Acheni Mungu Aitwe Mungu!
Macho yaliyofumbwa sasa yamefunguliwa, kila kilichokuwa gizani sasa kipo nuruni.
Uongozi huu wa kidhalimu na njama zake zote zinawekwa hadharani mchana mweupe...
Tazama, hata picha zipo kuonyesha nani alikuwa wapi, nadhani waliopanga udhalimu huu walifikiri njia za giza walizozoea kutumia kufanikisha udhalimu wao zitabaki gizani milele!
Hatuhitaji kutafuta mchawi, hatuhitaji kuundiwa tume, hatuhitaji kuwa wataalamu wa 'nuclear science' kujua nani alikuwa anawindwa na bomu hilo, na kujua aliyelirusha alikuwa na dhamira gani.
Roho inaniuma sana kuona tumepoteza wapiganaji wetu kwa uroho wa kubaki madarakani wa watu wachache na serikali yao ya kidhalimu.
Lakini kama Andiko linavyosema, Hakika Neno la Mungu Litasimama!
Damu iliyomwagika pale Soweto itakuwa chachu ya mabadiliko.
Na sijui kwa nini siku hiyo mkutano mkubwa ulifanyika mahali panapoitwa Soweto.
Tujaribu kujikumbusha historia ya SOWETO kwenye mapambano ya kuwaondoa madarakani makaburu wa Afrika ya Kusini!
Mungu Awalaze Pema makamanda wetu waliopoteza maisha, na Awape nguvu ya uponyaji wote waliojeruhiwa!
Aluta Continua!