Hhahahaha, kama Steve shabiki wa Yanga, mana hata kulia hawezi, tayari yupo bongo movie, kaazi kweli kweli.Sidhani kama kuna aliyesomea sanaa. Ukiwa na kaumaarufu tu hata ka mavazi tayari wewe ushakuwa muigizaji. Baada ya movie 3 basi director au script writer!
Samahani lkn iv wasanii hawaoni fursa nn. Wanashindwa kutengeneza muvi kupitia tukio la wastegate, mafisadi tanzania, shekh ponda, kapuya, madawa ya kulevya tanzania, mambo ya polisi ccm, kimbunga, na hata mauaji ya tembo na kushamiri kwa wachina na wahind bongo
mtu tupo na demu wake supermarket NUSU SAA NZIMA afu muvi ina saa moja na nusu
akipigwa ngumi anaangalia pa kuangukia kwa usalama wake asijeumia. milio ya risasi kama unawasha njiti za kibiriti
Mtu analia lakini machozi hayatoki mwisho anaishia kukunja uso tu kwa nguvu...!!
Kahaba lazima avute sigara.....jambaz lazma livae koti refu na miwan myeus....mganga wa kienyeji lazma awe porini,mchafu,halaf anaongea kwa ukali!
Mapenz yanaanza pale mwanamke anapoharibikiwa na gari af mwanaume anatokea kumsaidia......au wanapopigana vikumbo,mafaili ya dem yakidondoka mwanaume anaokota fasta anampa af wanatabasamu...kwisha kazi!