Bunda: Lissu atangaza kubadili Sheria ya madini, kwamba atajayeyagundua kwenye ardhi yake yatakuwa yake

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,718
218,266
Nchini Tanzania kwa sheria za sasa , shambani kwako kukikutwa madini , basi haraka sana madini hayo na shamba lako hilo vinageuzwa kuwa mali ya serikali , na baada ya muda mfupi wataletwa wawekezaji wa kiarabu au wa kizungu kuchimba madini hayo , huku wewe ukitimuliwa kwa mijeledi au hata bunduki bila huruma .

Lakini kwenye shamba lako hilo kukikutwa Bangi jua umekwisha , utamilikishwa bangi hiyo na kupigwa pingu .

Sasa leo Tundu Lissu amesema kwamba atakayekuta madini kwenye eneo lake hayo madini yatakuwa yake .mwenyewe , ataamua cha kuyafanya

Screenshot_2023-09-06-20-56-42-1.png

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)-Bara, Tundu Lisu ametaja mambo manne yatakayorekebishwa kwenye sheria ya madini pindi chama hicho kitakapoingia madarakani ili kuwanufaisha wachimbaji wadogo nchini.

Lissu amesema hayo leo Jumatano, Septemba 6, 2023 wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa Operesheni +255 Katiba mpya, eneo la Kinyambiga, Bunda mkoani Mara.

Amesema licha ya sheria ya madini kusema madini yote nchini ni mali ya umma chini ya udhamini wa Rais kwa niaba ya Watanzania lakini amedai kiuhalisia madini ni mali ya Rais.

Lissu amesema suluhisho la kwanza, Chadema itakapoingia madarakani ni kubadilisha sheria hiyo akidai madini yanatakiwa yawe mali kwanza ya wenye ardhi ambaye ataelewana na atakaye yagundua kwenye ardhi yake.

Pili, sheria iseme machimbo ambayo yanatakiwa yawe kwaajili ya wananchi wa kwetu tu na ukweli ni kwamba sheria ndivyo inavyosema ya sasa lakini shida ni CCM...hizi zinazoitwa PMR remaining licence hizi ni leseni zinazotolewa kwaajili ya watanzania," alisema Lissu akihoji wageni wanakujaje mahali hapo.

Alisema wananchi, vijiji, halmashauri na Serikali kuu wanatakiwa kunufaika na rasilimali ya madini yaliyopo kwenye maeneo yao.

Tatu, linalohitaji mabadiliko ni Serikali inapotoa leseni kwa kampuni kubwa lazima kuwe na mgawanyo wa umiliki na faida zake.

Nne, ni kushugulika na mamlaka ya Rais, akidai Katiba iliyopo sasa siyo tu inamfanya Rais amiliki rasilimali za nchi yakiwemo madini, misitu na wanyama pori bali pia inampa nguvu ya kumiliki nchi na watu wake.
 
Lissu kachanganyikiwa. Hicho anachokisema ni ujinga mtupu. Bora hata angesema kwamba madini yakigunduliwa kwenye ardhi yako na wewe unakuwa shareholder wa kampuni itakayochimba uwe unapata mrabaha.
 
Lissu kachanganyikiwa. Hicho anachokisema ni ujinga mtupu. Bora hata angesema kwamba madini yakigunduliwa kwenye ardhi yako na wewe unakuwa shareholder wa kampuni itakayochimba uwe unapata mrabaha.
Uko sahihi Lakini shida itakuja kwenye kujua kiasi Cha madini kilichopatikana Ili upate mrabaha wako.
Mpaka serikali yenyewe imekwama inapigwa Kila kukicha
 
Mhuu hili kidogo lina walakini, kwani sheria inasema ardhi ni mali ya Serikali, ukinunua unapewa possession right tu lakini siyo mali yako. Aisee labda kama ataanza kwa kulibadili hilo.
Ndio maana yake
 
Lissu kachanganyikiwa. Hicho anachokisema ni ujinga mtupu. Bora hata angesema kwamba madini yakigunduliwa kwenye ardhi yako na wewe unakuwa shareholder wa kampuni itakayochimba uwe unapata mrabaha.
Ukishakuwa shareholder ndio ushakuwa mmiliki
 
Lissu kachanganyikiwa. Hicho anachokisema ni ujinga mtupu. Bora hata angesema kwamba madini yakigunduliwa kwenye ardhi yako na wewe unakuwa shareholder wa kampuni itakayochimba uwe unapata mrabaha.
Nadhani mjinga ni wewe. Afadhali tufuate sheria za Marekani.
 
Hawa ndio wapuuzi wa kuongelea sector ya natural resource na mambo ya mikataba ya uwekezaji kweli.

Toka 1960’s makubaliano ya kimataifa ni kwamba natural resources ni mali ya serikali.

Shida ni uelewa wetu mdogo tu kama jamii jinsi mambo yalivyo duniani kwenye kanuni za biashara and ‘law of contract’.

Facts ni kwamba Shivji, Lissu, Kabudi, Mwakabusi and many other nonsensical you call experts their knowledge is very limited on principles.

Elimu yao ya uelewa wa ‘law of contract’ ni sheria yetu. Ambayo na yenyewe ukisoma definition zake misingi ya what forms a legal binding commercial contract are based on (U.K. laws) be it sheria yetu ime cover hayo mambo very simply.

Overall sheria za U.K. zina tafsiri pana sana na hako ka sheria ketu tulikopi nusu bila ya kuelewa misingi ya hizo kanuni tulikokopi. Huko kwao kutokana na scenario tofauti za dispute vitu vyote vilivyopo kwenye sheria yetu vina maelezo zaidi ndio maana DPW wanataka kwenye dispute itumike U.K. law of contract it covers a lot through precedence; ambapo sheria yetu huko kwao ni elementary tu.

Lissu hana uelewa wa hayo, wala Shivji and many other nonsenses; Mwabukusi ndio kabisa kiazi. Mwenye afadhali ni Dr Nshala hila hata yeye mjadala na mtu kama mimi atoboi miaka 800.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom