Nisingeweza kuyasema hayo vizuri zaidi.Inawezekana kabisa Mayor Masaburi akawa hana hatia,ni mtu safi, lakini kwa kipindi hiki ambacho yuko kwenye uchunguzi si busara hata kidogo kuonekana kwenye hiyo picha na Rais. Psychologically inampa Mayor Masaburi nguvu kubwa sana.
Kitu kingine ambacho kinanipa shida ni nani analipia hizi futari za kila juma? Nauliza hili kwa nia njema kabisa, na natambua hiki ni kipindi muhimu kwa waislam na nilitegemea Rais angefutarisha watu lakini (LAKINI) sikutegemea angefutarisha kwa kasi hii. Nchi masikini ambavyo inakopa kila kukicha kwa nini Rais anashindwa kutambua concept ya 'kubana matumizi'?.
Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi nusura ikwame kwa sababu ya kukosa fedha, Raisi yeye anazo mpaka za kununua zawadi kwa Watuhumiwa wa rushwa? Umpe mtu chakula na zawadi pia? Washauri wa Rais wanafanya nini? Kwanza mmeona hiyo mifuko ya zawadi? ni kiasi gani mfuko mmoja? Hawa waliofutarishwa wana njaa gani mpaka wapewe chakulana Rais?.
Kama ni lazima kufutarisha kila juma basi wafutarishwe watoto yatima na wasukuma mikokoteni. Hawa ndio wanataka chakula lakini sio wakina Mayor Masaburi.
Sijui tumefikaje hapa. Sijui!
Kama ukiwa na kashfa huna hatia mpaka itakapodhihirika, mbona Katibu Mkuu Jairo kaambiwa asikanyage wizarani?
ukitaka kuona makalio ya kuku mpaka upepo upulize.yaani ina maana kwamba bunge liache kumchunguza huyo swahiba wake katika madili waliyofanya au wanataka kufanya jijini dar.
Hamkuelewa kile alichomaanisha Hosea wa takukuru mbele ya balozi wa Marekani bado?
.
lakini bado hana hatia, sivyo? Kwa hiyo inawezekana kuanza kunyimwa haki/mambo fulani hata wakati tunasubiri kuthibitisha hatia.Issue ya Jairo ina ushahidi wa moja kwa moja kwa kuwa ...
Duh, kumbe na wewe tajiri?Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku
Unatarajia nini kutoka kwa kiongozi mahiri mzururaji? Wa Tatanzania hiyo ni miaka yenu ya kuumia. mpaka mshike adabu kwa wrong choice ya uprezida
Kwa kuwa bado anachunguzwa hana hatia, mpaka pale itakapodhihirika kuwa ametenda kosa, kwa maana hiyo yuko huru kukutana na kila mtu hadi pale kosa lake litakapobainika.
<br Hakupeleka mgao alitaka kuwapiga kimya.Kama ukiwa na kashfa huna hatia mpaka itakapodhihirika, mbona Katibu Mkuu Jairo kaambiwa asikanyage wizarani?
(Hawa waliofutarishwa wana njaa gani mpaka wapewe chakula na Rais?. Kama ni lazima kufutarisha kila juma basi wafutarishwe watoto yatima na wasukuma mikokoteni. Hawan ndio wanataka chakula lakini sio wakina Mayor Masaburi.)
kweli kabisa,hata mbele za Mungu funga yako itapokelewa.
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku