Bungeni Live: Juni 3, 2012 [Morning Session]

stop parables! Dadavua mkuu

Wanachuana kuhusu miongozo na kanuni mpaka sasa dakika zimepita kumi huyu akisema kanuni hii na Mhagama anatoa kanuni hii ili mradi tu mambo yanakwenda, naona simbachawene amesimama kumwambia mwenyekiti Mhagama kwamba kanuni nyingi na miongozo inakwenda kinyume na kupoteza muda na ametoa ukweli muda unakwenda
 
nimeshangazwa sana na huyu mama kuongea huku akihema wakati akijaribu kumdhalilisha Mh mnyika!inaonyesha mama tangu maepigwa chini na jamaa mambo yake ni pupa pupa tu!
Mbona huyu mama nasikia ana "viumbe" anawafuga?
 
Hana jipya zaidi ya kujizalilisha anataka watu wamlipue mtuhumiwa wa EPA

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Naanza kuchelea wewe ndio unayewashwa....maana leo kila thread unayochangia huachi taja hilo neno! Tangaza tu kuwa unatafuta mkunaji...wapo wengi humu JF!
kwani wale ambao kila wakichangia hawakosi neno "dhaifu" ndani yake,,, nao ni dhaifu??
 
mfumaniwaje naye anaona wivu mnyika kusimama na kuomba muongoza mara kwa mara.
"Chimba cha mwena naye ucho umemchuka hana ata usu"
 
Mkasomali na Mnyika waomba mwongozo kufuatia mgogoro wa madaktari na uendeshwaji wa Bunge hapo jana

Mwenyekiti bi Jesta Mhagama awazima, Mnyika aomba mwongozo

Kuna haja ya upinzani ku review tena ushiriki wao bungeni kwani kwa hali inavyoendelea dhidi ya upinzani ni dhahiri hawataweza kuchangia sawasawa. Wabunge waitishe kikao cha upinzani waamue kama wataendelea kushiriki bunge la namna hii au la!! Sisi wananchi hatufurahishwi kwa jinsi CCM wanavyozima hoja za upinzani kibabe ili kuficha ukweli na UDHAIFU wa Serikali. This is too much wabunge waachieni CCM wenyewe kwani kuna siku mtarushiana viti
 
Njia za kujibizana na CCM bungeni haziwezi kutoa matunda zaidi ya wabunge wa CDM kudhalilishwa tu tena wakisaidiwa na Spika na wenyeviti wa bunge.
CCM wameshapoteza credibility kwa wananchi wafanyalo ni kufanya wabunge wote wakiwemo wa CDM waonekane hamna kitu.
Wabunge wa CDM washinikizwe bunge kuendeshwa kwa haki.ikibidi hata kwa kususa maana hakuna la maana mpaka sasa.Mijadala muhimu inazimwa alafu wabunge wetu hawachukui hatua yoyote,ule moto wa wabunge wetu uko wapi? Au kwavile mmeanza kunywa nao bia mitaani mnaoneana haya?

Tunataka wabunge wa CDM kuwa aggresive kama Mh Lema (mpuuzeni Lema lakini ndivyo CCM wanavyotakiwa kupelekeshwa). inawezekanaje muongoza bunge atukane unawashwa alafu tukae kimya?

Bora msuse bunge hili mrudi mtaani kuwapa elimu ya Katiba wananchi tujue moja maana mnapoteza muda wenu bure na kuishia kutukanwa na kudhalilishwa!
 
Nadhani mwigulu Nchemba anataka kuvuruga mchakato wa bajeti au katumwa ?

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Nadhani mgomo wa madokta umeandaliwa mahsusi ili bajeti zipite kiulaini, maana wabongo hubadili maada kutokana na hot nyuuuzi.
Naye mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.
 
Huyu Mwigulu Njemba nafikiri ameletwa bungeni kuvuruga hoja za upinzani.
 
ww kama huna utitiri kwenye kichwa chako ,una viroboto...Kwa akili yako ya kimagamba upumbavu wa jana bungeni ndo unaushabikia ..badilika usiwe kama mende ukugeuka basi ndo mwisho wako wa kuishi.....come up ..

Yale yale Mh. Washwa washwa na dawa ya kitu kinacho washa ni kukunwa tu
 
Kila anayetoa hoja anatafuta umarufu. Haijibiwi hoja linatolewa hitimisho. Hitimisho la kumkatisha tamaa mtoa hoja. Lengo la viongozi wanasingizia kila anayetoa hoja kinyume na wao ni kufanya watu wasiifikirie hoja hiyo bali waone haja ya kutoa hoja ni umarufu tu. Ndiyo kusema viongozi hawa ni maadui wa umarufu. Hawautaki umarufu waupate watu wa upande tofauti nawao isipokuwa wa upande wao tu. Ni uchoyo na uroho wa UMARUFU unawatawala.

Lakini mtu anapataje umarufu pasipokuwa na jambo tofauti na wengine? Katika michezo (mpira) mchezaji maarufu ni yule anayecheza vizuri kuliko wachezaji wengine wote, katika vita ( Mayunga) ni hodari kuliko wapiganaji wengine katika uwanja wa mapambano. Katika siasa kwenye mashindano ya hoja, mwanasiasa maarufu ni yule mwenye hoja inayokubalika kwa wananchi waliowengi.

Dawa yake sio kusema Mayunga usiwe hodari vitani usije ukapata umaarufu, ni wewe pia kuwa mpambanaji hodari kumzidi Mayunga ndipo utatambulika. Halikadhalika katika siasa dawa sio kumkataza Mnyika kutoa hoja yake ili asijeakawa maarufu bali ni kutoa pia hoja inayoizidi ya Mnyika. Kumzima Mnyika sio jambo rahisi kama anavyofikiri Jenista Mhagama kwa sababu hoja hizo hutoka kichwani mwake, ndivyo anavyoyaona mambo na kufikiri tena kwa haraka.

Ukitaka kumzuia kuwa maarufu mzuie asifikiri vile anavyofikiri au utoe hoja yenye nguvu kuliko yake. Mashindano ya hoja ni hoja pia. Hoja ndiyo kitu pekee kitakacho mpa mwanasiasa umaarufu au kitamzuia kuwa maarufu. Spika hana uwezo wa kumzuia mtu kuwa maarufu ijapokuwa Spika anaweza kupata umaarufu kwa kuwa kiongozi mbaya kuliko wote waliopata bahati ya kuliongoza Bunge la Tanzania kwa kuzia hoja nzito zilizopata kutolewa wabunge makini kama Mnyika.

Lakini Bunge laweza kufaidika kwa kutumia hoja za watu makini kwa sababu kunena sio kutenda. Mbunge akinena serikali ikatekeleza, serikali ndiyo itasika zaidi na kujipatia umaarufu. ACTION SPEAKS LOUDER THAN WORDS. Waweza kupoka umaarufu mtoa maneno kwa kutenda yale aliyoyasema na watu wakasema '' Aaa bwana huyu maneno tupu lakini huyu mtu wa vitendo zaidi'' Serikali waacheni wapinzani wawe maarufu wa kusema lakini ninyi muwe maarufu wa matendo.

Umaarufu hugawanyika kila mtu kwa jambo lake.
 
Back
Top Bottom