Bobi Wine alaani Jeshi la polisi nchini Uganda kwa kujaribu kumzuia kwenda katika uchaguzi

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Aug 30, 2021
630
1,245
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi, al maarufu Bobi Wine, ametuma picha ya polisi na jeshi wakionekana nje ya nyumba yake kabla ya kampeni za uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika katika wilaya ya Kayunga.

Rais Yoweri Museveni anatarajiwa kutembelea katika wilaya ya Kayunga kumfanyia kampeni mgombea wa chama tawala anayewania nafasi ya uenyekiti.

Uchaguzi huo mdogo umepangwa kufanyika Alhamisi na chama tawala na upinzani kwa pamoja vinataka kuonyesha uwezo wao katika eneo hilo.

Bobi Wine ameshutumu jeshi na polisi kwa kujaribu kumzuwia kuondoka nyumbani kwake.
Vyombo vya habari nchini Uganda vimeripoti kuwa polisi na jeshi pia wamepelekwa Kayunga kabla ya kampeni za Jumanne.

#DictatorMuseveni is so shameless. He places me under house arrest, and then uses tax payer's money to ferry people to go see him in Kayunga! This is why we are not giving up until Uganda is free.#WeAreRemovingADictator pic.twitter.com/jENcenKaEm
— BOBI WINE (@HEBobiwine) December 14, 2021

images (13).jpeg
 
Back
Top Bottom