Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
Bongo daresalaaaaaaaaam
mkuu maneno yako sawia lakini unampigia mbuzi gitaa na hii ni kutokana na ujinga wetu watanganyika 1. sisi ni wanafiki 2. hatuna uzalendo 3. wengi wetu ni wachumia tumbo 4. sisi ni wajinga wakutupwa 5. watanganyika wote tunatumia masaburi kufikiri 6..... nakomea hapo maana naweza kutukana bure watu wasiojua kuwa wanatukanwa na wakati huo najitukana mwenyeweInawezekana kabisa Mayor Masaburi akawa hana hatia,ni mtu safi, lakini kwa kipindi hiki ambacho yuko kwenye uchunguzi si busara hata kidogo kuonekana kwenye hiyo picha na Rais. Psychologically inampa Mayor Masaburi nguvu kubwa sana.
Kitu kingine ambacho kinanipa shida ni nani analipia hizi futari za kila juma? Nauliza hili kwa nia njema kabisa, na natambua hiki ni kipindi muhimu kwa waislam na nilitegemea Rais angefutarisha watu lakini (LAKINI) sikutegemea angefutarisha kwa kasi hii. Nchi masikini ambavyo inakopa kila kukicha kwa nini Rais anashindwa kutambua concept ya 'kubana matumizi'?.
Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi nusura ikwame kwa sababu ya kukosa fedha, Raisi yeye anazo mpaka za kununua zawadi kwa Watuhumiwa wa rushwa? Umpe mtu chakula na zawadi pia? Washauri wa Rais wanafanya nini? Kwanza mmeona hiyo mifuko ya zawadi? ni kiasi gani mfuko mmoja? Hawa waliofutarishwa wana njaa gani mpaka wapewe chakulana Rais?.
Kama ni lazima kufutarisha kila juma basi wafutarishwe watoto yatima na wasukuma mikokoteni. Hawa ndio wanataka chakula lakini sio wakina Mayor Masaburi.
Sijui tumefikaje hapa. Sijui!
Attitude yako ndio inayolea ufisadi hapa nchini. The fact kuwa mtu anachungzwa anatakiwa kusimamishwa kazi hadi hapo matokeo ya uchunguzi yatoke. Sasa ikithibitika kuwa ni kweli alifanya ufisadi ina maana rais wetu ni sehemu ya ufisadi huo. Kumbuka usemi maarufu "Ukitembea na mwizi na wewe ni mwiziKwa kuwa bado anachunguzwa hana hatia, mpaka pale itakapodhihirika kuwa ametenda kosa, kwa maana hiyo yuko huru kukutana na kila mtu hadi pale kosa lake litakapobainika.
kitendo cha JK kmutaka mtoa rushwa kama amabvyo umeanisha nalo ni tatizo. Kutazama pembeni haisaidii, jiulize kama rasii angekuwa ni Nyerere huyo mhuni angekanyaga hata Ikulu?Hapa JK alikuwa hana jinsi. Alialika viongozi wazito wa jiji hili. Meya asingekosekana. Kwenye Umeya wa JIji hili JK alimtaka Saggaf. Masaburi akatoa dau kubwa zaidi kwenye uchaguzi wa Meya. Diwani mmoja aliniambia kila mmoja alipewa 1.8m. Saggaf alikuwa ametoa 1m. Ndio maana hata hapo kwenye picha JK anaangalia pembeni kabisa.
Kwani si huyo huyo JK alimshika mkono Lowasa kule Monduli alidai kuwa ni SAAAAFIII ...........!!! ............. Nini kilifuata...??? Ghafra Lowasa akawa GAMBA.......... HIVYO HUYO ALIYESEMA WATU WANAFIKIRI KWA KTUMIA MASABURI NAYE ASUBIRI............. Yeye hatakuwa gamba........bari shina la la MAGAMBA
Msahiki Meya wa Dar-es-Salaa, Didas Masaburi.
Wewe unasema nini? huyo mkuu haishi vituko, Rombo alimsimamisha Mramba na kumwita shoka lisilokwisha makali ilihali ana kesi mahakamani ya matumizi mabaya ya ofisi. Ahh! bora ninyamaze tuu maana tukisema sana tutachafua thread bure!MASA BURI bado ni Meya na anawakilisha jamii. HAFLA hiyo ilikuwa jijini dar so kama meya lazima aalikwe ikulu that is protocal; angekuwa amepewa barua ya likizo ili kupisha uchunguzi kisha mr president akampa mwaliko hiyo ni kesi ingine. msimamisheni kwanza!!!!
"DONT MAKE OTHER PEOPLE LAUGH AT YOUR BACK"