Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,867
Mkasomali na Mnyika waomba mwongozo kufuatia mgogoro wa madaktari na uendeshwaji wa Bunge hapo jana
Mwenyekiti bi Jesta Mhagama awazima, Mnyika aomba mwongozo
Mwenyekiti bi Jesta Mhagama awazima, Mnyika aomba mwongozo
Mh. Machali na Mnyika wameomba mwongozo kuhusu sakata la madaktari, kwamba imefika wakati sasa liruhusiwe kujadiliwa bungeni kwani serikali bado inafanya maamuzi kibabe wakati swala lipo mahakamani na Madaktari wanaendelea kugoma huku wananchi wakizidi kuathirika.
Pia Mh. Mnyika amelalamika kuwa jana Mwenyekiti aliwatolea kauli mbaya kwa Mbunge Machali na yeye yaliyokiuka kukiuka kanuni mbalimbali kwa kuwaambia kauli za matusi, maudhi na kashfa kufuatia kumwambia Mkasomali kwamba aache kimbelembele, anadandia hoja na anajitafutia umaarufu. Na kwa mnyika kuwa ameshindwa kujibu taarifa (kufatia hoja za Mwigulu ambazo sikubahatika kuzisikia) ambapo hajapewa nafasi ya kujibu na kuwa eti Mnyika anawashwa (kauli amabyo aliitafasiri kama ni tusi).
Majibu ya Mwenyekiti: Kuhusu sakata la madaktari hakutolea jibu lolote la maana, bali Mwenyekiti amemgeuzia kibao Machali na kusema yeye ndiye alivunja kanuni kwanza (hakutaja zipi), ila kuhusu Mnyika amesema atalijibu baadaye ama siku atakayoona inafaa.
Kama na mhimili huu utabaki kimya kwenye huu mgogoro wa madaktari na serikali, basi itabidi wananchi tutumie nguvu ya UMMA.