Bomu lilirushwa likaangukia hapa

Bomu lilirushwa likaangukia hapa

Duh! watu walikuwa nyomi ndo maana kuna watu walikasirika ili wanachi waogope kwenda kwenye mikutano ya CDM.
 
Mkuu Crashwise hakika tukio lile halitokaa linitoke. Na kwako Mungi, Mungu ni mkubwa sana kwani tulipoondoa miguu yetu pale pakarushwa lile bomu! Humu JF huenda kungekuwa na thread ya RIP Arushaone na Mungi.

poleni sana, na mie nilikuwepo but nilikuwa kule mwisho tulipopaki magari! Judy amenisikitisha sana sana jamani, Apumzike kwa amani.
 
serikali (watawala) tz wamezoea kuwaona raia wa tz wakiwa wapole kwa kila hali; sasa kwa kumwaga damu huku sidhani kama amani inayosadikika kuwepo itaendelea kudumu hata kwa miaka miwili ijayo!
Mungu ibariki Tanzania
 
Mrusha bomu alionekana mkuu, watu walitaka kumkamata lakini polisi waliingilia kwa kurusha risasi na mabomu.

I think ilikuwa hali ya taharuki hata polisi hawakujua nini kinaendelea na hawakujua kama kungekuwa na mabomu mengine ndio maana wakawahi kuingilia ili watu watawanyike.
 
Damu ya huyu mama na wengine zitaimaliza kabisa CCM. Haitachua muda mwingi hiki chama na wadhalimu wake watabakia historia katika nchi yetu. Tuzidi kumwomba Mungu. Yeye hapangiwi cha kufanya ila anafanya kilicho cha haki.

Inasikitisha kudhani kwamba damu ya huyo mama itaimaliza CCM.
Tafakuri jadidi inatosha kukujulisha kuwa CCM kamwe haihusiki na haiwezi kuhusika na upuuzi huo wa kurusha mabomu.
Jiangalieni ndani ya CDM mtajua nani kafanya hivyo na nini madhumuni yake.
Pia mjiulize kwa nini Kaloleni na kwa nini isiwe kata zingine tatu zilizobaki za Arusha au mikoa mingine.
Nataka kuwahakikishia tu kuwa what goes around comes also around. Kwani mwisho wa siku mtajua nani kawafanyia hivyo.
 
Serikali inakosaje huruma na kupofushwa na uadui wa kisiasa jamani? Hawa watu wana kosa gani kuisikiliza CHADEMA ilhali mfumo wa vyama vingi umeruhusiwa kisheria? Waufute basi kama hawataki kushindwa
Mkuu issue hapa ni halimashauri ya jiji la Arusha, CCM hawataki kuiachia kabisa na walijua kama uchaguzi ungefanyika ilikuwa mwisho wao......
 
Asante Mungu, asante kamanda na Mungu atuepushe la pepo la husuda kwa mafanikio ya Chadema.
 
Kwa maana hiyo Mh. Lukuvi anataka kutuaminisha kuwa CDM ilitaka viongozi wake wote wajiuwe ili wapate kura za huruma kutoka kwa wananchi. Naona dalili zote za nchi hii kuingizwa kwenye machafuko kwa kulazimishwa. Dhamana ya hii nchi bado ipo mikononi kwa watawala wenye dola halali kikatiba. Sasa sisi wananchi IMANI yetu tuifukize wapi?

Lukuvi ana mind set za kijinga na za kizamani sana. Hadi leo anadhani wananchi hawajui upumbavu wa CCM hao waliokufa mbegu yao haitakufa kamwe Tanzania itakuja kukombolewa siku moja. Kumbe hatujapata Uhuru kilichofanyika ni kubadili Mkoloni toka Mkoloni Zeruzeru hadi Mkoloni mweusi.
 
Lukuvi ana matatizo sana,huwa hajielewi kabisa.kati ya watu wenye upeo mdongo wa kuwazua mambo nafikiri anaongoza

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
siku zote panapofuka moshi ujue pana moto, na Dalili za mvua ni mawingu, hakika siku za mwisho za MAGAMBA zitaambatana na matukio mengi ya ajabu na kuogofya kama tuyaonayo xaxa. I do believe that the end will come justify the beginning. Eeeh MOLA wtu wa reheme zipokee toharani roho za marehemu hawa wasiokuwa na hatia wapate pumzika kwa amani.
 
Exactly unaweza kukuta mrusha bomu akaonekana hapo hapo kwenye picha!

Wenye picha wazipeleke vyombo husika.
Mkuu, unauliza kuhusu mrusha bomu au walioua kwa risasi...huhitaji elimu ya chuo kikuu kujua waliofanya unyama huo...hata hivyo ni swala la muda tena mfupi kila kitu kitakuwa wazi...
 

Lukuvi ana mind set za kijinga na za kizamani sana. Hadi leo anadhani wananchi hawajui upumbavu wa CCM hao waliokufa mbegu yao haitakufa kamwe Tanzania itakuja kukombolewa siku moja. Kumbe hatujapata Uhuru kilichofanyika ni kubadili Mkoloni toka Mkoloni Zeruzeru hadi Mkoloni mweusi.

mkuu ukisemacho ni KWELI na mkoloni mweusi yu mbion kuondolewa
 
Inasikitisha kudhani kwamba damu ya huyo mama itaimaliza CCM.
Tafakuri jadidi inatosha kukujulisha kuwa CCM kamwe haihusiki na haiwezi kuhusika na upuuzi huo wa kurusha mabomu.
Jiangalieni ndani ya CDM mtajua nani kafanya hivyo na nini madhumuni yake.
Pia mjiulize kwa nini Kaloleni na kwa nini isiwe kata zingine tatu zilizobaki za Arusha au mikoa mingine.
Nataka kuwahakikishia tu kuwa what goes around comes also around. Kwani mwisho wa siku mtajua nani kawafanyia hivyo.
pole sana kwa kuendelea kutetea chama cha wauwaji majangili lakini nikwambie kilichotokea tarehe 15/06/13 ni zaidi ya bomu, kilicho umiza wengi ni risasi zilizorushwa baada ya bomu kurushwa nina uhakika kabisa walioumia na bomu moja kwa moja hawazidi kumi lakini waliumia na risasi ni zaidi ya 50, nenda kawatembelee watu mahospitaliniutaona... na kwa kwa maelezo ya jeshi ambayo watanzania hatutaambiwa ni kuwa mabomu na risasi zimetoka china na zimetengenezwa mwaka huu ndiyo maana polisi jana wameshinda pale wakihangaika kujua, hawakujua kuwa ni mambomu na risasi ni mpya kabisa na hawakuwa na kumbu kumbu za mabomu hayo..kuna uzi humu uliweka vema swala hilo...utafute......
 
Back
Top Bottom