Brg Gen Mwakanjuki afariki dunia

Namkumbuka sana huyu Adam Mwakanjuki, wakati akiwa waziri wa Serikali ya Mapinduzi huko visiwani, alitembelea kwetu kirafiki, wazazi walipokuwa nje kikazi, tulimwandalia chakula cha mchana tukifikiria ni mwenzetu kiimani kwa vile jina la Adam Mwakanjuki si la ustaadhi Maalim. Alipokaribishwa alikula aina ya vyakula vyote vilivyowekwa mbele yake ila hakugusa nyama. Naona alifikiri ni kiti moto kwa vile siku iliyotangulia tulimtembeza kwa majirani wanaofuga kiti moto na kwetu kwenye zizi la ndama wa Maziwa.

Kwa vyo vyote tunamkumbuka alikuwa mstaarabu na asiye na ubaguzi na kujenga uvumilivu wa hali ya juu kwa ajili ya umoja wa kitaifa.
RIP Adam Mkwakanjuki.

RIP Brigadier General Mwakanjuki.


Lakini habari kwenye IPPMEDIA ya leo na sehemu zingine zinadai alikuwa mmoja wa Wakristo kama watatu hivi kwenye SMZ.
 
Duh,, mwaka huu Tanzania TUNAPATA darasa la Nguvu kutoka kwa MOLA. Yaani wakongwe wote wanaondoka, moja baada ya mwingine. R.I.P Mkuu. Poleni sana wafiwa.
 
Nawashukuruni wote kwa salamu za rambirambi, aidha kupitia hapa tutaendelea kuwa pamoja kwa taarifa zaidi juu ya msiba huu wa baba yangu mzazi.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.

Pole sana Best yangu Kibunango ... Mwenyezi Mungu akupe nguvu na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu sana.

Sote njia yetu ni hiyo ... ametutangulia, ipo siku nasi tutamfuata.

RIP Brig. Gen. Mwakanjuki
 
Nawashukuruni wote kwa salamu za rambirambi, aidha kupitia hapa tutaendelea kuwa pamoja kwa taarifa zaidi juu ya msiba huu wa baba yangu mzazi.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.

Poleni sana Mkuu kwa Msiba huu mzito. Mungu awape Nguvu na Subira.
 
Nawashukuruni wote kwa salamu za rambirambi, aidha kupitia hapa tutaendelea kuwa pamoja kwa taarifa zaidi juu ya msiba huu wa baba yangu mzazi.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.
well, hutakiwi kuwa mitandaoni kama baba yako mzazi amefariki, nenda uka focus msibani!
 
well, hutakiwi kuwa mitandaoni kama baba yako mzazi amefariki, nenda uka focus msibani!

Mtu aliyezoea kula kwa mikono hata umpe vijiko vya dhahabu atanawa mikono tu. Wewe kwa vile lazima uende internet cafe kupost humu basi unajdhani kila mtu ni hivyo. Kwa maana nyingine unamwambia aache kutumia simu vile yuko msibani, huoni uwepo wake hapa ni muhimu sana kutujulisha yanayojiri msibani..................Pole sana Kibunango
 
Kwa maana nyingine unamwambia aache kutumia simu vile yuko msibani, huoni uwepo wake hapa ni muhimu sana kutujulisha yanayojiri msibani.................
kutujulisha kwenye mitandao ili iweje? wenye uchungu wa kwanza na msiba wa baba yake akili zao ziko msibani, anatakiwa awe nao kimwili na kiroho, badala ya kushinda anaranda randa mitandaoni.
 
Nawashukuruni wote kwa salamu za rambirambi, aidha kupitia hapa tutaendelea kuwa pamoja kwa taarifa zaidi juu ya msiba huu wa baba yangu mzazi.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.

Mkuu Kibunango, pole sana kwa msiba wa Baba!.

Niliproduce documentary yake huko Zanzibar akiwa Waziri wa Kilimo. Ilirushwa TVT na TVZ.

Kwa sasa ni jirani yanu, niko nyumba ya tatu kutoka kwenu, next to Kahatano na Deo Mtui.

Mchana huu nimetoka hapo na kuelezwa uamuzi wa maziko Zanzibar au bara` utatolewa jioni hii!

RIP Brig. Gen. Mwakanjuki!.
 
RIP Uncle, wil miss you


Majenerali wa Ukweli wanaishia hivyo......tunabaki na MASHIMBOSHIMBO

RIP Mjomba

p+046.jpg
 
Alikuwa mkristu Muangilikan...............

Na asili yake ni Tukuyu Mwakaleli siyo Kyela, anaundugu na Prof Mwandosya kiaina.[/QUO


Thanks kwa masahihisho hayo. Kyela ameoa na kwa waliopo Mbeya ujomba wake upo pale Iyunga, ni Mzee Mwasambungu karibu na Kanisa la KKKT
 
Pole sana bwana Kibunango kwa kuondokewa na mzazi. Ni pigo kubwa sana kwa sababu yeye ndiye anayewaunga ninyi nyote. RIP the Bingwa. I think that is your nick name for him.
 
RIP Brigadier General Mwakanjuki.


Lakini habari kwenye IPPMEDIA ya leo na sehemu zingine zinadai alikuwa mmoja wa Wakristo kama watatu hivi kwenye SMZ.

Hii habari ya mnavyotofautina dini yake , sidhani kama inahusu hapa, ama itatupa faida ya kimsingi kwenu na kwetu. Awe Muislam au Mkristu, Pagani haijalishi.
Au mmealikwa kwenye ibada ya mazishi yake ?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom