Bukoba waendelea kupigwa kalenda stendi kuu ya mabasi, Serikali yasema mpaka itafute fedha

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,488
7,937
Pamoja na ukubwa na umaarufu wa Bukoba na mkoa wa Kagera kwa ujumla, mji ule hauna stendi inayoendana na jina lake, kuna eneo la wazi lenye vichochoro lukuki huku kukiwa hakuna urasmi wapi kwa kuingilia na kutokea pia nyakati za mvua hali ni mbaya.

Leo bungeni, mbunge wa viti maalum, Neema Lugangira amehoji ahadi iliyotolewa na makamu wa Rais kwa niaba Rais Samia Suluhu kujenga stendi ya kisasa mji wa Bukoba.

Majibu ya Silinde kwa niaba ya wizara ni kwamba wameainisha vipaumbele kwenye ahadi za viongozi na jukumu lao sasa ni kutafuta fedha kuhakikisha ahadi zinatekelezwa.

Najiuliza kwa hawa viongozi, unatoaje ahadi kumbe fedha za kutimiza ahadi hujui hata utazipata lini na utazitolea wapi! Yaani watu wachague katika ahadi sasa ndio waanze kutafuta fedha.
 
Hata Stand ya Arusha Mjini nayo inapigwa kalenda tu, CCM hawapendi upinzani hayo yote yanayotokea ni kama adhabu kwa wapinzani.
 
Nyinyi majirani zetu mna tabu sana hata VETA imejengwa juzi hapa! Usomi wote lakini mmmm!!!
 
Bado tumalizia kuing'arisha stand ya kwa Yohana.

Namshukuru sana mama maana bei za bidhaa zinashuka bei kila siku.
 
nyie wahaya achene uvivu, yaani kujenga stendi ya mabasi tuu adi serikali kuu iwajengee??? kuna halamashauri na hata manispaa nnyingi tuu hapa nchini zimejenga stendi kwenye maeneo yao tena za kiwango kabisaa,
 
Huku Mwanza tunazo mbili za kisasa kabisa,
1. Juu nyamhongolo Ilemela manicipal.
2. Chini Nyegezi Mwanza city.
Ajabu The Sunk Cost Fallacy atakasika.
images-10.jpg
images-11.jpg
 
nyie wahaya achene uvivu, yaani kujenga stendi ya mabasi tuu adi serikali kuu iwajengee??? kuna halamashauri na hata manispaa nnyingi tuu hapa nchini zimejenga stendi kwenye maeneo yao tena za kiwango kabisaa,
Kama zipi
 
Majibu ya Silinde kwa niaba ya wizara ni kwamba wameainisha vipaumbele kwenye ahadi za viongozi na jukumu lao sasa ni kutafuta fedha kuhakikisha ahadi zinatekelezwa.
Maendeleo yanategemea ahadi za Viongozi, kiongozi asipoahidi barabara ya kiwango cha lami, TANROAD hawajisumbui.
 
Back
Top Bottom