipokuwa naweza ku speculate kwamba inatokana na ilee habari ya UJINGA (kutojua) na ULIMBUKENI (kujua) wakifikiri wao wanajua kumbe hawajui...na ndio shina la mti Ubinafsi kuunda matawi yake..

Kama hujui kwanini hivi vyama kwa miaka 15 vimeshindwa kuungana licha ya kilio cha wao kuungana kimekuwa kikitolewa tangu mwanzo wa mageuzi, unafikiri ni kwanini leo ati watapata mwamko wa kuungana kwa sababu CCJ inakuja au inatishia kwenda peke yake?

asa maadam Pili, kutoelewa msingi wa kuwepo vyama vingi.. Demokrasia haimaanishi ni utengano baina ya watu kifikra ila ni umoja wenye itikadi (imani) tofauti. Politics zote za Bongo zinazungumzia Watu na Matukio, huu ndio muundo wa demokrasia yetu. Na huwezi kubadilisha tofauti hizi iwe kwa CUF, Chadema wala CCJ kwani wote pamoja na kuwa na itikadi zao bado wanaona hawana jukumu moja. Kila mmoja wao anafikiria yeye kuwa Mtawala kama yule Nyuki anayetaka kujenga mzinga karibu na mzoga.

Hizi tofauti za kuwa na mtazamo mmoja au kuwa na imani tofauti ndiyo sababu ya ugumu wa muungano. Ndio maana naita muungano kwenye mazingira hayo ni muungano wa udhaifu. NI lazima muungane kwanza katika msingi wa mambo mnayoyasimamia au itikazi mnazozisimamia. Sielewi muungano mnaotaka wa vyama vya upinzani uwe ni muungano wa majina tu?

Ssilaha kubwa ya CCJ ni itikadi ambayo ndio wanajivunia hiyo itikadi haiwezi kufanya kazi ktk mfumo usiotambua tofauti hizi..Politics za Tanzania zinazungumzia sana WATU na MATUKIO yao..lacking insight of the all idea behind Politics

Nadhani ni kwa sababu wananchii hawajapewa uchaguzi wa wazi wa tofauti za kiitikadi kwani ni kweli siasa zinazungumzia watu na matukio zaidi kama unavyosema. CCJ inataka kutoa pendekezo la tofauti za kiitikadi, sera na kimtazamo ili wananchi waweze kuchagua uongozi siyo kwa kuangalia watu tu bali pia kwa kuangalia itikadi ambayo imewekwa wazi na kueleweka.


Mkuu wangu, CCM waliunda mfumo wa vyama vingi for their benefit and advantage. Kwanza ni Tanzania na uongozi wake kukubalika kama nchi ya demokrasia kuweza kupata mikopo na misaada. Na hivyo kufanya mfumo mzima wa demokrasia nchini kuwa fake hata kama kuna tofauti za Kiitikadi ambazo hazitumiki. Ni sawa na kuunda sheria lakini wapo watu ambao ni above the law, kisha mnaendelea kuongeza sheria zaidi pasipo kufuta mamlaka ya wale walioko juu ya sheria.

Kuna ukweli hapo.

Sasa mkuu wangu mimi na wewe tusiwe kama wao, tufikirie tofauti na kuwakilisha mawazo yetu kwa Umma wa Watanzania ikiwa ni pamoja na viongozi wa vyama hivi. Tusiendelee kuunda vyama vingi ktk mfumo batili badala yake nguvu zetu ziwe ktk kubomoa muundo huo kwanza.

Kweli, lakini hilo linawezekana katika kuwa na msimamo wa nguvu. Wengine tumejaribu sana miaka hii iliyopita kuleta mapendekezo yetu ya kuleta muungano wa zaidi ya majina na vyama ili kuweza hatimaye kuwa na upinzani wenye nguvu. Juhudi hizo zimekwama kwa sababu vyama vilivyopo sasa haviko wazi kupokea mawazo mapya ya mabadiliko yenye lengo kubwa zaidi zaidi ya vyama. Kwa miaka 15 Watanzania wamependekeza vyama vya upinzani kuungana na kushirikiana lakini tofauti zao za malengo, mitazamo na itikadi zimefanya muungano wa aina hiyo kutowezekana kabisa kwani katika muungano huo kuna vyama vitatakiwa viachile baadhi ya mambo na vingine kukubali mambo ambayo hayakuwepo. Kwa mfano, Chadema na sera ya majimbo je kinaweza kuiachilia kwa ajili ya muungano? CUF na masuala fulani ya Zanzibar inaweza kuyaachilia ili iungane? utaona kumbe kuna mambo ambayo vyama vinashikilia sana kwa sababu ndiyo ya msingi kwake.
Na hatuwezi kufanya hivyo pasipo ushindi dhidi ya CCM.. Kwangu mimi CCM ni sawa na mtawala mkoloni na aje huyo Kingunge aniulize kama namjua Mkoloni!..Na kumwondoa mkoloni kwanza unahitaji Uongozi safi, umoja na nguvu ya wananchi, siasa za Mapinduzi na mwisho master plan.

Hilo ndio kosa; huwezi kuanza na hivyo halafu ukamaliza na master plan; utakuwa umemuweka farasi nyuma na mkokoteni mbele.

Tumechukua miaka kumsafisha Kikwete, chaguo lilikuwa la JK kutusikiliza au kutokutusikiliza lna sisi tuliifanya kazi yetu kila tulipoona makosa lakini ktk akili za wanaojua kumbe hawajui walifanya wao wanayoyaona bora zaidi na tumefika hapa. .
Hili ni kweli.

Na wewe Mwanakijiji pengine uliunda maadui kwa kufanya hivyo..lakini maadam ulikuwa na nia safi, lengo safi kwa maslahi ya taifa zima..Ujumbe wako ulipofika..

Hili ni sehemu ya gharama hiyo na ninaamini kwa kadiri naendelea kusimama ninaposimama nitajiongezea na tayari nimeshajiongezea maadui wengi zaidi na wenye nguvu zaidi. Lakini ni gharama ambayo nilikuwa tayari kuilipa miaka minne iliyopita kama nilivyo tayari kuilipa kwa miaka mingi ijayo. Ni matokeo tu ya maamuzi ambayo tunatakiwa kuchukua.
 
Na ningekuelewa kama CCM ni tatizo la CCJ sio wananchi kwa ujumla wake, kwani silaha na nguvu ulizonazo wewe CCJ hana Chadema au CUF lakini pia walizonazo wao wewe huna. Ndio maana unaanza kutafuta kusajili na umeshindwa kupita hapo wakati wenzako wameisha kuwa na nguvu hiyo, bado unatafuta nguvu ya wanachama acha mbali Wapiga kura ambao within four month uwe tayari umewashawishi vya kutosha. Hizi ni weakness zako lakini ni plus ktk umoja wa vyama.

Bila shaka Waanzilishi wa CCJ baada ya kuona kwamba vyama vilivyopo vimeshindwa kuwaondolea wananchi 'tatizo' wameamua kuingia ulingoni kama chama cha upinzani chenye mipango na mikakati wanayoamini inaweza kulishughulikia 'tatizo' ambalo limevishinda vyama vingine vilivyoanzishwa karibu miaka 15 iliyopita.

Kukilaumu CCJ kutoungana ama kukilazimisha kuungana na vyama vingine hakuna sababu. Tunavyojua ndani ya vyama vya upinzani suala la kuunganisha vyama sio priority kwao kwa sababu havionyeshi juhudu zozote za kutaka kuendeleza ile azma yao ya kutaka kuungana hata kama ni kugawana majimbo wakati wa uchaguzi ili kudhibiti mgawanyo wa kura na hatimaye CCM kupata ushindi. Mpaka sasa miezi minne kwenda kwenye uchaguzi tunaona kila chama kitaenda kwenye uchaguzi kivyake vyake.

Kingine cha kushangaza ni kwamba baadhi ya viongozi hao wa vyama vya ‘upinzani’ ambavyo CCJ inatakiwa iungane navyo wamekuwa wakisimama majukwaani kufagilia Serikali ya CCM ama kusifu yanayofanywa na viongozi wa CCM! Sidhani kwamba ni kazi ya upinzani kusifu viongozi ama Serikali ya Chama cha upinzani (CCM) pale yanapofanyika yanayostahili kutendwa na viongozi ama Serikali iliyo madarakani! Upinzani kazi yake si kusifu (hata kama Serikali imefanya mazuri) bali kama nia ya upinzani ni kutafuta kuongoza nchi, kazi ya kila kukicha ni kutafuta mapungufu na udhaifu wa Chama na Serikali iliyo madarakani na kupigia kelele kwa nguvu zote ili wananchi waweze kuelewa hatimaye wasikichague chama hicho tena.

Ninachokiona kinaendelea vichwani mwa baadhi ya watu baada ya CCJ kutaka usajili ni hofu ileile inayoonyeshwa na CCM kwamba huenda CCJ kitafanikiwa kufanya yale yaliyovishinda vyama vingine. Ni vyema tuwaache CCJ nao wajaribu pale vyama vingine viliposhindwa. Mpaka sasa vyama vya upinzani vimeshindwa kutoa elimu ya siasa kwa wananchi kwa ujumla, kushawishi ipasavyo wananchi na wanachama wa CCM wakatae kuwachagua wagombea wao na wakatae kukipa ushindi chama hicho. Vyama vya upinzani kwao wao kusimama majukwaani kuhutubia wananchi mara moja kwa msimu ndio wamemaliza kazi badala ya kuweka mikakati endelevu na ya kudumu ya kuwafikia wananchi wakati wote. Pia upinzani wameshindwa kuwashawishi wanachama wa CCM na viongozi waadilifu na wenye uwezo wa kuongoza watoke CCM waungane na vyama vyao.

Inawezekana sana kwamba kupitia nguvu itakayopatikana na ushawishi wa CCJ vyama vingine vyenye nia thabiti na vyenye kuitakia mema nchi yetu vinaweza kukubali kuunganisha nguvu ili kukishinda CCM. Kama kweli nia yetu ni kutaka tuondoe 'tatizo' nchini mwetu kuna ubaya gani kuungana na chama kipya ambacho kimeonyesha dalili za kuleta matumaini mapya? Kwa maoni yangu, udadisi mwingi usio na sababu una dalili za ubinafsi!
 
You must stand together as one, ndipo hili lidude likubwa li SISIEM, litang'oka, bila hivyo, tusubirie miaka 5 mingine!

sijui kwanini hili la kusimama pamoja ni gumu kueleweka. Hivi mnasimama pamoja katika msingi gani? NImekataa muungano wenye lengo moja tu la kuindoa CCM madarakani, huo ni muungano wenye msingi wa udhaifu. U have to unite in strength..
 
Mzee Mwanakijiji,
Maadam unaamini hivyo mkuu endelea na imani yako au yenu to the finals na hakika nakuombeeni kila la kheri even though najua hamtafika popote.. By the way I'm 100% sure kwamba watu kama Salim, Warioba, Sitta na wengineo waitwao wapiganaji waliowahi kupitia njia ngumu za mageuzi nchini hawamo ktk chama hiki cha CCJ - HAWAMO. I bet yah! hawa ni opportunist tu hakuna Tumaini Jipya hapa na pengine umeingizwa mkenge wewe.

Ikiwa umeshindwa kuelewa kwa nini CUF visiwani, NCCR-Mageuzi waliweza kushindana na CCM pasipo kuwepo upinzani wa vyama 18 sidhani kama utaelewa lolote kamawasivyoelewa wengineo..Ukishindwa kuliona hilo na ukafikiria Chama CCJ kama chama badala ya WATU kuunganisha nguvu zao sidhani kamautakuja kuelewa. Tutakuwa tunazungumza lugha ya JK kuwatukana kina Mgaya hali swala zima la TUCTA linawahusu wafanyakazi wote wa Umma.
 
Mzee Mwanakijiji,
Maadam unaamini hivyo mkuu endelea na imani yako au yenu to the finals na hakika nakuombeeni kila la kheri even though najua hamtafika popote.. By the way I'm 100% sure kwamba watu kama Salim, Warioba, Sitta na wengineo waitwao wapiganaji waliowahi kupitia njia ngumu za mageuzi nchini hawamo ktk chama hiki cha CCJ - HAWAMO. I bet yah! hawa ni opportunist tu hakuna Tumaini Jipya hapa na pengine umeingizwa mkenge wewe.

ni uwezekano mkubwa kweli lakini ni gharama ambayo niko tayari kuilipa. Katika life kuna risk takers.. I'm one of them.

Ikiwa umeshindwa kuelewa kwa nini CUF visiwani, NCCR-Mageuzi waliweza kushindana na CCM pasipo kuwepo upinzani wa vyama 18 sidhani kama utaelewa lolote kamawasivyoelewa wengineo..Ukishindwa kuliona hilo na ukafikiria Chama CCJ kama chama badala ya WATU kuunganisha nguvu zao sidhani kamautakuja kuelewa. Tutakuwa tunazungumza lugha ya JK kuwatukana kina Mgaya hali swala zima la TUCTA linawahusu wafanyakazi wote wa Umma.

Inawezekana kabisa ni kutokana na kile ulichokisema ni ujinga na upumbavu wa baadhi yetu na uwezo wetu mdogo wa kuelewa mambo haya ya umoja. Nyinyi wenzetu wenye uelewa mkubwa na uliopevuka tafuteni umoja kwenye hivi vyama 13 vingine mtufundishe sisi wengine.
 
ni uwezekano mkubwa kweli lakini ni gharama ambayo niko tayari kuilipa. Katika life kuna risk takers.. I'm one of them.
Inawezekana kabisa ni kutokana na kile ulichokisema ni ujinga na upumbavu wa baadhi yetu na uwezo wetu mdogo wa kuelewa mambo haya ya umoja. Nyinyi wenzetu wenye uelewa mkubwa na uliopevuka tafuteni umoja kwenye hivi vyama 13 vingine mtufundishe sisi wengine.
Mkuu wangu nimesema huwezi kunielewa na unazidi kutonielewa. hao vyama 18 pamoja na CCM hawana tofauti na wewe CCJ hivyo nitaweza vipi kupata Umoja kwa watu ambao mna asili moja? - Nyote hamuambiliki mkasikia ila mnayajua yenu!
 
Mkuu wangu nimesema huwezi kunielewa na unazidi kutonielewa. hao vyama 18 pamoja na CCM hawana tofauti na wewe CCJ hivyo nitaweza vipi kupata Umoja kwa watu ambao mna asili moja? - Nyote hamuambiliki mkasikia ila mnayajua yenu!

labda tuna uwezo mdogo wa kukuelewa mkuu maana mawazo yako yamepita uwezo wetu wa kufahamu au kukuelewa; ila usikate tamaa kujaribu kuendelea kutufahamisha.
 
Back
Top Bottom