Hivi unajua nilichoongea wewe?! FYI, kwa Talent Manager/Agency anayejua muziki, kwa mashindano kama hayo anaweza kumchukua mwenye powerful voice, na energy ya kutosha kama alivyosema my girl
Khantwe hapo juu na kumwacha anayeimba vizuri lakini amekosa hivyo vitu!!
Muziki unafundishika, na ndio maana Harmonize ambae aliimba hovyo sana pale BSS, alipooenda WCB na kukaa miaka miwili akipikwa, leo hii anasumbua kwenye game! Nilichosema kuhusu huyo dogo ni powerful voice inayoashiria kuwa na higher vocal range! Unaweza kuimba vizuri lakini ukawa na low or medium vocal range! Mtu mwenye higher vocal range anaweza kuimba wimbo wowote ule kwa sababu ana uwezo wa kupanda na kushuka, lakini mwenye vocal range ya kawaida, anapata shida sana kupanda, na ukimsikiliza utaona tu anavyo-struggle! Ukiwa studio, hakuna tatizo manake hivi sasa digital faking zimejaa studio lakini ukiwa kwenye live ndipo unapokuja kupata shida hapo!