So far so good! Nilitaka niwashauri mjaribu kuwasikiliza wale waliowahi kufika hayo maeneo yote mawili ndo mtapata mnachokilenga la sivyo naona wadandiaji ni wengi sana. Utaongeleaje kitu usichokijiua na hata hujawahi kufika?
NB: Hiyo ni Kagera ( Bukoba) katika picha ilivyo leo bado haijajengwa hata barabara, bado usafiri wa meli hakuna, bado stand hakuna. Imagine hivyo vitu vingelikuwepo leo make soon vitakuwepo, nipe tu picha patakuwa pana sura gani. Kuna mambo mengi ya kutizama na kupima ukiachia majanga yote yaliyopita pale bado unaweza ukafeel vipi isingekuwa yalitokea unafikiri leo hii Bukoba ingekuwa inalinganishwa na nini ..labda Tanga/Mbeya.
Na ukiangalia ukuaji wa hii miji miwili kwa miaka kadhaa ijayo unaona miji miwili tofauti lakini moja ikiwa na nafasi ya kukua zaidi kuliko nyingine as upande wa magh. wa Nchi yetu una link inayokua na kuimarika kwa kasi kama rasrimali zitaanza kutumika kwa kuunganisha mipaka ya nchi na mikoa ya ukanda huo. Mnahitaji kuongea kwa kutizama mambo hayo hata kama leo itakuwa ama inalingana ama hailingani kwani kwa kila mkoa kuna vitu fulani muhimu ukilinganisha na pengine na vinaonekana kwa macho. Anza na vyuo, barabara, majengo, huduma, mandhari, ukubwa wa eneo, wingi wa watu, biashara, mvuto wa macho n.k