Taasisi hii kwa sasa naona imeshindwa Kazi ya Kulilinda Taifa pamoja na rasilimali zake. Nachofahamu hawa jamaa ilibidi wawe proactive kwenye kuibua pamoja na kupangua njama mbalimbali zenye athari kwa Taifa. Kazi ambayo inatakiwa kufanyika kwa siri huku wakiweka uadilifu mbele ili kuepuka mazingira ya uonevu kwa namna yeyote ile.
Kwa matukio ya hivi karibuni nashawishika kusema ya kwamba hawa jamaa hawafanyi kazi kwa kufuata misingi ya sheria na haki. Badala yake wanatumika na wanasiasa kwa jinsi wapendavyo. Watu wanaogharimiwa na kodi za wavuja jasho wa nchi hii kwa sasa wamegeuka wasaliti na watu wa hatari dhidi ya wanyonge.
Aidha nashawishika kusema wanafanya yote haya kwa makusudi au bila ya kupenda. Kikubwa ninachokiona hapa ni mpasuko uliopo ndani ya jeshi hili kwa sasa " wapo wasiopenda mwenendo wa serikali - lakini ukishaingia humu kutoka sahau .....na hukumu ya usaliti inajulikana na wote" ...kwa upande mwingine " wapo wanaopenda huu mwenendo wa serikali - hawa ni wale wanaofaidika na actions za serkali kwa namna moja au ingine".
Mgawanyiko uliopo ndani ya TISS kwa sasa unatokana na sababu nyingi: kikubwa kikiwa ni usiri uliopo kwenye mambo mengi - angalia hawapendi hata kuhojiwa au kuweka hadharani ufanisi wao wa kazi. Hivi waziri wa ulinzi na usalama akisimama hadharani akasema " mwezi june - TISS imefanikiwa kuchunguza na hivyo kufanikisha urejeshwaji wa Tsh. Billion 300 zilizofichwa uswis nchini TZ" hapo kutakuwa na kipi kilichoharibika?. Ni mambo mengi sana yanayotakiwa yahojiwe kuhusu uhalali wa uwepo wa TISS katika kulisaidia taifa kwenye utatuzi wa mambo mbalimbali yaliyolikumba taifa hili. Mpaka leo hatuna majibu sahihi ya madubwana kama vile RICHMOND, DOWAN's, EPA, Meremeta, n.k.
Ukisoma heading yangu nauliza hivi ni sahihi kuendelea kusema tuna usalama wa taifa au tumetengeneza hatari nyingine kubwa zaidi. Nasema hivyo kwa sababu naliona hili ni joka lingine litakaloleta machafuko ndani ya nchi hii. Angalia matukio wanayohusishwa nayo kuya- engineer kila siku:
1) Kutuhumiwa kuvuruga chaguzi mbalimbali
2) Kutuhumiwa kufanya attempts mbalimbali za piga, kujeruhi na mara ingine vifo vyenye utata.
3) Kutuhumiwa kwenye wizi wa kiasi kikubwa cha fedha za wananchi
4) Kutuhumiwa ku- create matukio yanayo divert minds za watu na hivyo kuacha kujadili mijadala ya kitaifa mfano: kikombe cha babu nchi nzima.
Yote hayo kwa uchache tu ni kinyume na sheria ya uanzishwaji wa usalama wa Taifa inavyowataka kuenenda. Lakini watawala wanafanya yote haya kwa kupitia loophole ya usiri uliopo kwenye hiyo taasisi, wamesahau ya kuwa wanaongeza mpasuko uliopo. Haya yote yatakuja kuwarudi, wajiulize swali dogo sana - kwanini siri za serikali zinavuja? Jibu langu binafsi ni kwa sababu baadhi ya members wa TISS hawaridhishwi na ukiukwaji wa misingi ya Taasisi za usalama wa Taifa.
Kwa kumazia ndugu zangu, naombeni tuelezane ukweli....tutakuwa tunafanya makosa kusema hii ni taasisi hatarishi kwa usalama wa Taifa kutokana na mwenendo wa matukio ya sasa?
NB:
"Anayejimilikisha hati ya kutoa roho za wengine ajue nayeye hataishi milele ndani ya dunia hii iliyoumbwa na mwenyezi Mungu"