Bungeni Live: Juni 3, 2012 [Morning Session]

Bungeni Live: Juni 3, 2012 [Morning Session]

Siyo Chemba tu, bali bunge zima halina maana tena , siyo CCM siyo Chadema, wote nyanya nini wanachokifanya sasa. Wapishe vyama vingine wachangie
 
Kwa jinsi hali inavyozidi kuwa tete mahospitalini kutokana na serikali kucheza vibaya kete yake, hadi kufikia Ijumaa baadhi ya wabunge wa CCM wataibua hoja ya Bunge kuingilia kati suala hilo na kujadili ripoti ya Kamati ya Bunge ya Afya.

Wameamua kuchukua uamuzi mgumu kwa maslahi ya walalahoi, na hata kama wataonekana wabaya kwa wenzao basi, Liwalo na Liwe!!

Nawaombea kila la heri wafanikiwe.
 
Leo Mnyika amekuwa mbogo baada ya Mwigulu Nchemba kuleta propaganda bungeni badala ya kujadili bajeti ya serikali anajadili bajeti ya kambi ya upinzani na akagusia suala usalama wa taifa kutofanya kazi ipasavyo, ndipo Mnyika aliposimamia hapo kuwa usalama wa taifa wamezuia kujadili suala la EPA, kagoda na ufisadi mwingine bungeni na pia alisema katika wizi wa EPA Anahusika na ndipo alipopewa siku saba kuleta ushahidi.

Nawasilisha.
 
mie naona ni udhaifu wa mwenyekiti. maana anaongea kishabiki hana lolote.
 
CDM hawajajipanga namna ya kukabili ukiukwaji wa sheria za kuendesha bunge nje ya bunge.Ndani ya bunge tayari wananchi wanachanganywa tu. CDM Must do something very aggressive against this shit! Waache kucheza ngoma kama CCM.
Mipasho ya CCM inasaidia kununua muda bunge liishe bila kujadili na kuchukua hatua mambo ya msingi.CDM mpo bungeni miaka zaidi ya miwili sasa tunataka muwakabili CCM kwa namna yoyote ile hata ya kuwasusia bunge kuliko kuishia kupigizana kelele kama wao.

Enough is enough!
 
Siyo kwa CCM hii ya Stella Manyanya na Mchemba.Hii CCM haijawahi kuwa na uchungu kwa wananchi kiasi hicho kwani wasingewaibia na kupora rasilimali zao wezi wakubwa!!
 
siyo chemba tu, bali bunge zima halina maana tena , siyo ccm siyo chadema, wote nyanya nini wanachokifanya sasa. Wapishe vyama vingine wachangie

yaani inauma sana..wataalamu wa nchi hii wanavyopata shida halafu watu wanapewa magari,posho ya kutosha,mishahara mizury...bado wanaleta mizaha inauma sana.....watumishi wa umma hakuna namna ya migomoni lazima..tunavuja jasho makazini.hakuna viyoyozi wala nn.....tuna kila sababu ya kugoma
 
toka asubuhi mpaka saa sita na dakika arobaini hakuna kipengele chochote cha budget kilichojadiliwa ni mipashoo kwa kwenda mbeleee,mchemba leo kakabwa koo hakuweza kutoa matusi yake bila kupingwa
 
sasa ni dhaifu kila sekta.full commedy
 
Back
Top Bottom