Simulizi - DYLAN

Elton Tonny

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
260
1,871
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

WhatsApp +255 787 604 893

E-mail: eltontonny72@gmail.com

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★


2005

TANZANIA

Tunaona mvulana mdogo akiwa ndani ya chumba chake. Anatazama TV ndogo ukutani inayoonyesha filamu fulani kutoka kwenye deki inayomsisimua sana. Ameketi kitandani huku anaangalia kwa makini matukio ya kwenye filamu hiyo, na tabasamu lake linaonyesha wazi jinsi gani anavyofurahishwa na vitendo vinavyoonyeshwa.

Anashika rimoti ya deki, na kuanza kurudisha nyuma sehemu fulani ya filamu hiyo, kisha anaanza kuiangalia tena. Kila mara sehemu hiyo inapoisha, anairudisha tena na tena kuitazama kwa umakini. Sehemu hii inaonyesha watu wawili wakipigana, na chini yao kuna maji kiasi miguuni yanayotawala chumba walichopo. Pembeni yao kuna moto unaowaka kuwazunguka, nao wanapigana kwa mtindo wa kupeleka miili yao kwa sarakasi zenye ustadi sana.

"Dylan..."

Anasikia sauti hiyo anayoifahamu vizuri sana ikiita jina lake. Anageuka na kutazama upande wa mlangoni, na hapo anapata kumwona mama yake akiwa amesimama, huku anamwangalia kwa mshangao.

"...what are you doing? Kwa nini bado hujajiandaa?" mama yake anamuuliza.

Dylan anageukia TV tena na kuendelea kuangalia. Mama yake anamfata alipo na kumnyang'anya rimoti kisha kuisimamisha filamu hiyo.

"Aah..mama!" Dylan analalamika.

"Kimya. Una matatizo gani? Unajua nimekwambia ndege inaondoka mapema, halafu wewe umekaa kuangalia hiyo midude yako. Hivi kwanza umeipataje hiyo CD wakati nilikuwa nimeificha?" mama yake akamuuliza.

"Aheheheh...achana na mimi wewe!" Dylan akamwambia kiutani.

"Hebu acha sifa. Fanya haraka la sivyo utaona," mama yake akamtishia.

Dylan akaweka uso wa kununa.

"Jaquelin..."

Sauti hiyo ikasikika kutokea mlangoni, na wote wakatazama hapo. Ilikuwa ni baba yake Dylan.

"...simu yako inaita huko chini. Ni Alfred," akasema.

"Sa' siungeniletea?" mama yake Dylan akauliza.

"Aah..nzito bwana," mume wake akajibu.

Jaquelin akazungusha macho yake na kuanza kuelekea mlangoni. Alipomfikia mume wake akampiga kidogo kwa kalio lake kisha kuondoka, naye baba yake Dylan akatabasamu huku akiwa amekunjia mikono yake kifuani. Akamtazama Dylan, ambaye bado alikuwa anajifanya kanuna, kisha akamfata mpaka kitandani alipoketi na kukaa pamoja naye.

"Mama anasumbua eeh?" akamsemesha mwanae.

"Yaani!" Dylan akajibu.

"Ahahahah..unajua hiyo ni kwa kuwa yuko excited kwa sababu..."

"...ninaenda Brazil," Dylan akamalizia.

Baba yake akatabasamu.

"Baba, kwani lazima niende huko? Halafu nimesikia wanavuta mabangi sana kule, nikirudi mvuta bangi shauri yenu," Dylan akasema.

Baba yake akacheka na kuzungushia mkono wake begani kwa mwanae.

"Unataka kuwa mvuta bangi?" baba yake akamuuliza.

"Siyo mimi..ila inaonekana ndo' nyie mnachokitaka," Dylan akasema huku bado kanuna.

"Hapana Dylan. Tunafanya hivi ili uweze kuwa na maisha bora baadae. Na usiamini ulichosikia, kwa sababu wavuta bangi wako kila sehemu, lakini unanionaje mimi, navuta bangi?" baba yake akamuuliza.

Dylan akamgeukia, kisha akamnusa kwenye shati lake kidogo eti ili kuhakikisha.

"Siwezi kujua..huu utawala wa Kikwete labda kuna bangi zinanukia siku hizi!" Dylan akatania.

Wote wakacheka kwa pamoja na kuanza kusukumana kiutani, kisha Dylan akawa ameacha kununa sasa.

"Kuna nafasi nzuri hata zaidi ya wewe kupata mafanikio ukisomea kule. Fikiria, utajua lugha nyingine..." baba yake akasema.

"Boring..." Dylan akasema kivivu.

"Utakutana na watu wapya na kuona mambo mengi mazuri..."

"Boring..."

"Vitu vingi vizuri zaidi hata ya vya huku..."

"Boring..."

"Watoto wazuri..." baba yake akamtega.

Dylan akamwangalia usoni kisha akasema, "Cooling..."

"Ahahahah...kichwa chako!"

Wote wakacheka tena. Dylan alikuwa mvulana mwenye akili sana. Alianza kujifunza vitu mapema sana na kuingia shule akiwa na miaka mitatu na nusu tu. Kuanzia masomo ya awali mpaka ya msingi, kwenye masomo yote sikuzote alipata alama za juu, na alipenda michezo mingi na kujishirikisha nayo pia. Kutokana na werevu wake mwingi, baadhi ya walimu wake hata walimwita "Genius."

Wakati huu, alikuwa na safari ya kuelekea nchini Brazil, ambako shangazi yake, yaani dada mdogo wa baba yake aliishi. Alipendezwa sana na Dylan, hivyo akawa amewaambia wazazi wa mvulana huyu aende kusomea kule ambako angepata kujua mambo mengi na kupanua hekima yake hata zaidi kielimu na kitaaluma.

Hii ndiyo ilikuwa asubuhi ambayo Dylan alipaswa kupanda ndege ili aanzishe safari ya kuelekea kule, lakini yeye akawa anaangalia filamu ya The Protector aliyoipenda sana. Baba yake akachukua rimoti na kuiendeleza sehemu ile ambayo shujaa wa filamu alikuwa akipigana na adui yake. Dylan akaanza kuitazama tena kwa upendezi mwingi.

"Unampenda Tony Jaa?" baba yake akamuuliza.

"Ndiyo," akajibu.

"Mhm..naonaga unapenda sana kuiangalia hii sehemu. Unapenda anavyopigana hapo eeh?"

"Actually...naipenda hii sehemu kwa sababu ya adui yake, siyo yeye."

"Kweli? Kwa nini?"

"Angalia."

Akachukua rimoti na kurudisha tena sehemu hiyo, kisha kuanza kumwonyesha baba yake jinsi adui huyo alivyopigana kwa mtindo wenye ustadi sana.

"I just love it. Anavyofanya, kama anacheza muziki, lakini ni hicho ndiyo kinampoteza na kumchanganya huyu Tony Jaa," Dylan akaeleza.

"Yeah ni nzuri. Unajua hivyo vitu vimetokea wapi?" baba yake akamuuliza.

Dylan akatikisa kichwa kukataa.

"Hizo style zinatokea Brazil. Watu wa kule ndiyo wanaofanya sana mambo hayo na kuyasambaza kwa wengine ili wajifunze," akamtaarifu.

"Kweli?" Dylan akauliza kwa shauku.

"Ndiyo."

Dylan akatazama tena TV kwa kufurahi kujua hilo.

"Dylan, nisikilize. Kule unakoenda najua mazingira yatakuwa tofauti, na mwanzoni unaweza ukahisi labda..uko mpweke. Lakini..."

"Baba usikonde. Me ndiyo Dylan. Hanisumbui mtu kule," akajisifu.

"Ahahahah..safi sana. Ila kuhusu watoto wazuri, nilikuwa natania tu. Usije uka..." baba yake akaishia hivyo huku anamkata jicho.

"Aah..mimi tena? Wala hata usiwaze. Mtoto mzuri kule kwangu atakuwa ni ma'mdogo tu," akasema Dylan.

"That's my boy. Hop top..." baba yake akasema huku ananyanyua kiganja chake, kisha Dylan akakigongesha chake hapo.

"Dylan! hivi bado..."

Sauti ya juu ya mama yake ikasikika kutokea mlangoni akishangaa kuona Dylan hajajiandaa bado. Hapo hapo Dylan akakimbilia bafuni na kujifungia humo, akimwacha baba yake anacheka.

"Beatrice amejifungua!" Jaquelin akamwambia mume wake.

"Wow...kweli? Saa ngapi?"

"Alfred ameniambia usiku wa saa 10. Amejifungua kavulana."

"Ahah...inapendeza sana."

"Inabidi tumwahishe huyu ili tuelekee hospitali kumwona."

"Sawa."

Baada ya Dylan kumaliza kujiandaa na kuvaa vizuri, walimpeleka mpaka uwanja wa ndege na kumsihi awe makini mpaka atakapofika kule. Wakiwa nje ya sehemu ya kuingilia ndani kule, mama yake alirudia mara nyingi maneno yale yale aliyokuwa amekwishamwambia, na Dylan akawa ameshaelewa kuwa mama yake alikuwa na huzuni kiasi kumuacha. Hivyo akamkumbatia na kumkonyeza baba yake aliyekuwa amesimama nyuma ya mama yake, kisha akaanza kuelekea sehemu ya ndani ya uwanja wa ndege. Alikuwa mwenye kujiamini sana Dylan, na wazazi wake walijivunia sana kuwa naye kama mwanao.

Wazazi wake waliendelea kusimama hapo mpaka ndege ilipopanda angani, Dylan akiwa amewaacha kuelekea kwa shangazi yake.......


2021

Tunaingia moja kwa moja mpaka kwenye kampuni moja kubwa sana. Kampuni hii ni ya kisasa, inayohusiana na masuala ya ujenzi na ukandarasi (construction company) wa majengo, miundombinu mbalimbali, na masuala mengi kuhusiana na ukandarasi. Ni kampuni ambayo imekuwepo kwa miaka mingi, na imepatwa na panda shuka nyingi inapokuja kwenye suala la maendeleo.

Kampuni hii ilianzishwa na kuundwa vyema na baba yake Dylan. Ilianza kama duka la vifaa tu vya ujenzi na ukandarasi, na mwishowe ikakua kutokana na watu wengi kuvutiwa na huduma za haraka na zenye kutegemeka kutoka hapo. Wakati huu, kulikuwa kumezuka suala ambalo lilileta utata juu ya uendeshaji wa kampuni hii, kwa kuwa washiriki wakubwa waliowekeza hisa zao nyingi kwenye kampuni walihisi mafanikio yameanza kurudi nyuma.

Akishirikiana na mke wake, baba yake Dylan alijitahidi sana kuongoza kwa njia ambayo ingewahakikishia washiriki hao kuwa kampuni haingeporomoka, ijapokuwa mambo mengi yalionekana kwenda mrama.

"...ahadi nyingi unazotoa zinafanya matumaini yao yanyanyuke. Unafikiri itakuwaje wakipata kujua pesa zao hazifanyi kazi kama matarajio yao yalivyo, na zinaishia kupotea tu wakati hatupati faida kubwa?" akawa anafoka mwanaume mtu mzima ofisini kwa baba yake Dylan.

"Baba! Tafadhali...ninajua ninachofanya. Naomba uache niongoze kampuni kwa njia nayojua kuwa bora," baba yake Dylan akasema.

"Bora? Its more than obvious kwamba productivity levels within the company zinafeli!" akamfokea.

"NAJUA!!!" baba yake Dylan akafoka pia akiwa amenyanyuka kutoka kwenye kiti chake.

Wote wakawa wanatazamana kwa hasira sana ofisini hapo. Mzee wake baba Dylan alijua sana pia masuala mengi kuhusiana na kampuni hii, naye alikuwa mmojawapo wa wawekezaji wakubwa hapo. Alikuwa mwenye hasira kumwelekea baba Dylan na kila wakati angetafuta sababu za kumfanya ajihisi hawezi kushughulikia mambo kikamili.

"Basi jamani..mpaka mgombane?" akasema mama Dylan (Jaquelin), ambaye pia alikuwa hapo ofisini.

"Hauna adabu wewe. Unafikiri tu kwa sababu wewe ndiyo raisi wa kampuni basi haupaswi kuambiwa unapoboronga?" mzee akamwambia baba Dylan.

"Ninajua kinachoendelea. Ninaijua kampuni yangu vizuri, sihitaji uniambie vitu hivi. Kama hauwezi kunisaidia kutafuta suluhisho na kukaa tu unalalamika, ni bora uondoke!" baba Dylan akamwambia kwa ukali.

"Gilbert, hebu acha basi!" Jaquelin akamwambia baba Dylan.

Mzee wake akamsonta Gilbert na kidole huku amemkazia macho, kisha akaondoka ofisini humo kwa hasira. Gilbert akajishika kiunoni, na kuanza kuzunguka huku na huku akihisi ghadhabu kubwa pia. Kisha akachukua vitabu kutoka kwenye maktaba ndogo humo na kuvitupa chini kwa nguvu; akiitoa hasira yake namna hiyo. Jaquelin alikuwa anamwangalia tu kwa uso wa kutojali, kisha akazungusha macho yake kwa kejeli na kupigia mtu fulani simu. Akamwita aje ofisini hapo, kisha akakata simu.

"You and your dad acting like ten year olds (wewe na baba yako mlivyo kama watoto wa miaka kumi)," Jaquelin akamwambia Gilbert.

Gilbert akawa tu anaangalia nje ya kioo kipana cha jengo hilo huku amekunja sura yake kwa kuudhika.

"Mkutano unaofuata ni lini?" akamuuliza.

Gilbert akaendelea tu kukaa kimya.

"Si nakuuliza swali?" Jaquelin akasema kwa ukali.

"Kesho," Gilbert akajibu kibaridi tu.

"Ahah...umeshaandaa cha kuwaambia hao makolo au ndo' utakaa kuwatupia vitabu na wenyewe?"

"Jaquelin please...naomba uniache. Siko kwenye mood."

Ni hapa ndipo aliingia mwanaume fulani kijana ofisini humo baada ya kupiga hodi na kukaribishwa.

"Madam, nimefika..." akasema.

"Robert, chukua hayo mafaili uyasambaze kwa department zote ghorofa ya tatu, umeelewa?" Jaquelin akamwambia.

"Ndiyo madam. Zinahusiana na nini?" akamuuliza.

Jaquelin akamwangalia kwa ukali mpaka jamaa akajing'ata.

"S..sorry. Ngoja niwahishe," akasema huku anayachukua mafaili hayo, na kisha kuondoka.

"Pesa za kampuni unazotumia kuwahonga wanawake ndiyo zinaleta haya matatizo," Jaquelin akasema.

"Una uhakika gani ninahonga mwanamke pesa, Jaquelin?" Gilbert akauliza huku anamtazama.

"Ahahahah...just kidding. Najua hauna hayo masuala ya mahawala," Jaquelin akasema.

Ijapokuwa alionyesha kwa mume wake kwamba alitania tu, moyoni mwake alijihakikishia kwamba alichomwambia kilikuwa kweli. Kwa muda mrefu sasa, ndoa yao ilikuwa ikisumbuliwa na visa vya kutoaminiana kutokana na kila mmoja wao kudai mwenzake anatoka kimapenzi na mtu mwingine, lakini walijitahidi kuendelea kuisongesha kwa ajili ya kampuni na sifa yao ya hadharani (reputation).

"Kwa hiyo utafanyaje?" Jaquelin akamuuliza.

"Just give me until tommorow, I'll think of something (niache tu mpaka kufikia kesho, nitafikiria cha kufannya)," Gilbert akajibu.

"Wazo langu ulilitilia maanani, au ukali-bullshit tu?"

"Nini? Wazo...kuhusu..."

"Ndiyo."

"Jaquelin, sidhani kama itakuwa busara kwa sababu yeye hataki kujihusisha na haya masuala. Na mimi sitaki kulazimisha."

"Yaani unavyosema hivyo utafikiri hata umeongea naye."

"Ndiyo amerudi juzi tu. Hana mambo mengi anayoyajua kuhusu hapa. Sitaki kumbebesha mizigo ambayo hataki kubeba."

"Hataki? Unajuaje hilo? Imani yako yote uliyokuwa nayo kwake imeenda wapi? Gilbert, Dylan ndiyo anayeweza kuwa suluhisho letu. Usikae kusingizia kwamba hataki wakati unaogopa tu kwa sababu ya hisia zako za hatia..."

"Jaquelin..."

"...haihusu, Gilbert. Dylan ana uwezo wote wa kuhandle suala hili na kulitatua. Acha kuigiza kama haujui hilo. Ongea naye, na mimi nitaongea naye. Usipofanya hivyo kwa sababu ya kiburi chako, you'll get to see your own downfall..I promise you," Jaquelin akasema kwa mkazo.

Gilbert akawa kimya tu akitafakari maneno ya mke wake.

Jaquelin akamwacha ofisini humo na kuelekea kwenye ya kwake. Alipofika na kuketi kwenye kiti chake, akatoa simu na kumpigia Dylan, lakini hakumpata. Akajaribu mara nyingi sana bila mafanikio, kisha akaiweka simu mezani kwa hasira huku amekunja sura yake kwa kukosa subira.

"Ameenda wapi huyu?" akajiuliza.


★★★


Tunakuja moja kwa moja mpaka sehemu fulani ambayo iko mbali kwenye msitu mkubwa. Imejificha mno kutokana na watu walio huko kutotaka ijulikane kwa watu wasioruhusiwa kuingia. Kuna watu kadhaa ambao huwa wana kawaida ya kwenda hapo kwa ajili ya kujitumbuiza; kwa njia fulani ambayo siyo ya kawaida kama vitumbuizo vingine vinavyokuwa.

Ni sehemu maalumu kwa ajili ya mapigano ya mieleka ambayo hayatambuliki kisheria na ni haramu (illegal). Watu hutoa pesa za bahati nasibu (bet) kupitia mtandao fulani ambao umefichwa kisiri na wataalamu wa programu hiyo inayofanywa kwa ajili ya kuingiza pesa. Hii inamaanisha kwamba, mtu anaweza ku-bet kwa mpiganaji mmoja, na ikiwa atashinda, basi anapata kiasi fulani cha pesa kwa makubaliano aliyoweka.

Kunakuwa na wapiganaji ambao wanadhaminiwa na mtu fulani mwenye pesa, hivyo wao wanapigana mechi ambazo zinaonwa kuwa kubwa sana, na atakaeshinda anapata pesa nyingi sana ambazo zinaenda kwa anayemdhamini; yeye akilipwa kiasi alichoahidiwa. Wanaojua kuhusu jambo hili ni wale wenye mtandao huu, na wanapolipa wanaweza kuangalia mapambano haya hewani (online). Kwa kuwa hakuna ujuzi wa ni wapi yanapofanyikia, haiwi rahisi kwa vyombo vya usalama kutambua walipo ili wachukuliwe hatua.

Kila mpiganaji anakuwa anavaa kiziba uso (mask) ili kuficha utambulisho wao. Wanapewa majina ya sifa kuweza kuwatambulisha kwa mashabiki wao na wanaowadhamini. Kufikia wakati huu, mapambano haya yana wapiganaji 20 ambao wanafahamika kwa majina yao ya sifa, bila watu kujua kihalisi wao ni nani.

Mpiganaji anayependwa zaidi na watu, anajiita "Killmonger," jina linalofanana na mhusika fulani wa filamu ya kimarekani inayoitwa Black Panther. Anapendwa sana kutokana na mtindo wake wa kupigana ambao uko tofauti na mitindo mingine wapiganaji wanayotumia. Na kinachoongeza upendo wa mashabiki kumwelekea ni kwamba tokea alipojiingiza kwenye mashindano haya wiki tatu tu zilizopita, amepigana mara 9 na wapiganaji tofauti, na mechi hizo zote alishinda.

Wakati huu sasa ilikuwa siku ya pambano kama kawaida. Ikafika usiku wa saa 4, nayo ikawa ni zamu ya mpiganaji mmoja aliyejiita "Kishoka," pamoja na Killmonger. Wahuni walimwaga pesa kwenye mtandao huo ili kupata burudani maana Kishoka na Killmonger wote walikuwa hatari sana. Wadhamini wa Kishoka waliweka bet kubwa kwa Killmonger kushindwa, lakini kwa upande wa Killmonger, ilikuwa ni mashabiki tu; yeye hakuwa na wadhamini.

Wote wakaingia kwenye kiwanja cha vumbi kilichokuwa kimezungukwa na camera kadhaa juu na pembeni yao, zilizofuata nyendo zao ili kuwaonyeshea mashabiki waliotazama mtandaoni. Kuuzungukia uwanja huu, waliketi watu muhimu hapo waliouendesha mchezo huu na wale waliodhamini wapiganaji; watu wenye pesa.

Killmonger alikuwa mwenye kujiachia sana. 'Mask' aliyovaa ilimziba usoni kufikia puani, hivyo mdomo wake ulikuwa wazi. Alipendelea kutabasamu na kuchukulia kila kitu kimasihara sana. Alikuwa mrefu kiasi, mwenye mwili uliojengeka vizuri, na alipendelea kuvaa suruali ndefu na pana ya kimichezo kila alipopigana na kuacha kifua chake kikiwa wazi. Alikuwa na nywele ndefu zilizotengenezwa kwa mtindo wa rasi kichwani, naye alizibana kwa nyuma.

Hii ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Kishoka na Killmonger kupambana, hivyo watu walikuwa na hamu kuona ni nani angeibuka mshindi kati yao. Kabla pambano halijaanza, kulikuwa na mwanamke fulani mzungu aliyevalia nguo nyeusi yenye kumbana vyema, na viatu virefu chini, aliyeketi upande wa juu wa watu waliodhamini wapiganaji. Alikuwa akimtazama kwa makini Killmonger; jinsi ambavyo alionyesha uchangamfu kuelekea pigano hilo.

Kengele ilipogongwa, Kishoka alikunja ngumi na kusimama kwa pozi la utayari wa pambano. Yeye alivaa 'mask' iliyofunika kichwa chake chote na kuacha macho wazi, kama jasusi. Alikuwa na mwili mkubwa pia, na alipenda kuvaa T-shirt nyeusi iliyombana pamoja na suruali nyeusi pia. Mabuti yake yalimfanya aonekane kama jasusi kweli.

Lakini Killmonger hakuwa ametulia. Alicheza-cheza sana; akipeleka kichwa na mgongo wake huku na huku, akizungusha-zungusha miguu yake na kuwa kama anacheza muziki wa dansi kwa mtindo huo. Ilikuwa ndiyo njia yake ya kupigana iliyofanya watu wampende sana, maana sikuzote hakutabirika kuhusu chochote ambacho angefanya (mtindo huu wa kupigana huitwa Capoeira).

Kishoka akamfata kwa kasi na kurusha ngumi nzito ili impige, lakini Killmonger akafanya kama anataka kuruka sarakasi ya nyuma ila akazungusha miguu yake juu na kuukunja mmoja uliokipiga kisogo cha Kishoka na kumfanya akaribie kuangukia mbele. Killmonger alijirusha-rusha sana kwa sarakasi, mara huku, mara kule, mpaka Kishoka akawa anashindwa amfate vipi. Lakini mara tu alipoona amepata nafasi, akamrukia tena, lakini Killmonger tayari alikuwa ameshaona angekuja vipi, hivyo akamkwepa kwa sarakasi nyingine yenye utundu.

Alikuwa akiruka sarakasi nyingi na kurusha mateke yaliyompata Kishoka sehemu kadhaa. Ilikuwa ni kama Killmonger hakuguswa kabisa na Kishoka, kwa sababu aliendeleza michezo yake huku akimdukunyua hapa na pale jamaa. Baada ya kuanza kuona Kishoka anafanya mambo kwa hasira badala ya akili, Killmonger akajiachia ili jamaa ampige. Huu ndiyo ulikuwa mchezo wake. Alipenda kumfanya mwenzake apate matumaini, ili alegeze kidogo sehemu aliyoona kuwa na udhaifu, kisha autumie kummaliza.

Kishoka akampiga Killmonger tumboni jamaa alipokuwa amesimamisha mwili kichwa chini miguu juu huku ameweka mkono wake mmoja tu chini, naye akaanguka na kulala chini. Kisha, kwa ujanja, Killmonger akawa anajifanya ameumia hivyo ni ngumu kwake kunyanyuka, na hapo Kishoka akaanza kumfata taratibu huku anajisifu. Wadhamini wake walikuwa wanapiga kelele kwake kuwa ammalize Killmonger, huku yule mwanamke akimtazama kwa makini Killmonger pale chini.

Kisha wakati Kishoka aliposogea na kutaka kumkanyaga jamaa chini, Killmonger aliuzungusha mgongo wake kwa ufundi sana hapo chini, huku mikono yake ikimnyanyua juu kadiri alivyoendelea kuzunguka. Hii ilimshtua Kishoka, naye akashindwa kuelewa mwili wa adui yake ulikuwa katika mtindo gani. Hapo Killmonger akawa anazunguka kwa mikono yake kwa kasi sana, kisha akaushusha mguu mmoja akiwa ameunyoosha na kuupiga wa Kishoka kwa nguvu.

Kishoka alidondokea kisogo chake na kukibamiza kwa nguvu sana, huku Killmonger akizungusha mwili wake ukiwa umenyooka kwa kuweka mkono mmoja chini, na kuendelea kufanya hivyo kimasihara. Yule mwanamke akatabasamu baada ya kuona utundu huo mwingi wa jamaa, na sasa Killmonger akatua chini na kusimama kwa miguu huku anatabasamu.

Kishoka akajitahidi kusimama huku anaweweseka, lakini Killmonger akajirusha sarakasi hewani na kumtandika teke la shavu jamaa na kumfanya adondoke chini kama zigo zito. Akaja mwamuzi na kumwangalia Kishoka, kisha akamfata Killmonger na kuunyanyua mkono wake kuonyesha ndiye mshindi. Watu kadhaa waliokuwepo pale walimshangilia na kuanza kuimba, "Killmonger, Killmonger, Killmonger..."

Wadhamini waliopoteza pesa kwa sababu yake walikasirika sana, kwa kuwa kwa mara nyingine tena Killmonger alithibitisha hakuna anayemweza. Baada ya pambano hili, mtandao ulifungwa kwa wakati huo mpaka pambano lingine, hivyo kwa eneo hilo walilokuwepo wapiganaji, watu walianza kuchangamka ili waondoke. Killmonger alikwenda na kunywa maji, kisha akaja mtu fulani ambaye ndiye aliyemsaidia mpaka akaweza kufika kwenye mapambano haya.

"Oya mwanangu, safi sana. Umeua show na leo tena kama kawaida yako. Pesa imeingia bro, kama vipi tukapate bata club au siyo?" akamwambia.

"We nenda tu, Bosco. Me nna mambo mengine," akajibu Killmonger.

"Aaaaa...mbona unazingua kaka? Au unaogopa nitakuvulisha mask ukilewa?"

"Ahahahah..hicho hicho."

Wakaanza kufika baadhi ya watu sehemu hiyo na kumpongeza Killmonger kwa ushindi wake. Kisha akafika mwanamke fulani mwembamba na kumnong'oneza kitu fulani Bosco. Bosco akaweka uso wa kushangaa kiasi, kisha akamvuta Killmonger pembeni.

"Oya..zari baba," akamwambia.

"Tatizo nini B?" Killmonger akauliza.

"Huyo hapo demu, ametumwa na Queen, anasema anakuita," akamtaarifu.

"Ananiita ili iweje?"

"Sijui. Ila nafikiri anataka kuongea nawe kuhusu jambo la muhimu."

"Mwambie kibaraka wake sina huo muda. Nawahi nyumbani, sikuacha hela ya matumizi," Killmonger akatania.

"D...Killmonger...nisikilize. Hapa hauwezi..."

"Bosco, nimekwambia nawahi nyumbani. Kama alikuwa anataka kuongea na mimi si angeniita kabla mchezo haujaanza? Dada, nenda kamwambie nimeshaondoka," Killmonger akasema kwa kujiamini.

Kisha akachukua begi lake na kuliweka mgongoni na kumwambia Bosco anaondoka na angemjulisha wakati ambapo angepatikana tena. Ile anageuka kutaka kuondoka, akakuta wanaume wawili wenye miili mikubwa wakiwa wamesimama mbele yake. Aliwatambua haraka, nao walikuwa ni mabaunsa waliofanyia kazi hapo. Walikuwa kama wanamzibia njia asipite, lakini akapiga hatua kwa ujasiri ili awapite, na wao wakamzibia hata zaidi.

Mmoja akamshika begani ili kumlazimisha aende upande aliotaka yeye, lakini Killmonger akaushika mkono wake na kuubana kwa mtindo uliomuumiza baunsa huyo. Ndipo yule baunsa mwingine akatoa bastola kiunoni na kumnyooshea Killmonger, naye Bosco akaanza kumwomba asimdhuru na kumsihi jamaa aende walipotaka. Akamsihi Killmonger amwachie mkono baunsa yule, naye akauachia.

Yule dada mwembamba akampita Killmonger na kutangulia mbele yake, hivyo jamaa akaanza kumfata akisindikizwa na mabaunsa kwa nyuma. Hakutaka hata kidogo kwenda kwa "Queen" huyo, lakini hali ikamlazimu. Walifika kwenye chumba fulani na kuingia ndani humo. Killmonger akawa anaangalia mazingira ya humo na kuona kwa kiasi fulani yalipendeza; kumfaa mwanamke. Mbele yake alikuwa amesimama mwanamke yule mzungu huku ameshikilia glasi yenye wine mkononi. Akamgeukia Killmonger na kuachia tabasamu hafifu huku akimtazama kwa madaha.

"Unataka nini?" Killmonger akamuuliza.

Mwanamke huyo, Queen, akawafanyia kwa ishara mabaunsa wake kuwa waondoke, nao wakatii na kutoka, wakiwaacha Killmonger na Queen mzungu peke yao.

"Same thing as always (jambo lile lile kama sikuzote)," Queen akasema.

"Not interested (sina haja nalo)," akajibu Killmonger kwa uthabiti.

"Do not be such a sour puss. Unaweza kupata pesa nyingi zaidi. Take my offer," Queen akasisitiza.

"First off, huwa sifanyi hii kitu kwa sababu ya pesa, nimeshakwambia karibia mara 126. Pili, nahitaji kuondoka sasa hivi, kwa hiyo ikiwa ni hayo tu, baadae," Killmonger akasema.

Akageuka na kutaka kuelekea mlangoni, pale alipopigwa na machale ya haraka kuwa kuna hatari nyuma yake. Kutokea upande aliohisi hatari hiyo inatokea, alijipinda kwa kurukia upande mwingine kwa sarakasi na kukwepa kisu kilichomkosa shingo na kupiga mlango kwa nguvu. Alipomwangalia Queen hiyo, alikuwa anatabasamu kwa upendezi mwingi kumwelekea jamaa.

"That's what I like about you. You're so fast (hicho ndiyo nachokipenda kutoka kwako. Una kasi sana)," Queen akamsifia.

Killmonger akajinyanyua huku akiwa ameudhika. Kisha Queen akamfata aliposimama akitembea kwa maringo. Alipomkaribia, akaweka kiganja chake usoni kwa jamaa akitembeza vidole vyake kwenye 'mask' yake, kisha akashika nywele yake moja na kuichezea-chezea kwa vidole.

"Hii ndiyo itakuwa offer yangu ya mwisho. Usikae kupoteza kipaji chako huku chini wakati kuna sehemu za juu zaidi unaweza kukitumia na kufanikiwa zaidi," Queen akamshawishi.

Killmonger akamsogelea usoni zaidi na kunong'oneza, "Sitaki."

Queen alionekana kuudhika sana. Killmonger akageuka kwa mara nyingine ili aondoke, lakini mzungu huyu akataka kumpiga teke mguuni kwa hasira. Killmonger kwa ujuzi wake tayari alijua Queen angekuja vipi bila hata kumwangalia. Akamkepa, na hili likafanya Queen ateleze kidogo kutokana na kiatu chake kirefu, hivyo Killmonger akamwahi kwa ustadi na kukishika kiuno chake ili asidondoke chini. Kisha akamvuta na kuubana mwili wa bibie kwenye wake; nyuso zao zikiwa karibu sana sasa.

"Easy..." Killmonger akasema kumtuliza.

Tokea Killmonger alipojipatia umaarufu kwenye mtandao huo, Queen alikuwa akijaribu sana kumshawishi ajiunge naye, yaani amdhamini ili aweze kumtumia katika mashindano yenye kufanana na hili, nje ya nchi. Alikuwa akimwambia mara kwa mara kwamba angepata pesa nyingi zaidi huko kwa kuwa alikuwa mwenye ufundi sana, lakini sikuzote Killmonger alimwambia hakutaka jambo hilo hata kidogo. Kihalisi, mwanamke huyu alikuwa mwenye uzoefu sana na mambo haya, na hata mchezo huu kuendeshwa kisiri nchini kulichangiwa hasa na yeye; yaani katika waanzilishi, yeye pia alikuwemo. Alijua ikiwa Killmonger angekubaliana na ofa yake angepata faida nyingi, lakini jitihada zote za kumshawishi jamaa ziligonga mwamba kwa kuwa Killmonger hakulegeza msimamo.


Queen akawa anamwangalia sana jamaa mdomoni na machoni alipokuwa ameendelea kumshikilia vile, naye Killmonger akatabasamu kimajivuno kumwelekea. Kisha kwa makusudi, jamaa akalamba shavu la bibie na kumfanya ashtuke, kisha akacheka na kumwachia. Queen alijifuta shavu lake huku anamwangalia Killmonger kwa kutomwelewa, na hapo mwanaume akatoka na kuondoka zake akimwacha Queen anashangaa.


★★★


Ni nyumbani kwa wazazi wake Dylan, na sasa yapata saa 6 na dakika kadhaa usiku. Gilbert ameketi sebuleni pakiwa na giza kiasi, akionekana kuzama kwenye fikra za mambo fulani. Nyumba yake ilikuwa kubwa na pana sana kwenye eneo lililokuwa limejitenga na nyumba zingine. Ilikuwa na ghorofa moja refu na pana kuzunguka umoja wa nyumba yote. Vyumba vyake vilikuwa vingi, na vitu kwenye nyumba hii vilikuwa vya gharama na vya kisasa.

Mlango wa kuingilia ndani hapo unafunguliwa, kisha anapita kijana fulani na kuufunga. Anaanza kuelekea sebuleni lakini upande wa ngazi ili apande kuelekea juu.

"Dylan..." Gilbert anaita kutokea hapo alipo.

Kijana huyu ni Dylan. Naye amekuwa mtu mzima sasa mwenye mwonekano wenye kuvutia wanawake wengi (na hata wanaume mashosti). Anasimama baada ya kuwa amemsikia baba yake anamwita, naye anatazama upande huo alioketi. Baba yake ananyanyuka na kuanza kumfata polepole. Dylan anaangalia pembeni akiwa ameweka uso wenye kuudhika kiasi.

"Ulikuwa wapi?" baba yake akamuuliza.

"Misele," akamjibu kimkato.

Gilbert akasbusha pumzi na kuangalia pembeni.

"Umefikiria kuhusu tulichoongea?" akamuuliza.

"Hapana."

"Dylan...najua mambo mengi kati yetu hayajakaa sawa lakini...tujaribu kuyaweka pembeni yetu kwanza. Wewe ndiyo nguvu yangu Dylan. Ninajua kwa pamoja tunaweza kupata ushindi. Tafadhali..." Gilbert akamwomba kwa sauti ya upole.

Dylan akamwangalia kifupi, kisha akapanda ngazi kuelekea juu kwenye chumba chake. Baada kuufunga mlango, akatikisa kichwa chake akiwa amefumba macho kwa kusikitika, kisha akaingia kwenye bafu la humo na kujimwagia maji. Gilbert alibaki kule chini akiwa na huzuni sana. Uhusiano wake pamoja na mwanae ulikuwa umebadilika mno, na haikuonekana kama mambo yangerekebika hivi karibuni.

Dylan alikuwa amerudi kutokea Brazil miezi michache iliyopita baada ya kumaliza chuo kikuu kule. Alikuwa amesomea masuala ya Civil Engineering na kupata tuzo ya juu ya kuhitimu. Kule, aliishi na shangazi yake yule mdogo kwa miaka mingi, na alizoea maisha ya kule na kupata marafiki wengi. Watu wengi waliofahamu jinsi alivyokuwa na akili nyingi walimshawishi afatilie miradi mikubwa ambayo ingemwingizia pesa nyingi sana, lakini yeye akaamua kurudi nyumbani ambako hakuwa amekanyaga muda mrefu.

Kwa sababu nyingi sana za mambo yaliyoendelea miaka mingi ambayo alikuwa kule, zilifanya uhusiano wake mzuri aliokuwa nao na baba yake ushuke sana kwa kiwango kikubwa. Hawakuongea tena kama zamani, Dylan angefanya mambo yake tu, hata kama angeambiwa hivi na vile na baba yake angepuuzia, yaani kiufupi hawakupatana vizuri tena. Gilbert alijua vizuri kuwa Dylan ana uwezo mkubwa wa kusaidia kampuni yao ipambane na vikwazo vilivyokuwepo na kuvishinda, lakini bado kijana huyu hakutaka kujihusisha na kampuni hii.

Wakati huu alikuwa anajenga mgahawa wa kisasa kwa ajili ya kupata watu ambao angewapatia milo mingi tofauti-tofauti, kwa kuwa alipenda sana masuala ya misosi. Mama yake alikuwa amepinga sana wazo hilo, akisema anapaswa kufanyia kazi kile tu alichosomea, lakini Dylan aliendelea na mpango wake huo ambao kwake aliona ungempa furaha.

Miaka kadhaa aliyokuwa Brazil, alifanya kazi sehemu nyingi za vyakula, hivyo pesa aliyojitunzia ndiyo ambayo alitumia kujenga mgahawa huu mpya. Ijapokuwa angeweza kutumia pesa za familia, hakutaka kufanya hivyo. Alikuwa mtu mwenye kujiamini kama alivyokuwa wakati yuko mdogo, na alionyesha wazi kwamba alitumaini kwa uhakika kuwa wazo lake lingemletea faida kubwa.

Ilipofika asubuhi, kama kawaida wazazi wake walielekea kwenye kampuni yao. Leo ndiyo ilikuwa siku ambayo mkutano na viongozi mbalimbali ungefanywa kuanzia mida ya saa 3 asubuhi. Gilbert alijiandaa vyema ili kuwapa maelezo ya kuwahakikishia alikuwa na suluhisho la tatizo lililoiandama kampuni hii. Mkutano ulianza, naye Gilbert akatoa hotuba yake yenye kuchochea fikra sana. Aliwaonyesha maeneo mbalimbali ambayo wangeweza kufanya maendeleo zaidi ili kuiinua kampuni yao juu zaidi.

Baadhi ya washiriki wengi waliongelea shida zilizokuwa zinaikabili kampuni hii na kuuliza maswali mengi ambayo yalimzidi nguvu Gilbert kwa kadiri fulani. Jaquelin alikuwepo pia, naye alijitahidi kusaidia upande wa Gilbert, ijapokuwa lawama hazikuacha kuongezwa. Hata mmoja wa washiriki hao wa hii kampuni akapendekeza kubadili uongozi wa kampuni hii, kwa kuwa kulikuwa na viongozi hapo waliokuwa na mapato/hisa kubwa zaidi ya kuweza kuchukua madaraka.

Gilbert akaendelea kuongea, "...na ndiyo bila shaka tunaelewa kuwa hali inazidi kuwa tete. Lakini ikiwa wazo langu lingefanyiwa kazi mapema, tusingeface..."

"Haipatani na akili kufikiri kwamba teknolojia inaweza kusaidia masuala ya construction. Sisi tunadili na mambo physically. Hicho unachojaribu kusema hakitafanya kazi kwa upande wetu, kila mtu anajua hilo," mshiriki mmoja aliyeitwa Mr. Bernard akamkatisha.

Wengi wakatikisa kichwa kukubaliana nae. Ilionekana kama Gilbert alikuwa ameanza kupoteza mwelekeo kwao, na ijapokuwa alikuwa raisi wa kampuni, bado nguvu ya viongozi wengi hapo ilikuwa kubwa. Jaquelin akamwangalia kwa wasiwasi baada ya kuona anahangaika kutafuta kitu kingine cha kuweza kuwaambia ili awashawishi.

"Kilichopo hapa, ni kugawanya shares za juu za kampuni ili kuanza kufanya kazi collectively," akasema Mr. Bernard.

"Kwa nini unasisitizia jambo hilo sana Mr. Bernard?" Jaquelin akamuuliza.

"Kwa sababu ndiyo njia pekee iliyopo ya kuweza kuinua tena kampuni hii. Kazi zinazoendeshwa kwa njia mbovu hapa ni kwa sababu tumeshindwa kuchukua hatua za jambo hilo mapema, siyo masuala ya technology," akasema Mr Bernard.

"Hapana. Ni kwa sababu experienced workforce kubwa hapa ni ya watu ambao umri wao umesonga."

Wote waligeukia upande ambao sauti hiyo ilitokea. Jaquelin aliachia tabasamu la furaha, huku Gilbert akibaki kupigwa na butwaa baada ya kumwona Dylan akiwa amesimama mlangoni hapo.


★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★
 

Attachments

  • IMG_20220405_174740_807.JPG
    IMG_20220405_174740_807.JPG
    24.2 KB · Views: 67
Elton Tonny ▶ DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

WhatsApp +255 787 604 893

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA PILI

★★★★★★★★★★★★

Dylan akaanza kutembea kutokea mlangoni pale kama mwanamitindo. Alipendeza sana kwa kuvalia suti nyeusi iliyoubana mwili wake kiasi, ikiwa imefungwa kifungo kimoja tu kwenye koti. Kiatu chake cheusi kiling'aa, na kwa ndani alivalia shati jeusi pia aliloachia vifungo viwili kwa juu. Mkononi alivaa saa nzito ya rangi ya dhahabu iliyokuwa ya gharama, na nywele zake kichwani zilitengenezwa kwa utundu kiasi; pembe za kichwa zilikuwa zimenyolewa na kuacha nywele kidogo, huku kwa juu akiwa na rasi alizobana kwa nyuma na chache zikidondokea mbele ya uso wake pembeni ya jicho. Sikio moja alivaa hereni ndogo iliyolibana vyema, na mdomoni alitafuna jojo. Yaani jamaa alikuwa na kila sifa ya kuitwa bishoo!

Viongozi wengi pale walimshangaa kwa kuwa hawakumjua, naye akatembea kufikia kiti cha mbele cha baba yake na kusimama hapo. Gilbert akasimama na kutazamana naye machoni, naye Dylan akatikisa kichwa mara moja kumwonyesha kuwa walikuwa kitu kimoja sasa. Gilbert akafurahi sana moyoni baada ya kutambua mwanae aliyatilia maanani maneno yake.

"Wewe ni nani?" Mr. Bernard akamuuliza.

"Board members, I would like to introduce to you this very important person in the room, and my only son, Dylan Gilbert," Jaquelin akamtambulisha mwanae kwa kujivunia.

Wengi walionekana kushangaa kwa kuwa hawakutegemea angekuja hapo. Wengi wao walifahamu kuwa Gilbert na Jaquelin walikuwa na mwana, lakini hawakuwahi kumwona kabla; zaidi walisikia tu habari zake zamani za jinsi alivyokuwa mwerevu sana.

"Ana cheo gani hapa?" Mr. Bernard akauliza.

"Kila kitu unachokiona kwenye hii kampuni ni chake," Gilbert akajibu kwa uthabiti.

Dylan akacheka kimasihara kama kawaida yake. Mama yake alimwangalia kwa matumaini mengi sana, akijua bila shaka mwanae angeleta mambo mapya kwenye meza kuu.

"Kwa hiyo kijana wako ndiye atakaye..toa suluhisho la tatizo hili?" akauliza mshiriki fulani mzee kiasi.

"Ikiwa tu mtanisikiliza kwa makini," Dylan akasema.

Wote wakaweka utulivu kusikiliza alichotaka kuwapa kijana wa Gilbert. Gilbert mwenyewe akaketi kwenye kiti na kumwangalia mwanae kwa makini; akimruhusu aendelee kutoa mawazo yake.

"Kama ilivyo kawaida, matatizo yakianza kwenye kampuni, wengi hukimbilia lawama na kuanza kuingiza siasa," Dylan akasema.

"Siyo lawama kijana. Tunatafuta sul..."

"Naitwa Dylan. Usirudie tena kuniita kijana," akamkatisha mzee huyo kwa uthabiti sana.

Wote wakashangaa. Jaquelin akatabasamu kikejeli akiangalia chini.

"Tatizo siyo suluhisho tu. Ni kile ambacho nyie MMEKAZIA fikra. Mnaangalia zaidi tatizo badala ya njia za kulitatua," akasema Dylan.

"Unazungumzia tatizo gani Dylan?" akauliza Gilbert.

"Mawili. Kwanza, generation ya wafanyakazi wenye ustadi zaidi inazidi kukua kiumri. Mkiangalia, karibia wote walio na experience nyingi kwenye masuala haya ni wakubwa sana kiumri..soon wata-retire. Hiyo inamaanisha ni muhimu kutafuta mapema vijana wenye uzoefu wa kazi kwa kuwa project nyingi za masuala ya construction zinazidi kuwa ngumu...na demand ni kubwa," akaeleza.

"Kwa hiyo point yako inaelekea wapi Mr. Dylan?" akauliza Mr. Bernard.

"Wazo la president kuhusiana na ku-implement teknolojia kubwa hapa, ni sahihi kabisa," akajibu Dylan.

Wengi wakaanza kuangaliana kwa mashaka. Hata Jaquelin alishangaa kiasi kwamba Dylan aliunga mkono jambo hilo. Gilbert akaendelea kumkazia fikra mwanae.

"Now, now...najua wengi mnaona kwamba sekta ya ujenzi haihitaji teknolojia kwa sababu kazi zinafanywa in physical environments, lakini kuingiza technology kuna faida nyingi za pembeni kwenye sekta hii. Faida hizo ni kama..kufanya kazi kwenye mazingira salama zaidi, more efficient use of materials, improved health and safety, na recruitment process zenye ubora zaidi," Dylan akaeleza.

"Shida nyingine ni nini?" akauliza yule mzee.

"Mnahitaji kuacha ubaguzi. Mfanye kuajiri wanawake pia kwenye sekta hii, msijidanganye kwamba inawahusu 'macho-men' peke yao," Dylan akasema.

"Asa' wanawake watafanya nini? Sanasana labda kujiremba wakati wa kazi," akasema Mr. Bernard kwa dharau.

"Kumbuka kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji, Mr. Bernard," akasema Dylan kikejeli.

Gilbert, Jaquelin, pamoja na wengine baadhi wakacheka kidogo.

"Maoni ya namna hiyo yamepitwa na wakati. Kuna opportunity nyingi sana kwenye viwanda vya ujenzi mbali na kubeba matofali na zege tu, kuanzia kwenye mambo ya construction software mpaka design; na hata architecture. Siyo lazima walioajiriwa kufanya kazi wafanye kwenye maeneo ya ujenzi tu ili kuhusika. Hivi mnafikiri wenzetu kule wanazifanya vipi nchi zao mpaka zinakua kimaendeleo namna ile?"

Wote wakabaki kimya.

"Hii kama kampuni yenye usawa, inahitaji kuondoa wazo la kwamba 'ujenzi na ukandarasi ni kwa ajili ya wanaume tu.' Tafuta sehemu zote, utakuta wengi waliosomea masuala haya ni wanawake, na wana ujuzi mwingi sana kuweza kusaidia kuleta maendeleo. Lakini wanapuuzwa na kuishia kufanya kazi ndogo ndogo kujikimu kimaisha wakati wangekuwa sehemu kama hii. Msilazimishe watu wale wale tu, mtasababisha kampuni iwe ya ubabaishaji," akaeleza.

"Ndiyo. Ni kweli kabisa," Gilbert akapigia mstari.

"Yeah. Technology has opened a new world of possibilities for everyone. But HOW we unleash this potential is what will set us apart and help us deliver what's required in order to get what we expect to gain. Trust me, implementation hii ikifanywa haraka, ndani ya wiki tatu tu mtaona matokeo mazuri," akamalizia Dylan.

Wengi wakaonyesha kuafikiana na mawazo yake. Hivi ni vitu ambavyo kama wangeanza kufanya zamani, basi wangekuwa hawakabiliani na matatizo wanayopitia sasa. Lakini kwa sababu ya ubinafsi wa watu kadhaa, mambo sikuzote huwa yanaanguka vibaya, na Dylan alilijua hilo. Kwa hiyo akawa ameamua kuwasaidia waache ushamba na kuwekeza kwenye teknolojia kuweza kuokoa mipango ya kampuni.

Baada ya mkutano huo kuisha, wengi walizungumza na Dylan wakitaka kujua mawazo yake. Ijapokuwa wengi walivutiwa na werevu wake, baadhi walikasirishwa naye kwa kuwa aliongea vitu vya kweli. Mwishowe, Dylan akaongozwa na mama yake mpaka kwenye ofisi ambayo yeye angetumia hapo kwenye kampuni, ambayo alikuwa amemtunzia kwa muda mrefu sana.

Jaquelin alimpongeza sana kwa alichokifanya, na akasema alifurahishwa hata zaidi na jinsi alivyowapausha wenye viherehere mule ndani. Alipomuuliza jana alikwenda wapi, Dylan akasema tu alikuwa na mizunguko yake, kisingizio ambacho kilikuwa cha kawaida sana kwake kutumia. Akamwambia mama yake angependa kuifanyia ofisi yake marekebisho ya vitu kadhaa, naye akamruhusu.

Gilbert alifika pia na kumpongeza mwanae kwa msaada wake. Ijapokuwa alikuwa na ofisi hapa kwenye kampuni sasa, Dylan aliweka wazi kuwa wasitarajie atakuwa mtu wa kukaa tu ofisini akifanya makazi mengi kuanzia asubuhi mpaka jioni, maana alikuwa na mambo yake mengine. Gilbert hakuwa na neno kwa kuwa sasa alijua Dylan yuko pamoja naye, lakini Jaquelin akawa anamsisitizia kuwa ni lazima awe anakaa ofisini ili kushughulikia mambo hapo; kitu ambacho kwa Dylan hakikuwa serious sana.

Wazazi wake wakatoka na kumwacha akiwa mwenyewe ofisini anapitia mambo kadha wa kadha.

★★★

Ilipita wiki moja baada ya matukio hayo kwenye kampuni ya Gilbert. Mambo sasa yalikuwa yameanza kwenda vizuri zaidi kwa kuwa walifuata ushauri wa Dylan, na ni wiki moja tu tayari matokeo yakaanza kujionyesha kuwa mazuri.

Ilikuwa ni Jumamosi jioni ya saa 11 sasa. Gilbert, Jaquelin, pamoja na Dylan wote walikuwa nyumbani. Siku hii, kulikuwa na rafiki yake Jaquelin ambaye aliahidi kuwatembelea. Hawakuonana kwa kitambo kirefu sasa, kwa kuwa rafiki huyo alikuwa akiishi sehemu nyingine ya mbali kwenye jiji hilo.

Gilbert alikuwa sebuleni akipitia masuala fulani ya kazi kwenye iPad, huku Jaquelin akisaidiana na wasaidizi wa kazi kutengeneza chakula kitamu kwa ajili ya wageni. Dylan alikuwa upande wa nyuma wa nyumba ambao ulikuwa mpana sana na uliojengewa vitu vingi kwa ajili ya kuupendezesha. Alikuwa akifanya mazoezi ya mwili, akichanganya mikao tofauti na mitindo ya mazoezi hayo. Alipenda sana kufanya hivi nyakati za jioni, na ilimburudisha na kumfanya ahisi uchangamfu pia.

Baada ya dakika kadhaa, sauti ya 'horn' ya gari ilisikika kutoka nje ya geti la uzio kubwa la nyumba, naye mlinzi wa pale akafungua geti kuruhusu gari ipite ndani. Tayari Jaquelin alikuwa amesimama katikati hapo huku anatabasamu kwa furaha sana. Gari lilipoegeshwa, wakashuka wanawake wawili, kisha aliyekuwa akiendesha akamkimbilia Jaquelin kwa furaha na kukumbatiana naye.

"Wow jamani! Heh...shoga! Za siku?" akauliza rafiki yake.

"Nzuri jamani mpenzi. Nimeku-miss sana Beatrice," akasema Jaquelin.

"Heh...jamani yaani unazidi kupendeza tu. Gilbert kweli anakutunza. Sijui ulimpiga limbwata gani vile!"

"Hahaaa...hapa ndo' Kigoma mwisho wa reli, habanduki," akasema Jaquelin huku anapiga kalio lake, na wote wakacheka.

"Shikamoo aunt Jacky?" akasema mwanamke yule mwingine nyuma yao.

"Marahaba. Em' ngoja kwanza...huyu ni..." Jaquelin akauliza, naye Beatrice akatikisa kichwa kukubali.

"Haa! Jamani...Harleen umekua!" akasema Jaquelin huku anapanua mikono yake.

Mwanadada huyu, Harleen, akamfata akiwa anatabasamu na kumkumbatia. Alikuwa ni mtoto wa kwanza wa Beatrice. Mara ya mwisho Jaquelin amemwona alikuwa na miaka 14 tu, na sasa akawa anashangaa jinsi alivyobadilika na kuwa mdada mkubwa mwenye kuvutia sana.

Harleen alivalia gauni ndefu ya njano kufikia miguuni, iliyoubana mwili wake vyema na kufanya hips zake nene kiasi pembeni na kalio lake litokeze vizuri kwa nyuma. Kichwani, alitengeneza nywele zake kwa kuzisuka kwa rasta ndefu juu ya kichwa, pembe za kichwa chake zilikuwa na nywele fupi na laini, hivyo ilionekana ni kama kiduku fulani hivi. Alikuwa mrembo pia, mwenye mashavu makubwa kidogo na macho mazuri sana.

Beatrice alikuwa amesuka nywele laini za kulala na alivalia kigauni kifupi kufikia magotini; alipenda sana kujiachia kwa kuwa wote walipenda maisha ya kizungu kutokana na kuwa na pesa nyingi.

Jaquelin akawakaribisha wote ndani na kuingia nao mpaka sebuleni. Baada ya Gilbert kuwaona, akatabasamu na kufunga iPad yake, kisha akawafata waliposimama. Akatazamana na Beatrice kwa sekunde kadhaa, kisha wakakumbatiana kwa kuwa ilikuwa ni miaka kadhaa imepita bila kuonana na rafiki yao huyo. Akatambulishwa kwa Harleen, ambaye pia alimshangaa kwa jinsi alivyokua mkubwa. Wakaketi pamoja kwenye masofa ya kisasa hapo ndani na kuanza kuongea.

"...hahahah...yaani ulivyokunyugwa hiyo siku sitasahau!" Beatrice akawa anakumbushia maisha ya shule, akiwa anamwambia Gilbert.

"Aah...kitambo sana. Enzi hizo tulikuwa tunavaa maboksi nyuma ya kaptura mwalimu akianza kutembeza mboko zitupunguzie maumivu," akasema Gilbert, na wote wakacheka.

"Siku hizi wanafunzi wanaweka nini?" akauliza Jaquelin.

"Bado wanatumia maboksi, ila walimu ni wajanja sana. Wakiona nyuma panadunda wanahamishia kwenye supu," akasema Beatrice.

"Kwa shule ambazo fimbo haziruhusiwi ndiyo unakuta mwanafunzi akileta fujo, mwalimu hana jinsi ila kubaki anang'ata kucha tu," akasema Gilbert kiutani.

"Hahahah...kwa hiyo madam principal hauachani na chuo?" Jaquelin akamuuliza Beatrice.

"Hapana, bado sana. Napenda kufundisha. Ndiyo maisha yangu yaani," akajibu.

"Toka ulivyowekwa kuwa principal naona ni ming'aro tu," Jaquelin akasema kiutani.

"Ahahaaa...ming'aro mbona tokea kitambo? Tena kwa kuwa me ndiyo mkuu, ni kunyoosha miguu tu," akasema Beatrice.

"Wacha we!" akasema Jaquelin, na wote wakacheka.

"Umemaliza kusoma?" Gilbert akamuuliza Harleen.

"Ndiyo. Ninafanya kazi sasa," akajibu.

"Wapi?" akauliza Jaquelin.

"Hospitali kuu. Yeye ni daktari sasa hivi," akajibu Beatrice.

"Wewe! Acha basi!" Jaquelin akashangaa.

Harleen akatabasamu kwa furaha.

"Hongera sana. Umesheheni kwenye mambo yapi?" akauliza Gilbert.

"Mambo mengi. Nafanya upasuaji, ninadili na watu wenye matatizo mbalimbali yanayohusiana na organ muhimu mwilini; hata moyo pia," akaeleza.

"Haaa...Beatrice umekuza," Jaquelin akasifu.

"Ndiyo maana yake," akajibu Beatrice kwa kujivuna.

"Hongera sana. Wakati uko mdogo nakumbuka ulikuwa unalia-lia kweli," Gilbert akakumbusha.

Wote wakacheka.

"Lakini umekua binti mkubwa na mzuri sana. Me nikafikiria labda unafanya modelling," Gilbert akamwambia.

"Yaani kama angeenda huko, hakuna mtu angemfikia," Beatrice akamsifu binti yake.

Harleen akacheka kidogo, kisha akamwambia Gilbert, "Asante."

Jaquelin, alimwangalia sana Gilbert kwa jinsi alivyomtazama Harleen kwa upendezi. Kichwani kwake akawa anafikiri mume wake tayari amevutiwa na dada huyo mrembo sana na mwenye umbo lenye kuvutia, hivyo akaanza kuingiwa na hisi za wivu kumwelekea Harleen bila sababu yoyote.

"Nani yule?" akauliza Beatrice.

Alikuwa amemwona Dylan kupitia mlango wa kioo mbele zaidi ya sehemu waliyoketi, akiwa anakimbia-kimbia na hivyo kuvuta uangalifu wake.

"Ni Dylan," akajibu Jaquelin huku anatabasamu.

"Ni Dylan?! Wewee...amerudi lini?" akauliza Beatrice.

"Ana muda sasa. Kwani sikukwambia?" Jaquelin akauliza.

"Hamna hukuniambia."

"Mmmm...nilikwambia bwana."

"Hujaniambia nawe. Nisingeshangaa kama ningekuwa najua."

"Mh...basi... Amerudi. Ana..kama miezi minne mitano hivi."

"Hee! Twende tukamuone, sijui atatukumbuka?" akasema Beatrice, akimwambia Harleen hivyo.

Wanawake wote watatu wakanyanyuka na kuelekea kwenye mlango wa kioo ambao ulikuwa njia ya kupita kufikia uwanja ule mpana nyuma ya nyumba. Wakafika na kusimama nje hapo, wakimtazama Dylan ambaye alikuwa bize akifanya zoezi fulani wakati huu. Wote walipendezwa sana na jinsi alivyoonyesha wepesi katika kile alichokifanya.

Wakati huu, alikuwa ameweka mikono chini, kisha ananyanyua miguu yake juu taratibu, akijibeba namna hiyo mpaka inaponyooka kuelekea juu hewani, kisha anaisambaza hewani hapo akisimama kwa mikono. Alifanya hivyo kwa utulivu mkubwa sana na kuendelea kukaa namna hiyo hiyo kwa dakika kadhaa.

"Ndo' anafanya nini?" akauliza Beatrice.

"Mwenzangu hata najua! Mhm..toka aliporudi ana hiyo kawaida ya kufanya mazoezi...mengine ambayo hata sijawahi kuona," akajibu Jaquelin.

"Amekuwa mkubwa jamani!" akasema Beatrice.

Ni hapa ndipo Dylan aliirudisha miguu yake chini na kusimama wima.

"Dylan.." Jaquelin akamwita.

Jamaa akageuka nyuma na kupata kuwaona wanawake hao wamesimama pale wakimwangalia. Akaonyesha uso wenye udadisi na kuanza kuwaelekea pale waliposimama; huku akiwa kifua wazi na chini akivaa suruali na viatu vya mazoezi.

"Cheki kifua hicho Harleen!" Beatrice akamtania binti yake.

"Ahahahah...yaani wewe!" Jaquelin akasema.

Harleen akatabasamu na kukaa kimya tu, akimtazama jamaa alivyoendelea kuwakaribia huku anadunda.

"Unasema me nimekuza, ila nawe umekuza kwa kweli. Hadi natamani kuwa mdogo tena. Nisingemwacha mwanao salama," Beatrice akasema kiutani.

"Kwenda huko! Dylan wangu katulia, hapaparikagi na hivyo vitu," akajivuna Jaquelin.

Dylan akawa amewafikia akiwa anatabasamu.

"Aunty Beatrice!" akasema kwa shauku.

"Jamani...Dylan wangu mie!" akasema Beatrice kwa furaha.

"Dah! Ningekukumbatia sema nanuka mijasho!" akasema Dylan.

Wote wakacheka.

"Yaani unazidi kupendeza tu!" Dylan akamsifia Beatrice.

"Ndiyo kawaida yangu hiyo mwanangu. Na wewe umekuwa mbaba sasa. Eeeh..naona una rasi kichwani kama mbrazili kweli," Beatrice akamsifia pia.

Dylan akajipiga-piga kidevu chake kwa kiganja kuonyesha anajivuna, na wote wakacheka.

Harleen alikuwa anamtazama Dylan kwa uvutio mwingi sana. Alipendezwa na uso wake mzuri ambao kwa asilimia kubwa ulichangiwa na uzuri wa mama yake, Jaquelin. Alimtazama kifuani na kuona jinsi kilivyojikata vizuri na kutunisha matiti yake kiume zaidi, moja la upande wa kushoto likiwa na tattoo ya kichwa cha simba anayeunguruma, huku tumboni pakikazika haswa na kuonyesha 'six pack' zake vizuri. Mikono ya Dylan ilikuwa imejaa vizuri kuonyesha alikuwa mtu wa mazoezi sana.

Ni wakati huu ndipo Dylan akawa amemwangalia Harleen baada ya kumwona akiwa amesimama pembeni hapo. Akaanza kumfata huku amenyanyua kidole chake akimsonta, na usoni akionyesha kudadisi Harleen alikuwa nani. Harleen akawa anatabasamu tu.

"Wewe...binti-mashavu mashavu! Ni wewe kweli?" akasema Dylan kwa kushangaa.

Wanawake wote wakacheka.

"Haujasahau kumtania hivyo?" Jaquelin akamuuliza.

"Nisahau vipi? Huyu ni binti-mashavu kweli?" akauliza tena Dylan.

"Ahahahah... ndiyo ni mimi, bichwa wewe!" Harleen akatania pia.

"Ahahahah...eeh! Haki ya Mungu! Umekua..ume...umenona!" Dylan akamsifia.

"Heee! Wewe! Usianze mambo yako!" Beatrice akasema kiutani.

"Ahahahah...lazima mtoto asifiwe bwana. Utam-lock mpaka lini?" Dylan akamwambia Beatrice.

"Hakuna. Yaani badala unisifie mimi..."

"Hahaaa...hauna lolote. Kama kikongwe kikongwe tu," Jaquelin akamtania Beatrice.

"Ahahahah...za huko lakini kijana wangu?" Beatrice akamuuliza Dylan.

"Ah...nzuri tu. Mama, mbona hukuniambia kama ni aunty Beatrice na binti-mashavu ndiyo wanakuja?"

"Iih jamani, yaani hukumwambia?" Beatrice akamuuliza Jaquelin.

"Lakini Dylan..." Jaquelin akasema.

"Hakuniambia, aunty. Ningekuwa najua msingenikuta hivi. Yaani mama hujafanya fresh kabisa," Dylan akasema akijifanya kuudhika.

"Lione kwanza! Em' toka hapa nenda kaoge," Jaquelin akasema.

Dylan akawa anacheka kimasihara, nao wote wakatambua alikuwa anatania tu. Kisha akawaacha ili aende kujisafisha haraka na kurudi waweze kutumia muda pamoja kwa urafiki.

Wakati wakiwa wadogo, Dylan na Harleen walicheza pamoja, walisoma shule moja, na kuwa pamoja pindi nyingi ambazo wazazi wao walitembeleana. Jaquelin, Gilbert na Beatrice walikuwa marafiki kabla hata watoto hawajazaliwa, na walisaidiana kwa mambo mengi mno katika safari ya maisha yao. Ilikuwa ni kama Jaquelin na Beatrice ni dada wa damu maana walijuana vizuri na kusaidiana sana kwa mambo mengi kihisia. Baba yake Harleen alikufa wakati binti huyo alipokuwa na miaka 19, kwa kupigwa risasi vibaya na mtu fulani ambaye utambulisho wake haukujulikana mpaka leo. Hiyo ikamwacha Beatrice akiwa mjane mwenye watoto wawili; Harleen na mdogo wake wa kiume aliyeitwa David.

Kufikia wakati ambao Dylan alikuwa amemaliza kuoga na kuvaa, huko chini wadada wa kazi na Jaquelin walikuwa wanaandaa meza ya chakula huku Beatrice na Harleen wakiwa wameketi na Gilbert wakipata maongezi. Walikuwa sanasana wanaongelea kuhusu ujio wa Dylan kwenye kampuni ya Gilbert, nao walipendezwa kutambua kwamba kijana huyu alikuwa na werevu ule ule aliokuwa nao tokea udogoni.

Jaquelin akawaita na kuwaambia wakanawe kwenye sinki safi ili waende mezani kwa ajili ya kupata msosi. Kwa kuwa Beatrice alizoeana nao sana, ilikuwa rahisi kwake kujiachia mno hapo, lakini Harleen alikuwa mwenye utulivu sana. Hakuwa na papara sana kama mama yake ambaye alipenda kufanya mambo kwa uzungu mwingi wa uswahilini.

Baada ya wote kuwa wameketi, Jaquelin akawaambia wajisikie huru kuchukua chakula chochote hapo kwa upendo wao, hakukuwa na masuala ya kupakuliana. Meza hii ilikuwa ya duara yenye kioo kizito, ambayo ilikuwa pana yenye kuzungukwa na viti vitano vikubwa vyenye kwisheni (cushion) nene za manyoya kwa ajili ya kutuliza mwili. Katikati ya meza, kulikuwa na kioo cha duara kwa juu kilichotoshea kuwekea vyakula vingi, nacho kilizunguka ili mlaji aweze kuchukua chakula alichohitaji kwa wakati wake.

Wakati wanajiandaa kuanza kuzungusha kuchagua chakula, Dylan akasikika akishuka kutoka ngazini na wote wakatazama upande wake. Akafikia meza na kuketi kwenye kiti kilichokuwa wazi, kisha akachukua paja la kuku katikati pale na mboga za majani na kuweka kwenye sahani; kwa haraka sana. Wote wakawa wanamwangalia kwa jinsi alivyoonyesha utundu mwingi.

"Chicken looks great mom! (kuku inaonekana kuwa nzuri sana mama)" akasifia nyama ya kuku kwa mama yake.

"Dylan...manners (adabu)," Jaquelin akamwambia kwa sauti ya chini yenye mkazo.

Alikuwa amekaribia kuanza kula nyama yake, pale alipowatazama wote na kukuta wanamwangalia. Alipotazama sahani zao, akagundua hakuna hata mmoja wao aliyekuwa ameweka chakula.

"Ooh...sorry," akasema kiajabu-ajabu.

"D una miaka mingapi sa'hivi?" Beatrice akamuuliza.

"27," Dylan akajibu.

"Oooh kweli...Harleen anakuacha mwaka mmoja," akasema Beatrice.

"Eee...si kabibi kizee haka!" Dylan akamtania Harleen.

"Mhm...bado hajauacha utoto tu!" akasema Harleen, akimaanishia Dylan kufika na kuvamia nyama.

"Yaani!" Jaquelin akasema.

"Nyama ndio go yangu ya kwanza. Acha kujishaua binti-mashavu...kamata msosi hapo," akasema Dylan huku anachukua chakula kingine.

Wote wakaanza kuweka vyakula kwenye sahani zao taratibu, kisha wakaanza kula pamoja. Story walizopiga hasa zilihusiana na mambo ya zamani na maisha ya sasa. Pia walizungumzia kuhusu mdogo wake Harleen, yaani David, na Beatrice akawajulisha kwamba mwanae huyo alikuwa shule ya sekondari boarding; wakati huu akiwa kidato cha pili. Dylan alikuwa mwepesi sana wa kuongea, hivyo alifanya mazungumzo yawe yenye kuchangamsha sana kila wakati ambao angeongea.

"Mmmm...kweli?" akauliza Dylan.

"Ndiyo," akajibu Harleen.

"Mh? Hapana," Dylan akakataa.

"Ish...kwa hiyo hautaki au?" Beatrice akauliza.

"Siyo sitaki, ila bado siamini-amini. Huyu binti-mashavu alikuwaga anataka sana kuwa Wema Sepetu, sasa nashangaa sa'hivi mnaniambia ni daktari. Mwangalie tu kwanza alivyo, udaktari wapi na wapi!" Dylan akasema kichokozi.

"Bichwa lako!" Harleen akamwambia, na wote wakacheka.

"Ni daktari ndiyo. Tena daktari mzuri sana," Gilbert akasema, na Jaquelin akamtazama kwa umakini.

"Okay..kwa hiyo unatibu nini? Au ndiyo wale wale wa vikombe vya Loliondo?" Dylan akamtania Harleen.

"Naweza kuuchana-chana mwili wako wote na kuurudishia jinsi ulivyokuwa," akasema Harleen.

"Mmm..labda mwili wa maboksi," akasema Dylan.

Wazazi wao wote walifurahishwa sana na jinsi watoto wao walivyoonyesha ukaribu, ijapokuwa bado Jaquelin alimwona Harleen kwa njia tofauti sana.

"Umeshafanya upasuaji mara nyingi eti?" Jaquelin akamuuliza binti.

"Ndiyo. Kila mara napofanya upasuaji lazima tutoke washindi," akajisifu ili kumkera Dylan.

"Huwa unajisumbua tu wewe. Mnakaa huko mnapasua mende, akifa mnasema mmeshinda kwa kuwa haijawa-cost kununua dawa ya kupulizia," akasema Dylan na kufanya wote wacheke sana, hasa Beatrice.

"Hmm...hiyo kazi ngumu aisee. Unahifaji kuwa katili sana," akasema Gilbert.

"Ahahah...siyo sana. Na..nina muda sijafanya upasuaji, nilitaka kupumzika kwanza," akasema Harleen.

"Umeshapasua mende wengi eeh?" Dylan akamuuliza kichokozi.

"Siyo mende Dylan, ni watu," akasema Gilbert.

"Najua. Namtania tu," akasema Dylan kwa uthabiti kiasi.

"Kwa hiyo haujawahi kufeli upasuaji hata mara moja?" Jaquelin akamuuliza.

"Hapana. Unajua...hata wakati wewe ulipohitaji liver transplant, mimi ndiye niliyekufanyia upasuaji..pamoja na wengine," Harleen akamwambia Jaquelin.

Uso wa Jaquelin ukabadilika na kuwa serious. Gilbert, Beatrice na Dylan, wote walionekana kutotarajia jambo ambalo Harleen alisema.

Walikuwa wanajua kwamba Jaquelin alifanyiwa upasuaji wa ini miaka mitatu iliyopita, kwa hiyo haikuwa kile Harleen alichosema kilichowafanya waishiwe pozi, bali ni SABABU ya kile alichosema Harleen. Wanne hao walijua vizuri sababu iliyofanya Jaquelin ahitaji kubadilishiwa ini, lakini Harleen hakujua. Yeye alijua sababu ya kidaktari ilikuwa ni kwamba Jaquelin alipatwa na kansa ya ini, lakini siyo kilichopelekea mpaka akaipata.

Harleen akaendelea kula, bila kujua kwamba alikuwa amewarudishia kumbukumbu mbalimbali wanne hao. Alipomtazama Dylan, jamaa akavunja uso wenye kughafilika na kutoa tabasamu bandia.

"Kumbe?" akauliza ili kufanya Harleen ahisi mambo yako sawa.

Harleen akatikisa kichwa kukubali.

Gilbert pamoja na Beatrice wakazisawazisha sura zao pia na kuendelea kula. Ni Jaquelin pekee ndiye aliyeendelea kumtazama Harleen sana, mpaka dada wa watu akaanza kujishtukia.

"Aunt Jacky...uko sawa?" Harleen akamuuliza.

"Aa...yeah..am fine. Sikujua kwamba..wewe pia uli....asante,"Jaquelin akasema bila raha.

"Hey Dylan, chuo ulichosomea kiliitwaje? Beatrice akauliza ili kubadili mada kijanja.

"Aam...USP. University of Saõ Paulo," akajibu.

"Aa-aaah...iseme kibrazili bwana," akasema Beatrice.

"Universidade de Saõ Paulo," akajibu.

"Wacha! Ahahaaa...umekuwa mtaalamu wa lugha yao. Hata Harleen anaweza Spanish pia," akasema Beatrice.

"Kweli?" akauliza Gilbert.

"Yeah," akajibu Harleen.

"Ahahah...naona nyie lenu moja. Yaani aunty hata kama utasema binti-mashavu anajua kuendesha ndege, tayari atajua," Dylan akatania.

"Hivi we vipi? Kwa hiyo unafikiri tu ni wewe ndiyo unaweza Spanish?" akauliza Harleen.

"Sijasema hivyo. Lakini wewe..aagh..huwezi," Dylan akamkejeli.

"Culo!" Harleen akamwambia Dylan, akimaanisha 'tako!'

Dylan akatoa macho, kisha akaanza kucheka.

"Vipi? Amekwambiaje?" akauliza Beatrice.

Harleen akamwangalia Dylan kiukali, kama kumwambia 'ole wako useme!'

"Ahahah...ameniambia eti me boya," jamaa akapindisha maana.

Gilbert alijua Spanish kiasi, hivyo alikuwa ameelewa kihalisi Harleen alichosema. Akatabasamu tu na kuendelea kula.

"Unajua Spanish kweli?" akauliza Dylan.

"Ndiyo," akajibu Harleen.

"Con fluidez? (vizuri kabisa?)"

"Kabisa."

"Huna lolote wewe. Hapo najua umeotea tu," Dylan akamwambia Harleen.

"Hebu msemeshe uone," akasema Beatrice.

"Cúal es tu nombre? (unaitwa nani?)" Dylan akamuuliza binti.

"Me llamo Harleen (naitwa Harleen)," akajibu.

"Ahahahah...umeotea," Dylan akakejeli tena.

"Ah-aah we endelea kumsemesha," Beatrice akasisitiza.

"De donde eres? (unatokea wapi?)" akauliza Dylan.

"Tanzania," akajibu Harleen.

"Vosotros de donde sois? (unatokea wapi?)" akauliza tena Dylan.

"Tanzania," akajibu Harleen.

Hii ikamfanya Dylan atabasamu.

"Ahahah...eti anajaribu kunichanganya kwa kuniuliza swali lile lile kwa njia tofauti," Harleen akamwambia mama yake.

"Hahaa... umemuweza," akasema Beatrice.

Muda wote walioendelea kula na kupiga story baada ya hapo, Jaquelin pamoja na Gilbert hawakuchangia sana maongezi. Ilikuwa ni kama walipatwa na jambo fulani baya sana kwenye akili zao, hasa Jaquelin, ambaye alionekana kukosa uchangamfu kabisa.

HAPA KUNA SIRI KUBWA IMEJIFICHA. JE, NI SIRI GANI HIYO?

★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

Ni matumaini yangu kwamba mmeenjoy sehemu ya pili ya hadithi ya DYLAN.

Waweza ipata yote WhatsApp. Njoo tubonge ili kunipa mimi mwandishi wenu support pia. Asante 😉

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

WhatsApp +255 787 604 893

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★


Walipomaliza kula, waliketi kwenye masofa tena na kuendeleza maongezi yenye kufurahisha. Angalau muda huu Jaquelin alijitahidi kuonyesha kachangamka. Beatrice alipendekeza kwamba Dylan awe anatoka kufanya mazoezi na Harleen, na kwa kuwa Dylan alisema asubuhi huwa ana kawaida ya kwenda kukimbia (jogging), basi Beatrice akasema ikibidi waanze kesho. Harleen yeye aliishi kwenye chumba cha hoteli kubwa ya kisasa (apartment) katikati ya jiji, kwa dhumuni la kuwa karibu na hospitali kwa kuwa nyumbani kwao palikuwa mbali. Kila mmoja wao alikuwa ameshaelewa kwamba Beatrice alitaka sana kuwafanya Harleen na Dylan watengeneze uhusiano wa karibu zaidi. Wazo hilo lilikuwa zuri kwa vijana, hivyo wakakubaliana kukutana kesho asubuhi na mapema maeneo fulani ili waanze zoezi.

Ilipofika saa 5 usiku, wageni hao wapendwa wakaagana na rafiki zao ili waelekee hotelini kupumzika.

Hakukuwa na jambo lolote lililowaunganisha wanafamilia hao watatu pindi wageni walipoondoka. Jaquelin alienda zake chumbani, Dylan pia, na Gilbert akabaki mwenyewe sebuleni akisoma vitu mitandaoni. Ilikuwa imebadilika kuwa familia yenye nafasi kubwa zilizoachwa wazi ilipokuja kwenye suala la mahusiano ya karibu baina yao, na kulikuwa na sababu iliyofanya hali iwe hivyo. Harleen aliposema kuhusu upasuaji wa Jaquelin, alikuwa amewakumbusha sababu hiyo. Hivyo kila mmoja wao akawa amejitenga tena kama ilivyokuwa kawaida yao.

Asubuhi ikafika. Dylan aliwahi sana kuondoka nyumbani, kukiwa bado na giza-giza la alfajiri na baridi kiasi. Alivalia nguo za mazoezi, kisha akabeba maji, taulo, na kuchukua gari lake kuelekea kule alikoahidiana na Harleen kukutana. Alipofika, akatoka ndani ya gari na kuelekea sehemu iliyokuwa na uwanja mpana uliofyekwa nyasi vizuri. Akaanza kupasha mwili wake kwa mazoezi rahisi mpaka pale Harleen alipofika.

Alikuwa amevalia nguo za mazoezi zilizoubana mwili wake vyema na kuchora umbo lake vizuri. Ijapokuwa alikuwa na mwili ulionawiri, hakuwa na manyama makubwa au likitambi. Nguo yake ya mazoezi ilikuwa ya aina hiyo hiyo na rangi ya kijivu, juu yenye mikono mirefu, na suruali yenye kubana iliyovutika na kufanya kalio lake lijikate vizuri kwa nyuma kwenye mstari wa katikati. Alivaa na raba nyeupe za mazoezi, huku nywele zake zilizosukwa akiwa amezibana kichwani kwa juu.

Walipoanza mazoezi ya kadiri, Dylan angemtazama mwilini mara kwa mara, akiangalia jinsi mikunjo iliyonona ya mwili wa binti ilivyokuwa yenye kutia hamasa kwa mwanaume yeyote yule kumtazama sana. Nyakati ambazo angemwelekeza jinsi ya kuweka mikono, miguu, mgongo, angehitaji kumshika kwa nyuma, na hilo lilifanya jamaa aweze kumwangalia kwa upendezi hata zaidi kutokana na ukaribu huo. Angetabasamu au kuchekea pembeni kila mara wazo la kiutundu lilipoingia kwenye akili yake kumwelekea daktari huyu, lakini baadae angepotezea tu.

Walipomaliza ya kujinyoosha, wakaanza ya kukimbia, nao walitumia takribani dakika 40. Kwa Dylan, zilikuwa ndogo sana. Lakini aliona zimempasha binti vyema, hivyo akaona waache ili wapumzike kidogo. Harleen alikuwa anapumua kwa kasi kiasi, akijaribu kurudisha mfumo mzuri wa upumuaji. Dylan akamwongoza warudi kwenye uwanja ule na kuketi sehemu waliyokuwa wameweka vitu vyao vichache. Harleen akanywa maji kiasi na kuketi chini. Dylan akaketi karibu yake pia.

"That was...heatful!" akasema Harleen kwa shauku.

"Ahahah..hauna kawaida ya mazoezi eti?" Dylan akamuuliza.

"Oh huwa ninafanya mazoezi. Sema, sijakimbia kama wiki sasa. Na wewe yako ni magumu mno," akasema kiutani.

"Ahahah...you big baby," Dylan akatania.

"Ndiyo hivyo."

"Okay I guess...kila kitu unaweza. Kunipasua unaweza, mazoezi unaweza, lugha unaweza, wewe..ni mweza," akasema Dylan.

"Ahahahah..acha mambo yako bwana. Kila mtu ana vipawa fulani. Unapoamua tu kuvi...extend..unaweza," akasema Harleen.

"Yeah ni kweli. Kwa nini ulijifunza Spanish? Ni wivu tu kwamba nilienda Brazil au?" akauliza Dylan kiutani.

"Ahahahah..mwone kwanza, eti wivu!"

Dylan akatabasamu.

"Me gusta español mucho (napenda Spanish sana)," akasema Harleen kwa ufasaha sana.

"Wow!" Dylan akapendezwa na hilo.

"Nilitaka sana kujua lugha hiyo kwa kuwa nilianza kuiona kama kiswahili vile. Na pia niliwaza..huyu bichwa akirudi atakuwa ameshasahau kiswahili..kwa hiyo nikajiweka tayari," akaeleza binti.

"Kumbe? Inafurahisha sana kujua ulijifunza kwa ajili yangu," Dylan akasema kichokozi.

"Ahahah...kwa sehemu tu..wewe siyo sababu yote," akasema Harleen, na wote wakacheka.

"Ustedes como aprendieron? (ulijifunza vipi?)" Dylan akamuuliza.

"En linea (online/mtandaoni)," akajibu.

"Oooh.."

"Yeah. Las personas en este...grupo han ayudado me mucho (ndiyo. kuna watu kwenye...grupu fulani mtandaoni ambao wamenisaidia sana)," akasema Harleen.

"Ahahah... Napenda unavyokiongea. Kama mzawa wa kule kabisa," Dylan akasema.

"Muchas gracias (asante sana)," akajibu Harleen.

"Aunty umemwacha anakoroma?"

"Ahahahah... hakoromagi bana."

"Wee! Nakumbuka vizuri wakati tunaishi kwenye ile nyumba bado. Alikuwaga akija kwa mama kufanya sleepover anakoroma huyo! Nilikuwa naweka mito kwenye masikio ili nilale kwa amani," Dylan akatania.

"Ahahahah ameacha siku hizi. Halafu..hiyo nyumba yenu ya kule iliuzwa au?" Harleen akauliza.

"Hapana. Kuna kipindi mama alitaka waiuze lakini baba akakataa. Alisema anaitunza kwa ajili yangu."

"Wow! Ni nyumba kubwa nakumbuka. Walipojenga hii nyingine ndiyo wakaiacha tu eeh?"

"Yes. Huwa naenda pale mara kwa mara kui-check, nafikiria kuja kuipiga remake ya ukweli halafu nikakae kwenye mansion langu hilo."

"Ahahah... itapendeza. Unajua imekuwa kitambo sana. Natamani kupaona tena kule," akasema Harleen.

"Ukipenda twaweza kwenda..upaone. Kama utakuwa na nafasi lakini," Dylan akapendekeza.

"Ndiyo. Nina nafasi zaidi leo. Vipi tukienda mida ya saa 10? Au una mazoezi muda huo?" akasema Harleen

"Hapana. Mazoezi hayafati ratiba hususa. Nitakupitia basi," akasema Dylan.

"Sawa."

Baada ya kuwa wamepata maongezi hayo, wote waliachana muda mfupi baadae na kuelekea makwao. Kwa kuwa Dylan hakwenda kazini wala Harleen kwenda hospitali, ilikuwa ni siku huru kwao kutembelea mazingira yale ambayo kwa kipindi fulani waliyaishi pamoja wakiwa wadogo.

Harleen alijihisi uchangamfu wa hali ya juu sana; fikra ya kuwa na rafiki yake wa kitambo sehemu waliyokua na kucheza pamoja ilimsisimua sana. Kuna mambo mengi kuhusu Dylan ambayo yalimfanya ajihisi huru sana nyakati zote ambazo aliwahi kuwa pamoja naye, na sasa hisia hizo zilikuwa zimeamka tena.

Ilipofika saa tisa na nusu, Dylan alitoka kwao na kuelekea hotelini kwa Harleen kumpitia. Alikuwa amewahi ili waweze kuondoka mapema kwa sababu mwendo wa gari kufika kule kwenye nyumba ya Dylan ilikuwa saa zima. Baada ya kufika na kumtaarifu kuwa amefika, Dylan alikaa ndani ya gari lake akisubiri binti amalize kujiandaa ili waianze safari.

Zikapita kama dakika 10 hivi, na mtoto mzuri akaonekana akilifata gari la jamaa taratibu. Dylan aliweza kumwona kwa mbele, naye alipendezwa na mwonekano wa rafiki yake huyo daktari. Alikuwa amevaa kigauni chepesi chekundu kilichoishia kwenye magoti yake. Mkononi alishika mkoba mwekundu, na miguuni alivaa viatu virefu vyekundu. Nywele zake aliziachia kwa nyuma na mdomoni alipaka 'lipstick' nyekundu iliyoupendezesha mwonekano wake mzuri sana.

Akiwa anakaribia kulifikia gari lilipoegeshwa, Dylan akamwashia taa za mbele mara mbili, kama kumkonyeza, naye Harleen akaonekana akitabasamu. Kisha akaingia siti ya mbele baada ya kufika na kuketi.

"Umependeza!" Dylan akamsifia.

"Asante."

"Road trip?"

"Twen'zetu," akasema Harleen.

Kisha safari ikaanza. Walipiga story za hapa na pale, huku Dylan akimsimulia jinsi mambo mengi ya huko kwenye nyumba ile yalivyobadilika. Baada ya nusu saa hivi, wakawa wamefika upande huo wa jiji na kuelekea kwenye nyumba hiyo. Ilikuwa na uzio wa ukuta mrefu kuizunguka, na geti jeusi lenye mwonekano mkuukuu. Dylan akashuka na kwenda kulifungua, kisha akarudi ndani ya gari na kuliingiza mpaka ndani. Akashuka na kurudi tena getini kupafunga, akimwacha Harleen ameshuka pia akiangalia-angalia eneo hilo.

Nje hapo palikuwa tu kama jinsi binti alivyopakumbuka. Akaiangalia nyumba ile, ambayo ilikuwa na ghorofa moja pana, naye akatabasamu baada ya kukumbuka michezo mingi waliyofanya pamoja na Dylan kwenye nyumba hii. Upepo ulikuwa unapuliza kwa nguvu wakati huu, hivyo kulikuwa na baridi kwa kadiri fulani.

"Mashavu, twende ndani. Tutaganda hapa," sauti ya Dylan ikasikika nyuma yake.

Wakauelekea mlango wa kuingilia ndani ya nyumba, kisha Dylan akaufungua na kisha kuufunga baada ya wote kupita ndani. Macho ya Harleen yalizungukia nyumba hii, akitambua kuna vitu kadhaa vilikuwa vimebadilika sana.

"Pamebadilika eti?" Dylan akamuuliza.

Harleen akatikisa kichwa kukubali.

"Yeah, uko sahihi. Wazazi wetu walipenda sana jinsi mpangilio wa hapa ulivyokuwa. Vitu vingi vimeondolewa," akasema Harleen.

"Yeah ni kweli. Ila muda siyo mrefu ninataka kuja kupajaza hapa," Dylan akamwambia.

"Nyumba nzuri sana. Kwenye masuala ya ujenzi kweli uncle Gilbert yuko vizuri," Harleen akaisifia.

"Speaking of which, njoo huku uone. There's something you might be interested in seeing," Dylan akasema.

"Wapi?" akauliza Harleen.

"Sigueme (nifuate)," Dylan akamwambia kwa ki-spanish.

Harleen akamfuata jamaa mpaka usawa wa dirisha kubwa upande mwingine wa nyumba. Sehemu hiyo ya nje ilipendeza sana kutokea hapo waliposimama. Walitazama uwanja huo uliokuwa na swimming pool, miti kadhaa na sanamu ndogo ya simba iliyokuwa imejengwa chini kama pambo.

"Wow! Hiyo sanamu bado ipo!" Harleen akasema kwa shauku.

"Ahahah...yeah."

"Nakumbuka tulikuwaga tunaisemesha na kuigiza hapo kwamba simba anatung'ata..." akasema Harleen huku akicheka.

"Eee ndiyo. Ile michezo ilifurahisha sana," akasema Dylan.

"Sana. Nakumbuka karibia kila jambo tulilofanya hapa."

"Mimi pia."

"Hivi unaweza kuamini muda umepita haraka sana namna hii? Tulikuwa tukikaa muda mwingi mno kwenye hiyo pool pamoja. Yaani ni kama vile sa'hivi tuko kwenye maisha mengine," akasema Harleen kwa hisia.

"Yeah ni kweli. Los momentos... (nyakati hizo)," akasema Dylan.

"La alegria (zile shangwe)," akasema Harleen.

"La risas (vicheko)," akasema Dylan.

Harleen akatulia kidogo kisha akasema, "La espera (kusubiri sana)."

Dylan akamgeukia taratibu na kumtazama. Harleen pia akamwangalia kwa hisia. Maneno hayo ya mwisho ya bibie yalimfanya Dylan atambue kuwa kuna kitu fulani Harleen alitaka kusema, hivyo akampa umakini wake. Harleen akaonyesha wazi kuna jambo alitaka kumwambia jamaa kwa kumgeukia vizuri.

"Nakumbuka ulikuwaga unanichungulia nilipokuwa huko nyuma. Tena sanasana nilipoenda kuogelea. Ningejifanya kama vile sikukuona, ila nilijua ulikuwa unanitazama," akasema Harleen kwa hisia huku anatabasamu.

"Ahahah...asa' ulitegemea nini? Ulikuwa ndiyo msichana mzuri zaidi ya wote mtaani, nami nilikuwa ndo' nimeanza kupata mahisia," Dylan akajitetea.

"Hahah...eti mahisia."

"Ni kweli. Huo ulikuwa muda mrefu sana uliopita. Check sa'hivi tulivyo, yaani inaonekana ni kama jana tu."

"Do you still think about me? (bado huwa unanifikiria?)" Harleen akauliza kwa hisia sana.

"What do you mean? (unamaanisha nini?)" Dylan akauliza.

"Huwa..unanifikiria kama ulivyokuwa unanifikiria kipindi hicho? You know..me..coming out of the pool...wet... (yaani... kama jinsi nilivyokuwa natoka ndani ya pool..nikiwa nimelowana)."

Dylan tayari aliweza kukisia mazungumzo haya yalikuwa yanaelekea wapi, lakini kwa sababu fulani alikuwa hataki yafike huko ijapokuwa kwa jinsi mambo yalivyojitengeneza hapa, ingekuwa ngumu sana kukwepa.

"Kwa nini unauliza?" akamuuliza pia badala ya kutoa jibu.

"Curiosity. Me nikienda kuogelea mara kwa mara huwa nakumbukia hilo," akasema Harleen.

Kwa kuwa sasa Dylan alijihakikishia kwamba mtoto anataka kuingia ndani ya 18, akaona amfungulie milango. Akamsogelea usoni zaidi huku anamtazama kwa macho yenye hisia na utundu mwingi.

"Curiosity killed the cat (udadisi ulimuua paka)," Dylan akatania.

Harleen akacheka kidogo huku akiitazama sana midomo ya jamaa.

"I'll be honest. Nilipenda kukuangalia sana kwa kuwa vinguo vya kuogelea vilifanya sehemu kubwa ya mwili wako ionekane. Sikuwahi kuona msichana akiwa bila nguo, na wewe ulikuwa umekaribia jambo hilo. Uli...ulinisisimua," akasema Dylan kwa sauti yenye hisia, huku anausogelea mdomo wa Harleen kichokozi.

Harleen akabaki kumtazama tu kwa ukaribu huo, kama anasubiri kwa hamu jamaa afanye kitu fulani. Mara Dylan akarudi nyuma na kufanya matarajio ya rafiki yake huyo yakate.

"Anyway, jioni inaingia. Tumalizie tour yetu kwenye nyumba halafu tuondoke. Kuna jambo lingine unataka kuona?" Dylan akabadili mada ghafla.

Harleen akaangalia nje kupitia dirisha, kisha akasema, "Nimeshaona kila kitu nilichohitaji kuona. Imerudisha kumbukumbu nyingi nzuri sana. The best part about all this is that...nimeweza kukuona tena," Harleen akasema kwa hisia.

"Asante," akasema Dylan.

"I want to go swimming (nataka kwenda kuogelea)," akasema Harleen.

"Wewe! Hayo maji ni ya baridi sana," Dylan akamtaarifu.

"Najua. Lakini sitakaa ndani ya maji muda mrefu. Nataka twende wote. Itakuwa fun," akasema kwa shauku.

"Kuna mambo mengine fun zaidi ya kufanya hapa..ila hilo...mh..."

"Hayo mengine hayataburudisha sana kama kuogelea humo. Najua unataka kujaribu pia, wewe si ndiyo Dylan asiyeogopa chochote?"

"Ndiyo mimi. Ila wewe nakuonea huruma, sitaki ushikwe na baridi," Dylan akasema kwa kujali.

"Usiwaze. I want to do something crazy, kama wewe ulivyozoea."

Dylan alimwangalia Harleen na kuona kweli alikuwa na hamu ya kufanya jambo hilo. Kwa muda huu, hakuonekana kama mwanamke mwenye umakini wa kidaktari tena, bali kama yule Harleen aliyemzoea wakati wako wadogo. Hakukuwa na pointi ya kubishana naye tena, hivyo jamaa akalegeza.

"Haya..ngoja nikafate taulo," akasema Dylan.

"Thank you," akasema Harleen kwa furaha.

Upesi Dylan akapanda kuelekea chumbani ili kufata taulo. Akachukua mbili, moja kwa ajili yake na nyingine kwa ajili ya rafiki yake huyo. Jambo hilo walilopanga kufanya halikuwa sehemu ya mambo aliyofikiria yangefanyika hapa, na aliliona kuwa wazo baya kiasi. Lakini kwa kuwa lilingempa furaha mtoto, akaona ni vyema kuacha afanye kile kilichomfurahisha; na yeye ajaribu kufurahi pamoja naye pia.

Akarejea kwa Harleen na kukuta anavua nguo zake. Alisimama na kumtazama kwa makini. Juu alikuwa ameshatoa kigauni chake, hivyo akawa amebaki na sidiria ya kijani iliyong'aa na chupi nyepesi ya aina hiyo hiyo. Ngozi yake nyeupe ilimng'arisha vizuri sana, na umbo lake liliyavutia sana macho ya Dylan.

Wakati huu alikuwa anafungua mikanda midogo ya viatu vyake miguuni, hivyo alikuwa ameinama na kufanya kalio lake libinuke kwa nyuma. Dylan akawaza bila shaka Harleen pia alikuwa mwenye uzungu mwingi maana hakuwa na aibu kuhusu kuvua nguo akiwa na rafiki yake wa kiume peke yao kwenye nyumba moja. Alipomaliza, akasimama na kuzibana nywele zake vizuri kwa nyuma. Dylan akaanza kumwelekea polepole huku anatabasamu. Harleen akamgeukia na kuachia tabasamu huku anamwangalia jamaa kwa hisia.

"Damn," Dylan akamsifia kwa ufupi.

Harleen akacheka kidogo kisha akasema, "Es tu turno (zamu yako)."

Bila kuchelewa, Dylan akavua shati lake mbele ya Harleen na kuliweka pembeni. Kisha akaanza kufungua mkanda wa suruali yake kimadoido ili kucheza na akili ya Harleen, naye binti akatazama pembeni akizungusha macho kiutani. Dylan akacheka, kisha akaishusha suruali yake na kuitoa yote; akiwa amebaki na boxer sasa.

Harleen alitazama kwa matamanio sana mashine ya jamaa. Jinsi ilivyokuwa imejichora juu ya boxer yake ilimsisimua, lakini akajitahidi kukwepesha macho yake ili jamaa asimshtukie. Vitu hivi kwa Dylan pia vilikuwa vya kawaida kwa kuwa kule Brazil watu huishi kwa kujiachia sana. Alikuwa amekwishatembelea sehemu nyingi kama beach, ambazo zilijawa na wanawake wengi waliovalia chupi na sidiria tu, hivyo kumwona mwanamke akiwa namna hii hakukuwa jambo geni. Sema ilipokuja kwa Harleen, ni kwa kuwa hakuwa amemwona kwa muda mrefu sana, na sasa siku ya pili tu tayari rafiki yake huyu akawa ameanzisha michezo yenye kusisimua, hivyo Dylan alipenda sana hali hiyo.

"Okay. Nimemaliza," Dylan akasema.

Harleen akamshika mkono na kuanza kumwongoza kuelekea nje kwenye swimming pool. Dylan alikuwa anachekea kichini-chini jinsi kalio la mtoto lilivyonesa-nesa huku na huku kila alipopiga hatua. Akaanza kumtania kwa kuupigisha ulimi wake ndani ya mdomo kufatisha mwendo wa kalio la Harleen, naye Harleen akacheka kidogo kwa furaha.

Walikubaliana kwamba wakifika usawa wa swimming pool, wangekimbia kwa pamoja na kujirusha ndani ya maji. Baada ya kuhesabu 1, 2, 3, wote wakayakimbilia maji wakiwa wameshikana mikono bado, kisha wakajirusha na kudumbukia ndani kwa nguvu; maji yakiruka juu. Ilionekana kama muda unapita sana walipokuwa ndani ya maji baada ya kujitupia, kisha taratibu miili yao ikaanza kupanda juu tena. Walipofika juu, kila mmoja alikuwa akicheka kutokana na burudisho hilo walilopata pamoja, na kama Dylan alivyokuwa amesema, maji hayo yalikuwa baridi sana.

Hivyo Dylan akamshika Harleen na kuanza kuogelea naye kuelekea kwenye kingo ya swimming pool ili waweze kutoka. Akatoka kwanza, kisha akamvuta mtoto, ambaye alikuwa akitetemeka sana. Dylan akamwongoza kuelekea ndani mpaka sehemu ile waliyoacha taulo. Akaanza kumfuta maji Harleen kwa taulo moja, kisha akachukua nyingine na kumfunika nayo. Ijapokuwa Harleen alitetemeka kutokana na baridi, bado alijitahidi kutabasamu kwa kuwa jambo walilofanya lilimburudisha kwa kiwango kikubwa.

Dylan akamketisha Harleen kwenye sofa moja lililokuwa hapo, kisha yeye akaelekea sehemu ya jikoni kuangalia ikiwa angeweza kupata kiberiti ili atafute kuni na kuwasha moto wa kuipasha miili yao. Alitafuta lakini akakosa, huku naye mwili wake ukihisi baridi pia. Akarejea kwa rafiki yake na kukuta amejifunga taulo moja kuanzia kifuani mpaka ilipoishia mapajani, na alipotazama kwenye kiti cha pembeni akaona sidiria na chupi ya bibie zimewekwa hapo; kama kuanikwa.

Harleen alikuwa ameketi kwenye sofa, huku mdomo wake ukitetemeka kiasi, naye alikuwa anatumia taulo nyingine kujifutia nywele.

"Mashavu..." akamwita.

Binti akamtazama na kuacha kujifuta nywele.

"..samahani...nimekosa kitu cha kukupasha mwili joto...sijui kupasha joto mwili..mwili joto kuupasha..." Dylan akawa anababaika kuongea.

Harleen akatabasamu na kumrushia taulo jamaa, kisha akasema, "Usijali."

Dylan akaanza kujifuta-futa maji mwilini huku anamtazama rafiki yake. Nywele za Dylan zilikuwa zimemwagikia kuzunguka kichwa chote, hivyo akaanza kuzifuta pia kwa fujo. Harleen akawa anamwangalia kwa njia yenye uvutio mwingi sana; kama alikuwa anataka kumwambia vitu vingi ila akawa anashindwa. Dylan alipomaliza kujifuta, akamwambia anakwenda chumbani mara moja. Alikuwa anataka kuitoa boxer yake iliyolowana ili avae taulo kwa chini, kwa kuwa hakukuwa na nguo zingine hapo za ziada tokea walipoiacha nyumba hii.

Baada ya kumaliza kuvua boxer, kuvaa taulo kiunoni, na kurudi, alimkuta Harleen akiwa ameketi vile vile huku ameibana mikono yake kwa viganja ili asitiri baridi aliyohisi. Akaenda usawa wa sehemu aliyovulia nguo zake na kutoa simu kwenye suruali ili atazame muda. Akakuta ni saa 12 jioni na dakika kadhaa tayari.

Dylan alijua wazi kuna njia nyingine ya kumsaidia Harleen ili apate joto kiasi, lakini akawa anahofia labda rafiki yake angechukulia vibaya. Alitaka kupendekeza kwamba, aketi naye karibu, kisha amkumbatie ili miili yao itokeze joto ambalo lingesambaa kadiri ambavyo muda ungekwenda. Lakini kujua kwamba hawakuwa wamevaa nguo zozote isipokuwa taulo tu, kulimtia wasiwasi kiasi. Ila bado Dylan aliona haingefaa kumwangalia tu, kwa hiyo akaona ajaribu kutoa wazo hilo. Akamfata pale alipokuwa na kuweka simu yake pembeni, kisha akamwangalia.

"Aam...Harleen..." akaita.

Harleen akamtazama.

"...nina wazo. Unaonekana kuhisi sana baridi. Vipi tuki..cuddle? Najua inaweza kuwa inappropriate, but...nataka tu kusaidia," akamwambia.

Harleen akatabasamu na kusema, "Haina shida. Let's do it."

Dylan akafarijika na kumfata alipoketi kisha kukaa karibu yake. Akazungushia mikono yake kwenye mwili wa bibie na kuubana vyema kwenye wake ili watengeneze joto. Dylan alihisi jinsi Harleen alivyokuwa wa baridi, hivyo akawa anasugua-sugua ngozi yake pia kwa kiganja ili kuleta joto haraka.

Baada ya dakika chache, Harleen akasema, "Umeniita kwa jina langu... nimependa."

Dylan akatabasamu na kusema, "Ila ujue ni gumu sana kutamka. Napendelea binti-mashavu."

"Ahah... Napenda ukiniita hivyo pia," akasema Harleen.

Zikapita dakika chache tena za ukimya, na sasa Harleen, ambaye alikuwa bado amelalia kifua cha Dylan, akajisawazisha kidogo na kukunja miguu kwa kupiga nne, kitu kilichofanya sehemu kubwa ya paja lake kuelekea kiunoni ionekane. Dylan akawa anayaangalia mapaja ya Harleen jinsi yalivyoonekana kuwa laini na manono, naye akaachia tabasamu lake la kimasihara kama kawaida. Harleen akanyanyua uso kidogo kumtazama machoni jamaa na kukuta analiangalia paja lake.

"Enjoying the view? (unaufurahia huu mwonekano?)" akamuuliza huku akitabasamu kwa mbali.

"Ahahah... Nilikuwa nahakikisha uko sawa. Dakika chache nyuma ulionekana kama unataka kufa," Dylan akamwambia huku anamtazama usoni.

"Ndiyo, nilikuwa nakaribia."

"Yeah, ndiyo ujue sasa jinsi gani wazo lako halikuendana hata kidogo na hali ya hewa."

"Ahahah..sikusema ni wazo zuri. Nilisema tu itaburudisha. Na huwezi sema haijaburudisha."

"Hapo siwezi kubisha."

"Halafu pia umepata kuona sehemu kubwa ya mwili wangu. Si ndiyo ulichopendaga sana kufanya zamani?"

"Kumbe ndiyo lilikuwa lengo lako?"

"Ahahah...hapana. Sikufikiria kufanya hivi mpaka tulipofika hapa. Nilichotaka mwanzoni ilikuwa kupaona hapa, pamoja nawe. Nimepitia mambo fulani magumu huu mwaka mmoja uliopita, so nilihitaji kufanya jambo fulani wild for a change," akasema Harleen kwa hisia.

"Pole dear. Nimejionea pia baadhi ya wanawake ambao huwa wanapitia nyakati ngumu maishani; angalau wewe una pesa, wenyewe hata hawajui watalisha nini watoto wao. Maisha yako tofauti kwa watu mbalimbali, na najua haifai kulinganisha watu kwa kuwahukumu jinsi wanavyoonekana kwa nje tu. Unapopitia wakati mgumu kama hivyo, unapata kujua kuwa kuna wakati utahitaji kuituliza nafsi na kusonga mbele; ndivyo maisha yalivyo. Najua hata wewe mtoto wa Beatrice unaweza, tena sana. Na kitu kizuri hata zaidi ni kwamba unakuwa mrembo mara mia kila unapokuwa happy," Dylan akamwambia kwa hisia pia.

Harleen akanyanyua uso wake na kumwangalia tena jamaa. Alionekana kutaka sana kumwambia jambo zuri kwa kuwa uso wake ulionyesha furaha.

"Asante. Maneno yako mazuri sana," akasema Harleen.

"Siyo kama wewe," Dylan akamwambia kichokozi.

"Unajua ni kwa nini nilikuwa na hamu ya kutaka kuja huku?" Harleen akauliza.

"Ndiyo, niambie."

"Well, mbali na kutaka kuiona tu nyumba hii, ni kwa sababu nilitaka kuwa pamoja nawe sana. Sikuzote tokea tulipokuwa wadogo nilifurahia sana kuwa karibu yako. Na ijapokuwa tumeishi mbali kwa miaka mingi, bado ninaweza kuhisi upendezi wako uliokuwa nao kunielekea upo. Wewe ni mtu mmoja ambaye unapendezwa nami kwa jinsi nilivyo, kwa kuwa wanaume wengi wanachoangalia kwangu ni pesa, na sex," Harleen akafunguka.

Sehemu hii ilijawa na msukumo mkubwa wa kihisia (tension) baada ya Harleen kunena vile. Dylan alikuwa amemwelewa vizuri sana, na asingekaa kuigiza kwamba hakujua kihalisi mtoto alimaanisha nini. Akamwangalia kwa hisia sana, huku wimbi kubwa la hisi za kimahaba kumwelekea Harleen likitembea mwilini mwake kwa kasi mno.

"Yaani Harleen...sijui hata nisemeje," akasema Dylan.

Harleen akajinyanyua taratibu kutoka kifuani kwa Dylan na kumwangalia usoni vizuri zaidi. Dylan aliweza kuona jinsi Harleen alivyoonyesha hamu kubwa ya kimapenzi kumwelekea, hivyo akaifata midomo yake polepole na kuibusu taratibu kwa juu. Midomo yao iligandiana kwa nguvu, kisha wakaifungua na kutoa ndimi zao kwa wakati mmoja na kunyonyana kimahaba sana. Ilikuwa denda laini, ya taratibu, iliyojawa na mahaba ya hali ya juu huku wakiwa wamefumba macho yao kusikiliziana.

Hisia walizojengeana hapa zilikuwa nzuri ajabu, nao wakaendelea kwa dakika chache zaidi.


★★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★

Kumpiga Harleen busu kulichangamsha sana hisia, lakini Dylan alitaka jambo lingine zaidi kwa kuwa akili yake sasa ilizama kwenye fikira za kupata raha zaidi kutoka kwa mwanamke huyu. Akaivunja busu taratibu na kuanza kushusha mdomo wake chini mpaka shingoni kwa Harleen. Harleen akanyanyua kidevu juu ili kumruhusu jamaa aibusu shingo yake vyema. Aliilamba na kuibusu kwa upendo, kisha akashuka mpaka sehemu ya juu ya kifua cha bibie. Wakati akimbusu sehemu hiyo, akatumia mkono wake wa kushoto kuliminya titi la kulia la Harleen, ambalo bado lilikuwa limefichwa na taulo aliyovaa. Harleen akatoa pumzi ya juu juu huku bado akiwa amefumba macho na kung'atang'ata mdomo wake wa chini.

Kisha Dylan akarudi juu na kumbusu kwenye shavu, naye Harleen akafumbua macho na kumtazama kilegevu. Dylan akatabasamu kwa kiburi baada ya kuona amemwamshia mtoto hisia nyingi, hivyo akaanza (........).

(.........).

(.........).

Jua sasa lilikuwa limezama, hivyo ndani hapo palianza kuingiwa na giza taratibu. Dylan akasitisha zoezi la (........), kisha akaivuta simu yake aliyokuwa ameiweka kwenye kiti pembeni na kuwasha tochi yake; naye akaiweka ikiwa imefunikwa ili mwanga umulike juu. Hakutaka kunyanyuka kwenda kuwasha taa kwa kuwa utamu ulikuwa umekolea haswa kufikia hatua hiyo.

Akamwangalia binti na kukuta anamtazama kwa matamanio mno, hivyo akaifata tena midomo yake na kumjaribu kwamba anataka kumbusu. Harleen aliposogeza yake ili aipokee ya jamaa, Dylan akakwepesha na kuirudisha nyuma kimchezo. Harleen akatabasamu kivivu kutokana na kupenda utundu wa Dylan, kisha jamaa akaweka paji lake la uso juu ya paji lake Harleen. (..........).

(..........).

(..........).

(..........).

(..........).

Zilipita zaidi ya dakika 50 hivi Dylan akiwa juu ya Harleen anajilia vyake, na wote wakatua mizigo yao wakihisi uchovu wa kimahaba baada ya kupeana raha hizo ambazo kwa kipindi kirefu sana walitamani kupeana, lakini hali zikawa zinawazuia. Dylan, akiwa na jasho mwilini, akausogelea uso wa Harleen na kumbusu shavuni, naye mtoto akarudisha upendo kwa kumbusu jamaa mdomoni kwa dhati kubwa. Wote walijihisi furaha sana kuwa pamoja namna hii, na walijua bila shaka nafasi zingine zingetokezwa wakati ujao ili kufurahishana namna hii tena.

Baada ya wawili hao kupeana mapenzi hayo motomoto, walinyanyuka baada ya dakika chache na kwenda bafuni kuoga pamoja. Ilikuwa usiku sasa, na Harleen akamwambia Dylan alihitaji kurudi hotelini kupumzika kwa ajili ya kazi kesho. Akawahi kutoka bafuni na kurudi sebuleni, kisha akavaa gauni yake tu kwa kuwa sidiria na chupi yake havikuwa vimekauka. Dylan akatoka bafuni na kuelekea sebuleni pia, akiwa amejifunga taulo tu, na kumkuta Harleen amesimama usawa wa meza ya chakula. Akamfata hapo na kumkumbatia kwa nyuma.

"Si tungekaa tu hapa hapa Harleen?" Dylan akasema huku anaibusu shingo ya bibie.

"Mhmm... unajua tuna kazi kesho...ni muhimu kurudi," akajibu kwa sauti yenye deko.

"Screw the jobs...let's spend more time together (potezea kazi..tutumie muda zaidi tukiwa pamoja)," Dylan akasisitiza.

"We'll get the chance again...don't worry (tutapata tu nafasi tena..usijali)," Harleen akajibu huku amefumba macho akisikilizia busu za Dylan kwenye shingo yake.

"Why not now? (kwa nini siyo sasa hivi?)" Dylan akauliza kwa kubembeleza.

"Yo trabajo demasiadas horas. Deseo que yo tenga mas tiempo (Ninafanya kazi kwa saa nyingi. Natamani ningekuwa nina muda wa kutosha)," akajibu Harleen kwa ki-spanish.

"Ser el propio dueño de tu tiempo Harleen (kuwa mmiliki wa muda wako mwenyewe Harleen)," Dylan akamwambia pia.

Harleen akamgeukia na kumtazama machoni.

"Ningependa sana kufanya hivyo. Lakini...you know wagonjwa wananihitaji siyo? Na mimi napenda sana kuwasaidia," akasema kwa hisia.

Dylan akashusha pumzi na kuketi kwenye kiti karibu na meza hiyo.

"Najua. Una moyo mzuri na...una bidii sana. Nimekuelewa," akamwambia kiupole.

"Usijisikie vibaya lakini Dy..."

"No, no, no. Sijisikii vibaya. Baada ya hiyo mechi kali hivyo nitajihisije vibaya?"

"Ahahah... sawa. Bila shaka unasikia njaa, siyo? Twende ukale kitu fulani," Harleen akashauri.

"Ningependa kukula wewe tena," Dylan akatania.

Harleen akacheka kidogo na kuanza kuzichezea rasi mbili za Dylan. Kwa kuwa Dylan alikuwa ameketi, kifua cha Harleen kilikuwa karibu na uso wake huku anamwangalia binti machoni. Alipoangalia kifua cha Harleen, aliona jinsi matiti yake yalivyoinyanyua gauni yake nyepesi kwa mbele, na hilo likamsisimua. Akatumia vidole viwili kushusha pande za katikati za gauni hilo zilizoyaziba. (.........).

(.........).

(.........).

(.........).

Dylan akamsaidia ashuke kutoka mezani baada ya mechi hiyo kali ya nyongeza, kisha akamsifia jinsi alivyokuwa mtamu sana. Harleen alitamani hata kuendelea zaidi, lakini hakusema kwa sababu alikuwa ameshamwambia Dylan walitakiwa kuondoka, hivyo jamaa akazifata nguo zake na kuanza kuvaa. Mambo yalikuwa yamepamba moto sana kati ya hawa marafiki wawili.

Waliondoka kutoka kwenye nyumba hiyo ikiwa ni kwenye mida ya saa 2 usiku. Dylan alikuwa amemwambia Harleen angempeleka sehemu fulani nzuri ili wapate chakula pamoja, kisha angemrudisha hotelini. Wakati wakiwa mwendoni, simu ya Dylan iliita, na alipoangalia mpigaji, akaipuuzia na kuendelea kuendesha gari huku akipiga story zenye kufurahisha na Harleen. Iliita tena mara mbili zaidi, hata Harleen akamwambia apokee tu, lakini Dylan akasema halikuwa na umuhimu sana. Kisha, aliyekuwa anapiga akamtumia ujumbe mfupi. Dylan hakuwa na kawaida ya kusoma SMS akiwa anaendesha lakini akaona aisome tu.

Baada ya kuona ujumbe huo, aliishiwa pozi kabisa na kuweka uso wenye kuonyesha umakini sana. Akasimamisha gari, kisha akamwambia Harleen kuwa kuna dharura ilikuwa imejitokeza, hivyo wasingeweza kwenda kupata msosi pamoja kwa kuwa alihitajika sehemu fulani haraka. Harleen akamuuliza ikiwa kulikuwa na tatizo, lakini akakanusha na kumwambia ilikuwa ni masuala ya kazi tu. Binti alihuzunika kiasi, lakini Dylan akamuahidi kwamba angemtoa tu kupata chakula wakati mwingine unaofaa kwa kuwa jambo hili lilikuwa muhimu kwake. Basi mwishowe Harleen akakubali, hivyo upesi Dylan akaanza kuelekea hotelini kule kumrudisha mrembo wake.

Wakafika baada ya dakika kadhaa, nao wakapeana denda ya kihisia sana, kisha Dylan akamuaga binti na kumsindikiza kwa macho alipoelekea ndani ya jengo la hoteli ile. Dylan akaichukua tena simu yake na kusoma ujumbe huo aliotumiwa, kisha akaiweka pembeni na kuligeuza gari kwa kasi sana kuondoka eneo hilo.

★★★

★★★

"Boss, amefika," sauti ya mwanaume ikasema.

"Mwache aingie ndani," akajibu mwanamke.

Mwanaume huyo akatoka, kisha akaingia mwanaume mwingine ndani ya chumba hiki akiwa amevaa mask usoni. Huyu alikuwa ni Killmonger. Mwanamke huyu alikuwa ni Queen, yule yule mwanamke mzungu anayetaka sana kumfanya Killmonger awe mpiganaji wake ambaye alitaka kumtumia mpaka nje ya nchi. Sasa akawa hapo kwenye chumba cha Queen, kama ofisi yake ya sehemu hii, akimtazama kwa mkazo sana. Queen akaachia tabasamu huku akiwa ameketi kwenye kiti chake, na pembeni yake walisimama mabaunsa wawili, huku nyuma ya Killmonger akisimama mwanaume yule aliyemruhusu kuingia.

"Welcome...my favourite Tanzanian fighter (karibu...mpiganaji wa kitanzania nayempenda sana)," Queen akamkaribisha Killmonger.

Jamaa akawa anamtazama tu kwa hisia kali sana.

"Ulikuwa kwenye hiatus...watu wameku-miss. Nafurahi umeamua kurudi," Queen akasema.

"Bosco yuko wapi?" Killmonger akauliza kwa mkazo.

"Oh...kwani ninaishi naye?" Queen akauliza kikejeli.

"Sina muda na michezo yako Queen. Naomba uniambie Bosco yuko wapi," Killmonger akasema kwa ujasiri.

Queen akanyanyuka polepole na kuanza kumfata Killmonger taratibu. Alikuwa amevaa nguo ndefu na nyepesi sana yenye kuubana mwili wake, huku nywele zake akiwa ameziachia kwa nyuma na usoni akipendeza kwa kupaka lipstick nyekundu mdomoni. Akamsogelea Killmonger mpaka usoni na kuanza kumwangalia kama anamtathmini.

"Dy..lan. Una jina zuri," Queen akamwambia kwa madaha.

Killmonger akatambua kwamba alikuwa amepatikana haswa. Queen alitambua jina lake sasa, na bila shaka alijua hilo kupitia Bosco. Ujumbe aliotumiwa wakati yuko na Harleen kwenye gari ulikuwa kutoka kwenye simu ya Bosco, lakini aliyeutuma alikuwa Queen. Alikuwa amemwambia ikiwa anamjali rafiki yake, basi angekutana na Queen ili wayajenge, la sivyo Bosco angeumizwa.

"What do you want?" Killmonger/Dylan akauliza.

"Acha kujifanya kama hujui ninachotaka already. You make me lose a lot of patience man. Why are you so stubborn? Ninakupa offer nzuri, unakataa. Nahitaji kujua wewe unachotaka ni nini hasa hapa kwenye hii Fight Club. Ikiwa hupigani kwa ajili ya pesa tu, what is it that you are really after, huh?" Queen akamuuliza.

"Queen, jambo hili halipaswi ku-escalate namna hii. Mimi...ndiyo sipigani kwa ajili tu ya pesa, niko kwenye haya mashindano kama kujifurahisha tu," Killmonger akasema.

"Kujifurahisha? Are you kidding me?" Queen akamshangaa.

"Ni ngumu kuamini ndiyo, lakini ni kweli. Najua wengi lengo lao ni kupata pesa, lakini kwangu huwa ni njia nzuri tu ya kushusha misongo. Sina tatizo na yeyote ninayepigana naye. Simjui, hanijui. Tunaingia arena tunapigana punch mbili tatu, basi...hivyo tu," Killmonger akaeleza.

Queen akacheka sana.

"Mbona umekuwa mpole ghafla? Kiburi chote kimeenda wapi?" Queen akamuuliza.

"Bosco yuko wapi Queen? Tafadhali ninakuom..."

"Don't tafadhali me!" Queen akamkatisha kwa ukali.

Killmonger, yaani Dylan, akawa kwenye hisia za kuudhika sana. Alimwangalia Queen kwa mkazo mno, akijitahidi kuzuia hasira yake ili acheze sambamba na mchezo wa mwanamke huyu mpaka ahakikishe Bosco yuko salama.

"I'm not the type of a person who takes no for an answer (Mimi siyo aina ya mtu ninayepokea hapana kama jibu)," akasema Queen.

"Queen please jaribu kuelewa. Iko nje ya...yaani..."

"Acha kujing'ata, kuwa kama mwanaume basi!" Queen akasema.

Killmonger/Dylan akamshika kiunoni na kumvutia kwake kwa nguvu, akiubana mwili wake na wa mzungu huyo. Wale mabaunsa wakajaribu kumfata Killmonger ili wamdhibiti, lakini Queen akanyanyua mkono wake kuwazuia, naye akaachia tabasamu la hila kumwelekea Killmonger. Kisha, akatumia mkono wake kuibandua mask ya jamaa kutoka usoni pake, na kwa mara ya kwanza akauona uso wa Dylan kikamili. Queen alipendezwa na sura ya kijana huyu, na alishangazwa kiasi kwa kuwa baada ya kuweza kumwona vizuri alitambua alikuwa kijana mdogo tu, lakini amekwishawaaibisha wababa watu wazima kwenye mapigano yote aliyofanya. Dylan alijua kwamba Queen alipenda masuala ya kibabe-babe, ndiyo maana akachukua hatua hii ya kumbana kwake.

"Let's make a deal (tufanye makubaliano)," Dylan/Killmonger akasema.

Queen akaachia tabasamu huku anamwangalia mdomoni, kisha akasema, "Break it."

"Wherever you are holding Bosco, let him go, on one basis. I fight someone of your choice, and if he wins...I go with you. But if I win...you forget this bullshit once and for all (Popote ulipomweka Bosco, mwachie, chini ya jambo moja. Nipigane na mtu yeyote unayetaka, na ikiwa atanishinda, basi nitakwenda nawe. Lakini nikishinda..usahau kabisa huu upuuzi wote," Killmonger akasema.

"Ahahah...wazo hilo ni rahisi sana, just poppin' in your head right? Well no, sikubali," Queen akasema.

Kisha akajitoa kwenye mwili wa Killmonger/Dylan kwa nguvu na kumwangalia kwa hisia kali.

"Kama kweli unataka kumwokoa rafiki yako, utapaswa upigane na watu watatu leo...na ukiwashinda, ndiyo nitakupa mtu wako. Fair enough right?" Queen akasema.

"Lakini Queen...hakukuwa na haja ya kufanya haya...hauoni ni kama unapoteza muda? Wako wengi wanaojua zaidi yangu..watafute...mimi nina maisha ya..."

"Blah, blah, blah, blah, blah, blaaah... I don't care. Get your ass in that pit...then we'll see (...sijali. Nenda kwenye ulingo huko ndiyo tutaona)," Queen akamwambia kwa njia iliyoonyesha hakujali.

Dylan alikuwa na wakati mgumu hapa. Hakujua Bosco yuko wapi, na alijua mwanamke huyu kwa kiasi kikubwa alikuwa mwenye kiburi sana asiyetaka kushindwa, hivyo angefanya lolote ili kutimiza lengo lake. Kupigana na wanaume watatu ambao hakujua wangekuwa nani kuliifanya akili yake itambue kuwa bila shaka Queen alipanga mambo kwa njia fulani ili kuhakikisha anashindwa, lakini akajiweka sawa kifikira na kumkubalia Queen jambo hilo. Queen akaondoka, naye Dylan/Killmonger akaongozwa na mabaunsa wale mpaka kwenye chumba cha kupasha mwili kabla ya pambano.

Kwenye mtandao huo ambao pambano lilirushwa, iliwekwa wazi kuwa usiku huo Killmonger angepigana na watu watatu, siyo wote kwa wakati mmoja, ila mmoja baada ya mwingine. Mashabiki wengi wa mchezo huu walifurahi sana na kuanza kumwaga pesa nyingi za kubashiri pambano hilo; Killmonger akipewa kipaumbele kuwa angewashinda wote. Dylan alijiandaa vyema na kwa nia moja tu akilini mwake; kushinda. Alihitaji kupambana kwa ustadi wa hali ya juu ili kuwachengua wote ambao angepigana nao, na ili kumtoa rafiki yake kutoka mikononi mwa mwanamke huyo.

Ilipofika saa 6 kamili usiku, pambano la kwanza likaanzishwa. Killmonger, yaani Dylan, alikuwa anapambana na mtu aliyejiita Kumalija. Ijapokuwa jina hili lilikuwa la mtu (😁), yeye tokea mwanzoni alilitumia kama la sifa, siyo lakwake kihalisi. Alikuwa mwanaume mwenye mwili mdogo kiasi cha kumfikia Dylan, naye alivaa mask nyeupe yenye sura ya katuni anayecheka. Alifahamika kupigana kwa staili ya 'boxing' mara nyingi, na aliwahi kushinda mapambano kadhaa kipindi cha nyuma. Hii ilikuwa ni mara yake ya pili kupigana na Killmonger; mara ya kwanza walipopigana Killmonger alimshinda.

Kengele ikagongwa, na pambano likaanza. Mwanzoni wote walikuwa makini sana kukwepa mapigo ya mmoja na mwenzake lakini baada ya muda Killmonger aliweza kupata njia za kumwingizia Kumalija maumivu sehemu za mwili zenye udhaifu. Wakati huu kiukweli Dylan alipigana kwa umakini wa hali ya juu ili kuhakikisha anashinda, na ikawa hivyo. Alimshinda baada ya kama dakika 20 hivi, naye akamnyanyua na kumpa mkono wa amani, Kumalija akimpa pia kuonyesha 'peace.' Wakati huu Dylan hakupigana kwa njia ya masihara hata kidogo, kwa kuwa alijua usalama na uhuru wa rafiki yake ulitegemea ushindi wake hapo.

Baada ya hapo akafata mpiganaji mwingine aliyefahamika kama Jiwe. Alikuwa na mwili mkubwa zaidi ya Killmonger, naye alivalia mask nyeusi yenye sura ya kondoo. Ilikuwa ngumu kumtia maumivu usoni kwa kuwa kiziba uso chake hicho kilikuwa kigumu, lakini Killmonger alikuwa amewahi kumshinda kipindi cha nyuma, kwa hiyo hii ilikuwa mara yao ya pili kupambana pia. Killmonger akampa mkono wa amani kabla hawajaanza kupigana, naye Jiwe akaupokea kukubali. Kisha pambano likaanza. Pigana, pigana, pigana. Jiwe angalau aliweza kumtia maumivu sehemu kadhaa Killmonger, lakini bado ustadi mwingi wa Killmonger ulimshinda jamaa. Pambano lilichukua dakika 30 hivi, kwa kuwa kila mmoja wao hakutaka kukubali kushindwa, lakini mwishowe Killmonger akashinda. Fujo zilijaa kwenye mtandao huo baada ya Killmonger kufanikisha matarajio ya wengi. Alikuwa anahisi uchovu na maumivu sehemu za mwili wake, lakini akajikaza kiume kwa ajili ya pambano lililofuata.

Hazikupita dakika nyingi na mpambanaji mwingine akaingia. Huyu alijiita "The Crusher," naye alijulikana sana kwa kupigana kwa mtindo wa kutia maumivu makali kwenye miili ya wale aliopigana nao. Yaani kila mara alipopambana ilibidi mpambanaji mwenzake awe amekuja na daktari pembeni! Hakuwa amewahi kupigana na Killmonger, kwa hiyo hii ndiyo ilikuwa mara yao ya kwanza na watu walikuwa na hamu kubwa ya kuona nani angeibuka mbabe kati yao. Killmonger akampa mkono wa amani The Crusher, lakini jamaa akaupiga pembeni kwa dharau. Hivyo Dylan alijua angepaswa kupigana kwa uhodari wote maana huyu mtu bila shaka hakuelewa neno amani. Queen, alikuwa ni mdhamini wa The Crusher pia. Kabla ya pambano hilo kuanza, alikuwa amemwita pembeni mpiganaji huyo na kumwambia ahakikishe kwa hali na mali anashinda, naye jamaa akamwambia asihofu hata kidogo. The Crusher alivaa kiziba uso chenye rangi nyekundu kilichoyaacha macho na mdomo wake wazi. Alikuwa na mwili uliolingana na wa Killmonger, ila alimzidi urefu kiasi.

Baada tu ya kengele kugongwa, papo hapo The Crusher akamfata Killmonger kwa kasi sana na kumrukia kwa nguvu kisha kumtandika kwa ngumi usoni. Killmonger hakuwa ametarajia kasi hiyo, na kutokana na uchovu aliohisi alianguka chini. The Crusher alionyesha hataki mchezo hata kidogo kwa kuwa alimfata na kuanza kumpiga ngumi nyingi hapo chini kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake bila kupumzisha. Kwa ustadi, Killmonger akaigeuza nguvu ya The Crusher na kumsukumia upande aliokuwa ameegamiza mwili wake, kisha akajinyanyua huku akihisi maumivu. The Crusher hakuwa aina ya mpambanaji aliyetaka kumpumzisha adui; alipenda kupigana kwa kasi na kutumia nguvu nyingi aliporusha mapigo yake.

Killmonger alikuwa anahitaji utulivu wa kiakili ili apigane vizuri, lakini The Crusher hakumpa hiyo nafasi. Kila sehemu Killmonger aliyoenda tayari angekuwa hapo, na hili likafanya aanze kupoteza mwelekeo. Kama ni sehemu ambayo Dylan aliumia sana, basi ilikuwa ni kwenye ubavu wake wa kushoto. Alijitahidi kutoonyesha kwamba ameumia hapo ili adui yake asipakazie fikira, na kila mara alipoangushwa chini na kuulizwa na mwamuzi pembeni ikiwa alitaka kuacha, angekataa, na The Crusher angeanza kumshushia kipondo tena.

Ilifikia hatua Killmonger alihisi hasira sana kwa kuwa alitambua kwamba huyu jamaa alipigana namna hiyo kwa maagizo ya Queen. Aliwaza atumie njia ipi ili amzingue huyu bwege, na njia moja aliyofikiria ambayo hakuwa ameitumia bado ni ile ile aliyotumia sikuzote, yaani, capoeira. Alikuwa amelala chini, hivyo akajinyanyua kwa mtindo wa kulewa-lewa na kuanza kuupeleka mwili wake huku na huku kama anacheza muziki. The Crusher alicheka kwa dharau kwa kuwa alijua mtindo huu wa Killmonger ndiyo uliopendwa na wengi, lakini kwa wakati huu aliona usingemsaidia chochote. Akamfata na kumrukia, lakini Killmonger akajiviringisha chini na kunyanyukia upande mwingine. Kila mara The Crusher alipojitahidi kumvaa jamaa, Killmonger alitumia ufundi mwingi sana wa sarakasi ili kumkwepa na mara nyingine hata kumpiga kidogo hapa na pale.

Queen alikasirika sana baada ya kuona Killmonger/Dylan ameanza kuugeuza mchezo kwa faida yake, naye akasimama alipokuwa ameketi na kupaza sauti kumwelekea The Crusher akisema, "Finish him!"

Kwa kutiwa hamasa hiyo na boss wake, The Crusher alianza kumfata Killmonger kwa kasi zile zile kama mwanzoni, lakini Killmonger akawa ameshazizoea; yaani alijua jamaa angekuja vipi, hivyo akawa anamchenga na kumpiga kwa ufundi sana, hasa kwenye miguu. Kihalisi Dylan alikuwa anajitahidi sana kusitiri maumivu yake aliyoyahisi, na sasa akaanza kuona The Crusher amechanganywa na mitindo yake ya kupigana. Hivyo, kwa werevu Killmonger akamsubirishia wakati ambao The Crusher alianza kumfata tena, kwa kuwa jamaa alikuwa amezoea tu kwamba Killmonger angemkwepa, wakati huu Killmonger akafanya kama anapiga shuti la mpira kwa nguvu huku mwili wake ukizunguka hewani mara mbili akiwa amejikunja, na alipojikunjua akamfumua The Crusher teke la usoni lililofanya jamaa ashtue mshipa wa shingo yake kwa nguvu baada ya kukigeuza kichwa kwa kasi kutokana na pigo hilo.

The Crusher alidondoka chini na kutulia hivyo hivyo tu, na baada ya mwamuzi kumwangalia, akathibitisha kuwa jamaa alikuwa ameumia sana, hivyo wakaita daktari hapo amhudumie. Killmonger alikuwa amekaa chini, akipumua kwa uchovu mwingi huku akikaza meno yake kusitiri maumivu ya kichwa na ya mwili. Baadhi ya wadhamini waliokuwepo hapo walianza kumpigia makofi, huku kelele za mashabiki mitandaoni zikisikika wakimshangilia mwanaume. Akanyanyua uso wake kumwelekea Queen, nao wakatazamana kwa sekunde kadhaa, huku baadhi ya watu wakija kumsaidia jamaa anyanyuke. Yeye kutokuwa na wa kumdhamini hapo ilimaanisha kwamba hakuwa na daktari endapo angehitaji kupoza maumivu, na kiukweli hakuhitaji daktari kwa kuwa sikuzote alijiamini vya kutosha kujua kwamba angeshinda tu.

Watu hao wakampeleka mpaka kwenye chumba kimoja na kumketisha, kisha wakaanza kuhudumia sehemu walizojua aliumia sana. Alishangazwa na jambo hili kwa kuwa hakutambua ni nani aliyewaagiza wafanye haya. Ndipo baada ya dakika kadhaa mlango wa chumba hicho ukafunguliwa na Queen kuingia akiwa na mabaunsa wake nyuma. Akawaambia wote watoke na kuwaacha wawili humo, nao wakatii, kisha akamsogelea Killmonger/Dylan na kumtolea mask yake usoni. Akamwangalia jinsi alivyokuwa ameweka sura iliyoonyesha uchovu, huku damu ikionekana kuvuja puani na ikitoka mdomoni pia. Akachukua kikaushio na kuanza kumfuta taratibu huku Dylan akimwangalia tu.

"Once again...you've proven that I was right about you. You are very talented (kwa mara nyingine tena umethibitisha nilikuwa sahihi kukuhusu. Una kipaji sana)," akasema Queen kwa sauti ya chini.

"Bosco....yuko wa..?" Dylan akauliza kivivu.

"Dont worry. He is fine," Queen akasema.

Kisha akatoa ishara ya vidole kwa mabaunsa wake, na mmoja akatoka nje ya chumba hicho.

"Nilifanya kila jambo kuhakikisha unashindwa...but you're just so stubborn ain't ya? (...lakini wewe ni mgumu sana eti?)" Queen akauliza.

"Queen....I know you're powerful. But I have the right to choose what I wanna do with my gifts. I...I DON'T do this for money. I.... (Queen..najua una nguvu sana. Lakini nina haki ya kuchagua ninachotaka kufanya na zawadi nilizonazo. Sifanyi hii kitu kwa sababu ya pesa. Nina...)"

"I understand," Queen akamkatisha.

Dylan akabaki kumtazama kivivu tu. Ni hapa ndipo Bosco akaingia pamoja na yule baunsa, akionekana kuwa nzima kabisa. Akaanza kumwangalia Dylan hapa na pale na kumpa pole.

"I'm so sorry bro...nimekusababishia haya yote," Bosco akamwambia.

"Niko sawa. Vipi wewe? Hawajakuumiza hawa?" Dylan akamuuliza.

Queen akacheka na kutikisa kichwa chake.

"Hamna. Walinifungia tu...kwenye chumba na kuniacha humo masaa machache," Bosco akasema huku anamwangalia Queen kwa hofu kiasi.

"Una moto mwingi sana ndani yako Dylan ambao niliona ni kama unapotea tu bure huku. Wenzako wanapata pay nzuri, lakini najua kama ungekubaliana na wazo langu ungepata nyingi zaidi. Najua pia kwamba pesa zote ambazo umepata toka umefika huwa unampa Bosco ili azigawe orphanages...ahahah... who does that I mean? You are special. I just...wanted to help make it so your talent doesn't go to waste (..huwa unampa Bosco agawe pesa kwenye vituo vya watoto yatima....wewe ni wa kipekee. Nilitaka kusaidia tu ili kipaji chako kisiwe cha kazi bure)," Queen akaeleza.

"Na ili upate pesa nyingi kupitia kwangu," Dylan akasema.

"Ahahahah...yeah," Queen akajibu.

Dylan akasimama huku amejishika ubavuni.

"So what happens now? (kwa hiyo nini kinafuata sasa?)" Dylan akauliza.

Queen akatabasamu, akamsogelea Dylan usoni na kulamba shavu lake kidogo, kisha akamwambia, "Nenda ukaoge...Killmonger."

Dylan akaachia tabasamu hafifu akikumbukia siku ile alipomfanyia Queen hivyo, na hapo hapo Queen akaondoka pamoja na mabaunsa wake.

"Oy Dylan... nisamehe sana mwanangu. Queen kanichukua tu leo na kuanza kuniuliza vitu kuhusu wewe...nilipokuwa nakataa kusema wakaanza kunipiga mangumi mwanangu halafu wakanifungia kwenye...."

"Bosco usijali, hao ni washamba tu. Mechi zote tatu nimeshinda, kwa hiyo hakikisha hiyo hela...nusu uniletee....sss aagh..."

"Dylan, hauko sawa. Twende hospitali," Bosco akasema kwa kujali.

"Agh..hamna. Me na...kuna sehemu naenda kwanza," Dylan akasema.

"Sa'hivi saa 8 Dylan...unaenda wapi?"

"Siwezi kurudi home nikiwa hivi. Nitaenda sehemu nyingine kwanza."

"Lakini..."

"Usijali kuhusu mimi Bosco. Wewe fanya kama nilivyokwambia," Dylan akasema.

Baada ya hapo, akaelekea pamoja na Bosco mpaka kwenye gari lake kule nje. Sehemu hii, kama mtu angefika kwa mara ya kwanza na kuingia, angedhani ni jengo dogo la michezo ya kamari (casino), lakini kwa ndani zaidi ndiyo kulikokuwa na sehemu ile ya mapambano, iliyofichwa vyema. Sikuzote wamiliki (kutia ndani Queen) walihakikisha hakuna mtu yeyote ambaye hakuwa na kibali cha kwenda hapo aweze kupita; walikuwa makini sana. Dylan, akisaidiwa na Bosco, akaingia ndani ya gari lake na kuketi kimaumivu, lakini akajikaza tu na kuliwasha ili aondoke. Wote hawangeweza kutambua kwamba Queen alikuwa ndani ya gari lake pembeni akimwangalia sana Killmonger wake huyo.

Dylan akaliondoa gari hapo na kurudi mpaka kwenye ile nyumba yake tena; alikotoka na Harleen muda fulani uliopita usiku huo. Alifika hadi ndani na kwenda chumbani, ikiwa ni usiku wa saa 10 kasoro sasa, naye akajivuta polepole mpaka bafuni na kujimwagia maji (kwa bomba la mvua). Akarejea chumbani na kujilaza kitandani kiuchovu sana. Shughuli kali ya mara mbili pamoja Harleen, pambano dhidi ya watu watatu wenye nguvu, jumuisha na njaa vilikuwa vimemfanya ahisi kutojiweza sana kwa wakati huu. Akalala tu hapo huku akiyazoea taratibu maumivu aliyohisi, kisha usingizi ukamjia.

Alikuja kuamka saa 2 asubuhi, lakini kutokana na kuhisi usingizi mwingi bado, aliendelea kulala mpaka saa 6 mchana. Akaamka na kujivuta taratibu, akihisi maumivu sana sehemu ya ubavu wake, miguuni, mikononi, na kichwani pia. Akajikongoja hivyo hivyo mpaka bafuni/chooni na kukojoa. Kisha akajimwagia maji kwa zaidi ya dakika 15. Alitoka na kujikausha, kisha kwa kujikaza akavaa nguo zake na kuichukua simu. Alikuta 'missed call' nyingi kutoka kwa watu kadhaa, hasa mama yake. Harleen alikuwa amemtumia jumbe nyingi pia za upendo bila kujibiwa. Dylan akaona ampigie mama yake kwanza.

"Dylan! Uko wapi? Tokea jana...kwa nini haupokei simu?" Jaquelin akalalamika upande wa pili.

"Nilipatwa na dharura..."

"Dharura gani?"

"Aam...ni mambo fulani tu nafatilia. Niko nje ya mkoa," Dylan akasema.

"What?! Yaani unaondoka bila taarifa Dylan... una matatizo gani? Unajua kuna mambo huku yanakuhitaji halafu unafanya hivyo kweli?"

"Najua mama....samahani..."

Jaquelin alishangaa kiasi. Hakutarajia Dylan angemwomba samahani kwa kuwa alimzoea kuwa mtu asiyekosa sababu ya kujitetea.

"Dylan....uko sawa?" Jaquelin akauliza kwa kujali.

"Yeah... Nipo sawa, nitarudi ndani ya siku chache. Nipe tu update za mambo yatakayotokea...we'll be in touch," Dylan akamwambia.

Jaquelin akabaki kimya tu, kama kuhisi kulikuwa na tatizo upande wa Dylan maana hata sauti yake haikuwa kwa jinsi alivyoizoea. Akaona amkubalie tu bila kumuuliza sababu ya kuwa huko, kisha akakata simu.

Dylan akamtafuta na Harleen, akimwambia pia kwamba dharura yake ilimpeleka nje ya mkoa na angerudi siku chache baadae; binti akimwambia kwamba angem-miss sana hivyo angepaswa kujitahidi kuwahi kurudi. Baada ya hapo, Dylan alijitahidi kutoka na kwenda kutafuta dawa za kuituliza misuli yake, naye akajinunulia na chakula pia ili ale kuongeza nguvu. Akaendelea kujiuguza mwenyewe kwenye nyumba yake hiyo kwa siku chache, bila yeyote kujua yuko hapo na mambo aliyoyapitia.

★★★

Hii ikiwa ni wiki ya pili tokea mara ya kwanza Dylan alipojiunga kwenye kampuni ya baba yake, mambo yalikuwa yameanza kwenda vizuri sana. Washiriki wengi wa bodi ya kampuni na wafanyakazi kwa ujumla waliona jinsi mawazo mengi ya Dylan yalivyowaletea faida. Uingizaji wa teknolojia za hali ya juu hapo ulisaidia sana kurahisisha kazi nyingi, na pia Dylan alikuwa ameagiza vifaa vingi vya ulinzi zaidi viwekwe maeneo yaliyozunguka kiwanda cha kampuni, kama camera, kengele za hatari (alarms), kuweka taa kubwa eneo la nje zenye kuzunguka kwa ajili ya usiku, na makontena magumu ya kutunzia vifaa; kwa kuwa kulikuwa na wizi uliofanywa wa vifaa uliosababisha kushuka kwa viwango bora kwenye masuala yao ya ujenzi. Wengi walimpongeza sana Gilbert kwa mambo haya mazuri, lakini yeye alizielekeza sifa zote kwa mwana wake tu.

"I can't believe this!" akasema Mr. Bernard kwa sauti ya juu, huku akiwa ametupa rundo la vitabu chini.

Alikuwa kwenye chumba fulani, sehemu fulani, wakati fulani, pamoja na MTU fulani. Kulikuwa na hali yenye mkazo sana ndani ya chumba hiki.

"....halafu mimi kipanyabuku kile kinakuja kunifanyia zengwe hili? Hapana haiwezekani. Yaani siamini hata inawezekanaje hako katoto kameweza kuleta haya mambo haraka hivyo....katakuwa kametumwa siyo siri!" Mr. Bernard akaendelea kulalamika, akimwambia huyo mtu.

Mtu huyu alikuwa ameketi kwenye sofa moja huku ameshikilia glasi yenye wine mkononi, naye akanywa kidogo na kuendelea kuwa kimya tu.

"Sa'hivi wameleta hadi surveillance equipment za hali ya juu...haitakuwarahisi kuiba vifaa pale. Board members wameanza kufurahishwa na Gilbert tena, sasa hivi mambo yanaenda kuharibika," Mr. Bernard akalalamika.

Mtu huyu akawa anamwangalia tu bila kusema lolote. Mr. Bernard akamsogelea karibu.

"Mbona husemi lolote? Kumbuka kwamba letu ni moja, na matatizo haya lazima tuyasuluhishe sote. Ukikaa kimya haisaidii kitu," Mr. Bernard akamwambia.

"Kwa hiyo kichwa chako bado kina tope sana kiasi kwamba hujui la kufanya?" mtu huyu akamuuliza Mr. Bernard kwa kejeli.

"Tunafanyaje? Ili kisasi chako kitimie, na ili mimi hatimaye niichukue kampuni, ni lazima tumwangushe Gilbert now. Mambo yalikuwa yameanza kuwa advantageous kwetu lakini sasa..."

Mtu huyu akanyanyua kiganja chake kumkatisha Mr. Bernard.

"Nikumbushe maneno ambayo huyo kijana alisema mara ya kwanza kufika kwenye kampuni," mtu huyu akamwambia.

"Hivi kweli unaniambia ma..."

"Yaseme!" mtu huyu akamkatisha kwa ukali kiasi.

Mr. Bernard akashusha pumzi na kumwambia, "Alisema kwamba tunaangalia sana tatizo badala ya njia za kulitatua."

"Huoni kwamba ndiyo unachokifanya sasa hivi?" mtu huyu akamuuliza.

"Lakini tutafanya nini sasa? Methali hazisaidii," Mr. Bernard akasema kwa mkazo.

Mtu huyu akatoa picha fulani na kuiweka mezani. Ilikuwa ni picha ya Dylan. Mr. Bernard akamwangalia kwa makini.

"Hiki...ndiyo kitu kinachompa Gilbert nguvu. Na ili ashuke, ni lazima nguvu hiyo itoweke," mtu huyu akasema.

"Mr. Bernard akatafakari kidogo, kisha akauliza, " Unamaanisha...tum...?"

Mtu huyo akaachia tabasamu la hila na kuichukua glasi yake yenye wine, kisha akaanza kuimiminia picha hiyo. Kwa kuwa wine ilikuwa na rangi nyekundu kiasi, ilionekana kama damu imeifunika picha hiyo, na hapo Mr. Bernard akawa ameelewa mtu huyu alichomaanisha.

JE, WATI DU YU SINKI WILI HAPENI NEKSTI?

★★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★★

Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi kali ya DYLAN. Mwenye kuihitaji yote anaweza ipata kwa sh. 2000 tu WhatsApp. Njoo tubonge 😉

WhatsApp no: +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TANO

★★★★★★★★★★★★

Ni asubuhi na mapema nyumbani kwa Gilbert na Jaquelin. Wawili hawa walikuwa kwenye harakati za kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini, na walipomaliza na kuelekea nje pamoja ili kuchukua gari, getini ikasikika 'horn' ya gari kwa nje. Wakasubiria mpaka mlinzi alipokwenda kufungua ili waone ni nani, na hapo likaingia gari la Dylan mpaka sehemu ya kuegeshea. Wote wakaangaliana kimaswali, kwa kuwa hata wakati ambao Dylan alipanga kurudi nyumbani hakuwa amewaambia. Akashuka kutoka kwenye gari na kuwafata karibu.

"Eeeh...mfalme naona umerudi," Jaquelin akasema kikejeli.

"Najua napaswa kuwaambia shika..moo lakini, sijazoea kabisa," Dylan akasema.

Gilbert akacheka kidogo.

"Za huko ulikokuwa?" Jaquelin akauliza.

"Ah fresh. Nilihitaji muda wa kuwa peke yangu angalau...natumaini haijawa-affect vibaya," Dylan akasema.

"Hakuna shida. Ila tu mama yako anasisitiza uwe unatoa taarifa. Anaogopa utapotea," Gilbert akamwambia.

"Siyo kupotea, me sipendi uwe unaondoka tu hata husemi lolote. Usirudie tena," Jaquelin akamwambia.

Dylan akamkumbatia na kusema, "I won't."

Wazazi wake walikuwa wameshajadili sana kumhusu tokea alipoondoka ghafla, bila kuwa na uhakika wa ni nini kilimpata mpaka akakaa huko muda wote, na hata mikataa mingi waliyofikia ilikuwa makisio tu. Baada ya Dylan kumwachia mama yake, akawaambia watangulie, naye angefata muda si mrefu. Kisha akaenda zake ndani kujiandaa akiwaacha wenyewe wanaingia kwenye gari. Maumivu aliyohisi siku chache zilizopita yalikuwa yamefifia kufikia siku hii, hivyo alikuwa tayari kurudi kazini na kufanya mambo mengine pia.

Baada ya kufika kwenye kampuni, alihudhuria mkutano fulani wa washiriki wa bodi, akatoa mawazo yake mapya, na wengi wakampongeza kwa mafanikio yaliyokuwa yameanza kujengeka ndani ya muda aliosema kweli yangetimia. Mr. Bernard alikuwepo pia, akiendeleza unafiki wake wa kum-support Dylan na Gilbert, huku nyuma ya pazia akiwa ameficha jambo baya sana kuielekea familia hiyo.

Walipomaliza, Dylan akaelekea ofisini kwake na kukaa kama masaa mawili hivi, kisha akampigia simu Harleen. Alimjulisha wakati huu kuwa alikuwa amesharudi, naye binti akawa mwenye hamu sana ya kumwona. Dylan akapendekeza watoke kupata chakula cha mchana pamoja kwenye sehemu ambayo alisema ingemfurahisha sana bibie, kwa kuwa mara ya mwisho kuonana walipanga kwenda kula pamoja lakini dharura ilipotokea ikashindikana. Harleen aliafiki, ijapokuwa alimwambia kwamba angehitaji kurudi upesi hospitali baada ya mlo huo.

Hivyo bila kuchelewesha Dylan akafunga mambo yake ya kazi na kuelekea kwenye hospitali kuu kumpitia mrembo huyo. Alipofika nje ya uzio mpana wa hospitali kwa mbele, alimjulisha Harleen kuwa yuko hapo tayari, na baada ya dakika chache mtoto mzuri akatoka na kulifata gari lake jamaa kisha kuingia ndani. Alikuwa amevalia blauzi nyepesi ya njano na suruali ya jeans yenye kubana pamoja na viatu vya kuchuchumia vya rangi ya njano, na mkononi alibeba pochi ndogo tu.

Walipeana denda yenye hisia nyingi sana baada ya kuonana tena tokea usiku ule wa mwisho kuwa pamoja, kisha Dylan akaliondoa gari hapo ili ampeleke daktari wake huko alikomwambia. Harleen alimsimulia mambo mengi aliyofanya ndani ya wiki hiyo, naye Dylan akajaribu kubuni-buni tu story kuhusiana na dharura aliyomwambia ilimpata mpaka kwenda mbali kwa muda wote huo. Harleen aliuliza ni sehemu gani hiyo ambayo Dylan alipanga kumpeleka, lakini Dylan akamwambia asubiri ili ajionee mwenyewe. Wakafika maeneo fulani ya mjini, naye Dylan akasimamisha gari lake na kuliegesha pembeni ya barabara.

"Hapa ndiyo umenileta...tupate chakula?" akauliza Harleen.

"Yeah! Let's go," akajibu Dylan kwa shauku kisha kushuka ndani ya gari.

Harleen akashuka pia, akionekana kutopendezwa sana na mazingira ya hapo. Ilikuwa ni sehemu ya mjini ambayo ilizungukwa na watu wengi wakifanya harakati mbalimbali. Dylan alipenda sana kupata vyakula vya sehemu ya mamantilie, na alikuwa na tabia ya kwenda sehemu mbalimbali za namna hiyo kutokea kwenye mizunguko yake na hata kazini mara kwa mara ili kupata msosi.

"Twende pale hivi. Nina siku nyingi sijaenda," akamwambia Harleen.

"Ahah...na wewe unaendaga sehemu za hivyo?" Harleen akauliza.

"Sure I do! Wanatengenezagavyakula vya ukweli yaani ukila huwezi kuacha kujilamba vidole," Dylan akasifia.

"Ahahahah...na nisipojilamba?"

"Basi hujashiba!"

Harleen akacheka kutokana na utani mwingi wa Dylan.

Wakaliacha gari hapo pembeni ya barabara na kuelekea mpaka kwenye mgahawa ule. Ulikuwa mgahawa wa kawaida tu, na watu kadhaa eneo hilo waliwatazama sana kutokana na jinsi walivyoonekana kuwa wa kishua. Dylan alisalimiana na baadhi ya walioketi kwenye mabenchi nje ya sehemu kama maduka, huku wanaume wengi wakimwangalia Harleen jinsi alivyokuwa amenona kwa nyuma.

Walipoingia ndani ya mgahawa huo, wakanawa mikono yao sehemu ya pembeni iliyokuwa na ndoo safi yenye koki ya kufungulia maji na sabuni ya maji. Kulikuwa na meza na viti vya plastiki vilivyopangiliwa viti vinne kwa meza moja. Kulikuwa pia na baadhi ya wateja ambao waliwaona na kuwaangalia sana, lakini Dylan na Harleen wakawapuuzia. Dylan akamwonyeshea Harleen meza aliyopendelea wakakae, kisha wakaanza kuifata. Wakati wamepiga hatua chache, pochi ya Harleen ikawa imemponyoka kwa tukio baya, hivyo Dylan akainama kuiokota huku Harleen anatabasamu.

Baada ya kumpatia mrembo pochi yake, akageuka ili waanze kuielekea meza ile, pale alipopamiwa na mtu fulani aliyekuwa anakuja upande wake kutokana na Dylan kutoona mbele kwa uharaka. Mtu huyu alikuwa ameshika jagi mkononi na glasi yenye maji, hivyo maji yaliyokuwemo yakammwagikia Dylan kwenye T-shirt yake iliyokuwa ndani ya koti alilovaa kwa juu bila kufunga vifungo, na kumlowanisha kuanzia kifuani mpaka tumboni.

Aliponyanyua uso wake kumtazama mtu huyu, akakutana ana kwa ana na mwanamke mwenye sura nzuri sana. Mwanamke huyu alionekana kuwa na hofu usoni baada ya kummwagia maji Dylan, hivyo akaweka jagi na glasi kwenye meza tupu ya pembeni na kutoa tishu nyingi safi zilizokuwa kwenye meza hiyo ili amfute.

"Samahani jamani...nisamehe..." akawa anasema kabla hajaanza kumfuta.

"Kwa nini huangalii mbele?" Harleen akauliza kwa kukereka.

"No..its cool. Hamna shida," Dylan akasema kwa utulivu.

"Hapana..samahani sana. Wacha niku..." akasema mwanamke huyo huku akianza kumfuta jamaa kifuani.

Dylan alimwangalia kwa upendezi fulani hivi. Alikuwa mdada ambaye kwa haraka Dylan alikadiria ana miaka kati ya 22 mpaka 26, na alikuwa na uso wenye kuvutia sana. Ngozi yake ilikuwa ya weusi wa maji ya kunde, na nywele zake zilikuwa laini na nyingi, ambazo alizichana kuelekea juu vizuri na pembeni kunyoa kiasi; kama kiduku. Kwa kuwa mwanamke huyu alionyesha woga uliofaa na bidii ya kutaka kurekebisha hali hiyo, Dylan alitaka kumtuliza, ili kumfanya aone kwamba hakuwa amekasirika kuhusiana na jambo hilo kabisa kwa sababu halikutazamiwa.

"Ah..ahahah..unanitekenya!" Dylan akatania kiuchokozi.

Hii ikamfanya mwanamke huyo amtazame vizuri machoni Dylan. Jamaa alikuwa anatabasamu kirafiki tu, naye Harleen alisumbuliwa kiasi na jinsi hali hiyo ilivyojitengeneza namna hiyo.

"Usijali. Niko sawa. Asante," Dylan akamwambia kwa upole.

Dada huyu akashusha mkono wake taratibu huku bado anamwangalia Dylan.

"Twende tukakae," Dylan akamwambia Harleen.

Wakaifata meza yao waliyochagua na kuketi hapo. Harleen akamuuliza Dylan ikiwa alikuwa sawa kukaa amelowana, naye akamwambia haikuwa na shida.

"Karibuni. Mngependa chakula gani?" ikauliza sauti ya mwanamke.

Dylan aliponyanyua macho kumtazama, ilikuwa ni yule yule dada aliyemwagia maji. Sasa akawa ametambua kuwa alifanya kazi hapo kama muhudumu.

"Kuna vyakula gani wakati huu?" akauliza Harleen.

Dada huyo akaanza kusema ni vyakula vilivyokuwepo.

"Aaam...pilau yenye nyama nyingi tafadhali," akasema Dylan huku anamtazama.

"Pilau...yenye nyama nyingi?" Harleen akauliza.

"Yeah. Nawekewa nyama nyingi nijisevie, siyo za kuishia kwenye meno," Dylan akatania.

"Ahahah...okay. Aam..mimi naomba...sijui hata niagize nini," akasema Harleen.

"Mletee kama mimi tu," Dylan akamwambia dada huyo.

"Sawa," akajibu huyo dada, kisha akaondoka kuwafatia maagizo yao.

"Ndiyo mara yako ya kwanza kuja sehemu kama hii?" Dylan akauliza.

"Mh...hamna. Sema tu nina muda mrefu. Zamani tulikuwa tunakuja sehemu kama hii ila baadae nikaacha," akajibu Harleen.

"Okay sawa. Utafurahia sana hapa. Vipi hospital? Kuna mapya huko?" Dylan akauliza.

"Ooh...jana tulikuwa na kazi nyingi zenye kuhuzunisha sana," akajibu Harleen.

"What happened?" akauliza Dylan kwa kujali.

"Tulikuwa tunadili na waliojeruhiwa kwa ile tragedy."

"Tragedy gani?"

"Hukusikia?"

"Kusikia kuhusu nini?"

"Kuna kampuni moja..sijui inaitwaje vile..kuna mashine zake zililipuka na kuwajeruhi wengi...wengine walikufa pia," Harleen akamtaarifu.

"Wewe! Kweli?"

"Ndiyo ni kweli. Kwa hiyo tulikuwa tunajitahidi sana kuwasaidia watu hao. Walitia huruma sana."

"Masikini! Pole yao kwa kweli. Zililipuka vipi hizo mashine? Usiniambie magaidi wameshaingia huku na kuanza yao..."

Ni wakati huu ndipo yule dada akaleta vyakula vyao, vikiwa juu ya sinia pana la shaba. Kisha akaanza kuvitengenisha na kuwapangia mezani kwa jinsi walivyoagiza.

"Hapana, siyo magaidi. Kuna..kitu fulani kimefichika. Polisi wanachunguza chanzo," akasema Harleen.

"Yeah..wafanye hivyo. Dah! Tunaweza tu tukawa tumekaa hapa af' unashtukia puuf!" Dylan akatania.

"Ahahahah...usiombee," akasema Harleen.

Wakati huu, yule dada alikuwa akiweka chakula cha Dylan karibu yake, hivyo Dylan aliweza kuivuta harufu yake nzuri sana ya manukato. Ni hapa ndipo akapata nafasi ya kumtazama mwilini vizuri. Alikuwa amevaa gauni ndefu nyeupe yenye kuvutika, iliyokuwa na mapambo ya nyota-nyota za rangi mbalimbali. Iliubana mwili wake vyema na kufanya hips zake pamoja na kalio lake nene kwa nyuma litokeze vizuri. Alipomtazama usoni, akakuta mwanamke huyo anamwangalia pia kwa njia fulani ya uvutio, kisha akakwepesha macho yake.

Baada ya kuwa amemaliza kuwawekea, akaanza kuondoka sasa. Jinsi kalio lake lilivyonesa-nesa kwa nyuma ilimfanya Dylan aachie tabasamu la mbali kwa kuvutiwa na myumbuliko huo matata! Waliendelea kupata chakula hapo huku wanafurahia maongezi ya hapa na pale. Nyakati zote ambazo yule dada alionekana pale, akiwahudumia watu, Dylan angemtazama sana, naye angemwangalia pia kisha kuendelea na mambo mengine. Ilikuwa ni kama wanataka kusemeshana jambo fulani, na macho yao tu ndiyo yakawa yanafikishiana ujumbe huo usioeleweka kwa njia isiyo ya moja kwa moja.

Baada ya kumaliza msosi, alikuja muhudumu mwingine na kutoa vyombo vile. Kisha akarudi tena kuchukua pesa ya malipo, naye Dylan akampatia. Kwa kuwa Harleen alimwambia wawahi ili arudi hospitali, wakanyanyuka na kuanza kuelekea mlangoni ili watoke. Lakini walipofikia mlango, Dylan akageuka na kumwona tena yule dada upande wa kuelekea jikoni kule. Alikuwa amesimama akiongea na muhudumu mwenzake, kisha akamwangalia jamaa kwa mara nyingine tena.

Harleen akawa ametangulia kutoka nje, hivyo Dylan akatumia sekunde chache kumwangalia tu mwanamke huyo. Kisha akafanya kama kutabasamu kumwelekea, naye dada huyo akatabasamu pia na kuangalia pembeni. Uvutano huu mzuri kati yao ukawa wenye kuichangamsha sana akili ya Dylan, naye akatoka nje akihisi raha sana bila kuelewa kihalisi chanzo ni nini.

Dylan akamwendesha Harleen mpaka hospitali, na wawili hawa wakaagana kwa kupeana busu kimahaba sana ndani ya gari. Kisha daktari huyu akaelekea jengoni, naye Dylan akaanza kuelekea kwenye kampuni yao pia. Wakati wakiagana, walikubaliana kwamba baadae Dylan aende hotelini kwa Harleen ili waweze kuwa pamoja, kwa kuwa Harleen alimsihi afanye hivyo. Ratiba yake pale hospitali haingemchukua muda mrefu kuondoka ndiyo maana akataka watumie nafasi hiyo kuwa pamoja tena.

Dylan bila shaka alikuwa amekubali, naye aliporejea ofisini alishughulikia masuala mengi haraka kisha kuelekea nyumbani baadae kwa ajili ya kujiandaa kukutana na mtoto hotelini. Walikuwa wamekwishawasiliana tena, na Harleen akawa amemjulisha kuwa tayari alikuwa kwenye chumba chake; akimsubiria. Mwanaume akajisafisha vyema na kuvaa nguo nzuri; T-shirt nyepesi yenye rangi mbalimbali ilivyombana na kuchoresha kifua chake vizuri, suruali ngumu nyeupe na viatu vyeupe vya 'sneaker.' Akavaa na saa yake na miwani, kisha akarejea kwenye gari na kuanza kuelekea kwa mtoto mzuri.

Alifika nje ya hoteli ile na kuegesha gari lake, kisha akaanza kuelekea huko ndani. Ilikuwa hoteli yenye jengo pana la kifahari, lenye ghorofa 7, nayo iliitwa "Queen Hotel." Alielekea moja kwa moja mpaka ghorofa ya nne, kisha akaanza kuuelekea mlango wa chumba ambacho Harleen alikuwa. Alipoufikia, akapiga hodi, naye Harleen akafungua.

Mtoto aliachia tabasamu la furaha baada ya kumwona Dylan hapo. Dylan akamtazama mwilini, naye binti akawa anamwangalia kwa hisia sana. Harleen alikuwa amevaa kigauni chepesi kilichofikia magotini, nacho kiliachia njia kubwa kifuani na kufanya sehemu za mwanzo za matiti yake yaonekane. Wakati huu, alikuwa amesuka mtindo mwingine wa nywele, ambazo zilikuwa nyingi na laini, zikimwagikia mgongoni.

Dylan akaigiza kuwa vampire kwa kujaribu kuingia lakini akashindwa. Alijifanya kama amejigonga sehemu ya wazi mlangoni kisha akarudi nyuma akiigiza kuumia. Harleen akacheka kidogo, akiwa ameelewa alichomaanisha. Kwenye filamu nyingi, ma-vampire huwa hawawezi kuingia kwenye nyumba ya mtu mpaka wakaribishwe. Hivyo Dylan alikuwa anamwambia Harleen kwa njia isiyo ya moja kwa moja kuwa amkaribishe ndani.

"Come in."

Akamkaribisha, naye Dylan akamfata akiwa anatabasamu. Akaitoa miwani yake machoni na kuanza kumpiga busu laini mdomoni. Wakaendelea kupiga denda kwa dakika chache, kisha Harleen akaivunja busu na kuanza kurudi nyuma huku anamwangalia jamaa kwa hisia. Dylan akafunga mlango na kuanza kumfata, lakini Harleen akamkimbia na kuanza kumkwepa. Wakawa wanakimbizana huku wakicheka, kisha Dylan akafanikiwa kumkamata na kuanguka naye kwenye sofa moja hapo.

Chumba hiki kilikuwa ni kipana na chenye vitu vingi vya kisasa. Kilikuwa na mlango wa kuingilia kwenye chumba cha pembeni ambacho ndiyo kilikuwa na kitanda kipana cha kulalia, hivyo sehemu hii waliyokuwepo ilikuwa kama sebule.

"I missed you," Harleen akamwambia.

"Mhm..masaa mawili tu?" Dylan akauliza.

"Kwangu ilikuwa kama eternity."

"Chumvi hiyo imekuwa magadi."

Harleen akacheka, kisha akambusu kwa upendo mdomoni.

Wakanyanyuka na kuketi vizuri kwenye sofa hilo, huku wakiwa wameshikana mikono.

"Ngoja nikuletee juice," akasema Harleen kwa sauti nyororo.

Kisha akanyanyuka na kuelekea kwenye kabati za vyombo zilizojengewa ukutani na kutoa glasi mbili, halafu akaifata friji iliyokuwa upande wa mbele na kusimama hapo akikandamizia glasi kwenye kifaa cha kwenye friji kilichotoa juice na kuijaza glasi. Dylan alikuwa anamwangalia kwa nyuma, jinsi kalio lake lilivyoinyanyua nguo yake kidogo kwa nyuma na kuyaonyesha mapaja yake, naye akashindwa kujizuia.

Akamfata hapo aliposimama na kulishika kalio lake akiwa karibu naye zaidi. Harleen akatabasamu na kuiweka glasi ya juice pembeni, kisha akageuza shingo yake na kuanza kudendeshana naye taratibu. Dylan aliliminya-minya kalio la bibie na kumfanya aanze kupandisha hisia za mahaba kwa kasi. Harleen akaivunja busu taratibu na kumshika jamaa kidevu kwa kiganja chake alichokuwa amerudisha kwa nyuma.

"Tunywe juice kwanza," akasema kwa sauti yenye deko.

"Me nataka kunywa nyingine kwanza," akasema Dylan.

"What?"

Harleen hakuelewa kile alichomaanisha Dylan, na hapo hapo jamaa akashuka mpaka chini na kukaa. Harleen alipotaka kuugeuza mwili wake, Dylan akamzuia na kumwambia asimame hivyo hivyo, kisha akapitisha kichwa chake katikati ya miguu ya Harleen na kuwa kama anamchungulia kwa chini.

"Dylan, unafanya nini?"

Mwanaume hakujibu. Akayashika tu mapaja manono ya mwanamke wake na kuanza kutembeza vidole vyake hapo kwa wororo. (..........). Harleen akawa ameweka mikono yake kwenye vishikio vya milango ya friji, huku anamwangalia Dylan akiwa chini yake.

Kisha Dylan akapandisha mikono yake mpaka kwenye mikanda ya chupi ya Harleen na kuishusha mpaka usawa wa magoti ya bibie. Ilikuwa inavutika sana, naye Harleen akakunja mguu mmoja na kumfanya Dylan aweze kuitoa, kisha akaurudisha mguu wake jinsi ulivyokuwa. Alipenda sana mitindo ya huyu jamaa, na hapa akawa anasubiri kwa hamu penzi ambalo Dylan alikuwa anaandaa kumpatia.

Dylan akawa anakitazama (.........).

(..........).

"Mmmm...delicioza (tamu)," Dylan akasifu.

"..mmhhm.....you're just saying that......"

"Ni kweli. I know anyone would want it so bad..." akaendelea kumsifia.

"...mmmhhh...anyone?" Harleen akauliza huku anasikilizia raha aliyopewa.

"...anyone. Hata wanawake," Dylan akatania.

"...mmhhm....na wewehhh.....do you want it?" Harleen akauliza kimahaba huku amefumba macho.

"Mtambo wangu mgumu ndiyo jibu lako!" Dylan akajibu kichokozi.

Kisha akaacha na kunyanyuka juu. Harleen akamgeukia na kumkumbatia, huku anampiga denda, akiwa ameshapagawa na penzi la Dylan. Dylan akaanza kurudi naye nyuma-nyuma mpaka kwenye mlango uliongia kwenye chumba chenye kitanda. Walipokikaribia, Dylan akaiachia midomo ya Harleen na kuvua T-shirt yake huku Harleen (.........).

(.........).

(........).

(........).

(........). Sauti ya mwitikio wake Harleen wa mshindo huu wa pili ilikwaruza, hivyo ikabidi Dylan asitishe kwanza zoezi maana aliona binti kazidiwa; asije akafa bure.

Kiukweli, wakati huu mtindo aliotumia Dylan ulikuwa wa nguvu sana, hivyo Harleen alizidiwa kwa kuwa mwili wake haukuutegemea. Lakini alipenda sana jinsi kijana huyu alivyomwajibikia leo, naye akawa anataka waendelee tena. Dylan akawa anamtuliza kwa kuzipa 'massage' nyonga zake ili mwili wake urudie hali ya kawaida kwa kuwa mshindo wake ulikuja kwa nguvu mno. Alipoanza kutulia, Dylan akajilaza pembeni yake na kuanza kumbusu mdomoni, naye Harleen akajibu pigo hizo taratibu kwa kuibananiza miili yao zaidi.

Busu yao ilitoa sauti za mifyonzo iliyosisimua, kisha wakaachiana midomo taratibu huku Harleen akiwa amelegea kweli.

"Ulikuwa unataka kufa?" Dylan akamtania.

"Mhmm...kichwa chako!" Harleen akasema kwa deko.

"Ahahah...binti-mashavu we mtamu sana," Dylan akamsifia.

Harleen akatabasamu kilegevu na kumbusu tena mdomoni. Dylan akajilaza, naye Harleen akalaza kichwa chake kifuani kwake.

"That was amazing," akasema Harleen.

"Anytime.

"Mhm...mara ya kwanza hukuwa hivyo. Nini kimekubadilisha leo?"

"Ahah...sijabadilika. Nilitaka tu ufurahi zaidi mpaka uhisi kufa."

"Bichwa lako Dylan! Usinitanie hivyo," Harleen akasema huku anamfinya.

"Sawa...lakini bichwa langu la huko chini si limekupagawisha?"

"Wala hata!"

"Unajikana mwenyewe! Binti-mashavu bwana...eti oh..ah..oh..Dylan!"

"Hahahah...Dylan nitaacha kukusemesha!"

"Ahahah...unalo bibie!"

Harleen akacheka kwa furaha na kujiona mwenye fahari sana kuwa pamoja na Dylan. Dylan alijitahidi kwa utundu wake mwingi kumfanya bibie ajihisi kuwa mwenye upekee mno; alimtania, alimsifia, alimdekeza pia kwa maneno yake mazuri sana.

"Nikuulize kitu?" Harleen akasema huku anatembeza kiganja chake kwenye kifua cha Dylan.

"Bila shaka," Dylan akajibu.

"Una nyumba ambayo ni yako sasa...kwa nini bado unakaa kwa wazazi?"

"Ahah... Umesubiria hizo siku zote ndiyo umeona uniulize leo, why?" Dylan akauliza.

"I guess imekuja tu akilini now...do you mind?"

"No I don't...yaani...ahahah...inakushangaza kwamba bado niko home eti?"

"Haishangazi. Ni kwamba tu najua wewe unapenda kujiachia sana kwa hiyo nilitarajia ungekuwa ushatoka hapo."

"Well...baada ya mama ku...kufanyiwa operation..nilitaka niwe karibu naye lakini sikuweza cause nilikuwa mbali na nilibanwa. Nimerudi miezi michache tu iliyopita, nilihitaji sana kuwa karibu naye..." Dylan akaeleza.

"Yeye tu? Au na baba yako pia?" Harleen akauliza.

Dylan akakaa kimya.

"Dylan...ni mambo ya familia najua, lakini...kiukweli naona kama kuna vitu vingi vilitokea...vitu fulani hatari pia..."

"Kwa nini unasema hivyo?"

"Najua sababu hasa ya mama yako kuhitaji liver transplant haikuwa kile ambacho walisema ndiyo tatizo lililomkumba..."

"Unamaanisha nini?"

"Najua aunty Jacky alikumbwa na paracetamol overdose iliyosababisha fulminant hepatic failure na kuliharibu ini lake Dylan; hiyo ikimaanisha alikunywa sumu. Angeweza kufa haraka kama asingefanyiwa transplant upesi," Harleen akaeleza.

Dylan akakaa kimya kidogo akiyasawazisha maneno ya Harleen kwenye akili yake. Binti alikuwa ameongea ukweli ambao Dylan alijaribu sana kutoukumbuka kutokana na wakati mgumu aliopitia kihisia kipindi kile jambo hilo lilipompata mama yake.

★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

WhatsApp no: +255 787 604 893
(Hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo unaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)


★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SITA

★★★★★★★★★★★★

"Ulijuaje hilo?" Dylan akauliza kwa utulivu.

"Me ni daktari Dylan. Walijitahidi kuficha origin ya tatizo kwa sababu nisizozijua, lakini kwa kuangalia tu jinsi thrombocytopenia ilivyokuwa severe mwilini mwake nilitambua haraka," Harleen akasema.

"Dah, madaktari nyie na hayo madude yenu sijui thomborositepainia, huwa mnayawekaje vichwani?" Dylan akauliza kiutani.

Harleen akacheka kidogo kisha akasema, "Samahani, its a force of habit."

Dylan akatulia kidogo kisha akasema, "Ndiyo, uko sahihi. Mama alikunywa sumu... lakini mpaka leo sijajua ilikuwa ni kwa nini."

"Pole Dylan..."

"Ahah... asante. Unajua... ukweli ni kwamba bado niko nyumbani kwa sababu nahofia huenda hata akaingiwa na mood swing inayoweza kusababisha atende kwa njia mbaya kama kipindi hicho... ijapokuwa siwezi kumwangalia muda wote lakini angalau kuwepo pale kunanipa ahueni. Mara nyingi nilipokuwa Brazil, niliwaza sana ingekuwa vipi kama... ingetokea mama angekufa kipindi hicho halafu sikuwa nimekaa naye kwa muda mrefu vile. Kwa hiyo sasa hivi najitahidi kufidishia muda huo," Dylan akaeleza kwa hisia.

Harleen akasogeza mdomo wake kwenye mdomo wa Dylan na kuanza kumpiga busu ya faraja.

Wakaendelea kudendeshana kwa sekunde chache, nao wote wakasikia simu ya Harleen ikiita kutokea sehemu ya sebule. Dylan akaivunja busu taratibu na kumwambia Harleen angemfatia simu yake pamoja na zile juice ili wanywe, lakini Harleen akawa anakataa na kumng'ang'ania ili waendelee na mapenzi yao. Dylan akasisitiza kuifata simu kwa kuwa iliendelea kuita karibia mara 7, hivyo alijua huenda ingekuwa muhimu. Hatimaye akafanikiwa kumkimbia mrembo huyo na kwenda kuifata akiwa bila nguo, na alipoichukua ilikuwa ikiita huku jina la aliyepiga likisomeka "Ray."

Akarejea kwa Harleen na kumpa huku anamwambia ni Ray ndiyo anapiga. Harleen alikuwa amejilaza kwa pozi lenye kuamsha hisia za mwanaume endapo angemtazama kwa uvutio lakini baada tu ya Dylan kusema jina "Ray," akaketi vizuri na kwa umakini akaichukua simu yake. Dylan yeye akawa anatabasamu tu kwa furaha, naye Harleen akatoa tabasamu la kujilazimisha, kisha Dylan akaelekea sebuleni tena. Harleen akapokea simu yake lakini alizungumza kwa sauti ya chini sana kiasi kwamba hata Dylan hangeweza kujua ikiwa alipokea simu. Mwanaume akarudi akiwa na zile juice mikononi na kupanda nazo kitandani, na hapo Harleen akaagana na aliyekuwa akiongea naye kisha kuiweka simu pembeni.

Dylan akampa juice moja, naye akabaki na moja, kisha wakagongeana glasi na kuanza kunywa taratibu huku wanatazamana kwa hisia. Kisha kwa utundu, Dylan akaisogeza glasi yake yenye juice karibu na kifua cha Harleen ambacho kilikuwa wazi, kisha akakimiminia juice kidogo iliyolowanisha kifua chake kwa michirizi. Harleen alishtuka kiasi na kuachama mdomo wake, naye Dylan akacheka tu. Kisha binti akaiweka juice yake pembeni na kuichukua ya Dylan pia na kuiweka pembeni. Dylan bila kuchelewa akakisogelea kifua cha bibie na kuanza kukilamba kwa wororo; akizipa umakini sehemu ambazo michirizi ya juice ilipita. (.........).

Wawili hawa waliurudia mchezo wao mtamu; (..........). Wote wakawa wameridhishwa na mmoja na mwenzake, na hapo wakalala pamoja na usingizi kuwapitia.

Dylan alikuwa wa kwanza kuamka, huku Harleen akiwa amelala pembeni yake kwa kuonekana amechoka. Jamaa akatabasamu na kumbusu kwenye shavu, kisha akaivuta simu yake Harleen aliyokuwa ameiweka pembezoni mwa kitanda na kuiwasha ili aangalie muda. Ilikuwa ni saa 2 usiku sasa, na wakati anataka kuirudisha alipoitoa, akaona ujumbe fulani kwenye kioo hicho cha simu uliovuta umakini wake. Ujumbe huu ulisomeka 'excited for tomorrow my dearest,' yaani 'nina hamu kubwa kwa ajili ya kesho mpendwa wangu.' Mtumaji wa ujumbe huo alikuwa ni Ray, naye Dylan akajua bila shaka ni yule yule jamaa aliyepiga muda ule. Hakujua ni nani, lakini akapotezea tu na kuiona kuwa jumbe ya kirafiki kutoka kwa mtu aliyefahamiana na bibie.

Akanyanyuka na kwenda kujimwagia maji, kisha akarudi chumbani na kuvaa nguo zake. Akamwangalia Harleen kwa upendezi sana, ambaye bado alikuwa amelala huku mwili wake ukiwa bila nguo, naye akamsogelea kitandani hapo na kumfunika vizuri kwa shuka. Akarudi sehemu ya sebule na kuchukua peni na karatasi kutoka kwenye daftari dogo, kisha akaandika ujumbe mfupi wa kumuaga mrembo huyo na kuuweka mezani. Aliona ni bora amwache apumzike, kwa sababu yeye alihitaji kwenda sehemu fulani haraka.

★★★

"Okay sawa. Hapana, iko ofisini....nikifika kesho nitaituma mapema wala usijali. Yeah... kila jambo liko safi kabisa. Okay asante sana. Kwa heri..."

Huyu alikuwa ni Dylan akiongea na mtu fulani kutokea upande mwingine wa jiji kwenye simu kuhusu masuala ya kazi. Alikuwa akiendesha gari bado baada ya kuondoka kwa Harleen, na sehemu aliyokuwa akielekea wakati huu ilikuwa ni kule mgahawa wake ulipokuwa. Alihitaji kwenda kuangalia mambo yako vipi kwa kuwa ulikuwa karibu sana kukamilika kwa kila jambo alilohitaji pale. Hakuwa ameweka simu sikioni wakati anaongea na mtu huyo, bali kifaa cha sikioni kilichounganishwa na simu yake (Bluetooth).

Akiwa anaendelea na safari yake hiyo, alipata kumwona mwanamke fulani pembezoni mwa barabara akitembea kuelekea upande alikoelekea yeye. Mwonekano wa mwanamke huyo haukuwa mgeni sana kwa Dylan, kwa kuwa nguo aliyovaa ilifanana pia na nguo ya yule dada mhudumu wa ule mgahawa walikoenda na Harleen mchana kwa ajili ya chakula. Kwa hiyo alivuta umakini wake kwa sababu moja kwa moja alimfikiria dada yule. Dylan akampita na kumwangalia kupitia kioo cha pembeni (side mirror) ya gari, na sasa akawa amehakiki kuwa ilikuwa ni huyo huyo dada baada ya kuuona uso wake kupitia kioo hicho. Akaegesha gari upande huo wa barabara na kusubiri afike usawa wake.

Akashusha na kioo cha mlango wa gari, na mwanamke huyu akawa amefika usawa huo.

"Hey..." Dylan akaita.

Dada huyo akasimama na kumwangalia kupitia uwazi wa mlango wa gari. Alikuwa ameweka uso wa kawaida tu, huku Dylan akitabasamu.

"Mambo?" Dylan akamsalimu.

"Poa tu," akajibu huku naye akitabasamu.

"Unanikumbuka?" Dylan akauliza.

Huyo dada akatikisa kichwa kukubali.

"Unaelekea wapi... nyumbani?" Dylan akauliza.

"Ndiyo."

"Aaaa... unaishi maeneo ya huko mbele?"

"Eee."

"Kama vipi panda nikupe lifti maana naelekea upande huo pia."

"A... ahah..hapana... asante. Ninaenda tu hapo mbele kuchukua bajaji..."

"Bajaji ya nini sasa wakati ndinga kali hii hapa?"

"Mhm... kwani nani amekwambia me nina uhitaji wa kupanda ndinga?"

"Oh... samahani... sikumaanisha vibaya. Yaani... nimeona tu nikusaidie kidogo..." Dylan akasema kwa upole.

"Wala usijali. Mimi nitapanda tu bajaji... na... wewe si kuna sehemu unaenda au?"

"Ndiyo, lakini kama unaelekea upande huo haina shida... nitakupeleka halafu kwanza... itaku-save hela..."

"Haina shida. Me..."

"Come on, usiwe hivyo. Me sitafuni watu bwana."

Dada huyo akacheka kidogo.

"Ingia twende. Halafu pia... gari langu linanukia vizuri kuliko bajaji... kwa hiyo humu ni bora," Dylan akatania.

Mwanamke huyu akamwangalia kwa sekunde chache, kisha akafungua mlango wa mbele na kuingia ndani ya gari. Dylan alifurahi, naye akaliingiza gari barabarani tena na kuendelea na mwendo.

"Utakuwa unanielekeza eti?" Dylan akamwambia.

"Kwani unanipeleka hadi nyumbani?"

"Sawa tu, kwa kuwa umeniomba."

"Ahahah... wewe ni mtu wa wapi?" dada huyo akauliza.

"Kwa nini?"

"Unavyoongea... hiyo lafudhi siyo ya kitanzania."

"Ahahah... Me mbona mtanzania? Mzawa kabisa."

"Kabila gani?"

"Hayo masuala huwa sina habari nayo kabisa," Dylan akasema.

"Mhm..." dada huyo akaguna na kutazama mbele.

"Jina lako ni nani?" Dylan akauliza.

"Niambie la kwako kwanza."

"Ninaitwa Dylan."

"Aaaa... sawa."

"Na wewe unaitwaje?"

“Naitwa Fetty," akajibu.

"Oooh... msukuma eeh?" Dylan akatania.

"Hapana. Kwa nini umefikiri me msukuma?"

"Well... jina lako hilo bila shaka limetolewa kwenye Fatuma kama sikosei," Dylan akatania tena.

"Ahaaah... Kwa hiyo wooote wanaoitwa Fatuma ni wasukuma?"

"Ndiyo navyojua. Labda kama mambo yamebadilika sasa hivi lakini..."

"Ingia hapo hivi," Fetty akamkatisha ili kumwelekeza pa kuelekea.

"Kwa hiyo umefanya kazi pale kwa muda mrefu?" Dylan akauliza.

"Siyo sana," Fetty akajibu kifupi.

"Sawa."

Dylan alikuwa ametambua mwanamke huyu alikuwa mwenye utu fulani wa kivyake sana. Alitaka kujua mengi kumhusu, na hili lilichochewa na jinsi walivyoangaliana leo wakati wapo kwenye ule mgahawa.

"Unakaa na wazazi nyumbani?" Dylan akauliza.

"Hapana, nimepanga," Fetty akajibu.

"Aaaa... okay. Nilipenda jinsi ulivyokuwa unaniangalia leo pale unapofanyia kazi, na sijui ni kwa nini..." Dylan akasema.

Fetty akamwangalia na kuachia tabasamu. Dylan pia akatabasamu baada ya kuona amemfurahisha binti.

"Nilifikiri ni kama vile hukutosheka na maji yaliyonimwagikia kwa hiyo nikahisi labda unataka kuniongezea," Dylan akatania.

"Ahahahah... hamna hata. We umeona vibaya," Fetty akakanusha.

"Mmmm hamna bwana, nilikuona vizuri kabisa..."

"Kwani hupendi kuangaliwa?"

"Nisingetabasamu ikiwa ningekuwa sipendi."

Fetty akatabasamu na kuangalia mbele.

"Kwa hiyo... ndo' sipati jibu au?" Dylan akauliza kichokozi.

"Mwenzangu nayefanya naye kazi pale alikuwa anakusifia sana... anasema wewe mzuri," Fetty akajibu.

"Hahah... kwa hiyo ukawa unaniangalia sana kwa ajili yake au?"

"Hamna. Alikuwa anataka nimsaidie ili muongee maana alikuwa anaona aibu... na pia alikuwa anamwogopa yule dada uliyekuja naye."

"Hivi kweli... yaani kashaniona niko na mtu mwingine halafu anakushurutisha uongee nami... kwa nini asingefanya hivyo yeye mwenyewe? Anaogopa nini wakati hii nchi huru bwana?"

"Kata kona hapo hivi... Me mwenyewe nilimwambia anajisumbua tu maana mnaonekana ni watu wenye hela na... yule ni mke wako sijui?" Fetty akasema.

"Hapana... siyo mke wangu."

"Ni girlfriend?"

"Mmmm... hatujafikiria kuweka mambo kati yetu kwa njia hiyo rasmi zaidi lakini ni mtu wangu wa karibu sana."

"Sa' si ndiyo girlfriend au?"

"Ahahah... ndiyo. Ukisema kwa njia hiyo ni kweli."

Fetty akaangalia chini na kusema, "Ni mzuri."

Dylan alihisi kitu fulani. Yaani ni kama Fetty alikuwa anaficha jambo lililohusiana na yeye baada ya kumwambia ana girlfriend, hivyo akaona amchokoze kwa utundu.

"Ndiyo ni mzuri... lakini siyo kama wewe."

Fetty akageuka na kumtazama Dylan kwa makini, huku jamaa akiangalia mbele tu kwa utambuzi wa kwamba binti alikuwa anamwangalia. Akajua bila shaka maneno hayo yalimwingia mtoto kwa njia yenye kusisimua. Akamgeukia pia, na wote wakaangaliana machoni kwa sekunde chache.

"Fetty..." Dylan akaita.

Fetty akaendelea tu kumwangalia.

"...tumekaribia kufika au bado?"

Baada ya Dylan kuuliza hivyo, Fetty akawa kama ameshtuka kutokana na kuzubaa.

"Ai... simama, tumepapita," akasema kwa uharaka.

Dylan akasimamisha gari huku akitabasamu. Fetty akashuka ili arudi kwa miguu, naye Dylan akashuka pia na kumwahi.

"Wewe vipi... mbona faster hivyo?" akamuuliza.

"Aa... asante sana. Nimefika tayari ni hapo tu hivi naingia," Fetty akajibu.

"Sa ndo' unaondoka hata kuaga hamna jamani?"

Fetty akabaki kumwangalia tu usoni.

"Ahahah... usiniogope Fetty. Mimi nataka tu tuwe marafiki. Sijui ni kwa nini lakini napendezwa nawe sana."

"Aliyekwambia nakuogopa nani?" Fetty akauliza.

"Sasa kinachokufanya ukimbie ni nini?"

"Nilikuwa nawahi..."

"Siyo tabia nzuri," Dylan akajifanya kaudhika.

"Sawa. Nisamehe," Fetty akasema.

"Nipe namba yako ndiyo nitakusamehe," Dylan akamwambia huku anatabasamu kwa utundu.

Fetty akatabasamu pia na kuanza kumtajia namba zake. Dylan akaziandika, kisha akamshukuru na kumwacha aelekee kwake. Akarejea kwenye gari na kuanza kuelekea kwenye mgahawa wake akijihisi furaha fulani ambayo ilichochewa sana na mwanamke huyo mwenye kuvutia.

★★★

Siku iliyofuata, Dylan alikwenda kwenye kampuni kama kawaida kwa ajili ya kazi. Sasa alikuwa anafurahia zaidi kuwa ofisini kuliko mwanzo, kwa kuwa mambo mengi aliyofanya yalikuwa yanaleta matokeo mazuri aliyotarajia, na hata ingawa wengi walimsifia, hakujigamba kwa kiburi. Ilipofika mida ya mchana, alimpigia simu Harleen mara kadhaa lakini hakupokea. Akamtumia ujumbe kuwa alitaka kwenda kupata chakula kwenye ule mgahawa wa jana pamoja naye ikiwa alikuwa na nafasi, au kama alikuwa amebanwa sana basi haingekuwa na shida.

Baadae, Harleen alimjibu kwa ujumbe kuwa hangeweza kwa kuwa alibanwa sana leo, hivyo wangeenda siku nyingine pamoja. Dylan alipomuuliza ikiwa angepata nafasi ya kukutana baadae zaidi, Harleen alikanusha na kusema haingewezekana kwa leo, na angemjulisha endapo angepata nafasi. Dylan kama Dylan hakuhisi chochote kwa njia mbaya, akamuaga tu na kuendelea na mambo yake, kisha akaondoka kuelekea kwenye ule mgahawa.

Kichwani kwake aliwaza kwenda pale hasa ili kumwona rafiki yake mpya, Fetty. Hakuwa amemtafuta kwa simu tokea usiku wa jana alipoipata namba yake, kwa hiyo aliwaza pia kwamba angetafuta nafasi ya kuongea naye kidogo. Alifika pale na kwenda moja kwa moja mpaka mezani, kisha mwanamke fulani akaja alipo, naye akiwa ni muhudumu wa hapo.

"Ungependa kupata chakula gani kaka?" akamuuliza.

"Ningependa uniitie Fetty tafadhali. Asante," Dylan akajibu.

Mwanamke huyo akashangaa kidogo, lakini akaona tu atii ijapokuwa halikuwa jibu alilotegemea. Sekunde kadhaa zikapita, naye Fetty akaonekana akija upande wa Dylan. Dylan alitabasamu kwa furaha, naye Fetty akashindwa kujizuia kutabasamu. Jamaa alimwangalia jinsi alivyokuwa na mwili mzuri sana, na wakati huu Fetty alikuwa amevaa T-shirt ya kijani na suruali ya jeans ya samawati (blue) yenye kubana ambayo ilichoresha hips zake vyema. Akafika hapo karibu na kumsalimu.

"Mbona kimya?" Dylan akamuuliza.

"Unamaanisha nini?" Fetty akauliza pia.

"Hujanitafuta kwa simu!"

"Aliyechukua namba si wewe? Ningekutafuta vipi wakati hukunipa yako?"

"Shida ndiyo hiyo... kwa nini hukuniomba?" Dylan akauliza kimasihara.

Fetty akacheka kwa chini na kutikisa kichwa. Dylan akatabasamu pia.

"Unahitaji chakula gani?" Fetty akamuuliza.

"Ish... yaani chakula kinauliza nahitaji chakula gani? Mhudumu katoka hapa sasa hivi nimemwambia aniletee chakula, kimefika tena kinaniuliza nataka chakula gani!" Dylan akatania.

"Hivi wewe..." Fetty akashangaa huku anatabasamu.

"Ahahahah... au hujui kwamba wewe ni chakula?"

"Acha mambo yako. Nina... kazi za kufanya, niambie basi..." Fetty akaomba.

Dylan alipendezwa sana na ustaarabu wa Fetty. Akamwambia chakula cha kawaida tu, kisha Fetty akamfatia. Wakati Fetty anarejea nacho, Dylan alipigiwa simu na Bosco, ambaye alimjulisha kwamba kuna mpiganaji ametoa 'challenge' ya kupigana na Killmonger kwa kuweka dau kubwa sana kutoka kwa wadhamini wake. Fetty akamwekea Dylan chakula mezani, naye Dylan akamwonyeshea kwa midomo ishara ya 'asante,' naye Fetty akarudia kazi zake zingine akimwacha Dylan anaongea na simu.

Bosco alimshawishi sana Dylan akubali maana alikuwa na uhakika angeshinda tu, lakini Dylan akakataa na kusema awapige chini. Bosco akamwambia nafasi hiyo iko wazi mpaka kufikia saa 4 usiku, hivyo ikiwa angebadili mtazamo wake amshtue tu; na alimsihi afanye hivyo. Dylan alijua jamaa yake huyo alipenda na kujali tu pesa ambazo angepata, hivyo akampotezea na kuendelea na msosi.

Mpaka anamaliza kula, Fetty hakuwa ameonekana sehemu hiyo tena, ikionekana alikuwa anafanya kazi fulani huko nyuma. Hivyo akanyanyuka na kumfata mhudumu mwingine, kisha akampa noti ya elfu kumi na kumwambia ampatie Fetty. Akaondoka na kuingia kwenye gari lake, naye akamtumia Fetty ujumbe huu: Asante kwa chakula, chakula wewe 😉. Kisha akaondoka hapo na kuelekea kwenye jengo la mgahawa wake mpya ili kuuangalia.


★★★


Baadae alirudi nyumbani, akiwa hana jambo lingine la kufanya kule kwenye kampuni, naye akaanza kufanya mazoezi yake ya viungo mpaka alipotosheka. Akausafisha mwili wake vizuri na kuketi tu chumbani kwake, akipitia jambo fulani kwenye simu. Ilikuwa ni mida ya saa 12 na nusu jioni sasa, naye akafikiria kumshtua Harleen. Lakini wazo bora hata zaidi likamwingia. Kwa nini asiende hotelini kule kabisa ili akamfanyie 'surprise?' Alijua huenda asingemkuta, lakini kama ingekuwa hivyo basi angeenda hospitalini kabisa ili kumwona. Harleen alikuwa ameanza kumwingia vyema Dylan, kwa hiyo akaona hii ingekuwa njia nzuri ya kunogesha mambo kati yao; ijapokuwa binti alisema mambo yalikuwa mengi kwa leo, lakini hata kumwona tu ingetosha.

Akavaa viatu haraka na kwenda kwenye gari lake. Dakika hazikupita nyingi sana naye tayari akawa amefika nje ya Queen Hotel. Akashuka na kuelekea kule juu, akiwa na hamu kubwa sana ya kuona itikio la mrembo wake wakati angemwona ghafla yuko hapo. Kabla hajafika mlangoni kwa Harleen, alipata ujumbe kutoka kwa Fetty, aliyesema asante pia kwa shukrani ya Dylan ya chakula. Dylan akamtumia ujumbe wa utani kuwa hapa alipo anaenda kukamua chakula kingine, hivyo angemshtua baadae tena. Fetty akakubali, kisha Dylan akaendelea kwenda mpaka kwenye mlango wa bibie. Akaugonga na kusubiri ufunguliwe, akitumaini Harleen yuko ndani, na baada ya sekunde chache, ukafunguliwa.

Ilikuwa ni Harleen, akiwa amevaa kigauni kirefu na chepesi sana kilichoonyesha viungo vyake vya mwili kwa mbali. Alishangaa kumwona Dylan hapo, naye Dylan akawa anatabasamu tu kwa kuwa alitegemea itikio hilo la mshangao.

"D....Dylan..."

Harleen akaita kwa sauti ya chini huku akiwa bado ametoa macho. Dylan akaingia ndani na kumfata moja kwa moja mdomoni mwake, akimpiga denda ya furaha. Harleen alikuwa anaipokea busu ya Dylan, lakini kwa njia fulani kama vile alikuwa anataka kuiepuka. Kisha akajitoa mdomoni kwa Dylan na kurudi nyuma kidogo. Dylan akawa anamwangalia kwa matamanio.

"Dylan... mbona uko hapa?" Harleen akauliza.

"Surprise!" Dylan akajibu kwa shauku.

Harleen akageukia upande wa mlango wa kuingilia kwenye chumba chenye kitanda, kisha akamtazama tena Dylan kwa uso wenye kuonyesha wasiwasi.

"Dylan... now's not a good time... tutaonana kesho..." Harleen akasema kwa sauti ya chini.

"Unamaanisha nini?" Dylan akauliza kwa kutoelewa.

Harleen akageukia tena upande ule na kumwangalia tena Dylan kwa uso wenye hofu. Dylan akaangalia huko pia na kumtazama tena.

"Is there a problem?" Dylan akauliza.

"Aam..." Harleen akashindwa kuongea.

"Oh! Aunty Beatrice yuko hapa?" Dylan akauliza kwa kunong'oneza.

Harleen akawa kama anatikisa kichwa kukubali, na hapo hapo sauti ikasikika ikiuliza, "Harleen, vipi ni nani?"

Dylan alishtushwa na sauti hiyo. Alishtuka kwa sababu ilikuwa ni ya mwanaume ambaye hakutambua ni nani. Akabaki kumwangalia Harleen kwa njia ya kawaida lakini kimshangao, huku Harleen akimtazama kwa wasiwasi mno.



★★★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★★★


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi kali ya DYLAN. Waweza ipata yote kwa sh. 2000 tu WhatsApp.

WhatsApp no: +255 787 604 893 (hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo utaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

WhatsApp no: +255 787 604 893
(Hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo unaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)


★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SITA

★★★★★★★★★★★★

"Ulijuaje hilo?" Dylan akauliza kwa utulivu.

"Me ni daktari Dylan. Walijitahidi kuficha origin ya tatizo kwa sababu nisizozijua, lakini kwa kuangalia tu jinsi thrombocytopenia ilivyokuwa severe mwilini mwake nilitambua haraka," Harleen akasema.

"Dah, madaktari nyie na hayo madude yenu sijui thomborositepainia, huwa mnayawekaje vichwani?" Dylan akauliza kiutani.

Harleen akacheka kidogo kisha akasema, "Samahani, its a force of habit."

Dylan akatulia kidogo kisha akasema, "Ndiyo, uko sahihi. Mama alikunywa sumu... lakini mpaka leo sijajua ilikuwa ni kwa nini."

"Pole Dylan..."

"Ahah... asante. Unajua... ukweli ni kwamba bado niko nyumbani kwa sababu nahofia huenda hata akaingiwa na mood swing inayoweza kusababisha atende kwa njia mbaya kama kipindi hicho... ijapokuwa siwezi kumwangalia muda wote lakini angalau kuwepo pale kunanipa ahueni. Mara nyingi nilipokuwa Brazil, niliwaza sana ingekuwa vipi kama... ingetokea mama angekufa kipindi hicho halafu sikuwa nimekaa naye kwa muda mrefu vile. Kwa hiyo sasa hivi najitahidi kufidishia muda huo," Dylan akaeleza kwa hisia.

Harleen akasogeza mdomo wake kwenye mdomo wa Dylan na kuanza kumpiga busu ya faraja.

Wakaendelea kudendeshana kwa sekunde chache, nao wote wakasikia simu ya Harleen ikiita kutokea sehemu ya sebule. Dylan akaivunja busu taratibu na kumwambia Harleen angemfatia simu yake pamoja na zile juice ili wanywe, lakini Harleen akawa anakataa na kumng'ang'ania ili waendelee na mapenzi yao. Dylan akasisitiza kuifata simu kwa kuwa iliendelea kuita karibia mara 7, hivyo alijua huenda ingekuwa muhimu. Hatimaye akafanikiwa kumkimbia mrembo huyo na kwenda kuifata akiwa bila nguo, na alipoichukua ilikuwa ikiita huku jina la aliyepiga likisomeka "Ray."

Akarejea kwa Harleen na kumpa huku anamwambia ni Ray ndiyo anapiga. Harleen alikuwa amejilaza kwa pozi lenye kuamsha hisia za mwanaume endapo angemtazama kwa uvutio lakini baada tu ya Dylan kusema jina "Ray," akaketi vizuri na kwa umakini akaichukua simu yake. Dylan yeye akawa anatabasamu tu kwa furaha, naye Harleen akatoa tabasamu la kujilazimisha, kisha Dylan akaelekea sebuleni tena. Harleen akapokea simu yake lakini alizungumza kwa sauti ya chini sana kiasi kwamba hata Dylan hangeweza kujua ikiwa alipokea simu. Mwanaume akarudi akiwa na zile juice mikononi na kupanda nazo kitandani, na hapo Harleen akaagana na aliyekuwa akiongea naye kisha kuiweka simu pembeni.

Dylan akampa juice moja, naye akabaki na moja, kisha wakagongeana glasi na kuanza kunywa taratibu huku wanatazamana kwa hisia. Kisha kwa utundu, Dylan akaisogeza glasi yake yenye juice karibu na kifua cha Harleen ambacho kilikuwa wazi, kisha akakimiminia juice kidogo iliyolowanisha kifua chake kwa michirizi. Harleen alishtuka kiasi na kuachama mdomo wake, naye Dylan akacheka tu. Kisha binti akaiweka juice yake pembeni na kuichukua ya Dylan pia na kuiweka pembeni. Dylan bila kuchelewa akakisogelea kifua cha bibie na kuanza kukilamba kwa wororo; akizipa umakini sehemu ambazo michirizi ya juice ilipita. (.........).

Wawili hawa waliurudia mchezo wao mtamu; (..........). Wote wakawa wameridhishwa na mmoja na mwenzake, na hapo wakalala pamoja na usingizi kuwapitia.

Dylan alikuwa wa kwanza kuamka, huku Harleen akiwa amelala pembeni yake kwa kuonekana amechoka. Jamaa akatabasamu na kumbusu kwenye shavu, kisha akaivuta simu yake Harleen aliyokuwa ameiweka pembezoni mwa kitanda na kuiwasha ili aangalie muda. Ilikuwa ni saa 2 usiku sasa, na wakati anataka kuirudisha alipoitoa, akaona ujumbe fulani kwenye kioo hicho cha simu uliovuta umakini wake. Ujumbe huu ulisomeka 'excited for tomorrow my dearest,' yaani 'nina hamu kubwa kwa ajili ya kesho mpendwa wangu.' Mtumaji wa ujumbe huo alikuwa ni Ray, naye Dylan akajua bila shaka ni yule yule jamaa aliyepiga muda ule. Hakujua ni nani, lakini akapotezea tu na kuiona kuwa jumbe ya kirafiki kutoka kwa mtu aliyefahamiana na bibie.

Akanyanyuka na kwenda kujimwagia maji, kisha akarudi chumbani na kuvaa nguo zake. Akamwangalia Harleen kwa upendezi sana, ambaye bado alikuwa amelala huku mwili wake ukiwa bila nguo, naye akamsogelea kitandani hapo na kumfunika vizuri kwa shuka. Akarudi sehemu ya sebule na kuchukua peni na karatasi kutoka kwenye daftari dogo, kisha akaandika ujumbe mfupi wa kumuaga mrembo huyo na kuuweka mezani. Aliona ni bora amwache apumzike, kwa sababu yeye alihitaji kwenda sehemu fulani haraka.

★★★

"Okay sawa. Hapana, iko ofisini....nikifika kesho nitaituma mapema wala usijali. Yeah... kila jambo liko safi kabisa. Okay asante sana. Kwa heri..."

Huyu alikuwa ni Dylan akiongea na mtu fulani kutokea upande mwingine wa jiji kwenye simu kuhusu masuala ya kazi. Alikuwa akiendesha gari bado baada ya kuondoka kwa Harleen, na sehemu aliyokuwa akielekea wakati huu ilikuwa ni kule mgahawa wake ulipokuwa. Alihitaji kwenda kuangalia mambo yako vipi kwa kuwa ulikuwa karibu sana kukamilika kwa kila jambo alilohitaji pale. Hakuwa ameweka simu sikioni wakati anaongea na mtu huyo, bali kifaa cha sikioni kilichounganishwa na simu yake (Bluetooth).

Akiwa anaendelea na safari yake hiyo, alipata kumwona mwanamke fulani pembezoni mwa barabara akitembea kuelekea upande alikoelekea yeye. Mwonekano wa mwanamke huyo haukuwa mgeni sana kwa Dylan, kwa kuwa nguo aliyovaa ilifanana pia na nguo ya yule dada mhudumu wa ule mgahawa walikoenda na Harleen mchana kwa ajili ya chakula. Kwa hiyo alivuta umakini wake kwa sababu moja kwa moja alimfikiria dada yule. Dylan akampita na kumwangalia kupitia kioo cha pembeni (side mirror) ya gari, na sasa akawa amehakiki kuwa ilikuwa ni huyo huyo dada baada ya kuuona uso wake kupitia kioo hicho. Akaegesha gari upande huo wa barabara na kusubiri afike usawa wake.

Akashusha na kioo cha mlango wa gari, na mwanamke huyu akawa amefika usawa huo.

"Hey..." Dylan akaita.

Dada huyo akasimama na kumwangalia kupitia uwazi wa mlango wa gari. Alikuwa ameweka uso wa kawaida tu, huku Dylan akitabasamu.

"Mambo?" Dylan akamsalimu.

"Poa tu," akajibu huku naye akitabasamu.

"Unanikumbuka?" Dylan akauliza.

Huyo dada akatikisa kichwa kukubali.

"Unaelekea wapi... nyumbani?" Dylan akauliza.

"Ndiyo."

"Aaaa... unaishi maeneo ya huko mbele?"

"Eee."

"Kama vipi panda nikupe lifti maana naelekea upande huo pia."

"A... ahah..hapana... asante. Ninaenda tu hapo mbele kuchukua bajaji..."

"Bajaji ya nini sasa wakati ndinga kali hii hapa?"

"Mhm... kwani nani amekwambia me nina uhitaji wa kupanda ndinga?"

"Oh... samahani... sikumaanisha vibaya. Yaani... nimeona tu nikusaidie kidogo..." Dylan akasema kwa upole.

"Wala usijali. Mimi nitapanda tu bajaji... na... wewe si kuna sehemu unaenda au?"

"Ndiyo, lakini kama unaelekea upande huo haina shida... nitakupeleka halafu kwanza... itaku-save hela..."

"Haina shida. Me..."

"Come on, usiwe hivyo. Me sitafuni watu bwana."

Dada huyo akacheka kidogo.

"Ingia twende. Halafu pia... gari langu linanukia vizuri kuliko bajaji... kwa hiyo humu ni bora," Dylan akatania.

Mwanamke huyu akamwangalia kwa sekunde chache, kisha akafungua mlango wa mbele na kuingia ndani ya gari. Dylan alifurahi, naye akaliingiza gari barabarani tena na kuendelea na mwendo.

"Utakuwa unanielekeza eti?" Dylan akamwambia.

"Kwani unanipeleka hadi nyumbani?"

"Sawa tu, kwa kuwa umeniomba."

"Ahahah... wewe ni mtu wa wapi?" dada huyo akauliza.

"Kwa nini?"

"Unavyoongea... hiyo lafudhi siyo ya kitanzania."

"Ahahah... Me mbona mtanzania? Mzawa kabisa."

"Kabila gani?"

"Hayo masuala huwa sina habari nayo kabisa," Dylan akasema.

"Mhm..." dada huyo akaguna na kutazama mbele.

"Jina lako ni nani?" Dylan akauliza.

"Niambie la kwako kwanza."

"Ninaitwa Dylan."

"Aaaa... sawa."

"Na wewe unaitwaje?"

“Naitwa Fetty," akajibu.

"Oooh... msukuma eeh?" Dylan akatania.

"Hapana. Kwa nini umefikiri me msukuma?"

"Well... jina lako hilo bila shaka limetolewa kwenye Fatuma kama sikosei," Dylan akatania tena.

"Ahaaah... Kwa hiyo wooote wanaoitwa Fatuma ni wasukuma?"

"Ndiyo navyojua. Labda kama mambo yamebadilika sasa hivi lakini..."

"Ingia hapo hivi," Fetty akamkatisha ili kumwelekeza pa kuelekea.

"Kwa hiyo umefanya kazi pale kwa muda mrefu?" Dylan akauliza.

"Siyo sana," Fetty akajibu kifupi.

"Sawa."

Dylan alikuwa ametambua mwanamke huyu alikuwa mwenye utu fulani wa kivyake sana. Alitaka kujua mengi kumhusu, na hili lilichochewa na jinsi walivyoangaliana leo wakati wapo kwenye ule mgahawa.

"Unakaa na wazazi nyumbani?" Dylan akauliza.

"Hapana, nimepanga," Fetty akajibu.

"Aaaa... okay. Nilipenda jinsi ulivyokuwa unaniangalia leo pale unapofanyia kazi, na sijui ni kwa nini..." Dylan akasema.

Fetty akamwangalia na kuachia tabasamu. Dylan pia akatabasamu baada ya kuona amemfurahisha binti.

"Nilifikiri ni kama vile hukutosheka na maji yaliyonimwagikia kwa hiyo nikahisi labda unataka kuniongezea," Dylan akatania.

"Ahahahah... hamna hata. We umeona vibaya," Fetty akakanusha.

"Mmmm hamna bwana, nilikuona vizuri kabisa..."

"Kwani hupendi kuangaliwa?"

"Nisingetabasamu ikiwa ningekuwa sipendi."

Fetty akatabasamu na kuangalia mbele.

"Kwa hiyo... ndo' sipati jibu au?" Dylan akauliza kichokozi.

"Mwenzangu nayefanya naye kazi pale alikuwa anakusifia sana... anasema wewe mzuri," Fetty akajibu.

"Hahah... kwa hiyo ukawa unaniangalia sana kwa ajili yake au?"

"Hamna. Alikuwa anataka nimsaidie ili muongee maana alikuwa anaona aibu... na pia alikuwa anamwogopa yule dada uliyekuja naye."

"Hivi kweli... yaani kashaniona niko na mtu mwingine halafu anakushurutisha uongee nami... kwa nini asingefanya hivyo yeye mwenyewe? Anaogopa nini wakati hii nchi huru bwana?"

"Kata kona hapo hivi... Me mwenyewe nilimwambia anajisumbua tu maana mnaonekana ni watu wenye hela na... yule ni mke wako sijui?" Fetty akasema.

"Hapana... siyo mke wangu."

"Ni girlfriend?"

"Mmmm... hatujafikiria kuweka mambo kati yetu kwa njia hiyo rasmi zaidi lakini ni mtu wangu wa karibu sana."

"Sa' si ndiyo girlfriend au?"

"Ahahah... ndiyo. Ukisema kwa njia hiyo ni kweli."

Fetty akaangalia chini na kusema, "Ni mzuri."

Dylan alihisi kitu fulani. Yaani ni kama Fetty alikuwa anaficha jambo lililohusiana na yeye baada ya kumwambia ana girlfriend, hivyo akaona amchokoze kwa utundu.

"Ndiyo ni mzuri... lakini siyo kama wewe."

Fetty akageuka na kumtazama Dylan kwa makini, huku jamaa akiangalia mbele tu kwa utambuzi wa kwamba binti alikuwa anamwangalia. Akajua bila shaka maneno hayo yalimwingia mtoto kwa njia yenye kusisimua. Akamgeukia pia, na wote wakaangaliana machoni kwa sekunde chache.

"Fetty..." Dylan akaita.

Fetty akaendelea tu kumwangalia.

"...tumekaribia kufika au bado?"

Baada ya Dylan kuuliza hivyo, Fetty akawa kama ameshtuka kutokana na kuzubaa.

"Ai... simama, tumepapita," akasema kwa uharaka.

Dylan akasimamisha gari huku akitabasamu. Fetty akashuka ili arudi kwa miguu, naye Dylan akashuka pia na kumwahi.

"Wewe vipi... mbona faster hivyo?" akamuuliza.

"Aa... asante sana. Nimefika tayari ni hapo tu hivi naingia," Fetty akajibu.

"Sa ndo' unaondoka hata kuaga hamna jamani?"

Fetty akabaki kumwangalia tu usoni.

"Ahahah... usiniogope Fetty. Mimi nataka tu tuwe marafiki. Sijui ni kwa nini lakini napendezwa nawe sana."

"Aliyekwambia nakuogopa nani?" Fetty akauliza.

"Sasa kinachokufanya ukimbie ni nini?"

"Nilikuwa nawahi..."

"Siyo tabia nzuri," Dylan akajifanya kaudhika.

"Sawa. Nisamehe," Fetty akasema.

"Nipe namba yako ndiyo nitakusamehe," Dylan akamwambia huku anatabasamu kwa utundu.

Fetty akatabasamu pia na kuanza kumtajia namba zake. Dylan akaziandika, kisha akamshukuru na kumwacha aelekee kwake. Akarejea kwenye gari na kuanza kuelekea kwenye mgahawa wake akijihisi furaha fulani ambayo ilichochewa sana na mwanamke huyo mwenye kuvutia.

★★★

Siku iliyofuata, Dylan alikwenda kwenye kampuni kama kawaida kwa ajili ya kazi. Sasa alikuwa anafurahia zaidi kuwa ofisini kuliko mwanzo, kwa kuwa mambo mengi aliyofanya yalikuwa yanaleta matokeo mazuri aliyotarajia, na hata ingawa wengi walimsifia, hakujigamba kwa kiburi. Ilipofika mida ya mchana, alimpigia simu Harleen mara kadhaa lakini hakupokea. Akamtumia ujumbe kuwa alitaka kwenda kupata chakula kwenye ule mgahawa wa jana pamoja naye ikiwa alikuwa na nafasi, au kama alikuwa amebanwa sana basi haingekuwa na shida.

Baadae, Harleen alimjibu kwa ujumbe kuwa hangeweza kwa kuwa alibanwa sana leo, hivyo wangeenda siku nyingine pamoja. Dylan alipomuuliza ikiwa angepata nafasi ya kukutana baadae zaidi, Harleen alikanusha na kusema haingewezekana kwa leo, na angemjulisha endapo angepata nafasi. Dylan kama Dylan hakuhisi chochote kwa njia mbaya, akamuaga tu na kuendelea na mambo yake, kisha akaondoka kuelekea kwenye ule mgahawa.

Kichwani kwake aliwaza kwenda pale hasa ili kumwona rafiki yake mpya, Fetty. Hakuwa amemtafuta kwa simu tokea usiku wa jana alipoipata namba yake, kwa hiyo aliwaza pia kwamba angetafuta nafasi ya kuongea naye kidogo. Alifika pale na kwenda moja kwa moja mpaka mezani, kisha mwanamke fulani akaja alipo, naye akiwa ni muhudumu wa hapo.

"Ungependa kupata chakula gani kaka?" akamuuliza.

"Ningependa uniitie Fetty tafadhali. Asante," Dylan akajibu.

Mwanamke huyo akashangaa kidogo, lakini akaona tu atii ijapokuwa halikuwa jibu alilotegemea. Sekunde kadhaa zikapita, naye Fetty akaonekana akija upande wa Dylan. Dylan alitabasamu kwa furaha, naye Fetty akashindwa kujizuia kutabasamu. Jamaa alimwangalia jinsi alivyokuwa na mwili mzuri sana, na wakati huu Fetty alikuwa amevaa T-shirt ya kijani na suruali ya jeans ya samawati (blue) yenye kubana ambayo ilichoresha hips zake vyema. Akafika hapo karibu na kumsalimu.

"Mbona kimya?" Dylan akamuuliza.

"Unamaanisha nini?" Fetty akauliza pia.

"Hujanitafuta kwa simu!"

"Aliyechukua namba si wewe? Ningekutafuta vipi wakati hukunipa yako?"

"Shida ndiyo hiyo... kwa nini hukuniomba?" Dylan akauliza kimasihara.

Fetty akacheka kwa chini na kutikisa kichwa. Dylan akatabasamu pia.

"Unahitaji chakula gani?" Fetty akamuuliza.

"Ish... yaani chakula kinauliza nahitaji chakula gani? Mhudumu katoka hapa sasa hivi nimemwambia aniletee chakula, kimefika tena kinaniuliza nataka chakula gani!" Dylan akatania.

"Hivi wewe..." Fetty akashangaa huku anatabasamu.

"Ahahahah... au hujui kwamba wewe ni chakula?"

"Acha mambo yako. Nina... kazi za kufanya, niambie basi..." Fetty akaomba.

Dylan alipendezwa sana na ustaarabu wa Fetty. Akamwambia chakula cha kawaida tu, kisha Fetty akamfatia. Wakati Fetty anarejea nacho, Dylan alipigiwa simu na Bosco, ambaye alimjulisha kwamba kuna mpiganaji ametoa 'challenge' ya kupigana na Killmonger kwa kuweka dau kubwa sana kutoka kwa wadhamini wake. Fetty akamwekea Dylan chakula mezani, naye Dylan akamwonyeshea kwa midomo ishara ya 'asante,' naye Fetty akarudia kazi zake zingine akimwacha Dylan anaongea na simu.

Bosco alimshawishi sana Dylan akubali maana alikuwa na uhakika angeshinda tu, lakini Dylan akakataa na kusema awapige chini. Bosco akamwambia nafasi hiyo iko wazi mpaka kufikia saa 4 usiku, hivyo ikiwa angebadili mtazamo wake amshtue tu; na alimsihi afanye hivyo. Dylan alijua jamaa yake huyo alipenda na kujali tu pesa ambazo angepata, hivyo akampotezea na kuendelea na msosi.

Mpaka anamaliza kula, Fetty hakuwa ameonekana sehemu hiyo tena, ikionekana alikuwa anafanya kazi fulani huko nyuma. Hivyo akanyanyuka na kumfata mhudumu mwingine, kisha akampa noti ya elfu kumi na kumwambia ampatie Fetty. Akaondoka na kuingia kwenye gari lake, naye akamtumia Fetty ujumbe huu: Asante kwa chakula, chakula wewe . Kisha akaondoka hapo na kuelekea kwenye jengo la mgahawa wake mpya ili kuuangalia.


★★★


Baadae alirudi nyumbani, akiwa hana jambo lingine la kufanya kule kwenye kampuni, naye akaanza kufanya mazoezi yake ya viungo mpaka alipotosheka. Akausafisha mwili wake vizuri na kuketi tu chumbani kwake, akipitia jambo fulani kwenye simu. Ilikuwa ni mida ya saa 12 na nusu jioni sasa, naye akafikiria kumshtua Harleen. Lakini wazo bora hata zaidi likamwingia. Kwa nini asiende hotelini kule kabisa ili akamfanyie 'surprise?' Alijua huenda asingemkuta, lakini kama ingekuwa hivyo basi angeenda hospitalini kabisa ili kumwona. Harleen alikuwa ameanza kumwingia vyema Dylan, kwa hiyo akaona hii ingekuwa njia nzuri ya kunogesha mambo kati yao; ijapokuwa binti alisema mambo yalikuwa mengi kwa leo, lakini hata kumwona tu ingetosha.

Akavaa viatu haraka na kwenda kwenye gari lake. Dakika hazikupita nyingi sana naye tayari akawa amefika nje ya Queen Hotel. Akashuka na kuelekea kule juu, akiwa na hamu kubwa sana ya kuona itikio la mrembo wake wakati angemwona ghafla yuko hapo. Kabla hajafika mlangoni kwa Harleen, alipata ujumbe kutoka kwa Fetty, aliyesema asante pia kwa shukrani ya Dylan ya chakula. Dylan akamtumia ujumbe wa utani kuwa hapa alipo anaenda kukamua chakula kingine, hivyo angemshtua baadae tena. Fetty akakubali, kisha Dylan akaendelea kwenda mpaka kwenye mlango wa bibie. Akaugonga na kusubiri ufunguliwe, akitumaini Harleen yuko ndani, na baada ya sekunde chache, ukafunguliwa.

Ilikuwa ni Harleen, akiwa amevaa kigauni kirefu na chepesi sana kilichoonyesha viungo vyake vya mwili kwa mbali. Alishangaa kumwona Dylan hapo, naye Dylan akawa anatabasamu tu kwa kuwa alitegemea itikio hilo la mshangao.

"D....Dylan..."

Harleen akaita kwa sauti ya chini huku akiwa bado ametoa macho. Dylan akaingia ndani na kumfata moja kwa moja mdomoni mwake, akimpiga denda ya furaha. Harleen alikuwa anaipokea busu ya Dylan, lakini kwa njia fulani kama vile alikuwa anataka kuiepuka. Kisha akajitoa mdomoni kwa Dylan na kurudi nyuma kidogo. Dylan akawa anamwangalia kwa matamanio.

"Dylan... mbona uko hapa?" Harleen akauliza.

"Surprise!" Dylan akajibu kwa shauku.

Harleen akageukia upande wa mlango wa kuingilia kwenye chumba chenye kitanda, kisha akamtazama tena Dylan kwa uso wenye kuonyesha wasiwasi.

"Dylan... now's not a good time... tutaonana kesho..." Harleen akasema kwa sauti ya chini.

"Unamaanisha nini?" Dylan akauliza kwa kutoelewa.

Harleen akageukia tena upande ule na kumwangalia tena Dylan kwa uso wenye hofu. Dylan akaangalia huko pia na kumtazama tena.

"Is there a problem?" Dylan akauliza.

"Aam..." Harleen akashindwa kuongea.

"Oh! Aunty Beatrice yuko hapa?" Dylan akauliza kwa kunong'oneza.

Harleen akawa kama anatikisa kichwa kukubali, na hapo hapo sauti ikasikika ikiuliza, "Harleen, vipi ni nani?"

Dylan alishtushwa na sauti hiyo. Alishtuka kwa sababu ilikuwa ni ya mwanaume ambaye hakutambua ni nani. Akabaki kumwangalia Harleen kwa njia ya kawaida lakini kimshangao, huku Harleen akimtazama kwa wasiwasi mno.



★★★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★★★


Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi kali ya DYLAN. Waweza ipata yote kwa sh. 2000 tu WhatsApp.

WhatsApp no: +255 787 604 893 (hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo utaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)
Jaman jaman elton ngoja nikufate tu
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

ILIPOISHIA.....

Harleen anashangaa baada ya kufungua mlango na kumwona Dylan akiwa amesimama hapo. Dylan akaingia ndani na kumfata moja kwa moja mdomoni mwake, akimpiga denda ya furaha. Harleen alikuwa anaipokea busu ya Dylan, lakini kwa njia fulani kama vile alikuwa anataka kuiepuka. Kisha akajitoa mdomoni kwa Dylan na kurudi nyuma kidogo.

"Dylan...mbona uko hapa?" Harleen akauliza.

"Surprise!" Dylan akajibu kwa shauku.

Harleen akageukia upande wa mlango wa kuingilia kwenye chumba chenye kitanda, kisha akamtazama tena Dylan kwa uso wenye kuonyesha wasiwasi.

"Dylan...now's not a good time...tutaonana kesho..." Harleen akasema.

"Unamaanisha nini?" Dylan akauliza kwa kutoelewa.

Harleen akageukia tena upande ule na kumwangalia tena Dylan kwa uso wenye hofu. Dylan akaangalia huko pia na kumtazama tena.

"Is there a problem?" Dylan akauliza.

"Aam..." Harleen akashindwa kuongea.

"Oh! Aunty Beatrice yuko hapa?" Dylan akauliza kwa kunong'oneza.

Harleen akawa kama anatikisa kichwa kukubali, na hapo hapo sauti ikasikika ikiuliza, "Harleen, vipi ni nani?"

Dylan alishtushwa na sauti hiyo. Alishtuka kwa sababu ilikuwa ni ya mwanaume ambaye hakutambua ni nani. Akabaki kumwangalia Harleen kwa njia ya kawaida lakini kimshangao, huku Harleen akimtazama kwa wasiwasi mno.

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SABA

★★★★★★★★★★★★

"Dylan..." Harleen akaita lakini akashindwa kuongea.

Dylan akawa anamtazama tu kama mtu aliyezubaa, na hapo akatoka mwanaume fulani mweupe, aliyekuwa na mwili uliokaribiana na wa Dylan kwa upana. Alikuwa na nywele fupi zilizonyolewa vizuri, na ndevu nyingi kiasi zilizochongwa vyema kutokea kwenye timba. Alikuwa amevalia vest nyeupe na suruali nyepesi, naye akamwangalia Dylan kwa umakini.

"Habari yako?" mwanaume huyo akamsalimu Dylan.

"Ni nzuri. Vipi wewe?" Dylan akauliza kirafiki.

"Fresh. Mgeni wako?" mwanaume huyo akamuuliza Harleen.

Harleen alikuwa amepandwa na presha, lakini akajitahidi kujidhibiti.

"Ndiyo... Aam...Alex, Dylan. Dylan... Alex," akajibu na kuwatambulisha.

"Ooh...huyu ndiyo Dylan kumbe?" Alex akauliza.

"Ndiyo," Harleen akajibu.

"Okay. Nimefurahi kukutana nawe bro," Akex akamwambia Dylan.

Alimsogelea na kumpa mkono, naye Dylan akatoa wake na kumpa ili waitingishe pamoja kwa utambulisho.

"Harleen aliniambia kukuhusu. Wewe ni rafiki yake wa utotoni," Alex akasema.

"Ndiyo, ni mimi. Nimefurahi pia kukujua Alex," Dylan akajibu kistaarabu.

"Please...niite tu Ray. Harleen anapenda kuniita kwa jina langu la mwanzo ila nimeshazoea la mzee," Alex akasema kiutani.

"Aaaa...sawa sawa, Ray," Dylan akasema.

Hapa Dylan akawa ametambua kuwa bila shaka huyu ndiyo Ray aliyempigia simu Harleen jana. Aliingiwa na hisia za kujiona mpumbavu sana kutohisi lolote baya kumwelekea Harleen, na sasa akajikuta kwenye mzunguko wa mapenzi (love triangle).

"Aam...Harleen... utamwambia basi aunty Beatrice kuhusu ile ishu sawa?" Dylan akatokeza hadithi ya uwongo ili Alex asihisi chochote.

Harleen, kwa wasiwasi, akasema, "S..sawa. Nitamwambia."

"Okay. Samahani kwa...ahah..kuja bila taarifa. Nilikuwa nampitishia huyu ujumbe," Dylan akasema kwa kujikaza.

"Oh usijali kabisa," Alex akajibu.

"Kwa hiyo...we ndo' shem au siyo?" Dylan akauliza kwa njia ya masihara, lakini alikuwa anachimba ukweli.

"Ahahah...yeah. Nimekuja leo tokea South Africa kumtembelea huyu sweetheart," Alex akasema huku akikibana kiuno cha Harleen kwake kwa upendo.

Harleen akatoa tabasamu la bandia akijifanya mambo yako sawa, lakini mapigo yake ya moyo yalidunda kwa nguvu sana.

"Okay sawa. Basi, wacha me niende. Tutaonana...wakati mwingine," Dylan akasema.

"Sawa sawa. Harleen mbona uko kimya? Anaaga," Alex akamwambia.

"A..aa..sawa. Nita...nitakujulisha..nitamjulisha mama..kuhusu ujumbe," Harleen akasema kwa kubabaika.

"Haya, usiku mwema kwenu," Dylan akawaaga na kuondoka hapo upesi.

Alirudi kwenye gari lake akiwa amevunjika moyo kwa kiasi fulani. Lilikuwa ni jambo ambalo hakutegemea kutoka kwa Harleen, hasa kwa sababu alikuwa ni rafiki yake wa muda mrefu pia. Aliondoka eneo hilo na kuendelea kuendesha gari bila kuwa na sehemu maalumu ya kwenda. Alihisi hasira pia, naye alitaka kufanya jambo fulani ili azipunguze kwa kuwa alihisi huenda hata angefanya jambo baya.

Kisha wazo moja likaja. Alikumbuka kwamba Bosco alimwambia kuhusu 'challenge' ya mpiganaji fulani dhidi yake leo usiku, na nafasi bado ilikuwepo ya kukubali au kukataa moja kwa moja mpaka kufikia saa 4. Ilikuwa saa 2 kasoro sasa, hivyo akasimamisha gari na kumpigia simu Bosco kumjulisha kuwa alikubali challenge hiyo. Bosco akafurahi na kusema angesaini karatasi mapema ili yeye akifika kule show ipigwe kiaina.

Wazo la Dylan lilikuwa ni kwenda kuzipunguza hasira zake kule, siyo kupata pesa. Akaelekea kule upesi na kujiandaa kwa ajili ya pambano hilo ambalo lilisubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa mchezo huo haramu kwenye mtandao. Dylan, akijulikana kama Killmonger hapo, alivaa mask yake na kuingia kuziruka pamoja na jamaa yule aliyejiita The Crusher. Huyu jamaa alikuwa ametoa challenge hiyo kwa kuwa siku ile Dylan alimfumua vibaya pamoja na kwamba alikuwa amechoka, hivyo ni kama alikuwa anataka kumlipa, kwa kuwa alijisifu kuwa usiku huu angehakikisha anamwonyesha Killmonger nini maana ya jina lake The Crusher, yaani mvunjaji.

Wala hata jina lake halikumtisha Dylan, kwa kuwa pambano lilianza kwa The Crusher kupigwa vibaya na Killmonger mpaka akaishiwa nguvu. Yaani usiku huu Dylan alihakikisha haguswi sehemu hata moja, na ijapokuwa alizoeleka kupigana kwa mtindo wa masihara, sasa alihakikisha anatia maumivu mengi kwenye mwili wa mwanaume huyo. Alimpiga sana, hata iliposemwa tayari ameshinda, bado akaendelea kumpiga tu na kusababisha azimie; hii ikiwa ni mara ya pili anamzimisha huyo mwanaume!

Ilibidi mabaunsa kadhaa waingie kumzuia asiendelee kwa kuwa kama angeendelea basi angemuua. Dylan/Killmonger akatoka hapo akiwa anapumua kwa hasira sana, na hakusemeshana na yeyote yule hadi akatokomea. Queen, na hata Bosco mwenyewe alishindwa kuelewa nini kilikuwa kimetokea, na baada ya hapo shindano hilo likasitishwa mpaka wakati mwingine.

★★★

Dylan akawa ofisini kwake siku iliyofuata akiendelea na kazi. Harleen alikuwa amepiga simu mara 28 tokea asubuhi, lakini Dylan hakupokea. Alimtumia jumbe nyingi sana pia, lakini Dylan hakusoma hata moja. Ilikuwa ni kama haoni na hasikii, naye alikuwa mbali mno kwenye kujali tena kwamba Harleen angehisije. Dylan alikuwa ni mtu makini sana ilipokuja kwenye suala la mapenzi, na ndiyo maana hakuwa kwenye uhusiano na yeyote tokea aliporudi nchini. Hata kule Brazil, alikuwa makini pia kutojiingiza kwenye masuala ya mapenzi kwa kuwa aliwahi kupitia hali zenye kuvunja moyo.

Lakini kwa Harleen alihisi labda kungekuwa na afadhali kwa sababu ni mtu aliyemjua tokea utotoni, na hata ingawa hawakuwa pamoja kwa muda mrefu, alimwamini kama rafiki wa karibu, hivyo hakufikiria angemfanyia vile. Wakati huu hakutaka kusikia maelezo yoyote kutoka kwa mwanamke huyo, kwa kuwa aliona yasingesaidia lolote lile zaidi tu ya kurudisha kumbukumbu zenye kukwaza.

Kwenye suala la marafiki pia, Dylan alikuwa aina ya mtu asiyejichanganya na watu hata kidogo, ijapokuwa alikuwa mtu mchangamfu na mwenye kufunguka sana. Mpaka anakuwa rafiki ya mtu ilihitajika awe amesitawisha upendezi wa hali ya juu kumwelekea mtu huyo; kama ilivyokuwa kwa Bosco na Fetty.

Baadae, aliondoka ofisini pale na kuelekea nyumbani. Karibia kila mtu kwenye kampuni ambaye alimwona Dylan angeweza kutambua kwamba jamaa hakuwa sawa siku hiyo kutokana na kuwa serious muda wote. Walikuwa wamemzoea kuwa mwanaume mchangamfu lakini thabiti, ila kwa wakati huu alikuwa amekaza mno.

Dylan aliporudi nyumbani alifanya zoezi kiasi tu, siyo kwa jinsi alivyozoea, kisha akaondoka kwenda tu kutembea. Bosco alikuwa amemtafuta baada ya kushangazwa na jinsi alivyotenda jana usiku, naye Dylan akasema tu alikuwa na stress ndiyo maana. Jamaa alimwambia pamoja na yote lakini bado pesa alipewa, hivyo ikiwa angeihitaji sehemu yake angemletea, lakini Dylan akamwambia abaki nayo tu.

Alikwenda sehemu ile ambayo mara ya kwanza ametoka na Harleen waliitumia kwa ajili ya mazoezi ya asubuhi. Uwanja huo ulikuwa bila watu wengi wakati huu, na walioonekana hapo walikuwa mmoja mmoja au wawili wawili waliokaa sehemu za mbalimbali, hivyo palikuwa pametulia sana. Akaketi kwenye jiwe dogo la msingi, akiwaangalia watu fulani wawili kwa mbele walioonekana kuwa wapenzi; wakipiga story zenye kufurahisha bila shaka. Kichwani kwake alikuwa anawaza vitu vingi; vilivyotokea, vinavyotokea, na huenda hata ambavyo vingetokea baadae. Kwenye suala la mapenzi alikuwa amefeli wapi? Mwili na sura nzuri anavyo, pesa anayo, akili ndiyo usiseme, kwa nini bado moyo wake ulitangishwa ilipokuja kwenye suala la mahusiano?

Giza lilikuwa linaanza kuingia, na sasa Dylan alipata wazo kwamba labda aondoke tu hapo na kwenda sehemu fulani apate kinywaji. Lakini kutoka kwenye mfuko wa suruali yake, alihisi simu yake ikitetemesha paja lake, kuashiria ujumbe mpya umeingia. Alijua bila shaka ingekuwa ni Harleen tena, na kufikia wakati huu alijua binti angekuwa na mambo mengi aliyotaka wazungumze pamoja; sanasana labda kujitetea. Hakuona haja ya kuendelea kukausha, hivyo akaona aweke usawaziko kidogo na kuitoa simu yake. Lakini aliyetuma ujumbe wakati huu hakuwa Harleen, bali Fetty. Akaachia tabasamu la mbali.

'uko wp?' ujumbe ulisomeka hivyo.

'niko kwenye kiwanja fulani huku town,' Dylan akamjibu kwa text.

'unafany nn?'

'nimekaa tu.'

'nije na mimi tukae wote?'

Dylan akatabasamu.

'sitakuwa mwenye kuburudisha sana leo,' Dylan akamwandikia.

"Acha uwongo," Fetty akasema.

Dylan aligeuka nyuma na kukuta Fetty amesimama hapo huku anamwangalia. Aliachia tabasamu na kusimama akishangaa kiasi kwamba hakuweza kuhisi uwepo wa mwanamke huyu nyuma yake.

"Hey... kumbe ulikuwa hapo muda wote!" Dylan akasema.

"Siyo muda wote. Nilikuwa napita kule nikakuona...ndiyo nikasogea," akajibu.

"Aaaa...unatokea kazini?" Dylan akauliza.

"Ndiyo."

"Sawa."

"Na wewe? Kwa nini uko hapa?"

"Napenda kuja hapa mara nyingi. Huwa nafanyiaga na mazoezi ya asubuhi huku," Dylan akajibu.

"Aaaa...lakini sasa hivi kwani unafanya mazoezi?"

"Aam... hapana. Nilitaka tu kuja kuituliza akili."

"Mh...ahahahah... Leo unaigiza mpole kweli utafikiri umepatwa na shida kuuubwa," Fetty akasema kiutani.

"Kwani me ni nani nisipatwe na shida?"

"Aah.. nyie watu huwa mna shida gani sasa pesa ikiwepo? Shida gani itakayokupata wewe labda? Au umetendwa nini? Ahahahah..." Fetty akamtania.

Dylan akaangalia chini kwa njia iliyoonyesha ana huzuni, nalo tabasamu la Fetty likafifia baada ya kuwa ametambua kuna kitu kinamsumbua jamaa.

"Ume...umetendwa?" Fetty akauliza.

"Siwezi kusema kwa njia hiyo lakini... ndiyo. Nimepatwa na shida fulani kimahusiano," Dylan akasema.

"Heh...pole mwaya. Yaani mabinti wa kibongo bwana," Fetty akasema.

"Kwani wewe ni binti wa wapi?"

"Wa bongo ndiyo lakini..."

"Sasa si ni wale wale tu!"

"Akha! Mimi hayo masuala huwa sina kabisa. Wengi waongo siku hizi...wanakuwa kwenye mapenzi ili kujichumia hela au kuondoa tu upweke."

"Ndiyo ni kweli. Najiona mjinga kwa sababu nahisi na mimi ni mmoja wa hao wanaotaka kuondoa upweke namna hiyo," Dylan akasema kwa hisia.

"Wewe si una hela? Upweke unatoka wapi?"

"Kuwa na pesa nyingi siyo chanzo kikuu cha furaha na kuridhika. Ni mahusiano ambayo hayana ubinafsi ndiyo humpa mtu furaha...lakinikama ulivyosema...watu wengi ni wabinafsi mno siku hizi," Dylan akamwambia.

"Ni...yule yule dada uliyekuja naye siku ile?" Fetty akauliza.

"Ndiyo. Nimegundua ghafla sana kwamba ana mwanaume mwingine."

"Hmmm...na uzuri wote ule! Mapenzi tuwaachie mnaoyaweza," Fetty akasema kiutani.

Dylan akatabasamu na kuuliza, "Ulikuwa unaenda nyumbani?"

"Ndiyo. Tena ni afadhali nimekuona ili unipe na lifti kabisa."

"Ahahah... leo bajaji hamna?"

"Bajaji ya nini wakati una gari linanukia vizuri zaidi ya mwanamke?" Fetty akatania tena.

Dylan alifurahishwa kwa kadiri kubwa na Fetty. Hakuwa ametegemea kufurahia chochote kwa leo, na sasa mwanamke huyu akawa ameweza kubadili matarajio yake. Walielekea kwenye gari na kuondoka eneo hilo, lakini Dylan hakumpeleka Fetty moja kwa moja kwake. Alimpeleka kwenye hoteli kubwa ya kifahari ili wapate mlo mzuri hapo. Fetty mwanzoni alikuwa anasita kwenda kwa sababu alijiona mchafu; ndiyo alikuwa tu ametoka kazini, lakini Dylan akamsisitizia kwenda bila kujali jinsi alivyojiona kwa kuwa yeye aliona yuko kawaida tu.

Fetty alifurahia sana kwa kuwa vyakula alivyoagiziwa vilikuwa vya gharama na vitamu mno. Walikula pamoja huku wanapiga story, hii ikimsahaulisha Dylan mawazo yake yenye kulemea aliyokuwa nayo. Walishiba na kuondoka hapo, Fetty akiwa ametunza nyama nyingi za kuku kwenye tishu na kuweka kwenye mfuko mdogo ili zikatumike nyumbani kwa kuwa Dylan aliagiza chakula kingi kupita maelezo.

Waliagana muda fulani baadae Dylan alipompeleka binti kule alipopanga, huku Fetty akimwambia kama vipi amtoe tena kesho, na wakati huu angehakikisha amependeza. Dylan alifurahi na kumkubalia, kisha akamwacha na kurudi zake nyumbani. Hakuhitaji kula alipofika kutokana na kushiba baada ya kula na Fetty, hivyo alienda zake chumbani na kuchukua hatua ya kwanza kumtafuta Harleen.

Wakati huu akili yake ilikuwa imetulia zaidi, hivyo akampigia, kisha akamwambia wakutane kesho kwenye sehemu fulani ili wazungumze; kama ataweza. Harleen alionekana kutaka kuongea naye zaidi, lakini Dylan akakatisha mazungumzo hayo na kuweka simu pembeni. Hakutaka kutenda kwa hasira kumwelekea Harleen ijapokuwa alikuwa amemuumiza hisia, hivyo akaona aingie tu kupumzika kwa ajili ya kesho.

★★★

Ilifika mida ya saa 9 alasiri siku iliyofuata, naye Dylan akawa amefika kwenye sehemu ile aliyokubaliana kukutana na Harleen. Alimkuta mwanamke huyu ameshafika; akiwa amevalia blauzi nyeusi iliyobana yenye mikono mirefu na suruali ya skinny nyeupe iliyombana vyema na kuchoresha umbo lake vizuri. Alikuwa amependeza sana usoni pia, naye Dylan akafika aliposimama na kumwangalia machoni kwa njia ya kawaida. Harleen akamkumbatia hapo hapo na kuanza kulia, huku Dylan akiwa ametulia tu bila kurudisha kumbatio la mrembo huyu. Kisha akamtoa kwake taratibu na kumfuta machozi, naye binti akawa analia kwa aibu tu.

"Harleen... nataka kujua ukweli. Alex...ni nani kwako?" Dylan akauliza kwa upole.

"Ni...ni mchumba...wangu," Harleen akajibu huku akilia.

Dylan akafumba macho kwa kusikitika sana. Harleen akaendelea kulia kwa huzuni.

"Basi inatosha Harleen... usilie," Dylan akamwambia kiupole.

"....Dylan... Dylan nisamehe...please my love...nisamehe..." Harleen akaanza kumwomba kwa huzuni.

"Harleen..."

"...haikuwa nia yangu kukufanyia vile...ni kwamba tu...Alex..." akashindwa kuendelea.

Dylan alikuwa anamtazama tu kwa makini.

"Dylan... mimi niko tayari kuachana na Alex kwa ajili yako...ninakupenda na ninaku..."

"Harleen... please. Inatosha, okay?" Dylan akamkatisha.

"Dylan..." Harleen akaendelea kulia.

"Mimi...sijui nisemeje yaani...kama ni kitu nachochukia kwenye mahusiano Harleen... ni betrayal. I've had a rough past when it came to relationships...nilifikiri kwako labda ningeweza kupata ahueni ila..."

"Dylan mimi ni wako...usikasirike mpenzi wangu kwa sababu...niko kwenye harakati za kuachana na Alex... hatujawa katika mwendo mzuri na mimi tayari nime..."

Dylan alitazama pembeni tu akiendelea kusikiliza jinsi Harleen alivyojitetea. Alitambua kwamba kwa kiasi fulani mwanamke huyu alikuwa mbinafsi, kwa kuwa kwa mambo mengi alichosema tu ilikuwa ni mimi, mimi, mimi. Ijapokuwa Harleen alikuwa mwenye kuvutia sana, mrembo, mwenye elimu ya juu, na mwenye sifa nyingi nzuri, jambo alilomfanyia Dylan lilikuwa limemaliza hamu yote mwanaume huyu aliyokuwa nayo kumwelekea. Ikabidi amshike na kumkumbatia ili atulie, kisha akaanza kuzungumza akiwa bado amemshikilia hivyo hivyo.

"Harleen... nimefurahi kwamba angalau nime-share jambo fulani zuri pamoja nawe, lakini nafikiri tutapaswa kuishia hapa. Alex... anaonekana kuwa mwanaume anayekupenda sana...hastahili hata kidogo kutendewa namna unavyomtendea. Unafikiri angejua kuhusu sisi hiyo ingekuweka wewe wapi? Nakuomba usiwe mbinafsi Harleen..." Dylan akasema kwa hisia.

"Lakini mimi nakupenda Dylan... siwezi tena kuwa bila wewe!" Harleen akasisitiza.

Dylan akamwachia na kumwangalia usoni.

"Ungehisije kama ungejua mimi pia nina mwanamke mwingine huku bado natoka nawe?" akamuuliza.

"Mimi sijali! Bado ningeendelea kuwa pamoja na wewe hata kama ungekuwa nao mia moja," Harleen akasema kwa uhakika.

Dylan akacheka huku amefumba mdomo, kisha akasema, "Basi wewe na mimi ni tofauti sana."

"Dylan...tafadhali nisamehe...nitaachana na..."

"No. Usiniambie hivyo Harleen. Kwa ufupi ni kwamba siwezi TENA kuwa nawe."

"Dylan..." Harleen akaanza kulia.

"Ikiwa utafanya hivyo mimi haitaniathiri kwa vyovyote vile, lakini wewe utakuwa umepoteza vyote. Kwa hiyo... nilichokuwa nataka nikwambie ni kwamba...nitaendelea kukuona kama rafiki, na siyo vinginevyo," Dylan akaeleza.

Harleen, akiwa analia, akamshika mikono Dylan na kuing'ang'ania ili amsisitizie kubaki naye. Lakini Dylan akaitoa na kugeuka ili aanze kuondoka. Harleen akabaki kumwita kwa huzuni, kisha akachuchumaa huku analia sana, akimwangalia jamaa anatokomea.

Dylan akarejea kwenye gari lake na kutulia kidogo. Akafumba macho akivuta taswira ya jinsi Harleen alivyokuwa akilia pale alipomwacha. Kihalisi kuondoka kwake pale upesi namna ile ilikuwa ni kukwepa zile hisia za huruma ambazo zingejengeka kumwelekea Harleen ikiwa angeendelea kumtazama anavyolia. Hakupenda usaliti kabisa. Na Harleen alikuwa mwenye pendeleo kwamba angalau Dylan alimwambia angeendelea kumwona kama rafiki, vinginevyo angemtolea nje mazima kabisa kwa kuwa sikuzote kama angechukia mtu, basi ilikuwa ni milele.

Akajiondokea hapo haraka na kwenda ofisini tena kujaribu kupiga kazi yoyote ili aondoe misongo kichwani. Kulipokuwa hakuna kazi alianza kucheza game la PS, akipoteza muda ili baadae amfate Fetty na kumtoa out kama alivyomuahidi jana. Simu yake iliita mara nyingi sana, na mpigaji alikuwa ni Harleen. Dylan hakupokea hata mara moja, na baada ya muda Harleen akaacha kupiga. Huu ndio uliokuwa wakati mgumu kihisia kwake kwa mara ya kwanza tokea aliporudi nchini. Hakutaka kuendelea kuhisi kama ameshuka moyo, hivyo akaondoka hapo na kumfata Fetty kule mgahawani.

★★★

Alifika mgahawani kwenye mida ya saa 12 jioni kukuta Fetty hayupo. Alipomuulizia, aliambiwa binti alikuws ameondoka mapema leo baada ya kazi kuisha. Alitegemea angemkuta hapo kwa kuwa aliona mara nyingi Fetty hurudi nyumbani giza likiwa limeingia, lakini ndiyo akaambiwa huwa anakaa tu na wenzake hapo wakipiga story baada ya kazi kuisha kisha ndiyo anakwenda nyumbani. Lakini wakamwambia leo alipomaliza tu kazi aliwahi kuondoka, hivyo Dylan akarudi kwenye gari lake na kumpigia simu.

"Vipi?" Fetty akasema baada ya kupokea.

"Uko wapi wewe?" Dylan akauliza.

"Ghetto...wewe uko wapi?"

"Aah... si tulikubaliana nitakupitia ama?"

"Nami si nilikwambia nitajiandaa vizuri? Ndiyo nimekuja kujiandaa, kwani uko wapi?"

"Unapofanyia kazi."

"Ai! Ahahahah... pole. Niko huku sasa," Fetty akasema.

"Haya, nakuja."

Akaondoka hapo mara moja na kuelekea kwa Fetty. Hii ilikuwa ni njia moja ya kumsaidia ili kutoikita akili yake kwenye mawazo kumwelekea Harleen. Alifika eneo la nje karibu na nyumba aliyopanga bibie, kisha akamwambia atoke. Fetty alitokea baada ya muda mfupi, na Dylan alipata kuona jinsi alivyokuwa amependeza kadiri alivyolikaribiagari. Alikuwa amevaa gauni yenye kubana mwili, iliyokuwa na mtindo wa rangi ya pundamilia. Ilikuwa ni aina ya vazi la kawaida tu, na hakujiremba kupita kiasi kana kwamba anatoka na boyfriend wake, lakini Dylan alipendezwa sana na jinsi mwonekano wake ulivyomfanya avutie.

Fetty akaingia ndani ya gari na kumwangalia Dylan huku anatabasamu, naye Dylan akamsalimu, kisha akaondoa gari hapo na kuelekea mpaka kwenye hoteli nyingine tofauti na ile ya jana. Ilikuwa ya kifahari pia, naye Fetty akatania kwamba alihakikisha hajala siku hiyo, hivyo angekula hotelini hapo mpaka Dylan angeona aibu. Dylan akamwambia asiwaze kabisa, chochote kile alichotaka angefanya.

Walifika na kuanza kutembea kidogo kuzunguka hoteli ile, wakiangalia mambo kadhaa yaliyovutia sana hapo. Wengi waliokuwepo walikuwa watu wenye pesa sana, na wazungu pia. Hoteli hii ilikuwa mbali kidogo kutokea kule wawili hawa walipoishi, na mandhari na vitu vingi vya kisasa vilimfurahisha sana Fetty. Ijapokuwa urafiki wake na Dylan ulikuwa mpya, alihisi ni kama amemjua kwa muda mrefu, hivyo kwa kadiri fulani aliweza kujiachia akiwa naye.

Baada ya muda fulani, Dylan alimpeleka sehemu ambayo wangepata vyakula. Alimwagizia binti burger (yenye nyama, mboga majani kidogo, na viungo mbalimbali), chips, nyama ya kukaangwa, na kinywaji kizito cha cream na maziwa (milk shake). Vilikuwa mara mbili, yaani Dylan pia aliletewa vya aina hiyo hiyo, kisha wote wakaanza kula. Maongezi yao yalikuwa kuhusiana na mambo ya shule, na kumbukumbu nyingi za zamani zilifanya mazungumzo hayo yawe yenye kufurahisha sana.

"Kweli?" Fetty akauliza huku wakiendelea kula.

"Ndiyo. Haitachukua muda mrefu sana nitaufungua," Dylan akasema, akimaanisha mgahawa wake.

"Halafu unajua...nilisahau tu kuuliza...hivi unafanya kazi gani?" Fetty akamuuliza.

"Nina...sijui nielezeeje...ni kazi....ya masuala ya ujenzi."

"Kwo' we fundi mwashi?"

"Ahahahah... yeah unaweza ukasema hivyo."

"Mmm... usinidanganye bwana."

"Kwa nini unafikiri nakudanganya?"

"Jinsi tu ulivyo...unavyoongea, unavyovaa...gari lako...vitu vingi ni vya kifahari tu. Nisingetolewa out na fundi mwashi kwenye sehemu kama hii," Fetty akasema.

Dylan akacheka sana.

"Hivi unawaonaje mafundi? Wana hela hao!" Dylan akasema.

"Lakini ni mabahili mno."

"Kwa hiyo kumbe una experience nao eeh?" Dylan akatega.

"Hamna...marafiki zangu tu husimulia."

"Mmh...kwani ungekubali sasa hata kama ni kweli?"

"Wala yaani me sinaga hizo kabisa. Tena nakwambiaje, yaani mimi nikijua tu mtu wa namna hiyo ananivizia-vizia nampiga chini faster...huwa sichelewi," Fetty akasema kwa uhakika.

"Kwa hiyo... tuseme siku moja unanikuta barabarani...niko kwenye mtaro napiga kazi huku nimepauka...halafu nikakusalimia, utaacha kuniitikia?" Dylan akauliza.

"Tena nakupita kama sikujui!" Fetty akajibu.

Dylan alicheka kwa furaha sana mpaka akasitisha kula. Fetty alikuwa akicheka pia huku anamwangalia jamaa kwa furaha.

"Dah aisee...itabidi nijipange," Dylan akasema baada ya kutulia.

"Kwa lipi?" Fetty akauliza.

"Kuhakikisha huji kunikuta hivyo siku moja."

"Kwani we ni fundi mwashi kweli? Acha masihara bwana."

"Aam... ninafanya kazi kwenye kampuni ya baba yangu."

"Kampuni gani?"

"GJD Construction Company... iko huko tulikotoka sijui kama unaijua."

"Ile ambayo...jengo lake liko karibu na ile round about..ukiwa unaelekea Exim Bank?" Fetty akauliza.

"Eee upande wa kushoto kutokea huko..."

"Kushoto eeh..."

"Ndiyo, hapo hapo."

"Lile jengo ni kampuni ya baba yako?!" Fetty akauliza kimshangao.

"Ndiyo."

"Aisee... kumbe nimekaa na tajiri mkubwa hapa!"

"Ahahahah... acha hizo bwana."

"Siyo poa...natamani nije niione nyumba yenu siku moja najua ina maghorofa kumi kama sikosei," Fetty akatania.

Dylan akacheka.

"Huwa unalala kwenye King size bed au siyo?" Fetty akatania.

"Hamna wala. Huwa nalala chini," Dylan akasema.

"Chini?"

"Yeah."

"Hmm? Hauna lolote wewe...yaani mna mihela halafu ulale chini?"

"Ahahah... najua ni ngumu kuamini lakini, ni kweli."

"Kwa hiyo unataka kuniambia huwa unalala chini kabisa?"

"Siyo chini kabisa. Sipendelei kulala kwenye kitanda. Huwa naweka godoro chini ndiyo nalala."

"Kwa nini sasa?"

"Huwa napenda tu. Tokea zamani sana...napenda mno kulala chini yaani najihisi comfortable."

"Mh... haya bwana tajiri. Kama mna pesa hivyo nataka kila siku uwe unaninunulia baga..."

"Ahahah... halafu unanipa nini?" Dylan akauliza kimasihara.

Fetty alikuwa anatabasamu, lakini baada ya Dylan kusema hivyo tabasamu lake likafifia. Akamwangalia Dylan kwa sekunde kadhaa, huku jamaa akiendelea tu kula taratibu, na akimtazama Fetty kwa makini pia. Alijua bila shaka swali lake la kichokozi lilimkonga nyoyo mwanamke huyu.

Fetty akavunja utizami huo kisha akasema kwa sauti ya chini, "Nilikuwa natania tu."

"Hata me nilikuwa natania tu," Dylan akajibu pia.

"Ona...sitaki ufikiri kwamba labda niko hapa kwa sababu..." Fetty akashindwa kumalizia.

Dylan alipomwangalia vizuri, akatambua kuwa sura ya Fetty ilionyesha kama... amekwazika. Akagundua kuwa kwa njia fulani huenda maneno yake bila kutarajia yalimfanya binti ajihisi vibaya, ijapokuwa alikuwa anatania tu.

"Oh... no, no, no, Fetty...please usifikirie hivyo. Nina... nafurahia company yako sana...jambo hilo halijaingia akilini mwangu kabisa, tafadhali niwie radhi kama nimekufanya ujihisi vibaya," Dylan akasema kwa upole.

"Sawa. Haina shida. Hata mimi... nafurahia company yako," Fetty akasema.

Dylan akatabasamu kisha akasema, "Sasa je! Mafundi mwashi hawaboi kama unavyofikiria."

Fetty akacheka kidogo na kusema, "Eti mafundi mwashi! Ni mafundi waashi."

"Wewe! Kiswahili cha wapi hicho?"

"Cha kitanzania...we unachoongea sijui ni cha wapi..."

"Hakuna...ni mafundi mwashi... haina wingi..."

"Hamna...washa simu uangalie kamusi Google..."

"Na nikikuta niko sahihi?"

"Basi mimi ndiyo nitalipia hiki chakula chote."

Dylan akacheka.

"Na tukikuta hauko sahihi, utapaswa...."

Kabla Fetty hajamaliza kuongea simu yake iliita, na alipoitoa, akakuta ni mama yake ndiyo anapiga. Akamwambia Dylan atafute Google aone, kisha akapokea huku Dylan akiwa anamwangalia tu na tabasamu.

"Halloo... Mama, mama, nini... subiri sikuelewi nini kimetokea?"

Dylan alianza kumwangalia kwa makini baada ya kutambua kulikuwa na tatizo upande wa mama yake.

Fetty akasimama ghafla na kuuliza kwa sauti ya juu, "NINI?!"

Dylan alishtushwa kiasi na jambo hilo. Yeye pia akasimama taratibu, huku sasa pumzi za Fetty zikianza kuongezeka kasi.

★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi kali ya DYLAN. Waweza ipata yote kwa sh. 2000 tu WhatsApp.

WhatsApp no: +255 787 604 893 (hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo utaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)
 
Back
Top Bottom