BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 422
- 1,049
Hayo yametokea katika mkutano wa hadhara ambapo wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Dilifu, kata ya Magamba wamesema Mlima Dilifu ambao ndio wenye machimbo ya dhahabu ni mali ya Wananchi wa kijiji hicho, ambapo wanakerwa na kupangiwa muwekezaji na kudai kunyimwa haki na uhuru wa uchimbaji huku wakidai wanapokonywa leseni ya uchimbaji katika machimbo yaliyoko ndani ya kijiji chao.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusufu amesema mbali na maridhiano kufanyika katika mgogoro huo lakini bado kuna baadhi ya watu wanakwamisha maridhiano ambayo yamekuwa yakifanyika.