CAG isiwe na kazi ya kutuletea taarifa ya majizi na pesa waloziiba serikalini ni bora watafute mbinu ya kuzuia wizi, hili pendekezo

Mzanzibari Huru

JF-Expert Member
Apr 17, 2014
373
225
Ndugu wana jamii

Wizi serikalini na katika mashirika ya umma ni tatizo sugu. Tatizo hili lipo miaka nenda miaka rudi. Tatizo hili ni shida sana kulitatuwa kwasabu ni tatizo lililomo kwenye damu ya watendaji.

Ikiwa kazi ya CAG ni kutowa ripoti kila mwaka juu ya wizi ulifanyika kila mwaka jana, hii haitokuwa tafauti sana na zile taarifa za habari tu na basi wizi hauwezi kung'oka. katika maiaka ya 80 wizi ulikuwa kwa milioni 4 au 5, sasa umekuwa kwa milioni 100 hadi mabilioni.

Njia ya kuzuia wizi 100% haipo na haiwezekani kabisa hata kufikiria hatuwa hizo, yaani hata ripoti ya CAG ya mwaka ujao itaonesha vile vile kuna wizi mzigo lala salama ulofanyika katika vitengo mbali mbali. Lakini uwezo wa kupunguza wizi huo hadi asilimia 80% upo.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuigeuza CAG badala ya kuhesabu wizi ulofanyika kila mwaka jana, sasa wazuie wizi unawoweza kufanyika mwaka huu na mwaka kesho. Njia pekee ni kubadilisha mfumo mzima wa ununuzi serikalini na katika mashirika ya umma. Ikiwa manunuzi yote yanapitia CAG na kupata approval ya CAG basi wizi ule wa kununua vitu hewa au kudai huduma hewa utazuilika hapo hapo. Tunajuwa hili inawezekana kwasababu hakuna manunuzi ya kila siku na CAG itajipanga kiuajari, kimajukumu na kitaalamu.

Pia tender zote za serikali na mashirika ya umma zipitie CAG. Hapo tender hewa na malipo yasiokua ya lazima yataweza kuzuiliwa moja kwa moja. Mfano zile riba zinazoongezeka kwasababu walipaji walizembea au walifanya kusudi ili wavune kidogo katika ile riba.

Ikiwa si hivyo kila mwaka tutakuwa tunazidi kulalamika kuliko mwka ulopia.
 
Huwezi kubuni mbinu bila kujua tatizo lilivyo kwani hata wizi nao huangalia udhaifu ulipo ndipo wabuni mbinu za kuiba
Anyway sikatai wazo lako.
Mambo ni vice versa!!
 
Safi kabisa, mimi husema, kazi ya CAG isiwe KUKAGUA tu, bali pia KUDHIBITI.
 
CAG awe na Ma - PP wake kabisa akimaliza kazi anawakabidhi taarifa wao ni kufungua kesi tu na CAG ndio anakuwa shahidi.

Sasa huyu CAG wa sasa ni kutoa ripoti tu kwa rais na bunge na hii imefanywa kwa makusudi ili kuwalinda wezi ambao ni watiifu kwa chama cha mapinduzi. Huo ndio ukweli.
 
Mbona mnatumia akili ndogo hivi?
Takukuru wafanye nini?
Hii taasisi kazi yake ni ukaguzi tu
 
'…Kazi yetu ni kuonesha mapungufu katika Mfumo wa Serikali katika maeneo tuliyokagua, na report yetu inaenda Bungeni…kazi ya Bunge sasa ni kusimamia yale Mapendekezo tuliyopendekeza …'-Prof Assad
 
CAG awe na Ma - PP wake kabisa akimaliza kazi anawakabidhi taarifa wao ni kufungua kesi tu na CAG ndio anakuwa shahidi.

Sasa huyu CAG wa sasa ni kutoa ripoti tu kwa rais na bunge na hii imefanywa kwa makusudi ili kuwalinda wezi ambao ni watiifu kwa chama cha mapinduzi. Huo ndio ukweli.

Basi itakuwa kila mwaka tunazungumzia na kuumiza vichwa maana mapesa yanayo ibiwa yatazidi kila mwaka. Hapana shaka juu ya hilo. Wakuu washajuwa kwamba zaidi ni kufukuzwa kazi tu.
 
Huwezi kubuni mbinu bila kujua tatizo lilivyo kwani hata wizi nao huangalia udhaifu ulipo ndipo wabuni mbinu za kuiba
Anyway sikatai wazo lako.
Mambo ni vice versa!!

Mkuu Emiir

Tatizo linajukikana na wala sio jipya. Laniki labda useme hatuna haja ya kubuni mbinu ya kulitatuwa tatizo hilo.

Katika mashirika yooote duniani ubadhirifu unatokeza katika manunuzi, wafanyakazi hewa na katika mikataba. Kikawaida wakuu hawaendi na mapauro kuchota pesa kiholela, wanakakuwa na mikakakti yao na zaidi inalala humo katika manunuzi, wafanyakazi hewa na mikataba.

Hayo yote yanazulika kiurahisi sana ikiwa kweli wakuu wako tayari kufanya hivyo. Hiyo niliyoitaja ni katika mbinu moja.
 
Ukisoma ripoti za CAG unaona mwishoni anatoa mapendekezo yake, hata hii ripoti ameelzea ni mapendekezo asilimia ngapi yamefanyiwa kazi, asilimia ngapi hayajafanyiwa kazi na mangapi yamepitwa na wakati.
Tatizo CAG hana meno kama angepewa nguvu zaidi ya ripoti yake kukabidhiwa kwa mwendesha mashitaka ni wazi makosa haya yasingekuwa yanajirudia.
 
Tatizo CAG hana meno kama angepewa nguvu zaidi ya ripoti yake kukabidhiwa kwa mwendesha mashitaka ni wazi makosa haya yasingekuwa yanajirudia.

Mwisho wake ni kupewa nguvu ya kusimamia uhariifu unaoendelea. Otherwise, itakuwa ni ripoti juu ya ripoti bila faida.
 
CAG pia anayo kazi ya kudhibiti..huyu man of the match wenu tunatambua amepewa kazi maalum..sisi sio wajinga.
 
Ndugu wana jamii

Wizi serikalini na katika mashirika ya umma ni tatizo sugu. Tatizo hili lipo miaka nenda miaka rudi. Tatizo hili ni shida sana kulitatuwa kwasabu ni tatizo lililomo kwenye damu ya watendaji.

Ikiwa kazi ya CAG ni kutowa ripoti kila mwaka juu ya wizi ulifanyika kila mwaka jana, hii haitokuwa tafauti sana na zile taarifa za habari tu na basi wizi hauwezi kung'oka. katika maiaka ya 80 wizi ulikuwa kwa milioni 4 au 5, sasa umekuwa kwa milioni 100 hadi mabilioni.

Njia ya kuzuia wizi 100% haipo na haiwezekani kabisa hata kufikiria hatuwa hizo, yaani hata ripoti ya CAG ya mwaka ujao itaonesha vile vile kuna wizi mzigo lala salama ulofanyika katika vitengo mbali mbali. Lakini uwezo wa kupunguza wizi huo hadi asilimia 80% upo.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuigeuza CAG badala ya kuhesabu wizi ulofanyika kila mwaka jana, sasa wazuie wizi unawoweza kufanyika mwaka huu na mwaka kesho. Njia pekee ni kubadilisha mfumo mzima wa ununuzi serikalini na katika mashirika ya umma. Ikiwa manunuzi yote yanapitia CAG na kupata approval ya CAG basi wizi ule wa kununua vitu hewa au kudai huduma hewa utazuilika hapo hapo. Tunajuwa hili inawezekana kwasababu hakuna manunuzi ya kila siku na CAG itajipanga kiuajari, kimajukumu na kitaalamu.

Pia tender zote za serikali na mashirika ya umma zipitie CAG. Hapo tender hewa na malipo yasiokua ya lazima yataweza kuzuiliwa moja kwa moja. Mfano zile riba zinazoongezeka kwasababu walipaji walizembea au walifanya kusudi ili wavune kidogo katika ile riba.

Ikiwa si hivyo kila mwaka tutakuwa tunazidi kulalamika kuliko mwka ulopia.
MAPENDEKEZO YOTE YALE HUKUYAONA? AU UNAANDIKA BILA KUJUA UNAANDIKA NIN?
 
Back
Top Bottom