Bongo movies...

Bongo movies...

Hata wapigane vipi, haivunjiki glasi, kabati wala meza ni mlio wa migumi tuu duushhh!
 
afu mzaz akitaka mwanae akasome, "utasikia mm na mama yako tumeamua mwanetu ukasome nje ya nchi"
 
Mdada anatoka kuamka full makeups usoni,wanja,lipshine inang'aa....
 
Sehemu kubwa ya muvi inasimuliwa kupitia maongezi......either wakiwa wamekaa kwenye kochi...au wamesimama mahali wanaongea.......kwa mfano utawasikia waigizaji...mimi nilizaliwa peke yangu.....wazazi wangu walifariki nikiwa mdogo.....nilitembea na housegirl wetu, akapata mimba.....akataka kuitoa nikamkataza......nikapata mtoto wa kike....badae housegirl akatoroka....nikamtafuta nikampata...nikamnyang'anya mtoto...akanipeleka mahakamani..tukapima DNA....kumbe mtoto sio wangu... Sasa sijui hapa tofauti ya muvie na novel ni nini ? ukijaribu kuwashauri kuhusu umuhimu wa kutumia screen writers, ni ugomvi......
 
yan hicho ndo kitu kinachoniboaga yan hata kama katoka bafuni kuoga bt usoni anang'aa ovyo
 
Damu hufanana na tomato sauce
Achani tu jana nimeangalia moja inaitwa yellow banana nusu nitapike mimi sijuo hawa waongozaji huwa hawajifunzi kutoka kwa wenzetu movie imechezwa na watu watatu inaboa to the extents .
 
Kahaba lazima avute sigara.....jambaz lazma livae koti refu na miwan myeus....mganga wa kienyeji lazma awe porini,mchafu,halaf anaongea kwa ukali!

Mzee hapo umetisha huo ndio ukweli jamaa sio wabunifu kabisa tatizo yanavamia fani kwa cc walevi wa movie tunapata shida sana ndo maana tunaangalia za wenzetu tu haya mabongo yanaboa sana sijui hayo ma movie yanawalipaje sas
 
Hizi muvi za kibongo ukiiona mwanzo wakati inaanza unajua na mwisho wake itaishaje, mapenzi, visa, mikasa ya usaliti wa mapenzi, uchawi ndio main theme... maisha yanabadilika kwa nini hawa watu hawabadiliki!? Ikiwa tatizo ni elimu washirikishe wadau wa sanaa si lazima kila muvi Jb awepo jamani....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom