RC Chalamila apongeza Jeshi la polisi na Barrick kwa kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa vitendo

Blasio Kachuchu

Senior Member
Sep 7, 2016
153
111

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila akiongea katika hafla hiyo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila (katikati) akikabidhi cheti cha shukrani kwa Afisa Mawasiliano wa Barrick,Abella Mutiganzi na Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa (Kulia) kutokana na kampuni hiyo kufadhili mafunzo ya utambuzi wa masuala ya jinsia yaliyoendeshwa na Jeshi la Polisi katika katika hafla ya kuhitimisha maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia iliyofanyika katika Chuo Cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (kushoto) ni Mkuu wa Chuo hicho, SACP Dk.Lazaro Mambosasa

Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa, akiongea katika hafla ya kuhitimisha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa jinsia iliyofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi cha Dar es Salaam.Mwaka huu Barrick ilishirikiana na Jeshi la Polisi katika maadhimisho hayo.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akikabidhi cheti kwa Mratibu wa madawati ya kijinsia kwenye vyuo vya kati na vya juu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Gift Msowoya,

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio katika hafla hiyo

Wanafunzi wa shule ya msingi Mgulani wakiimba wimbo kuhusu ukatili wa kijinsia katika hafla hiyo

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Barrick kuadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili kwa kijinsia kwa vitendo, ambapo limeweza kutoa elimu ya utambuzi wa vitendo hivyo na hatua za kuchukua wahanga wa vitendo hivyo katika shule za msingi,sekondari , kwenye maeneo ya biashara jijini Dar es Salaam.

Chalamila, alitoa pongezi hizo wakati wa hafla ya kufunga maadhimisho hayo iliyofanyika katika Chuo Cha Polisi cha Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka taasisi za kupinga vitendo hivyo.

Alisema pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika siku 16 kwa kufikisha elimu ya utambuzi wa vitendo hivyo bado kunahitajika nguvu ya pamoja kuendeleakuongeza ushawishi,kuhamasisha,kukemea na kuelimisha jamii ambayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo matatizo ya kisaikolojia yanaopelekea wananchi wengi kuelewa tatizo hilo na kujikuta vitendo hivi vinaongezeka kwa kasi hususani katika miji mikubwa kama Dar es Salaam.

“Natoa Pongezi kwa Jeshi la Polisi na Barrick, kwa kuungana pamoja kuhakikisha mnapeleka elimu ya utambuzi wa elimu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.Natoa wito kuwa muendeleze ushirikiano huu katika kampeni mbalimbali zenye lengo la kuleta mabadiliko chanya kama ambavyo mmefanya katika maadhimisho haya.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha Polisi cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam,SACP Dk.Lazaro Mambosasa,alisema kuwa jeshi la polisi kwa kutumia wataalamu wake waliopo katika madawati ya kijinsia yaliyosambaa katika mtandao mkubwa wa vituo vyake litaendelea kutoa elimu na kusaidia wahanga wa vitendo sambamba ba kuhakikisha wanaofanya vitendo hivyo wanafikishwa haraka kwenye vyombo vya sheria.

Naye Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa, alisema kuwa,Barrick Imekuwa mstari wa mbele kukabiliana na vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu hivyo siku zote itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika vita vya kupambana kutokomeza vitendo hivi vya ukatili wa kijinsia chini.

Awali akitoa taarifa ya kampeni hiyo kwa mgeni rasmi, Mratibu wa madawati ya kijinsia kwenye vyuo vya kati na vya juu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Gift Msowoya, alisema kuwa katika kipindi cha kampeni wameweza kufikia shule zaidi ya 10 za msingi na sekondari katika wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam,Kwenye masoko na mikusanyiko ya watu pia kupitia vipindi vya televisheni na vyombo vingine vya habari, elimu hiyo imeweza kuwafikia watanzania wengi.

Msowoya, pia alisema kuwa katika kipindi hicho cha kampeni waliweza kutembelea gereza la Segerea kupeleka elimu hiyo sambamba na kufanya matendo ya huruma ambapo waliweza kutoa msaada wa vifaa mbalimbali katika gereza hilo.

Maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ambayo huadhimishwa duniani kote na hapa nchini kuadhimishwa na taasisis mbalimbali na wadau wa masuala ya kijinsia mwaka huu yalianza tarehe 25 Novemba na kuhitimishwa tarehe 10,mwezi huu.
 
Back
Top Bottom