Bongo movies...

Bongo movies...

angalau kidogo siku hizi wanajitahidi..........lakini angalia actions katika bongo movies, ni vituko.
 
Kuna muvi moja niliiona kwenye Haya mabasi ya mikoani inaitwa "Inye". Jamani hivi ilikuwaje BASATA wakaachia upuuzi huh.
 
Mtu akifa lazima azikwe makaburi ya kinondoni....tena yale ya kikristo
 
Nimependa sana critics karbu zote nadhani kama wako humu watajirekebisha ila nawaomba umakini mliokuwa nao kugundua makosa kwenye hii tasnia mngeuhamishia kwenye kutuchagulia viongozi makini chaguzi zijazo hakika tutafika mbali
 
Waige mfano wa Tamthilia kama ya siri za Familia ambayo ukiitizama hauwezi kuwa bored,inaonyesha watu wamefanya mazoezi na wanajua wanachokifanya.Mi nashangaa siku hizi unakutana kundi la vijana wako kama mateja,wa kike na wakiume wamebeba vibegi migongoni na wana stendi za camera,ukiuliza kulikoni unaambiwa heti wana shoot movie,yaani hii taaluma imeingiliwa,.pia dosari zote zilizosemwa tatizo kubwa ni elimu na upeo,wengi walio kwenye bongo movie elimu yao ni la saba au kidato cha nne division 5,siku hizi ndio ytumeanza kupata graduate wachache ambao nao si kwamba wana wito na kazi bali sababu ya ukosefu wa ajira,Nigeria actors wengi tunao ona wana ama degree moja ama mbili na wamesomea hiyohiyo fani ya uigizaji.
bongo movie bado ina safari ndefu hadi kufikia pale ambapo bongo movie itakuwa haionekani kama kimbilio la walioshindwa shule ,mtu hana elimu yoyote lakini unamsikia anasema iko siku nitatoka tu kupitia bongo movie.Bongo movie nayo inahitaji akili za kutosha ili kuelewa audience wanataka nini,kama unemfeli shule utaishia commedy za kijingajinga tu lakini huwezi kuigiza movie zenye kueleweka ama kuvutia.
 
ukiondoa movie za south africa na zimbabwe, na sometimes wakenya wanajitahifi kwa baadhi ya tamthilia zao.
ila wanaijeria na watanzania mimi bado kabisa labda siri ya mtungi ndiyo niliielewa.
 
Njaa kali sana bongo movie jamani nyie acheni tu
Akili ndogo inalazimisha ifanye mambo makubwa
 
Ni katika bongo movies:
1. Majeruhi na maiti zinabebwa kwa mikono mitupu.
2. Maiti zinatetemeka macho
3. Ukitaka kucheka zaidi angalia scene za kipelelezi na za kimahakama.
4. Aliyepigwa risasi ana damu kama sample ya kupimia malaria.
5. ...endelezeni wenyewe mi bado naangalia.
Hahaha aisee sasa si wanaigiza mbona haujawaongelea wahindi?
 
Kuonyesha gari inakimbia sana wana bonyeza fast forward kwenye remote alafu wanarudia kile kipande ili ionekane gari imetembea umbali mrefu.

Duu nilicheka sana aibu aibu sana.
 
Hayo mabongo muvi mtajipa hasira za bure. Mi nilikua mpenzi wa maigizo yale ya kina mzee Jangara, yakaja yale ya kina Uledi na kina mama Siyawezi bila kumsahau Janta binti madebe wa nyama kilo 5 na kanga doti 2. Nadhani ni miaka ya 90.
Baada ya hapo nilivutiwa na maigizo ya kina mzee Jengua na sijui kundi lake lilifia wapi miaka ya 2000. Toka hapo sina habari na hayo matakataka ya bongo muvi.
Tena ili kujiepusha na karaha zao nikisafiri nachaji simu kisha nabeba earphone zangu.
 
hahahahaaaaaa..........kweli zinaboa,raia hawavai ule uhalisia,kibongo bongo its better u watch comedy movies...eg mzee majuto,jotti,n others u wont get bored
Ila mara nyingi wanazitolea maoni ni wateja wa Bongo movies, asiengalia hayo makosa atayaonea wapi. Kuna wengine huja hapa kuilaumu Cloud fm mara nyingi sana, ila ukijiuliza makosa haya anayasikia saa ngapi kwenye radio asiyoipenda kuisikiliza,
Jibu ni anasikiliza kimoyo moyo.
 
Yaa. Mi huwa naangalia sana, movie zinatengenezwa nchini kwetu lazima tuangalie kuna vitu vya kujifunza, kuburudisha nk. Ila ndio kuna hayo mapungufu, na kama wangeyafanyia kazi tungesonga mbele. Ila bongo muvi wanajiona wao maprofesa hawashauliki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom